chabuso
JF-Expert Member
- Feb 18, 2013
- 6,379
- 5,887
By Pasco,
Wanabodi,
Mwanamke kutoka Zanzibar kwa jina la Bi Nasra, aliyejitambulisha kama mke wa kwanza wa president wa kwanza wa Zanzibar, anashiriki shindano la Bibi Bomba la Clouds FM!.
Mwanamke huyo emedai kufanikiwa kupata mtoto mmoja na rais huyo wa kwanza na kusema yupo na mtoto yupo!.
Kwa wale wajuzi wa mambo ya Zanzibar, jee ni kweli president wa kwanza wa Zanzibar alikuwa na mke mkubwa?. Kama ni kweli, is it proper kwa mke wa president kushiriki shindano na kujiexpose kuwa yeye alikuwa ndiye mke wa kwanza wa president wa kwanza?!.
Namfahamu huko Zanzibar kuna mtoto wa nje wa Sultan aliyezaa na mjakazi wa mkewe na baada ya kupata ujauzito ikafanywa siri kubwa kumuozesha huyo mjakazi haraka haraka kabla siri haijafichuka!. Mwana mfalme huyo yupo na amejinyamazia kimya!.
Kama ni kweli rais wa kwanza wa Zanzibar atakuwa alikuwa na mke mkubwa, basi urais Zanzibar haushi vibwanga!.
Kimbwanga kingine ni kuna watoto wawili wa kiume wa rais, kaka mkubwa akawa rais kwa kipindi cha miaka 10, alipokaribia kumaliza mdogo mtu nae akautaka urais, akashauriwa yeye asigombee kwa sababu aliyemaliza ni kaka yake wa damu, hivyo urais wa Zanzibar ungeonekana kama usultani!. Mdogo mtu aligoma kujitoa kwa hoja kuwa mtoto halali wa rais aliyepaswa kuchukua urais ni yeye!, eti kakaye ni mtoto wa kufikia!
Visa vya marais wa Zanzibar havikuishia hapo. Kuna rais mmoja mpenda warembo, ila alikuwa akioa na kuacha, alipoa mke wa 5, aliporwa huyo mke na rafiki yake ambaye alikuwa ni rais wa nchi nyingine hapa hapa barani Afrika. Sasa ana mke wa 6 na ndio katulia kutokana na umri
Raisi wa kwanza wa zanzibar umekusudia hayati Abeid Amani Karume(R.I.P),kama mke wa kwanza wa president wa kwanza wa Zanzibar, anashiriki shindano la Bibi Bomba la Clouds FM! hayo yatakuwa maajabu mke wa pili Fatma Karume unamuona hali yake sasa huyo wa kwanza atakuwa hali gani hivi sasa,,,,naona atashinda hayo mashindano si unajua wazanzibari wanakula sana nazi hawazeeki 🙂