Tuondoe utata hapa: Ni wapi haswa chanzo cha Mto Nile?

Tuondoe utata hapa: Ni wapi haswa chanzo cha Mto Nile?

Chanz

Basically mto Nile una vyanzo viwili cha kwanza ni Rwanda au Burundi chanzo cha pili ni Ethiopia, sio kweli kwamba Nile chanzo chake in Jinja - na ukiangalia jwa umakini maji ya MTO Kagera yakiingia Ziwa Victoria yana rangi tofauti kabisa na unaona mkondo wake unavyo katiza ndani ya Ziwa.
Kuna ukweli mdogo hapa. Ili maji ya mto kagera yakatize ziwa vic bila kuchangamana. Itabidi mto ulikate vipande viwili. Inamaana upande wa ziwa la uganda magharibi maji yake yasichangamane na pande zingine. Mto wenyewe kwanza unahama njia kufuata mkondo wa ziwa unavyoenda.
 
Kuna ukweli mdogo hapa. Ili maji ya mto kagera yakatize ziwa vic bila kuchangamana. Itabidi mto ulikate vipande viwili. Inamaana upande wa ziwa la uganda magharibi maji yake yasichangamane na pande zingine. Mto wenyewe kwanza unahama njia kufuata mkondo wa ziwa unavyoenda.

Mimi ni mzaliwa wa huko, ninayo yasema nimeyaona kwa macho yangu, sasa sijui unabishi nini?
 
Inawezekana kweli ila mimi huwa narusha nyavu ndani ya mto kagera ukiwa ndani ya ziwa. Ni mda kidogo tu toka nitoke male beach. Huwa nauona mto unavyohamishwa na mkondo wa maji wa ziwa na namna mawimbi ya ziwa yanavyouchakaza mto. Mfano: kipindi cha kiangazi mto hupita upande wa kaskazini ikilinganishwa na kipindi cha masika. Hivyo kama mkondo wa maji ya ziwa unahamisha njia maji ya mto siwezi amin kuwa hayo maji hayachangamani. Kama wimbi linatoka kulia mwa mto na kukatiza mbaka kushoto mwa mto kisha linaendelea. Sitoweza kuamini kama haya maji hayachangamani
 
Maji ya MTO Nile yanaanzia milima ya Burundi Na Kongo, yanatengeneza MTO unaojulikana kama MTO Ruvubu. Baadae MTO huo unaungana Na MTO kutoka Rwanda ujulikanoa kama Ahakagera pale Rusumo. Kwa pamoja mito hiyo ikiungana inatengeneza MTO Kagera, ambao unamwaga Maji yake ziwa Victoria. Inasemekana kuwa ile kasi ya MTO Kagera inafanya Maji yake yasiweze kuchanganyika Na Maji ya ziwani, hivyo hupitiliza Na kutengeneza MTO Nile. Lakini pia bado kuna mito midogo kutoka mchi za Uganda , Sudani Na Ethiopia uongezeaka kwenye MTO Nile
Umenena vyema mkuu,nilikutana hili swali pahali ila kuna mtu alieleza sawa kabisa nawewe,,,,,, au niwewe mkuu?
 
sasa wewe ukitaka kuleta hizo technicalities ambazo hazipo basi chanzo ni mvua..., au twende mbali chanzo ni yale maji kabla hayajawa mvua na kubadilika kuwa mawingu ili mvua inyeshe...
 
Chanzo chake ni unapoanzia mto Kagera. ziwa victoria unapita tu kama unavyopita ziwa Kyoga. Kwanini siyo mto Mara? wanapotafuta chanzo cha mto wanaangalia tawi refu zaidi, mto kagera ni mrefu kuliko mara. Hii ndiyo sababu blue nile inayotoka ethiopia siyo chanzo rasmi, licha ya kuwa na maji mengi kuliko white nile ni mfupi. Ishu ya maji kutochangamana ziwani ni hekaya tu.
 
Kuna vyanzo mbalimbali vikielezea wapi chanzo kikuu cha Mto Nile. Lakini vyanzo hivyo vinakuwa vikipingana mara kwa mara juu ya utata huu.

Kwa chanzo chetu watanzania tulichoaminishwa kutokana na elimu yetu ni kwamba chanzo ni Ziwa Victoria.

Vyanzo vya Nile ni mito yote inayopeleka maji kwenda Ziwa Victoria Nyanza katika nchi za Tanzania, Burundi, Rwanda, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Uganda na Kenya.

Lakini watafiti wengine wanaeleza kuwa chanzo cha mbali kabisa ni Mto wa Luvironza huko Burundi unaoingia katika Mto Kagera na kufika Ziwa Victoria Nyanza.

Kwa upande mwingine wa Nile unaanza Ethiopia ukiitwa Abbai au Nile ya Buluu unatoka katika Ziwa Tana.

Hakuna mapatano kabisa Nile inaanzia wapi. Kawaida ya waandishi Waingerezani kuhesabu kuanzia Ziwa Victoria, waandishi wa mataifa mengine huwa wanaweza wakaita tayari Mto Kagera kwa jina "Nile ya Kagera".
Najua chanzo chake ni katika bonde la Luzizi nchini Rwanda / Burundi
 
Kwa nini chanzo kisiwe chattle?
Tumshukuru Rais wa awamu ya Tano mheshimiwa John Pombe Magufuli kwa kuwezesha MTO Nile kuanzia MTO Kagera ambao upo Tanzania na unapita Chattle!!
 
Kuna misitu inaitwa Tropical rainforest hii imeambaa ukanda wa equator huko mvua zinapiga mwaka mzima hakuna masika wala vuli,kuna Amazon rainforest south america na kwa africa hilo limsitu liko d.r.congo uko ndo pamekua vyanzo vya mito mingi inayomwaga maji ziwa victoria ikipitia rwanda na burundi
 
Back
Top Bottom