Henry Kilewo
JF-Expert Member
- Feb 9, 2010
- 899
- 1,108
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI.
Arusha Mjini kwa sasa kuna tatizo kubwa sana la msongamano wa Magari na tunauitaji mkubwa wa bara bara na hivyo sio jambo la busara hata kidogo Mtu mmoja kutumia nafasi yake au Cheo chake kufunga barabara .
Barabara ya Kanisa ilifungwa na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha Ndugu Isidori Shirima miaka michache iliyopita na tulivyohoji sababu tuliambiwa kuwa Mke wake asingependa kuona bababara hiyo inatumika kwani ilikuwa inaleta kero ya vumbi nyumbani kwa Mkuu wa Mkoa na familia yake.
Tulipoendelea kutaka barabara hiyo ifunguliwe Kaimu Mkurugenzi wa Jiji wakati huo Bwana Estomih Chan'ga alikiri kuwa hawezi kufungua barabara hiyo kwani hawezi kugombana na Mkuu wa Mkoa.
Sasa Watu wa Arusha hawewezi kuendelea kutokutumia barabara hiyo ambayo ingepunguza msongamano wa magari kwa kiasi kikubwa kwa sababu kama hiyo , na ni Imani yangu kuwa Mkuu wa Mkoa wa sasa Ndg Magesa Mulongo hawezi kuendelea kuwa na ubinafsi wa kumkinga Mke wake na vumbi na familia yake huku Wananchi tulio wengi tukiendelea kuteseka na msongamano wa magari.
Baada ya taarifa hii kwenda kwenye Radio mbali mbali jana kama vile Radio 5 , Mj Radio na nyinginezo , Jeshi la Polisi lilivamia kituo cha Radio 5 na kuwatisha kwa nini wamerusha hewani matangazo kuhusu ufunguzi wa hiyo barabara na kudai kuwa lugha iliyotumika kwamba hatuwezi kuendelea kuwakinga wake wa Wakuu wa Mikoa Arusha wasipate vumbi wakati Wananchi wengi wanahitaji huduma ya Bara bara hiyo , ilikuwa ni lugha ya uchochezi .
Nirudie kusema kama nilivyoongea jana na Radio , kwamba barabara hiyo haina sababu ya msingi kuendelea kufungwa , ni matumaini yangu kuwa Mkuu wa Mkoa wa sasa atakuwa na Uungwana wa kutosha wa kuona Wananchi wa Arusha wanatumia barabara hiyo.
Pia nalitaka Jeshi la Polisi kuacha kutumika kutishia usalama wa vyombo vya habari na Demokrasia katika Nchi yetu kitendo kilichofanywa na Jeshi la Polisi Mkoani Arusha jana tarehe 28/02/2013 ni muendelezo wa matendo yao kila mara kwenye vyombo vya habari . Hii ni hatari kubwa na hatuwezi kukubali matisho ya aina hii kwani ni njama na jitihada za kuondoa Uhuru wa Habari katika Taifa letu.
Mwisho " Dhambi kubwa kuliko zote Duniani ni uoga " Tunataka bara bara hiyo ifunguliwe na Wananchi waendelea kutumia barabara hiyo.
Godbless J Lema (MB