The boss unakuwa kama ni mgeni wa nchi hizi za kiafrika, kwa kiwango kikubwa katiba za nchi nyingi za kiafrika zinafuatwa kutegemeana na utashi wa kiongozi na wala sio katiba inasemaje. Katika nchi hizi za kiafrika ili mengi yaliyo kwenye katiba yafuatwe ni lazima kuwe na misuguano mikali na wakati mwingine misuguano hiyo hupelekea machafuko. Katiba hii iliyopo inaruhusu wapi rais kuzuia vyama vingine kukutana na kufanya siasa mpaka mwaka kiongozi huyo aliopanga? Kwa hiyo hata kama ingekuja katiba nzuri vipi bado isingefuatwa. Kwa maneno marahisi kabisa, hiyo rasimu ya Warioba ilikuwa ni matakwa yetu wananchi, lakini uliona bila aibu kundi la watu fulani waliondoa vifungu muhimu ambavyo vilikuwa moyo wa katiba ile kwa maslahi binafsi. Kwa hiyo hata kama ingepita kwa muujiza bado kundi lile lile lingeitekeleza kulingana na maslahi yao.