Tupike Pilau Nazi

Tupike Pilau Nazi

Hi guys,. Habari za siku nyingi
Bila kupoteza mda tupike pamoja pilau nazi

Kwenye sufuria yako ya kupikia utaweka mafuta, yakipata moto utaweka vitunguu na ( hoho ni optional)View attachment 3583627
Utakaanga kwa muda utaweka kitunguu saumu na tangawizi utaendelea kukaanga kwa mda kidogoView attachment 3583628
Utakaanga kwa mda tena kidogo utaweka pilau masala kijiko kimoja na garam masala nusu kijikoView attachment 3583629

Utakaanga tena kidogo utaweka nyama yako ambayo imeshachemshwaView attachment 3583631

Utakaanga kidogo then utaweka viazi na nyanya kidogo,. (Hadi hapa harufu iliwafanya waliochelewa kunywa chai waache watunze njaa kwajili ya pilau😹 )View attachment 3583632

Utakaanga tena hadi nyanya zilainike kidogo,. Utaweka chumvi halafu utaweka mchele ( mie nimetumia basmati) ila wakawaida ingekua poa sana😍View attachment 3583639

Utakaanga kwa mda kidogo ili viungo vishikane vizuri,. Then utaweka supu ya nyama utaweka na tui la nazi vikombe viwili au vitatu,. View attachment 3583640

Utakoroga taratibu taratibu then Utafunika utapunguza moto uache upikike kwa moto mdogo mdogo kwa dakika 25 au hadi nusu saa.
Then utafunua ugeuze na pilau yetu itakua tayari kama hiviView attachment 3583642

Utatengeneza na kachumbari kidogo,. ( mie niliweka carrot 🥕 hoho kitunguu nyanya na ndimu ) View attachment 3583643

Tukala tukashushia na mirinda nyeusi ya baridi ( pepsi ziliisha )View attachment 3583644

Hope you enjoyed 😋😍😘
Maaamaaee
 
Kwa sisi wa vijijini, pilau ni mpaka viazi na nyama? Je kuna pilau aina gani? Kuhusu wali na penda wali mweupe wenye ladha na harufu ya kutoa nyoka pangoni, upikaji sasa ni aibu! Kwako Leejay49
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom