Tundu Lissu unakumbuka kitu?

Tundu Lissu unakumbuka kitu?

Kwa sababu katiba iliyopo inampa Rais nguvu ya kutoa amri kwa jeshi la polisi
ingekuwa hana nguvu hiyo hata amri za kupiga marufuku asingeweza kutoa

Mkuu inakuwa kama bado hujanipata kidogo japo nakubalina na maoni yako kwa sehemu kubwa. Ngoja nikupe mfano mrahisi zaidi, leo hii polisi wamejipa mamlaka ya kutoa vibali, je sheria inasema polisi watoe vibali ili watu kukusanyika ama sheria inataka watoe ulinzi? Je hili linatekelezwa? Na kama halitekelezwi ni kipi kinachokupa imani kwenye katiba hiyo mpya wangeiheshimu? Hiyo katiba yangetekelezwa yale tu yasiyowabana watawala kwani ingechukua muda mrefu kubadili mindset za watawala.
 
Lakini katiba haisemi hivyo ila polisi wanafanya hivyo kwa amri kutoka juu kumbuka.

Ndo maana nchi zinazojali demokrasia zimepiga marufuku polisi kupokea amri kutoka juu
na sisi pia tungetaka tungeweza
Polisi inakuwa ni marufuku kupokea amri
wafanye kazi kwa sheria tu zilizopo...
 
Kuna wakati Baba wa Taifa alinukuliwa akisema "katiba hii ni nzuri sana, lakini akijitokeza kiongozi akaifuata watu watamuita dikteta "
Ndio kinachoonekana leo.
Upande wa pili wasije jisahau maana kufuata katiba ya nchi ni kiapo kinachompa mamlaka mkuu wa nchi kufanya chochote kwani ni yeye tu aliyeko juu ya sheria.
Chochote akifanyacho kijeshi ni amri.
Hili liwe funzo kwa upande wa pili kutokupuuza mambo ya muhimu kujadili kwani baadae itakuja kuwaghalimu sana .
Mkuu tusaidiane hapo, ni ibara ipi ya katiba inayosema raisi yuko juu ya sheria?
 
Mkuu inakuwa kama bado hujanipata kidogo japo nakubalina na maoni yako kwa sehemu kubwa. Ngoja nikupe mfano mrahisi zaidi, leo hii polisi wamejipa mamlaka ya kutoa vibali, je sheria inasema polisi watoe vibali ili watu kukusanyika ama sheria inataka watoe ulinzi? Je hili linatekelezwa? Na kama halitekelezwi ni kipi kinachokupa imani kwenye katiba hiyo mpya wangeiheshimu? Hiyo katiba yangetekelezwa yale tu yasiyowabana watawala kwani ingechukua muda mrefu kubadili mindset za watawala.

Mkuu kuna nchi ikithibitika tu kuwa Polisi wamepokea maagizo kabla ya kuchukua hatua
hao polisi wanaweza kuondolewa moja kwa moja na hata kupelekwa mahakamani

ndio mymain point here
ukiwabana polisi kisheria hawana jinsi
 
Na hata kina Lowassa,Sitta waliutaka urais
wangeshawishiwa kuwa tume huru ya uchaguzi itawapa nguvu popote kule watakapohamia....
nani anaejua leo tungekuwa wapi?
Hivi tume huru ya uchaguzi inategemewa kuwasaidia wasio na dola au wenye dola?
 
The Boss una hoja ya msingi sana, lakini kama umewahi kuisoma Rasmu hiyo uliyoiita ya "Sitta" utaona kuwa bado CCM walikuja na msimamo wa kumuonngezea Rais Madaraka. Hoja ya Tanganyika ilibeba mfumo tofauti na huu wa Rasmu ya Sitta yenye kutaka kuwa na Rais asiyehojika.

kwangu mimi tatizo langu na wapinzani wa CCM ni pale malengo yao yanapokwenda upogo kutokana na kukosa uzingativu katika hoja wanayoisimamia. Kwa mfano inaonekana ni kama vile Tundu Lissu anapambana na Serikali wakati ilitakiwa ionekane kuwa Lissu anapambana na serikali kwa niaba ya Watanzania wote.

kwa vyovyote vile CCM haiwezi hata kwa marungu kukubali Katiba inayopunguza madaraka ya Rais na kuyagawanya kwenye mihimili mingine, kwa kuwa chama chenyewe ni dhaifu sana kiasi kwamba bila ya kujiambatanisha na dola kitafutika kwenye Ramani ya Siasa Tanzania!!
 
Ndo maana nchi zinazojali demokrasia zimepiga marufuku polisi kupokea amri kutoka juu
na sisi pia tungetaka tungeweza
Polisi inakuwa ni marufuku kupokea amri
wafanye kazi kwa sheria tu zilizopo...
Shida kuu tuliyonayo sisi ni jeshi la polisi kuegemea upande wa chama tawala au tuseme kutekwa na wanasiasa na kujiingiza ktk siasa kwa kutumika kukandamiza upinzani kwa amri toka chama dola.
 
Kenya ya leo kisiasa ni nafuu kuliko Kenya ya Moi
sisi sasa ni kama tunafanana na Kenya ya Moi....
Labda hufuatilii tu siasa za Kenya, lakini hakuna unafuu wowote labda niseme mazingira yamebadisha watu wamekuwa na ufahamu zaidi lakini siyo katiba imewabadilisha. Ordinary Kenyan are still facing the same problems. Kwa mfano sasa hivi Kenyatta ameshawanunua baadhi ya wapinzani na anakifanyia chama chake kilichompeleka ikulu modification ya hali ya juu! Same wine, just a different bottle! Mimi mawazo yangu ni kuwa nchi zetu za kiafrika hata tuwe na katiba nzuri kiasi gani haitasaidia as long as wananchi wa kawaida hawajitambui na viongozi hawana willing ya kufanya kazi bali kuchumia matumbo yao1
 
The Boss una hoja ya msingi sana, lakini kama umewahi kuisoma Rasmu hiyo uliyoiita ya "Sitta" utaona kuwa bado CCM walikuja na msimamo wa kumuonngezea Rais Madaraka. Hoja ya Tanganyika ilibeba mfumo tofauti na huu wa Rasmu ya Sitta yenye kutaka kuwa na Rais asiyehojika.

kwangu mimi tatizo langu na wapinzani wa CCM ni pale malengo yao yanapokwenda upogo kutokana na kukosa uzingativu katika hoja wanayoisimamia. Kwa mfano inaonekana ni kama vile Tundu Lissu anapambana na Serikali wakati ilitakiwa ionekane kuwa Lissu anapambana na serikali kwa niaba ya Watanzania wote.

kwa vyovyote vile CCM haiwezi hata kwa marungu kukubali Katiba inayopunguza madaraka ya Rais na kuyagawanya kwenye mihimili mingine, kwa kuwa chama chenyewe ni dhaifu sana kiasi kwamba bila ya kujiambatanisha na dola kitafutika kwenye Ramani ya Siasa Tanzania!!

Tusisahau hao wanaCCM walioipinga Rasimu ya Warioba walikuwepo Lowassa na Sumaye pia
leo tunao huku tunalilia wote tume ya uchaguzi.....

point hapa ni kuwa watu wanaweza badili misimamo wakiona faida pana
nina uhakika kuna wana CCM now wanatamani Magufuli ashindwe 2020
lakini na wao watahitaji tume huru ya uchaguzi.....
 
Bado katiba hii yenye viraka chungu nzima pamoja na ubaya wake inaruhusu maandamano na mikutano ya vyama vya upinzani ambayo hakuna yoyote mwenye ruhusa ya kuwaamulia wapinzani nini kuzungumza kwenye mikutano yao na wapi pa kufanyia mikutano yao bila kujali kama wana mbunge kwenye jimbo husika au la. Na yeyote anayewazuia wapinzani kufanya hivyo anakiuka katiba ya nchi.
Lakini @BAK,wako wapi hao watanzania mnaowatetea humu,mbona nchi iko kimya?!Wameridhika na hali ya mambo waacheni waendelee kula mlo mmoja kwa siku.
 
Hili ni gumu kidogo kulijadili. Maana kila mtu ataweka sababu zake
 
Mkuu kuna nchi ikithibitika tu kuwa Polisi wamepokea maagizo kabla ya kuchukua hatua
hao polisi wanaweza kuondolewa moja kwa moja na hata kupelekwa mahakamani

ndio mymain point here
ukiwabana polisi kisheria hawana jinsi

Mkuu nchi za hivyo ni ngapi hapa africa? Hivi hujawahi kusikia neno linalochomekwa siku hizi, eti sisi tunafuata demokrasia ya aina yetu na wala sio kuiga kila kitu kwa nchi za magharibi? Huku kwetu baadhi ya mambo yanakuwa magumu kutekelezeka kutokana na hila na fitna.
 
Nakubaliana na wewe The Boss lakini hoja yangu ni kwamba wana CCM walikuwa "wanatamani" na hata sasa bado "wanatamani" kuwa na tume huru ya uchaguzi, lakini sote tunafahamu kuwa chama chao hakiruhusu kuwa na mawazo huru na hata wananchi nao wameaminishwa kuwa " kushughulikiwa" ni stahili ya "waasi" wote wa ndani na nje ya CCM. Hilo ndilo tatizo letu. Kwani si ndani wala nje ya CCM mtu atapata msaada akiendana tofauti na msimamo wa wakubwa!!
 
Huwezi pata kitu bila kutoa kitu UKAWA wanataka kupata kitu kikubwa zaid bila kutoa kitu that is naturally impossible
 
Back
Top Bottom