Mkuu issue yenyewe ni kwamba: Abdul Jumbe wakati Yuko madarakani, kama Rais wa Zanzibar na makamu wa rais ya Tanzania, alichapisha pesa, bendera za serikari ya mapinduzi Zanzibar, kisha akaenda UK akamwambia waziri mkuu Kuwa Tanzania bara inampango wa kuivamia Zanzibar na kuikalia kwa nguvu akaomba na msaada! Waziri akamuahidi kutuma jeshi kama itatokea kama ilivyofanya UK jeshi letu lilipoasi,
Aliporudi huku akamwambia Ml. Nyerere Kuwa kuna fununu kuna jeshi linataka kuivamia Zanzibar! Inahitaji ulinzi, Nyerere akatuma jeshi na vifaru Zanzibar kwa ulinzi,
Baada ya majeshi kujipanga Jumbe akapiga simu kwa Waziri mkuu wa UK Kuwa Yale aliyomwambia yametimia, UK haikufanya pupa, PM akampigia simu Nyerere kumuuliza sababu ya kuivamia Zanzibar na kuikalia kwa mabavu, Nyerere akashanga ndiyo ilibidi wakutanishwe ukweli ujulikane, ndiyo Jumbe akaonekana mchonganishi, kwa heshima yake akaombwa ajiuzuru na kukaa pembeni, Seif S Hamad alikuwa anauma huku na kule kwa lengo la kuchukua madaraka ya Jumbe ndiyo Rungu likamwangukia, na Urais wa Zanzibar ukamwangukia Alli Hassan Mwinyi kwa kipindi mpaka uchaguzi baada ya hapo akagombea bara na hatimae Kuwa rais wa Tanzania,
Kama mlisikia machafuko ya Zanzibar ndiyo hayo, hata UK wanalijua lililomwondoa Jumbe na kumuweka pembeni kisiasa.