Tundu Lissu unakumbuka kitu?

Tundu Lissu unakumbuka kitu?

Umeongea kitu cha maana sana The Boss.
Kosa la ukawa ndilo hilo,ccm wanaweza kukubali tume huru na vitu vingine lakini siyo kukubali serikali tatu,ukawa walikuwa na nafasi kubwa kutengeneza mazingira mazuri ya wao kufanya kazi kupitia bunge la katiba.

Mkuu kama ni kweli hicho unachosema ni kipi kilisababisha kila siku kanuni zikawa zinabadilishwa wakati wa bunge lile? Mbona kuna wajumbe walionyesha kupinga mambo mbali mbali na wakaishiwa kutishiwa maisha? Mkuu kwa ujumla bunge lile halikuwa linataka kuleta katiba ya wananchi bali bunge lile lilitawaliwa na itikadi za kisiasa. Wazo lilikuwa linapita kwa kuangalia ni chama kipi kimesimamia hoja fulani.

Kwa mtazamo wangu kama tulitaka bunge la katiba liweze kufanya kazi kwa maslahi ya taifa, idadi ya wanasiasa haikutakiwa kuzidi makundi mengine. Kwa kitendo kile cha kujaza wanasiasa ndio kulikopelekea bunge lile kuendeshwa kwa hila, fitina na hisia za kiitikadi. Kwa ujumla wajumbe wa bunge lile zaidi ya asilimia 80 walikuwa hawajui wajibu wao ni kama walibebesha mzigo mzito kuliko uwezo wao wa kupambanua.
 
Usipotumia akili na kuendesha siasa kwa mikakati endelevu, ndugu yangu utaandamana mpaka wamarekani wawahurumie kwa kuishiwa soli za viatu.
Kwani wewe unadhani hawana mikakati? Mwaka una siku 365, unataka kusema kwa siku zote hizo wapinzani huwa wanaandamana?
 
Hoja za tume huru ya uchaguzi haikufika
walitoka kabla....
Mkuu The Boss,kweli kabisa kutoka ndani ya mtima wako unaamini kabisa kama UKAWA wangebaki kwenye Bunge la Katiba hili la Tume huru ya uchaguzi lingeshughulikiwa ipasavyo?
 
The Boss kwanza inabidi kufahamu nia ya JK ilikuwa ni nini mpaka akaamua kukubali kuanzisha mchakato wa katiba mpya.
Tume ya Warioba ilikuwa fair na ikatoa rasimu nzuri kwa maslahi ya wananchi

1.Je JK binafsi alikubaliana na yale yaliyopendekezwa na tume ya Warioba ?

.Msimamo wa wapinzani ulikuwa unajulikana dhahiri wao walikubali

2.Je msimamo wa majority ya wawakilishi wa CCM kwenye bunge la katiba ulikuwa upi ?
 
Mkuu The Boss,kweli kabisa kutoka ndani ya mtima wako unaamini kabisa kama UKAWA wangebaki kwenye Bunge la Katiba hili la Tume huru ya uchaguzi lingeshughulikiwa ipasavyo?

swala si kuamini
swaa hapa ni 'hatujui ingekuwaje'
wangebaki ndo tungejua

usiseme walikuwa wachache wapinzani
walikuwa wachache wakati wa Escrow....lakini results tuliziona
wachache wakati wa Buzwagi lakini impact tuliiona....

hatujui nini kingetokea.....walitoka mapema sana
 
Kwani wewe unadhani hawana mikakati? Mwaka una siku 365, unataka kusema kwa siku zote hizo wapinzani huwa wanaandamana?
Mahali ambapo akili za hali ya juu ingetumika UKAWA wafanya mambo ya kijinga kuandamana na kususia vikao halali na vilivyo kaa kisheria.
Wamesusia bunge la katiba, wamesusia bunga, total work done ni zero.
 
Kwani katiba ya sasa na sheria zetu si zinatambua demokrasia na haki ya vyama kufanya siasa?, lakini mbona hawaiheshimu? Nakuhakikishia hata kama ingekuwa katiba ya Warioba, wangeamua kutoiheshimu wasingeiheshimu tu.
Swadakta!Huo ndio ukweli,ila tujiulize,ni kwanini wanafanya hivyo?ni kwa sababu hakuna wananchi wa kuogopwa.Nchi hii ukitaka kufanya ujinga ni utafikiria kuwadhibiti UKAWA tu,the rest ambao ni mamilioni ya watu they are just watching Tundu Lissu on ITV!Utawasaidia vipi watu hao?!Kiburi cha viongozi wa nchi hii kinatoka kwa wananchi wenyewe,wameiacha nchi ivurugwe,hadi leo wanafikiri viongozi ni malaika,wengine bado ni selfish,katika uselfish wao wanawaza one day na wao watapata nafasi ya "kupiga hela" serikalini,so wanaona hawa walioko ni fursa yao kutafuna na kuongoza nchi watakavyo!Tatizo la Tanzania si watanzania wachache(viongozi)bali watanzania wengi(wanaoongozwa).
Hivyo hata uandike katiba safi,bado viongozi wataivunja na hakuna wa kuwawajibisha.
 
Katiba ya sasa Rais anamteua mkuu wa polisi
ni rahisi kwake kumpa amri

ingekuwa katiba hana mamlaka ya kumteua mkuu wa polisi ingekuwa rahisi kuliko sasa
Uwezekano wa kubadilisha chochote ambacho si kwa maslahi ya wananchi na ukuaji wa demokrasia likiwemo hili,ungefanikiwa kwa kushiriki kwao UKAWA?
Mkuu wewe ni mgeni na amri kwa "kaukasi" ya CCM bungeni?
 
vita haikimbiwi ndugu bali kupigana ukawa wanakimbia badala ya kujenga hoja hilo ndo tatizo
 
boss kwanza inabidi kufahamu nia ya JK ilikuwa ni nini mpaka akaamua kukubali kuanzisha mchakato wa katiba mpya.
Tume ya Warioba ilikuwa fair na ikatoa rasimu nzuri kwa maslahi ya wananchi

1.Je JK binafsi alikubaliana na yale yaliyopendekezwa na tume ya Warioba ?

.Msimamo wa wapinzani ulikuwa unajulikana dhahiri wao walikubali

2.Je msimamo wa majority ya wawakilishi wa CCM kwenye bunge la katiba ulikuwa upi ?


Nimewajibu watu huko nyuma
hao unaowaita wawakilishi wa CCM bunge la katiba walikuwa pamoja na
Lowasa,Kingunge na wengineo ambao leo wako upinzani
hakuna anaejua kama wangejali maslahi ya chama kuliko ya Taifa...
only kama hoja ingeletwa kwanza
 
Kwani katiba ya Sitta,si ndio imebakia,sasa the Boss sioni hoja ya kumlaumu TL,kweli walitoka na katiba ikaadhimiwa. Uilaumu tume pamojan as erikali ni kwa nini hawaileti kwa wananchi tuipigie kura? kama fedha zilikuwepo hadi chenji ilirudi.
 
Uwezekano wa kubadilisha chochote ambacho si kwa maslahi ya wananchi na ukuaji wa demokrasia likiwemo hili,ungefanikiwa kwa kushiriki kwao UKAWA?
Mkuu wewe ni mgeni na amri kwa "kaukasi" ya CCM bungeni?

CCM caucus iliyokuwa na Lowassa na Kingunge?
tena wakiwa na nguvu ya Halamashauri ya Chama?
wasingeona umuhimu wa tume huru just in case wakihama CCM?
 
Nimewajibu watu huko nyuma
hao unaowaita wawakilishi wa CCM bunge la katiba walikuwa pamoja na
Lowasa,Kingunge na wengineo ambao leo wako upinzani
hakuna anaejua kama wangejali maslahi ya chama kuliko ya Taifa...
only kama hoja ingeletwa kwanza

JK mwenyewe aliyoanzisha mchakato alikuwa na msimamo gani baada ya Warioba kumkabidhi ile rasimu ?
 
Katiba iliyopo, ingawa ni mbovu, haikatazi mikutano na maandamano, wala haikatazi vyama kufanya shughuli za kisiasa.

Usichanganye hii mihemuko ya Magufuli na wateule wake na KATIBA, hii ya kwao ni "mizuka tu" , huwa hawafuati katiba!
 
Yaani polisi hawa hawa wangekataa amri toka juu kisa katiba!

Hauko makini je katiba inayotoa haki ya kukutana kufanya mikutano inaheshimiwa?
Nadhani labda ingekuwa chama kingine lakini sio kwa ccm unapoteza muda bure,
Mapambano ya kudai demokrasia yaendelee tuu #ukuta
 
Kura za kupitisha hicho kitabu cha Chenge zinajumuisha hadi kura zilizopigwa na watu walioenda Hijja, kura zilizopigwa na marehemu akiwepo marehemu mama yake Zitto , kwa makundi yote yaliyoteuliwa na jk kwa vivuli vya walemavu, waganga, wahadhiri , wachungaji, masheikh wote walikua ni makada wa ccm walikua ni geresha ambao kwa wingi wao iwe isiwe lazima matakwa ya Chenge na Sitta yalikua lazima yatimie.
Tundu Lissu hausiki na huu utomvu wa kijitabu cha Chenge.
 
Umeongea kitu cha maana sana The Boss.
Kosa la ukawa ndilo hilo,ccm wanaweza kukubali tume huru na vitu vingine lakini siyo kukubali serikali tatu,ukawa walikuwa na nafasi kubwa kutengeneza mazingira mazuri ya wao kufanya kazi kupitia bunge la katiba.
CCM walienda kwenye Bunge la Katiba wakiwa na msimamo wao,na hata wale wengine walioteuliwa kwa "maelezo maalum" ambao walikuwa ndio tegemeo la wananchi kuwa akidi yaweza kutimia kwa kuunga mkono rasimu ya Warioba,nao walikuwa na "kaukasi" yao ambayo isingewezekana kwa vyovyote vile hoja yoyote kinzani na maslahi ya CCM kupita.
Rejea upigaji wa kura.
 
JK mwenyewe aliyoanzisha mchakato alikuwa na msimamo gani baada ya Warioba kumkabidhi ile rasimu ?

JK huyu huyu ambae wenzie walimuimbia 'tuna imani na Lowaassa'?
JK sio kila kitu
hata Magufuli leo sio kila kitu ndani ya CCM
wapinzani wajifunze kutengeneza coalition za kuwezesha mambo muhimu kufikiwa...

wapo watu ndani ya CCM bado wanataka tume huru ya uchaguzi.....
 
Back
Top Bottom