Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,733
- 218,320
Taarifa ikufikie popote ulipo kwamba , Makamu Mwenyekiti wa Chadema , Tundu Lissu amelazimika kukatisha kuangalia Afcon huko Ivory Coast ili kuwahi maandamano ya Amani yaliyotangazwa na Chama chake , yatakayofanyika tarehe 24/01/2024 mapema asubuhi.
Akizungumza na vyombo vya habari vya Kimataifa , Lissu amefurahishwa na Jinsi umma wa Watanzania ulivyoitikia Maandamano hayo na kuahidi kushiriki kikamilifu , licha ya vitisho vya kishamba vya Mkuu wa Mkoa wa DSM , Chalamila mwenye asili ya Tanangozi huko Iringa.
Taarifa hii njema inazima kabisa kauli za uongo zinazoendelea kutolewa na viongozi wa ccm wenye upeo wa chini kwamba Lissu amepuuza Maandamano hayo.