Tuonjeshane kidogo machungu ya ndoa kwa waliofunga pingu

Tuonjeshane kidogo machungu ya ndoa kwa waliofunga pingu

Nlimwambia jamaa kama anamhitaji wife aende kwao akajieleze mi ntamkabidhi kiroho safi kabisa maana sina muda wa kugombea mwanamke ila nnachotaka ni kumkabidhi kwa kufuata utaratibu.

Wife nae nikamchana kwamba asijione kama yeye ni keki, kama anamhitaji jamaa aseme nikamkabidhi na mimi nitang'oa chombo kikali kuliko hata yeye. Akaniuliza kwani yeye mbaya, nikamuuliza anadhani ana uzuri gani...
Hivi wewe ni mtunzi wa filamu? Mbona unakatiza stori?
 
Na ulivyo mtata....maneno silaha yako
[emoji3] [emoji3] [emoji3] ulijuaje?yaani nikiskia unàchepuka nampigia simu namuambia kabisa Huyo mume wangu,na hapa asubuhi katoka amevaa hivi na hivi...!
nampenda simuachii[emoji8] [emoji8]
bidada we kua tu kiraka!hapa huingii ng'oo!
 
Anhaaa, inaonekana na wewe ndo zako hizi.

Maana mtu unakuta kila baada ya lisaa limoja kapiga simu. Upo wapi, upo na nani, unafanya nini. Anavyokomalia basi, ukimwambia nipo kwenye usafiri anakwambia mwambje dereva apige honi nisikie kama kweli upo kwenye usafiri.

Arrrhgghh.
Huyo wa kutaka honi sasa nae kazidi lols
 
Mtihani uliopo hapo ni je:
Usamehe?
Ulipize?
Umuache?

Ukiwaza hayo akili inazidi kupata moto.
Mm binafsi nafikiri swala lilipo ni kusameheana,kuliongea,kua wawazi wote wawili pasipo kua na kinyongo,chuki au hasira baina yenu!mapenzi hayakosi dosari na baada ya hapo penzi huwa tamu san maana mnakua mmefungua ukurasa mpyaa
Hasira hazijengi,kulipiza hakufai maana wote mtaambulia magonjwa na mengine meng
 
Ha,haaaaa.....
Maisha ya ndoa yanachangamoto nyingi,,na ni matamu ikiwa kila mmoja anasimama kwenye mstari wake(hasa yule anayependa kuitwa kichwa cha nyumba)
Nimeipenda hii
Halafu kitu kingine ambacho m huwa napenda kuwaambia watu kua katika ndoa/mahusiano yoyote kila mtu huwa ana nafasi yake ,kwa maana ya kwamba kuna changu(mme),chako(mke) na chetu(wote wa wili) yaani watu wakishayajua haya mambo matatu mtaishi kwa amani na raha tele kwwnye famili,sio kila kitu utake kujua kwa mkeo/mmeo mpe nafasi yake na yeye aweze kua happy aenjoy maisha!akitaka ku have fun na friends let her/him go !kikubwa zaid n heshima,upendo,uwazi,uaminifu(ingawa sikuhizi mmhh) na mambo mengine mengi.na muda mwingine mkigomba mezea tu sio kila kiti cha kukununisha ew mwanaume/ke
 
Hivi wewe ni mtunzi wa filamu? Mbona unakatiza stori?
Sio story mkuu.
Nlimpa fact tu kama wapo wazuri kuliko yeye, nikaanza kumchambua na nkamwambia akirudia namwacha, navuta chombo cha maana kuliko yeye.

Nadhani mpaka sasa kajidharau mwenyewe.
 
Mm binafsi nafikiri swala lilipo ni kusameheana,kuliongea,kua wawazi wote wawili pasipo kua na kinyongo,chuki au hasira baina yenu!mapenzi hayakosi dosari na baada ya hapo penzi huwa tamu san maana mnakua mmefungua ukurasa mpyaa
Hasira hazijengi,kulipiza hakufai maana wote mtaambulia magonjwa na mengine meng
Ndg yangu unapogundua mwenzako anakusaliti hata hisia za kulala nae zinaondoka kabisa maana anakua kama vile anawashindanisha kitandani na likitu linalovuliwa chupi na mtu mwingine unakuaje na hisia nalo?
 
Nlimwambia jamaa kama anamhitaji wife aende kwao akajieleze mi ntamkabidhi kiroho safi kabisa maana sina muda wa kugombea mwanamke ila nnachotaka ni kumkabidhi kwa kufuata utaratibu.

Wife nae nikamchana kwamba asijione kama yeye ni keki, kama anamhitaji jamaa aseme nikamkabidhi na mimi nitang'oa chombo kikali kuliko hata yeye. Akaniuliza kwani yeye mbaya, nikamuuliza anadhani ana uzuri gani...
Hahaha umeua...

Nahisi alikitafuta kioo kilipo akajihakiki...
 
ujue wengi hawajaoa bikra mkuu vilio vingi sana kwao ndoa chunguuuu
Kuna jirani yangu alioa bikira mwaka 1998 lakini kaja kusalitiwa mwaka 2013 alipoenda mkoani kufanya kazi kama ya mwezi mmoja.

Mkewe akaanza kuliwa na mtoto wa mchungaji wake ambaye alkua anamiliki kahoteli flani ambako huyo mwanamke alienda kuomba kazi.

Mbaya zaidi huyo jamaa alikua anaenda kumgegeda huyo mke wa mtu nyumbani kwake (anaplishi na watoto na mmewe).

Kinachouma zaidi ni watoto ndio walimwambia baba yao ukweli kwamba aliposafiri kuna baba mwingine alikuwa anakuja na wanaingia na mama chumbani huku wakiwalazimisha watoto kwenda kulala.

Jamaa alianguka chini akapoteza fahamu papohapo.

Ila Mungu ni mwema waliyaongea yakaisha na wanaishi pamoja ila jamaa ananiambia hamwamini mkewe na kidonda chake kitapona siku atakayovuta punzi ya mwisho na kuiachia.
 
Ndoa ni tamu kama utachagua mwenza sahihi, pili ukumbuke hamkuzaliwa na kulelewa nyumba moja kwahiyo kila mmoja ana tabia zake, ni vyema kusomana tabia ili kuepuka mikwaruzano, KIKUBWA UPENDO, Ukiwa na upendo wa kweli kwa nyote wawili basi ni rahisi kuvumiliana, na kingine ni USIKIVU ukikosea uwe tayari kuambiwa na kusikiza na kuomba msamaha na wewe unapokosewa sema na hata kama unataka kuombwa msamaha na mume hana tabia ya kuomba msamaha mwambie mie napenda ukinikosea uniombe msamaha, kuna vitabia vidogo dogo vinakera ila ni vyema ukawa unasema kuliko kulimbikiza moyoni kwahiyo KUAMBIANA NA KUSIKIZANA NI VYEMA,

Kila mtu kujua nafasi yake na wajibu wake, yani uvumilivu uwe kwenye mambo madogo madogo na sio unamletea mwenzako mwanamke ndani halafu unasema ndoa UVUMILIVU nope. kwa uchache HII LABDA ITASAIDIA KWA WALE AMBAO HAWAJAINGIA KWENYE NDOA,
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom