Tupike ndizi

Tupike ndizi

Leejay49

JF-Expert Member
Joined
Feb 10, 2023
Posts
19,430
Reaction score
61,341
Hi guys, habari za siku nyingi??
Bila kupoteza mda tupike ndizi nyama pamoja…

Kwenye sufuria yako ya kupikia utaweka mafuta kidogo sana, yakipata moto utaweka kitunguu hoho na karoti
IMG_3380.jpeg


Utakaanga vikilainika utaweka ndizi zako ambazo ulishamenya na kuzikwangua vizuri
IMG_3383.jpeg


Utazikaanga kwa dakika mbili au tatu halafu utaweka nyama yako ambayo ulishaichemsha na kitunguu saumu tangawizi na chumvi,. Then utaongea chumvi kidogo
IMG_3385.jpeg


Utakaanga tena kidogo then utaweka supu ya nyama pamoja na tui la nazi vikombe viwili,. Then utafunika uache zipikike kwa dakika tano hadi kumi
IMG_3398.jpeg


Then utafunua utageuza kwa kuzungusha sufuria ili ndizi zisijikate kate,. Then utaziacha zipikike zikiwa wazi kwa dakika 1 au mbili ,. Na ndizi zako zitakua tayari zimeiva
IMG_3401.jpeg


Utaserve and ready to chop
IMG_3402.jpeg
IMG_3405.jpeg


Hope you enjoyed 😍😋😘 min -me
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom