Tusipotoshane, ajira ina nafuu na uhakika zaidi kuliko kujiajiri

sky soldier

JF-Expert Member
Mar 30, 2020
5,408
19,014
Kwanza kabisa naomba tuyaelewe haya makundi matatu

KUNDI LA KWANZA - ALIEJIAJIRI / SELF EMPLOYED

1636723186836.png
1636723321962.png


Huyu biashara inamuhitaji ili iende, yeye ndie ngvu kazi kuu ya kuieiendesha biashara kwa bidii yake na hata akiajiri bado yeye inabidi ahusike kwa level ya juu sana ili biashara iende, Wengi wao inabidi aende dukani kila siku alfajiri mpaka usiku, kutembeza bidhaa mitaani (machinga), fundi cherehani, n.k kundi hili mara nyingi asipoenda ofisini hakuna pesa inaingia hapo, akiumwa hakuna malipo, n.k.
Kundi hili kusema kweli hakuna uhuru, mtu ukiwa kundi hili usije kujichanganya hata siku moja kujifananisha na watu wa kundi la pili, wenzetu wengi wa nchi zilizoendelea kwenye maarifa, mtu akiingia hili kundi anasota miaka hata mitano ili aingie kundi la pili, cha ajabu huku Tanzania ni kama vile watu wa hili kundi wamridhika kuwepo hili kundi ama hawanana mikakati ya kuingia kundi la pili, wengi nimewajua tangu nipo shule ya msingi bado wapo pale pale, nahisi ni kukosa maarifa kwa kudhani kwamba wapo kundi moja na kundi la pili.

KUNDI LA PILI - MMILIKI WA BIASHARA / BUSINESS OWNER

1636723243295.png
1636723271489.png


Hawa sifa yao kuu ni kwamba wameajiri watu wengine wawasaidie kuzalisha pesa, hawafanyi kazi ili wapate pesa kama kundi la kwanza na la tatu, pesa ndio inawafanyia kazi ..Yeye anaweza akanunua kiwanja akapageuza kuwa car wash, vijana wanakuja kuosha magari, ikifika jioni anakuja kuchukua mgao wake. Anaweza akawa ni Mo au Bakhresa ikifika asubuhi watu wanawahi kwenda kwenye viwanda vyao kufanya kazi ili kuwatengenezea pesa na wao kulipwa mishahara,

Hata kwa upande wa wasanii, Diamond yupo kundi la pili, kaajiri mameneja, wasanii, n.k ana magari ya kufahari kama rolls royce toleo la mwaka huu, escallade toleo la mwaka jana, v8 kama ya wabunge, n.k , wasanii wengi wapo kundi la kwanza wanatembelea toyota za mwaka 2014 zilizotumika mno.

KUNDI LA TATU- ALIEAJIRIWA (EMPLOYED)

1636800623482.png
1636723534441.png


Hili kundi lina nafuu kuzidi kundi la kwanza hasa wakiwa wanapata kipato sawa
  • Kazi anayoifanya haifanyi peke yake huwa wanasaidiana na wengine kwa hio mzigo haujamuelemea​
  • Mshahara wake atalipwa hata akiumwa ama kuwa na sababu maalum ya kutofika kazini​
  • anaweza kuingia kazini saa 2 na kutoka saa 10 / 11 jioni na kupata muda wa kukaa na watoto kama mzazi.​
  • Bima ya afya​
  • Mikopo kupatikana kirahisi​
  • Anapumzika siku za weekend zipatazo 104, sherehe za kidini na sherehe za kiserikali siku 20, kkizo ya mwezi siku 30, n.k​
  • Kipatoo ambacho ni mshahara atakipata kwa uhakika bila longo longo, pia kuna posho​
  • Anapata status kwenye jamii mfano baba flani ni mwanajeshi, injinia, muhasibu, dokta, hakimu, n.k. ukipata tatizo flani anaweza kutumia nafasi yake kukusaidia.​
  • Anaweza kuingia kundi la pili bila kupitia taabu za kundi la kwanza maana tayari ana mshahara na anapata mkopo bila longo longo unaoweza kuwa mtaji na ukagharamia mfanyakazi wa kumtengenezea fedha​
TUREJEE KWENYE MAADA.....

Huwa nashangaa sana mtu wa kundi la kwanza anaeshinda dukani masaa zaidi ya 12, anapigwa na jua mchana akitembeza bidhaa, n.k na faida yenyewe haizidi hata elf 30 kwa siku, Sijui ni wapi anautoa ujasiri wa kumdharau mtu wa kundi la tatu kwa kauli kama "ajira ni utumwa" hapo ikumbukwe yeye na mwenzake wanaingiza kipato sawa lakini mwenzake anafanyia kazi zake ofisini kwenye kiyoyozi, umeme ukikatika generator inawashwa, anafana kazi mpaka saa 10 tu jioni, ana siku siku 150 kati ya 365 za kupumzika kila mwaka, akiumwa bado anapata analipwa, kuna posho za ziada, anaweza kufungua biashara na kuajiri wasimamizi, n.k

Kauli nyingine ya kijinga ya kujifariji ni kuuliza swali "nitajie tajiri yeyote mkubwa nchini alietajirika kupitia mshahara?" Hapa mtu anauliza hili swali kwa maksudi kabisa ili kujifariji huku akijidanganya kwamba yupo kundi moja na kina bakhresa waliopo kundi la pili, anasahau kabisa kwamba watu wa kundi la pili ni Business owners (wamiliki wa biashara) wanaoajiri watu wawatafutie pesa, hata wakiuchapa usingizi mpaka saa nne pesa inaingia tu.

Kuponda ajira ni utumwa kwa mtu aliejiajiri ni sawa na "sizitaki mbichi hizi", nimeshushudia ajira zikitangazwa, hao waliojiajiri wanazishambulia sio mchezo, mtu anafunga duka lake kapata safari ya kwenda dar kufanya interview,

Kuna vijana wadogo wengi tu wameajiriwa, wanakunja mshahara zaidi ya milioni 2 kila mwezi na wamepiga hatua ya ziada kufungua biashara zao za kuajiri wenzao (kuwa business owners), kujenga wakiwa bado vijana wadogo, n.k Niambie vijana wangapi wa kundi la kwanza wanakuwa wamefika hizo level?

Jiulize kwanini hata wazazi wengi ambao wapo kundi la kwanza wanapigana kufa kupoma kuwapeleka watoto kusoma na kuwaambia wasome ili wapate ajira? Kwanini wasiwaambie wasome ili wawe kama wao?
 
Huo ni mtazamo wako wewe. Kwangu mie ni tofauti kabisa mkuu.

Kwanza hakuna mjasiriamali ambaye anaingia kwenye biashara bila;
Kujipanga.
Kuwa na malengo ya kukuza biashara.
Ku-take risk.
N.k
Hata hao wakinga unaowatolea mfano, wapo walioanzisha biashara na zika fail pia.
 
Kazni ni kuzea kazi tu, kazi nyingi hazina ugumu, ndio maana hata waliofoji vyeti wanapiga kazi fresh tu, Njoo kwene biashara sasa uone kam unaweza kufoji
Hapa umenikumbusha Kuna kazi nilikuwa naifanya napokea around 1200$ monthly Ila hii kazi mtu mwenye akili timamu namuelekeza anaifanya.sema ndo ivyo kigezo ni Bsc.in
 
Daah wabarbaig bwana... Yani tangu kuzaliwa kwako Hadi miaka 60..unategemea kupata million 90 au 100 Kama kiinua mgongo...Yani inakua ndoto za maisha yako Ni kuwa na millioni 90 au 100 kutoka kuzaliwa Hadi kuzeeka🤣🤣🤣...biashara ngumu lakini utatoka damu miaka 5-10..lakini growth yake iko sexy
Biashara mwanzoni unaumia Sana ,mfano ulikuwa unaendesha hiace unakomaa mpaka unanunua yako,ukiendesha miaka so chini utakuwa umenunua si chini ya hiace 4 hapo utaanza kula tu na kuweka watu walufanyie kazi.
Huyu sijui ni mwoga Sana afu anajionea kwa wafanyabiashara wa mtaani kwake.
Vidole havilingani
 
Mawazo yako yanaweza kuonekana finyu kwa mtu ambaye ameshaingia kwenye biashara na kufanikiwa pakubwa.

Ni ngumu sana kumshawishi mtoto wa Bhakressa ambaye amekulia kwenye mazingira ya biashara na kuona hizi 500M-1B figures kama mauzo ya kila siku kwamba ajira ya kumlipa million 25 kwa mwezi ni bora kuliko biashara!

Ila ukija kwa mtu ambaye baba yake anaendesha duka ambalo faida zake ni kati ya 9000-12,000 kwa siku ni ngumu sana kumshawishi kuwa biashara ni bora kuliko kulipwa 2.5 millions per each month!

Ajira inategemea unaingalia in which dimensions! Kwa maisha ya sasa na uchumi wetu ulivyodorora mtu anayepata ajira ya kumlipa 3.5-5m ana unafuu mkubwa kuliko wafanyabiashara wengi wadogo wadogo wenye mitaji chini ya million 3!
 
Ni mtizamo binafsi, ndiyo maana pamoja na bikira wa kisukuma kutoa inspirational quotes kipindi cha uhai wake lakini sikusikia wala kuona group kubwa la waajiriwa wakihamia kwenye kujiajiri au vinginevyo
 
Tatizo la kujiajiri ukiangukia pua aisee asikwambie mtu Kama huna mtu wa kukushika mkono utajua hujui!

Lakin pia biashara kuna mda inakuendea vizuri kabisa mpka unashangaa!

Mimi naona ukiwa na ajira + biashara apa ukiwa Makin kutoboa Ni rahsi

Biashara nyingi zinahitaji zwe na backup either ya biashara nyingine au ajira.
 
Daah wabarbaig bwana... Yani tangu kuzaliwa kwako Hadi miaka 60..unategemea kupata million 90 au 100 Kama kiinua mgongo...Yani inakua ndoto za maisha yako Ni kuwa na millioni 90 au 100 kutoka kuzaliwa Hadi kuzeeka🤣🤣🤣...biashara ngumu lakini utatoka damu miaka 5-10..lakini growth yake iko sexy
Bora nusu Shari kuliko Shari kamili🏃‍♂️🏃‍♂️
 
Huyu kaamua ajifariji

Mtoa uzi hebu tafta sehem tulivu, yenye upepo mwanana af upate kinyaji saaafi kabisa. Then chukua sim yako, washa data, ingia JF upitie huu uzi wako kwa umakini. Natumaini utaona aina na upuuzi ulokuwa kichwan mwako wakat unapost hii thread
 
Biashara ni nzuri ikiwa na mikakati ya kuipanua, Mfano kwa watu kama wakinga tunajionea kwa macho yetu ni next level, , pale mtu unaona live bila chenga jinsi biashara ilivyo tamu kuzidi ajira , Lakini kama huna mikakati ya kupanua biashara yako, hapo ni sawa na kukamua chungwa kavu yani unalikamua sana lakini juisi ni ndogo sana (the squeeze aint worth the juice)
Acha mawazo mgando,nchi hii kila mwaka wanahitimu wasomi zaidi ya laki wa kada mbalimbali wataajiriwa wapi?
 
46 Reactions
Reply
Back
Top Bottom