Tundu Lissu na Aboud Jumbe

Tundu Lissu na Aboud Jumbe

Kwa nini ma ccm huchukizwa sana Tundu Lissu akiwaweka uchi kuhusu mzee Jumbe?
hatutaki kupotoshwa nimekuwa nikisema lissu ni mpotoshaji watu wamekuwa hawanielewi´.....mikutano mingi ya hadhara lisu huwa anaseña si muumini wa mwalimu,kampeni zake,na hata ndani ya bunge na juzi bunge la katiba...kwasababu anachukia villagelization sasa hata kama yeye hapendi si busara kuendelea kupotosha uma....nitampinga lissu hadi kifo changu kwa sababu ni mchochezi na mtu asie na mapenzi mema na taifa letu.
 
Kwa kifupi tu, Jumbe alikuwa anauhoji muungano, akawa anatayarisha namna ya kumuingia Nyerere kuhusu Zanzibar kuwa na madaraka zaidi kwa mujibu wa matakwa ya Wazanzibari, wakati anaandaa makaratasi yake, sekretari wake akayaona na kumtaarifu Seif Sharif Hamad. Seif akamtuma Sekretari wa Jumbe kuiba makaratasi yake na kumpelekea Nyerere. Nyerere akambana Jumbe na kumlazimisha kujiuzulu.

The details and narrative varies according to different sources, but that is the main story.

Ndiyo maana mpaka leo kuna vikao vya Seif Sharif na Nyerere havijulikani walizungumza nini.

Ndiyo maana Tundu Lissu anapenda kumtumia Jumbe kama shujaa aliyediriki ku question uongozi wa Nyerere kuhusu Muungano.

je tundu lissu yupo sahihi kwa mtazamo wako shujaa kiranga
 
Historia si moja, siku hizi kuna internet hata wewe unaweza kuandika unachojua.

Ukikalia kulia lia "wame spin" bila.ya kuelezea historia halisi kwa mujibu wako unapunguza nafasi ya ukweli kwa mujibu wako kujulikana.

Ndio maana tumewaletea wajuvi wa Mambo mtudadavulie. Kuna kitu kizito kilifichwa wakati wa makubaliano ya muungano, hicho kitu lazima kilichangia kifo cha Karume Senior. Ma nahisi ndicho hicho kilichomsibu Jumbe...
 
hatutaki kupotoshwa nimekuwa nikisema lissu ni mpotoshaji watu wamekuwa hawanielewi´.....mikutano mingi ya hadhara lisu huwa anaseña si muumini wa mwalimu,kampeni zake,na hata ndani ya bunge na juzi bunge la katiba...kwasababu anachukia villagelization sasa hata kama yeye hapendi si busara kuendelea kupotosha uma....nitampinga lissu hadi kifo changu kwa sababu ni mchochezi na mtu asie na mapenzi mema na taifa letu.

Tusaidie, amepotosha wapi na nini? Ukweli ni upi?
 
Ahaaaa.... Seif amekana lakini mkuu Kiranga

Seif lazima akane, ulitegemea aseme "mimi msaliti"?

Mimi nimekaa na marehemu Seif Bakari na huyo mama aliyekuwa Sekretari wa Jumbe wamenipa play by play.

Sasa hapa utakuta watu hata hawamjui Seif Bakari nani watataka kuanza kubisha tu.
 
Last edited by a moderator:
Ndio maana tumewaletea wajuvi wa Mambo mtudadavulie. Kuna kitu kizito kilifichwa wakati wa makubaliano ya muungano, hicho kitu lazima kilichangia kifo cha Karume Senior. Ma nahisi ndicho hicho kilichomsibu Jumbe...

Karume senior kauawa kwa umajununi wake, wala si habari za siasa.

Kamuua baba yake Humudi halafu kampa Humudi cheo kwenye intelligentsia.

Humudi akampigilia risasi mbali kwenye kikao cha bao.

Sheikh Thabit Kombo Jumaa akaambulia za mguu. Mpaka anafariki alikuwa anachechemea kutokana na risasi za Humudi siku aliyouawa Karume.

Karume was Nyereres man, therefore was at no.risk of being ousted politically. Kwa sababu Zanzibar (angalau Unguja, Pemba is another matter) alikuwa na support na bara alikuwa na support.
 
Nimemsikia Shujaa Tundu Lissu mara kwa mara akihusisha Muungano na Kuwekwa kizuizini Aboud Jumbe.

Eti Nyerere, mwasisi wa CCM ndie aliyempiga BAN mzee Jumbe.

Mohamed Said na Yericko Nyerere na Pasco naombeni mje hapa tuungane na wadau wengine tuwekewe ukweli huu hasa kwa kizazi cha 1980's ambao wengi hawajui nini kilitokea kwa Jumbe na kwa nini Tundu Lissu ameishikia bango sana hiyo

Aaaah Pasco leo utampata wapi? Saa hizi yuko mbwiiiiiii anagida bia na mademu zake wa Kinondoni! Unacheza na Pasco wewe
 
Last edited by a moderator:
je tundu lissu yupo sahihi kwa mtazamo wako shujaa kiranga

Muungano wa Tanzania unahitaji kupigiwa kura ya maoni na Watanzania wote. Bila hivyo ni batili. Kwa sababu hata mabaraza ya wawakilishi yote hayajaupitisha.

Baraza la Mapinduzi ni party Politburo, si baraza la Wawakilishi.

Tundu Lissu anauliza maswali fulani ambayo utamaduni wetu wa "funga bakuli mwanaharamu apite" hauruhusu kuuliza.
 
Ndio maana tumewaletea wajuvi wa Mambo mtudadavulie. Kuna kitu kizito kilifichwa wakati wa makubaliano ya muungano, hicho kitu lazima kilichangia kifo cha Karume Senior. Ma nahisi ndicho hicho kilichomsibu Jumbe...

yah´kiranga mpe elimu huyu serikali tatu naona anapotosha sana kwa kujifanya mjumvi wa mambo anaishi kwa kusikia kama lissu
 
Karume senior kauawa kwa umajununi wake, wala si habari za siasa.

Kamuua baba yake Humudi halafu kampa Humudi cheo kwenye intelligentsia.

Humudi akampigilia risasi mbali kwenye kikao cha bao.

Sheikh Thabit Kombo Jumaa akaambulia za mguu. Mpaka anafariki alikuwa anachechemea kutokana na risasi za Humudi siku aliyouawa Karume.

Karume was Nyereres man, therefore was at no.risk of being ousted politically. Kwa sababu Zanzibar (angalau Unguja, Pemba is another matter) alikuwa na support na bara alikuwa na support.

Aisee! Hii historia inachanganya sasa. Si akina Mohamed Said wanasema Karume alitofautiana na kina Mohamed Babu ambaye alikuwa swaiba wa Nyerere? Si ishu ilikuwa kuhusu muungano ndo nyerere akatuma mtu kumuua Karume?
 
Last edited by a moderator:
Muungano wa Tanzania unahitaji kupigiwa kura ya maoni na Watanzania wote. Bila hivyo ni batili. Kwa sababu hata mabaraza ya wawakilishi yote hayajaupitisha.

Baraza la Mapinduzi ni party Politburo, si baraza la Wawakilishi.

Tundu Lissu anauliza maswali fulani ambayo utamaduni wetu wa "funga bakuli mwanaharamu apite" hauruhusu kuuliza.
tupe mfano wa maswali hayo ambayo unahisi anauliza?? Je vp mtazamo wako kwa mwl.nyerere in relation to lissu
 
Nimemsikia Shujaa Tundu Lissu mara kwa mara akihusisha Muungano na Kuwekwa kizuizini Aboud Jumbe.

Eti Nyerere, mwasisi wa CCM ndie aliyempiga BAN mzee Jumbe.

Mohamed Said na Yericko Nyerere na Pasco naombeni mje hapa tuungane na wadau wengine tuwekewe ukweli huu hasa kwa kizazi cha 1980's ambao wengi hawajui nini kilitokea kwa Jumbe na kwa nini Tundu Lissu ameishikia bango sana hiyo

We hulijui hili? Umezaliwa lini?
 
yah´kiranga mpe elimu huyu serikali tatu naona anapotosha sana kwa kujifanya mjumvi wa mambo anaishi kwa kusikia kama lissu

Wewe sasa unataka kutuharibia thread kwa kuleta uccm wako. Mwache mkuu Kiranga atoe darsa
 
Last edited by a moderator:
Aisee! Hii historia inachanganya sasa. Si akina Mohamed Said wanasema Karume alitofautiana na kina Mohamed Babu ambaye alikuwa swaiba wa Nyerere? Si ishu ilikuwa kuhusu muungano ndo nyerere akatuma mtu kumuua Karume?

Kuna kina Kassim Hanga, Makomredi hao hao rafiki zao kina Babu, Nyerere mpaka aliwarudisha Zanzibar wakaenda kuuawa na Karume.

Nyerere na Karume walikuwa damdam, kwa sababu Kenyatta alipomtolea nje Nyerere kuunganisha Tanganyika na Kenya, Karume si tu alikubali mara moja, ila pia akasema rais utakuwa wewe.

Karume was so loyal to Nyerere, it does not make sense kusema Nyerere alimtumia watu kumuua Karume.

Waliotaka kumpindua Karume ni kina Mahfudh wa UMMA party, ila tatizo wakamtuma Humudi, mtu ambaye baba yake aliuawa na Karume. Humudi badala ya kumkamata Karume akamuua, kwa mujibu wa Ali Haji Pandu.
 
Kwa mujibu wa kamanda Lissu, huyo mzee amepigwa BAN asiongee na media wala asiandike kitabu wala kutembelewa.

Kwa kweli ni mzee sana (miaka 94) sidhani kama anaweza kuongea sijui akili yake kama bado iko sharp.

Ila Mihangwa (I think) alishawahi kueleza kwa urefu kuhusu sakata hili kwenye makala za raia mwema. Na yeye mwenyewe alitunga kitabu cha The Partnership akaeleza mengi mule ijapokuwa hayakuwa na uhusiano wa moja kwa moja na kufukuzwa kwake.
 
Aisee! Hii historia inachanganya sasa. Si akina Mohamed Said wanasema Karume alitofautiana na kina Mohamed Babu ambaye alikuwa swaiba wa Nyerere? Si ishu ilikuwa kuhusu muungano ndo nyerere akatuma mtu kumuua Karume?

Eh tumbaku ya leo kali kweli! Kama alivyosema Kiranga, in hindsight Karume alifanya kosa kubwa sana kumpa cheo cha jeshi Humudi wakati alimuua baba yake. Kuna waarabu wana visasi kweli kweli na huyu ni mmoja wao.

Inasemekana Humudi alisema kama mara mbili hivi kwamba atamuua Karume, lakini father K alidhania ni utani tu.

Jamaa alipiga trenchcoat lake ndani ameficha mtutu, akaingia pale Kisiwandui - laa haulaaa! iliyobaki ni historia.
 
Eh tumbaku ya leo kali kweli! Kama alivyosema Kiranga, in hindsight Karume alifanya kosa kubwa sana kumpa cheo cha jeshi Humudi wakati alimuua baba yake. Kuna waarabu wana visasi kweli kweli na huyu ni mmoja wao.

Inasemekana Humudi alisema kama mara mbili hivi kwamba atamuua Karume, lakini father K alidhania ni utani tu.

Jamaa alipiga trenchcoat lake ndani ameficha mtutu, akaingia pale Kisiwandui - laa haulaaa! iliyobaki ni historia.

Umeandika kiudaku udaku sana ingawa ujumbe umefika. Hii historia imeandikwa wapi?
 
hatutaki kupotoshwa nimekuwa nikisema lissu ni mpotoshaji watu wamekuwa hawanielewi´.....mikutano mingi ya hadhara lisu huwa anaseña si muumini wa mwalimu,kampeni zake,na hata ndani ya bunge na juzi bunge la katiba...kwasababu anachukia villagelization sasa hata kama yeye hapendi si busara kuendelea kupotosha uma....nitampinga lissu hadi kifo changu kwa sababu ni mchochezi na mtu asie na mapenzi mema na taifa letu.
HOJA HOJA HOJA HOJA tu ndiyo itakusaidia kupambana na LISSU kitu ambacho najua huna unaendeshwa na uhafidhina usiojua sababu ya uhafidhina!!
 
inabidi vijana wajitahidi kuijua historia ya Kweli na sio utani wanaofanya sasa....
 
Back
Top Bottom