Drone Camera
JF-Expert Member
- Jul 25, 2017
- 14,121
- 14,032
Mtoto ni zawadi.Ndiyo alama yako utakayoacha hapa duniani. Hizo mali utakazoacha zitagombaniwa zitaisha.Ila jina lako atabaki nalo wewe na atalitumia kwa mjukuu wako kama jina lake la tatu. Tusitelekeze wala kuwapiga piga watoto.
Huwa najisikia vibaya pale mzazi au yoyote yule anamposhushia kipigo mtoto tena kilichozidi umri wake.Huku kitaa kuna mama huwa anampiga sana mwanae.Mwanae yupo la pili ni wa kike.Yule mtoto anafanya kazi nyingi jamani.Siku dogo alichelewa kurudi akarudi saa 9 badala ya saa 7 basi kaingia ndani tu hivi ndani kamsalimia mama kakutana na kipigo.Hapo hata hajauliza shida nn ya kuchelewa.
Kumbe dogo alikutana na wahuni wa shule huko yale madarasa ya juu wakampora baadhi ya vitu basi dogo akaenda kushitaki kwa ticha sasa hiyo process hadi ya kupata vitu vyake ndo muda ukapotea hapo.Sisi tumetulia hatuna habari tukashtushwa na kelele hiyo nyumba.Kelele yenyewe si ya kawaida! Ikabidi twende yawezekana shida ni kubwa.
Kumbe bhana sijui alikosa cha kumpigia humo ndani basi akatumia mwamvuli ile ncha iliyochongoka! Kampiga usoni! Mungu mkubwa alimiss jicho! La sivyo alikuwa analiondoa! Ilo usoni alimpompiga palianza kubreed! Sasa mtu wa hivi usipomuita mzazi ukamuita shetani utakuwa na kosa?
Jioni mzee wa nyumba aliporudi ikabidi amuulize kulikoni mwanae! Mtoto akajieleza vizuri huku baba anasikiliza kwa makini! Kilichofuata yule mama alitwangwa,alipigwa,alinyooshwa sana.Mimi huwa sipendi kuona au kusikia mwanamke anapigwa na mwanaume ila hiyo siku nilifurahi sana! Alipata dawa yake.Mtoto kama vile sio wake wa kuzaa.
Wengine hadi vitoto vidogo wakiwa wanaviogesha basi wanavichapa humo humo kwenye beseni.Vinalia hadi vinahuzunisha.Sio vizuri hivyo.
Wakati wa kutaka mwanao akuelewe kwa vipigo ushaisha huko! Mengine tuwaachie mababu zetu waliopenda waogopeke ili wakiingia nyumbani kutoka shamba basi watoto wajifiche.Huu muda ni wa kutengeneza urafiki na watoto wetu ili wawe huru kueleza changamoto zao kisha tuzitatue.
Watoto wa zamani waliwapenda bibi na babu zao sababu waliwasikiliza tofauti na wazazi waliopenda kutumia silaha ya mkono.
Mimi sitapiga mwanangu yoyote kabisakabisa.
Huwa najisikia vibaya pale mzazi au yoyote yule anamposhushia kipigo mtoto tena kilichozidi umri wake.Huku kitaa kuna mama huwa anampiga sana mwanae.Mwanae yupo la pili ni wa kike.Yule mtoto anafanya kazi nyingi jamani.Siku dogo alichelewa kurudi akarudi saa 9 badala ya saa 7 basi kaingia ndani tu hivi ndani kamsalimia mama kakutana na kipigo.Hapo hata hajauliza shida nn ya kuchelewa.
Kumbe dogo alikutana na wahuni wa shule huko yale madarasa ya juu wakampora baadhi ya vitu basi dogo akaenda kushitaki kwa ticha sasa hiyo process hadi ya kupata vitu vyake ndo muda ukapotea hapo.Sisi tumetulia hatuna habari tukashtushwa na kelele hiyo nyumba.Kelele yenyewe si ya kawaida! Ikabidi twende yawezekana shida ni kubwa.
Kumbe bhana sijui alikosa cha kumpigia humo ndani basi akatumia mwamvuli ile ncha iliyochongoka! Kampiga usoni! Mungu mkubwa alimiss jicho! La sivyo alikuwa analiondoa! Ilo usoni alimpompiga palianza kubreed! Sasa mtu wa hivi usipomuita mzazi ukamuita shetani utakuwa na kosa?
Jioni mzee wa nyumba aliporudi ikabidi amuulize kulikoni mwanae! Mtoto akajieleza vizuri huku baba anasikiliza kwa makini! Kilichofuata yule mama alitwangwa,alipigwa,alinyooshwa sana.Mimi huwa sipendi kuona au kusikia mwanamke anapigwa na mwanaume ila hiyo siku nilifurahi sana! Alipata dawa yake.Mtoto kama vile sio wake wa kuzaa.
Wengine hadi vitoto vidogo wakiwa wanaviogesha basi wanavichapa humo humo kwenye beseni.Vinalia hadi vinahuzunisha.Sio vizuri hivyo.
Wakati wa kutaka mwanao akuelewe kwa vipigo ushaisha huko! Mengine tuwaachie mababu zetu waliopenda waogopeke ili wakiingia nyumbani kutoka shamba basi watoto wajifiche.Huu muda ni wa kutengeneza urafiki na watoto wetu ili wawe huru kueleza changamoto zao kisha tuzitatue.
Watoto wa zamani waliwapenda bibi na babu zao sababu waliwasikiliza tofauti na wazazi waliopenda kutumia silaha ya mkono.
Mimi sitapiga mwanangu yoyote kabisakabisa.