Uchaguzi 2020 Tundu Lissu baada ya Uchaguzi

ZeMarcopolo

Platinum Member
May 11, 2008
14,017
7,220
Uchaguzi Mkuu wa Rais na Wabunge unazidi kukaribia. Wapinzani wanaoonekana maeneo mengi ya kampeni ni Tundu Lissu na Prof. Ibrahim Lipumba.

Kumekuwa na mijadala katika maeneo mbalimbali nchini juu ya hatma ya wagombea hawa baada ya uchaguzi kuisha.

Kwa upande wa Lipumba, kwa vile amekuwa mgombea kwenye chaguzi za siku za nyuma, watu wengi wanategemea atarudi kukiongoza chama chake cha CUF kama alivyofanya baada ya chaguzi zilizopita.

Kwa vile Tundu Lissu anagombea kwa mara ya kwanza, watu wamekuwa na maoni mbalimbali juu ya kile wanachotarajia akifanye baada ya uchaguzi. Miongoni mwa yaliyojirudiarudia ni kama ifuatavyo;

1. Tundu Lissu atataka kuchukua nafasi ya Uenyekiti ndani ya Chadema. Hatua hii itaongeza msuguano uliopo kati yake na Mbowe. Kwa vile hakuna uchaguzi wa ndani wa Chadema hivi karibuni, uwezekano wa Tundu Lissu kufuata njia hii ni mdogo.

2. Tundu Lissu atarudi Ubelgiji kuungana na familia yake. Kwa vile Tundu Lissu ameomba kutambuliwa kama mkimbizi nchini Ubelgiji, upo uwezekano mkubwa kuwa atarudi kule mpaka maombi yake hayo kukamilika ili familia yake iendelee kutunzwa na serikali ya Ubelgiji.

3. Tundu Lissu ataungana na Zitto Kabwe kwenye ACT. Kutokana na msuguano unaoendelea kati yake na Mbowe, iwapo ataamua kubaki nchini, anaweza kujiunga na Zitto kwenye ACT.

4. Tundu Lissu ataanzisha chama chake. Baadhi ya watu wanadhani Tundu Lissu ataibuka na kusajili chama chake kipya. Uwezekano wa kuanzisha chama baada tu ya uchaguzi ni mdogo. Historia inaonyesha vyama vingi huanzishwa unapikaribia Uchaguzi Mkuu au baada ya mivutano kwenye chaguzi za ndani za vyama.

5. Tundu Lissu ataomba nafasi kwenye serikali ya Magufuli. Wapo pia wanaoamini kuwa Tundu Lissu atamkumbusha Magufuli juu ya ahadi ya kumpa kazi. Kwa vile Magufuli alitoa ahadi hiyo hadharani, itakuwa ni uungwana kuitekeleza. Hii pia itasaidia kumuwezesha Tundu Lissu kujikimu na kuirudisha familia yake nchini.

Kama mnavyoona, matarajio ni mengi, lakini cha muhimu zaidi tuendelee kumuomba Mungu atijalie uchaguzi wa amani na utulivu ili tuendelee kuijenga nchi yetu.

Mungu Ibariki Afrika, Mungu Ibariki Tanzania.
 
Baada ya Septemba 7, 2017 wengi walitarajia hatoweza kuishi tena, Ila ikawa miujiza. Bila shaka baada ya Oktoba 28, 2020 itakuwa miujiza tena.

Tuombe Mungu tufike hiyo siku tukiwa wazima wa afya!
Kuna tetesi kwamba alitakiwa kuzikwa chapchap huku risala ya mazishi ikiandikwa na Ndugai, kuna tetesi pia kwamba pesa ya kuchimbia kaburi ilishalipwa tayari.
 
Lissu haongei na Mnyika, na Mbowe yupo upande wa Mnyika. Katibu Mkuu wa CHADEMA hataonekana tena kampeni hizi. Baada ya uchaguzi huu Kati ya Mnyika au Lissu lazima mmojawapo aondoke CHADEMA.

Wengi humu mmejaa ushabiki Ila huko jikoni hali sio shwari. Lissu kaja kuizika CHADEMA rasmi. Yeye anajipambania hawapiganii madiwani wala wabunge wake. Mdee na Lema hawajihusishi na kampeni za Lissu. Mwenye macho haambiwi tazama.
 
Lissu haongei na Mnyika, na Mbowe yupo upande wa Mnyika. Katibu Mkuu wa CHADEMA hataonekana tena kampeni hizi. Baada ya uchaguzi huu Kati ya Mnyika au Lissu lazima mmojawapo aondoke CHADEMA. Wengi humu mmejaa ushabiki Ila huko jikoni hali sio shwari. Lissu kaja kuizika CHADEMA rasmi. Yeye anajipambania hawapiganii madiwani wala wabunge wake. Mdee na Lema hawajihusishi na kampeni za Lissu. Mwenye macho haambiwi tazama.

Kwahiyo mkuu unadhani hatma yake baada ya uchaguzi ikoje?
 
Mtu ambaye hawezi kufanya mkutano wa hadhara na kushinda kutwa anasumbua wananchi kwenye miji na vijiwe vyao anaambiwa anafanya campaign ya kisayansi.. UVCCM mnajua kupeana moyo
 
Lissu haongei na Mnyika, na Mbowe yupo upande wa Mnyika. Katibu Mkuu wa CHADEMA hataonekana tena kampeni hizi. Baada ya uchaguzi huu Kati ya Mnyika au Lissu lazima mmojawapo aondoke CHADEMA. Wengi humu mmejaa ushabiki Ila huko jikoni hali sio shwari. Lissu kaja kuizika CHADEMA rasmi. Yeye anajipambania hawapiganii madiwani wala wabunge wake. Mdee na Lema hawajihusishi na kampeni za Lissu. Mwenye macho haambiwi tazama.
Mtu ambaye hawezi kufanya mkutano wa hadhara na kushinda kutwa anasumbua wananchi kwenye miji na vijiwe vyao anaambiwa anafanya campaign ya kisayansi.. UVCCM mnajua kupeana moyo
 
Kwahiyo mkuu unadhani hatma yake baada ya uchaguzi ikoje?
Atakuwa na hasira sana Ila itabidi aendelee kukaa nchini. Hawezi rudi Belgium au nchi za ulaya sababu Kuna pesa za watu mafia amekula akiwaaminisha atashinda uchaguzi huu. Kule wanaweza mmaliza. Na kuna diaspora wengi aliwachangisha,kurudi ulaya kutamkosesha amani. Ataona bora abaki humu humu ingawa itambidi akae kimya.

Na waweza kuwa mwisho wake kisiasa maana Mbowe hatakubali kumpoteza Mnyika sababu ya Lissu. Lissu anaropoka sana, Kama unakumbuka vizuri hata 2017 wiki chache kabla hajapigwa risasi alikuwa kivyake Chadema sababu kuna vitu anavyoongea wanaogopa kuwa karibu nae kuonekana lao moja.

Tafuta video YouTube angalia kwa makini mara nyingi alikuwa anaita waandishi bila support ya Chadema.
 
Lissu haongei na Mnyika, na Mbowe yupo upande wa Mnyika. Katibu Mkuu wa CHADEMA hataonekana tena kampeni hizi. Baada ya uchaguzi huu Kati ya Mnyika au Lissu lazima mmojawapo aondoke CHADEMA. Wengi humu mmejaa ushabiki Ila huko jikoni hali sio shwari. Lissu kaja kuizika CHADEMA rasmi. Yeye anajipambania hawapiganii madiwani wala wabunge wake. Mdee na Lema hawajihusishi na kampeni za Lissu. Mwenye macho haambiwi tazama.
hahaha yaan umeshikiwa akili msiba daah hahahahaha,watoto waliopatikana kwa kondom fake bana wana wenge kinyama
 
Atakuwa na hasira sana Ila itabidi aendelee kukaa nchini. Hawezi rudi Belgium au nchi za ulaya sababu Kuna pesa za watu mafia amekula akiwaaminisha atashinda uchaguzi huu...
Nakupata mkuu. Kama atabaki nchini itafaa Magufuli akimpa kazi kwenye kamisheni ya madini. Anaweza kusaidia vitu viwili vitatu.
 
Mkuu tubet, ukimuona Mnyika kwenye kampeni za Lissu najiondoa JF. Nina uhakika na ninachokwambia. Kwani Musiba kasemaje?..
kwa taarifa yako tu wote unaowaona kwenye kapeni za uraisi ni team ambayo ilishawailishwa tume kbla ivyo haiwezekan katikati ukajiongezea watu tu ndo maana wazir mkuu kachapwa mdomo kujihusisha na kapeni za uraisi sababu sheria inamnyima ,sheria mnazichakachua wenyewe alaf hamna muda wa kuzisoma na kuzijua,ndo maana ya utopolo sasa hii
 
Lissu haongei na Mnyika, na Mbowe yupo upande wa Mnyika. Katibu Mkuu wa CHADEMA hataonekana tena kampeni hizi. Baada ya uchaguzi huu Kati ya Mnyika au Lissu lazima mmojawapo aondoke CHADEMA. Wengi humu mmejaa ushabiki Ila huko jikoni hali sio shwari...
Mna bongo lala kweli nyie. Hao mliowataja hawajihusishi na kampeni kivipi wakati wa uzinduzi kikanda walikuwa wote? Kuhusu kufanya peke yao kwa niaba ya Lissu mmesikia mashtaka ya Majaliwa huko Tume?

Mwenye mamlaka ya kuzunguka nchini peke yake kumpigia kampeni mgombea ni mgombea mwenza tuu hivyo waziri mkuu anavunja sheria.
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Uchaguzi Mkuu wa Rais na Wabunge unazidi kukaribia. Wapinzani wanaoonekana maeneo mengi ya kampeni ni Tundu Lissu na Prof. Ibrahim Lipumba.

Kumekuwa na mijadala katika maeneo mbalimbali nchini juu ya hatma ya wagombea hawa baada ya uchaguzi kuisha...
Baada ya uchaguzi atafanya kazi gani nyingine wakati ni Rais?
Maswali mengine ya kipuuzi kweli!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom