Tundu Lissu ajeruhiwa tena

Tundu Lissu ajeruhiwa tena

Ndugu zangu,

Nimejaribu mara kadhaa jana kumpigia mdogo wangu Tundu aliyeko Ubelgiji lakini simu yake ilipokelewa na mtu aliyejitambulisha kama "Kaka mkubwa".Nikamwambia Lissu amemsikia au kusoma ujumbe wa Peter Geleti? Ghafla akachukua simu huku akisema "Kaka najua unataka kujeruhi nafsi yangu kwa kunukuu matamshi yangu kwenye sakata la Barrick mwaka 2017 mmeshinda,hongereni sana" akakata simu.

Kauli yake ilinikumbusha jinsi alivyowahi kusema kwa majigambo kuwa "mtashitakiwa na hamna hata haki mchanga licha ya dhahabu" kauli yake hii iliibua vijana ambao ni wafuasi wake wakaanza kunukuu kauli hiyo huku kila kukicha wakitupa wasifu wa "wazungu" waliokuja kujadili suala la makinikia.

Tuliambiwa mengi zaidi tuliambiwa sifa na wasifu wa Chief operating officer wa Barrick ambaye aliwa kuwa mwanajeshi eti huyu jamaa ni mwanamikakati balaa.Huku vijana wengine kila siku wakifuatilia na kuripoti jinsi gani wanasheria wa Barrick wanajiandaa kufungua kesi MIGA sijui ICJ nk.


Wengi wao leo wamebaki kimya,wameumbuka hakika Tundu Lissu amejeruhiwa tena.

Hii ni JF!
UNAKALIA UPANGA SIO
 
subiri niwapeleke watoto wangu driving school maana kila mtu atapata noah ntakuwa na jumla ya noah 15 pamoja na house girl zitakuwa 16. nafungua kabisaa Yard ya noah.
 
..sasa wameibuka vibaraka wa barrick.

..hatuwezi kushangilia "kishika uchumba" 300 million wakati ripoti za uchunguzi zimebainisha tunawadai 190 billion.

..hata tukisema watulipe 300 million kila mwaka itachukua zaidi ya miaka 600 kumaliza deni la 190 huku tukiwasamehe riba.
 
Kwani tumelipwa dola bilion 190?
Wanashangilia kitu ambacho hawajapata. Sawa na kushangilia mimba kumbe MTU avimba tumbo kwa safura.
Bado hawajiulizi kwanini zile tuu $300M za kishika uchumba na zenyewe hazijalipwa tuu?
Hawa wanacheza na akili za jiwe wanajuwa oktoba hakatizi ili waje wakubaliane na wenye weledi zaidi
 
Ndugu zangu,

Nimejaribu mara kadhaa jana kumpigia mdogo wangu Tundu aliyeko Ubelgiji lakini simu yake ilipokelewa na mtu aliyejitambulisha kama "Kaka mkubwa".Nikamwambia Lissu amemsikia au kusoma ujumbe wa Peter Geleti? Ghafla akachukua simu huku akisema "Kaka najua unataka kujeruhi nafsi yangu kwa kunukuu matamshi yangu kwenye sakata la Barrick mwaka 2017 mmeshinda,hongereni sana" akakata simu.

Kauli yake ilinikumbusha jinsi alivyowahi kusema kwa majigambo kuwa "mtashitakiwa na hamna hata haki mchanga licha ya dhahabu" kauli yake hii iliibua vijana ambao ni wafuasi wake wakaanza kunukuu kauli hiyo huku kila kukicha wakitupa wasifu wa "wazungu" waliokuja kujadili suala la makinikia.

Tuliambiwa mengi zaidi tuliambiwa sifa na wasifu wa Chief operating officer wa Barrick ambaye aliwa kuwa mwanajeshi eti huyu jamaa ni mwanamikakati balaa.Huku vijana wengine kila siku wakifuatilia na kuripoti jinsi gani wanasheria wa Barrick wanajiandaa kufungua kesi MIGA sijui ICJ nk.


Wengi wao leo wamebaki kimya,wameumbuka hakika Tundu Lissu amejeruhiwa tena.

Hii ni JF!
Hivi unadhani umewashinda Barick? Kwa lipi zaidi?
 
..sasa wameibuka vibaraka wa barrick.

..hatuwezi kushangilia "kishika uchumba" 300 million wakati ripoti za uchunguzi zimebainisha tunawadai 190 billion.

..hata tukisema watulipe 300 million kila mwaka itachukua zaidi ya miaka 600 kumaliza deni la 190 huku tukiwasamehe riba.
Mkuu nilipoona post hii nikasema mkuu JokaKuu kesha anza kutulisha matango pori kwenye hesabu? Kushika calculator nikashtuka kumbe kweli! Itabidi watulipe kwa muda wa miaka 633! Hakika hilo deni litakuwa linashika namba moja ulimwenguni kwa kulipwa kwa muda mrefu haijapata kutokea.
 
Mpaka kufikia hapo Lissu ana mchango mkubwa.
Wenda bila yeye watanzania tusingejua mengi zaidi.


Ila napishana nae katika mdomo wake unaotoa matamshi yenye kuchefua nashindwa kumtofautisha na Bajaji au Sukuma.
 
Ndugu zangu,

Nimejaribu mara kadhaa jana kumpigia mdogo wangu Tundu aliyeko Ubelgiji lakini simu yake ilipokelewa na mtu aliyejitambulisha kama "Kaka mkubwa".Nikamwambia Lissu amemsikia au kusoma ujumbe wa Peter Geleti? Ghafla akachukua simu huku akisema "Kaka najua unataka kujeruhi nafsi yangu kwa kunukuu matamshi yangu kwenye sakata la Barrick mwaka 2017 mmeshinda,hongereni sana" akakata simu.

Kauli yake ilinikumbusha jinsi alivyowahi kusema kwa majigambo kuwa "mtashitakiwa na hamna hata haki mchanga licha ya dhahabu" kauli yake hii iliibua vijana ambao ni wafuasi wake wakaanza kunukuu kauli hiyo huku kila kukicha wakitupa wasifu wa "wazungu" waliokuja kujadili suala la makinikia.

Tuliambiwa mengi zaidi tuliambiwa sifa na wasifu wa Chief operating officer wa Barrick ambaye aliwa kuwa mwanajeshi eti huyu jamaa ni mwanamikakati balaa.Huku vijana wengine kila siku wakifuatilia na kuripoti jinsi gani wanasheria wa Barrick wanajiandaa kufungua kesi MIGA sijui ICJ nk.


Wengi wao leo wamebaki kimya,wameumbuka hakika Tundu Lissu amejeruhiwa tena.

Hii ni JF!
PhD holder toka university of CCM
 
Back
Top Bottom