Tuonjeshane kidogo machungu ya ndoa kwa waliofunga pingu

Tuonjeshane kidogo machungu ya ndoa kwa waliofunga pingu

Amoxlin

JF-Expert Member
Joined
May 30, 2016
Posts
3,782
Reaction score
4,118
Salaam ndugu zangu,

Wahenga walisema "Ndoa ndoano" na wengine wakasema "Ndoa ni fumbo".

Yote hii inaashiria kuna jambo na vijambo ndani yake. Japo yapo mazuri mengi ila napenda hapa tuyamuulike yale machungu yanayopelekea wengine kuwa vichaa, kuikimbia ndoa au hata kutoa uhai wao.

Binafsi nilighafirika nilipogundua shemeji/wifi yenu ana hawara na kila akipost picha facebook anatu-tag wote na jamaa anaelewa kila kitu japo mi sielewi. Mpaka sasa simwamini tena.
 
1473152792015.jpg
 
Salaam ndugu zangu.

Wahenga walisema "Ndoa ndoano" na wengine wakasema "Ndoa ni fumbo".

Yote hii inaashiria kuna jambo na vijambo ndani yake. Japo yapo mazuri mengi ila napenda hapa tuyamuulike yale machungu yanayopelekea wengine kuwa vichaa, kuikimbia ndoa au hata kutoa uhai wao.

Binafsi nilighafirika nilipogundua shemeji/wifi yenu ana hawara na kila akipost picha facebook anatu-tag wote na jamaa anaelewa kila kitu japo mi sielewi. Mpaka sasa simwamini tena.
ndoa zina mitihani mingi Sana na imetofautiana..kikubwa kinacho takiwa Ni uvumilivu
 
Kila mtu ana mitihani yake anayopitia kwenye ndoa ni uvumilivu tu ndo kikubwa bola ya waislamu kuna talaka tofaut na wakristo kidogo kukaa vikao na kupatanishwa vumilianeni ndoa ni uvumilivu sisi wazazi wenu tumefikia umri huu tumepitia yote kinachotakiwa mvumiliane unaetaka kuingia kwenye ndoa ingia tu wala usiogope
 
Watu wanadumu kwenye ndoa si kwa kuwa ndoa hazina changamoto bali ni kutokana na umahiri wao na uwezo wa wanandoa kupambana na changamoto hizo........

Ingia katika ndoa ukiwa na hisia chanya juu ya ndoa...hii itakupa mbinu na uwezo wa kupambana na changamoto zilizomo kwenye ndoa.....ukiingia kwenye ndoa huku ukiwa na maoni hasi na hisia hasi.....itakupunguzia uwezo wa kupambana na hizo changamoto na kujiona kama vile upo kwenye gereza la mateso makali huku wenzio upande wa pili wakifurahia maisha ya ndoa.....kama wapo paradiso.....
 
Watu wanadumu kwenye ndoa si kwa kuwa ndoa hazina changamoto bali ni kutokana na umahiri wao na uwezo wa wanandoa kupambana na changamoto hizo........

Ingia katika ndoa ukiwa na hisia chanya juu ya ndoa...hii itakupa mbinu na uwezo wa kupambana na changamoto zilizomo kwenye ndoa.....ukiingia kwenye ndoa huku ukiwa na maoni hasi na hisia hasi.....itakupunguzia uwezo wa kupambana na hizo changamoto na kujiona kama vile upo kwenye gereza la mateso makali huku wenzio upande wa pili wakifurahia maisha ya ndoa.....kama wapo paradiso.....
Kwa msimamo wako juu ya ndoa,sikutegemea kama ungeandika haya.........Vipi ushaanza kulegeza kamba?....
 
Ndoa inakuwa tamu...kama nyote mmeingia kwaajili ya kujenga na kuendeleza ambacho tayar mmeanzisha. Kugombana kupo...lakini mwisho wa siku mnapatana in a good way. Sio vitu vidogo ushapiga nyumbani...Hamtadumu wala.
Wanandoa pia tunashauriwa kuwa wabunifu ili tusichokane...maana kama wanaume ni wepesi sana wa kukinai.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom