Tundu Lissu: Serikali imenilipa nusu ya stahiki zangu, nikilipwa fedha za matibabu sitazirudisha kwa walionichangia

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Feb 7, 2022
2,309
5,464
Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu ameulizwa kama Serikali imeshakamilisha malipo ya kiinua mgogo chake alichokuwa anadai, majibu yake ni haya:

“Nilikuwa nadai kiinua mgogo cha miezi 44 niliyokuwa Bungeni, nimelipwa kiinua mgongo cha miezi 20 bado cha miezi 24.

“Nilikuwa nadai fidia ya fedha zote nilizotumia kwenye matibabu baada ya kushambuliwa Septemba 7, 2017, hizo sijalipwa. Nimezidai kwa kuwa Sheria ya uendeshaji wa Bunge inasema Mbunge akiugua akiwa kazini anapwa kulipiwa gharama ya matibabu yake, sijaomba kitu ambacho kipo nje ya sheria.

“Niambiwa niandike barua, nimefanya hivyo na nimeambatanisha na risiti zote nikizotumia kuanzia Nairobi hadi Ubelgiji.

“Katika matibabu yangu kuna fedha ambazo zililipwa na Chama, kuhusu fedha nilizochangiwa na watu mbalimbali wakati wa matibabu kama nikilipwa zitakuwa zangu kwa kuwa nazihitaji.

“Miaka takribani minne nimekaa hospitali, maumivu yote yale, ndio maana Sheria inasema niliowe hizo fedha ili ziweze kunisaidia kwa mambo mbalimbali.

“Pia hao waliochanga hawajaniambia niwarudishie, hawakunikopesha, walinisaidia kwa sababu Serikali ilitaka nife nisipate msaada.”


Chanzo: Edwin Odemba
 
So what are you not getting from his statement? Ukinichangia ugonjwa, akaja mtu baadaye akalipia matibabu yote , huwezi kunidai nirudishe ile ulionichangia . Mie kuwepo kitandani kama mgonjwa kwa Mda mrefu kumeondoa kabisa kipato kinachotokana na shuguri zangu.

Hivyo in that case, pesa ulionichangia, to some extent itasaidia kusolve matatizo ambayo pesa niliyokua naipata nikiwa mzima ilikua inayatatua. Kumbuka mtu anapokua kitandani kwa ugonjwa hata shuguri za uzalishaji kipato zinasimama. Ufafanuzi ni kwa wale vichwa maji wasioelewa kirahisi
 
“Katika matibabu yangu kuna fedha ambazo zililipwa na Chama, kuhusu fedha nilizochangiwa na watu mbalimbali wakati wa matibabu kama nikilipwa zitakuwa zangu kwa kuwa nazihitaji.
Ni kwakukwa walikupa hawakukukopesha, ni kama michango ya harusi, ukioa mkiachana huwezi kudaiwa mrudishe michango
 
Sheria ni kweli zipo , lkn kipindi Cha magufuri aliamua tu kuto kumhudumia mhe Lissu ili afe kwa kukosa matibabu , lkn shukrani ziwaendee wale woote waliochangia matibabu ya mhe Lissu .. Magufuri kupitia Job Ndugai akiwa spika enzi hizo aligoma kutoa hela za matibabu lkn wakaona wamvue kbs na ubunge.... Kwahiyo tunapo sema nchi hii kwa miaka 6 ilipitia kipindi Cha mpito msikasilike nyie team magufuri
 
CHIBA KAPEWA MABURUNGUTU YA ASALI.

CHADEMA MJIANDAE KUSALITIWA KAMA 2015.
Usaliti hauwezi kuisha hapa chini ya jua ndg... kwahiyo ukiwa na mawazo hayo huwezi kufanya jambo kwa kuhofia usaliti... Na usikute usaliti ni sehemu ya maisha yako ndo maana unawaza hivyo
 
Lissu is like a Chichidodo,a chichidodo is a bird that eats maggots which are found in human excrement, at the same time it hates very much human excrement!!!

Poor lissu,only idiots can understand this person!!
Chichidodo2-768x742.jpg
 
Back
Top Bottom