The Dictator
JF-Expert Member
- Jul 20, 2018
- 4,426
- 12,161
Kuna vyanzo mbalimbali vikielezea wapi chanzo kikuu cha Mto Nile. Lakini vyanzo hivyo vinakuwa vikipingana mara kwa mara juu ya utata huu.
Kwa chanzo chetu watanzania tulichoaminishwa kutokana na elimu yetu ni kwamba chanzo ni Ziwa Victoria.
Vyanzo vya Nile ni mito yote inayopeleka maji kwenda Ziwa Victoria Nyanza katika nchi za Tanzania, Burundi, Rwanda, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Uganda na Kenya.
Lakini watafiti wengine wanaeleza kuwa chanzo cha mbali kabisa ni Mto wa Luvironza huko Burundi unaoingia katika Mto Kagera na kufika Ziwa Victoria Nyanza.
Kwa upande mwingine wa Nile unaanza Ethiopia ukiitwa Abbai au Nile ya Buluu unatoka katika Ziwa Tana.
Hakuna mapatano kabisa Nile inaanzia wapi. Kawaida ya waandishi Waingerezani kuhesabu kuanzia Ziwa Victoria, waandishi wa mataifa mengine huwa wanaweza wakaita tayari Mto Kagera kwa jina "Nile ya Kagera".
Kwa chanzo chetu watanzania tulichoaminishwa kutokana na elimu yetu ni kwamba chanzo ni Ziwa Victoria.
Vyanzo vya Nile ni mito yote inayopeleka maji kwenda Ziwa Victoria Nyanza katika nchi za Tanzania, Burundi, Rwanda, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Uganda na Kenya.
Lakini watafiti wengine wanaeleza kuwa chanzo cha mbali kabisa ni Mto wa Luvironza huko Burundi unaoingia katika Mto Kagera na kufika Ziwa Victoria Nyanza.
Kwa upande mwingine wa Nile unaanza Ethiopia ukiitwa Abbai au Nile ya Buluu unatoka katika Ziwa Tana.
Hakuna mapatano kabisa Nile inaanzia wapi. Kawaida ya waandishi Waingerezani kuhesabu kuanzia Ziwa Victoria, waandishi wa mataifa mengine huwa wanaweza wakaita tayari Mto Kagera kwa jina "Nile ya Kagera".