Tunamkumbuka Edward Sokoine - Mtu wa Watu

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,478
40,000
Leo ni miaka 23 tangu Waziri Mkuu Edward Moringe Sokoine atutoke ghafla na kuacha simanzi na wingu la huzuni. Siku ile ya machozi na majonzi imebakia katika kumbukumbu za Watanzania wengi kama vile jana. Mfano wake ni kumbukumbu ya Wamarekani waliposikia habari za kuuawa kwa Rais John F. Kennedy.

Kila mtu aliyekuwa mtu mzima wakati ule anakumbuka vizuri siku hiyo alikuwa wapi na alikuwa anafanya nini. Je pengo aliloliacha marehemu limeanza kuzibwa?

Je, kuna kiongozi yoyote ambaye anakaribia sifa na utendaji kazi wa Marehemu Sokoine? Leo tunamkumbuka Edward Sokoine.

Pata kidogo chini hapa toka kwa mkuu Kyoma:

 
Ndugu Mwanakijiji shukrani kwa kutuwekea Kumbukumbu ya Bwana Edward Moringe Sokoine,Ambao waliwahi kufanya kazi na huyu mtu watakubaliana nami kwamba alikuwa mtu wa watu na asiyependa makuu.

Siku ya Msiba wa Mzee Sokoine naikumbuka vizuri!,wengine tulikuwa ndio tunaanza utumishi serikalini, tulikuwa tupo Dodoma kwenye vikao vya Bunge ambapo Mzee Sokoine aliondoka mchana kuwahi majukumu mengine Dar, baada ya vikao vya Bunge.

Kwa maelezo ya wasaidizi wa Marehemu walipofika Dumila wilayani kilosa ndipo lilipotokea gari lililokuwa linaendeshwa na Mkimbizi Dumisani Dube na kuligonga gari la Marehemu.

Habari za ajali ya Waziri Mkuu zilifika Dodoma mapema,na watu wote waliondoka Dodoma kuwahi Morogoro ambako Marehemu Sokoine alikimbizwa kwenye Hospitali ya Mkoa.Nakumbuka majira ya saa mbili za Usiku aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro (Mama Anna Abdalah), akifuatana na Spika wa Bunge Chifu Sapi Mkwawa (marehemu) na Daktari wa Mkoa Dr Msimbe (Marehemu) walidokeza viongozi wa Mkoa kwamba PM amefariki.

Mwalimu JK alilihutubia Taifa usiku huo huo, na kutangaza wiki moja ya maombolezo! Jamani nakumbuka ilikuwa siku ya Hudhuni mkubwa, Nchi nzima ilizizima kwa kuondokewa na kipenzi cha watu.

Tumkumbuke Marehemu Sokoine kwa kuimarisha Uongozi Bora na kujali Matakwa ya wengi! Tufuate nyayo zake kwa kuwajibika kwa Dhati na kuwa Watumishi wa kweli wa Umma wa wa-Tanzania.
 
Tunapaswa kumkumbuka kwa kutekeleza yale yote aliyoyapigania kwa nguvu zake zote hasa haki sawa kwa watanzania wote na kupunguza pengo kati ya walio nacho na wasio nacho.
 
Mzee Mwanakijiji,

Heshima yako kwanza,

Nakumbuka mwaka 1995, katika hotel ya Kirimanjaro, Eda Sanga, aliyekuwa mtangazaji wa Radio Tanzania, alishauri umuhimu wa kuwa na utaratibu wa kuwaandaa viongozi wa kitaifa. Alimkumbusha Mwalimu Nyerere jinsi alivyokuwa "akim-groom" Moringe Sokoine kuliongoza taifa baada ya yeye kung’atuka, lakini mauti yakamkuta. Mwalimu hakuwa mtu wa kutoa machozi hadharani, lakini Eda Sanga aliwakumbusha waandishi wa habari jinsi kifo cha Sokoine kilivyomliza Mwalimu. Alimuuliza Mwalimu kuwa, kwa nini tusiwe na utaratibu wa "kuwa-groom" viongozi wa kitaifa?

Mwalimu alijibu kwamba yeye hakuwahi "kum-groom” Sokoine ili achukue nafasi yake aking'atuka. "Sokoine alikuwa kiongozi chini yangu, lakini kama mambo yalikuwa hayaendi vizuri, ananiambia kuwa Mwalimu mambo hayaendi vizuri”. Kulikuwepo ukimya wa dakika kama mbili, alafu aliendelea kusema kuwa Sokoine hakuwa na sababu ya kutokumwambia mkubwa wake wa kazi kuwa mambo hayaendi vizuri”.

Katika tukio lingine mwaka 1995, nyumba ya mwalimu ya msasani ilikuwa inafanyiwa matengenezo, hivyo, akawa anaishi kwa muda kwenye nyumba ya Waziri Mkuu karibu na St. Peter, Osterbay. Aliitisha mkutano na waandishi wa habari kuongelea sakata la kumchuja mgombea uraisi ndani ya CCM. Nakumbuka Lowasa na Kikwete walikuwa na mtandao ambao ulikuwa umepenyaza hata kwenye vyombo vya habari. Pia ilikuwepo minong'ono ndani ya vyombo vya habari kuwa Mwalimu alikuwa anampinga Lowasa.

Katika mkutano huo, mwandishi mmoja wa habari ambaye hakutumia utaratibu wa kunyoosha mkono kuuliza swali, na alikuwa nyuma, aliamua kupaza sauti gafla, na kusema kuwa, miongoni mwa wagombea wa CCM kuna anayefaa kuongoza kwasababu ni mchapa kazi, kijana, na ni Mmasai kama alivyokuwa Sokoine. Ingawa hakutaka kumtaja jina, lakini ilijulikana bayana kuwa kambi iliyokuwa inataka kujulikana kwa hizo sifa ni ile ya Kikwete na Lowasa. Nyongeza ya Mmasai, iliashiria kuwa mlengwa alikuwa Lowasa.

Ulikuwepo ukimya wa muda mfupi. Hilo halikuwa swali, bali maelezo katika mtindo wa ulopokaji, na aliyeyatoa hayo maelezo hakujitambulisha anatoka chombo gani cha habari. Katika hali ya kawaida, mwalimu alikuwa hajibu maelezo ya namna hiyo. Kwa mshangao, Mwalimu hakuuliza jina la mtu mwenye hizo sifa, bali aliamua kutoa maelezo mafupi yaliyoashiria kuwa alimfahamu mlengwa, na hakutaka hata kutaja jina lake katika hayo maelezo. Alisema Watanzania watafanya makosa kudhani kuwa wamasai wote ni kama Sokoine. Pamoja na madaraka aliyokuwa nayo, Sokoine alikufa na pair mbili za viatu.

Baada ya mwalimu kutoa hayo maelezo, mwandishi mwingine alinyoosha mkono na kutoa maelezo kuwa watanzania sasa hivi wamechoka kuongozwa na wazee, na wako tayari kuongozwa na vijana. Aliongeza kuwa miongoni mwa wagombea ndani ya CCM, wapo wenye sifa hizo na sura nzuri zenye mvuto wa watu zitakazo irahisishia CCM ushindi dhidi ya tishio la Mrema. Mwalimu alimkatisha huyo mwandishi na kumwambia kuwa hatufanyi posa, bali tunamtafuta Raisi wa nchi. Kama unaona kuna mmojawapo wa wagombea ndani ya CCM ana sura nzuri, basi kanywe naye chai.

Bahati mbaya, mtu kama mimi na wengine ambao ni kizazi chetu, hatukupata nafasi ya kushuhudia kwa macho yetu utendaji kazi wa Sokoine kwa sababu ya umri tuliokuwa nao wakati huo. Ningefurahi kama tungekuwa na vitabu vingi vinavyoelezea maamuzi aliyokuwa akiyafanya Sokoine na mazingira yaliyosukuma hayo maamuzi. Ingekuwa ni hazina kubwa kwa vizazi vijavyo, kama watu waliofanya kazi na Sokoine wangetuandikia vitabu vinavyoonyesha sifa zilizomfanya awe tofauti na viongozi wenzake kwa wakati huo. Kuna kitabu kimoja tu cha maana kuhusu maisha ya Sokoine ambacho kwa mawazo yangu hakitoshi.

Kuna manabii wa uongo wanaotaka kujifananisha na Sokoine ili kukoga nyoyo za watanzania, na kutulaghai sisi ambao hatukubahatika kuona matendo yake. Wasiwasi wangu ni kuwa hawa manabii wataendelea kujitokeza hata siku za usoni. Maneno ya mwalimu katika mikutano miwili na waandishi wa habari niliyoielezea juu, yalikuwa ni bakora ya kuwashushuwa hawa manabii. Ningefurahi kuyaona haya maneno kwenye vitabu vya historia ya nchi yetu.

Kutokana na simulizi za watu waliomjua Sokoine, na kwa kusikia maneno ya Mwalimu ambaye alikuwa mkuu wa Sokoine kikazi, naamini kuwa Sokoine alikuwa miongoni mwa watu wachache waliounganisha cheo, busara, na uongozi katika nafsi ya mtu mmoja. Watu mithiri yake, ni kama Kakakuona, kwa maana kwamba, wanazaliwa mara moja katika miongo kadhaa.
 
Jamani ukweli kuhusu kifo cha Sokoine usemwe maana walioshuhudia wengine wanazeeka na kufa. Tuweke sawa historia, after all hata kama kuna siri kwenye secret files miaka zaidi ya 20 imepita tayari.

Ule uvumi kuwa alikuwa na majeraha ya risasi kifuani uwekwe wazi ,kwa nini dube hakuchukuliwa hatua? kuna tetesi kuwa maelezo ya Dube yalikuwa mwiba kuendelea kuwepo nchini, wanadai yeye alisema baada ya ajali alishuhudia mtu mrefu mweusi akiongozwa na askari ku-escape akitembea mwenyewe na alishangaa kusikia huyo mtu alikufa. Je, waliomuhamisha kwenye gari lingine walifanyaje?

Ni wakati wa kusafisha hali iliyokuwepo, na kama hizi ni imani potofu ziondoke masikioni mwa watu..kwa nini isiundwe tume ili ukweli ujulikane na kama kuna waliotuhumiwa waweze kusafishika if possible?

Nawasilisha!
 
Kama huna sababu mhimu sana inayokuzuia kukusanya habari za marehemu Sokoine na kuziweka kwenye kitabu, basi inafaa ufikirie kuifanya kazi hiyo.

Sababu ya wewe kuwa mdogo wakati huo sio ya msingi. Si lazima uandike peke yako, lakini unaweza kuwa chachu na mshiriki imara kati ya kundi la watu kama akina Mawado mnaoweza kuendesha na kuifanikisha shughuli mhimu kama hiyo.

Baadhi ya matatizo yetu mara nyingi ni haya ya kutegeana. Kumsubiri mtu mwingine afanye.
 
Mwendapole na wengine, mkumbuke kuwa katika Tanzania hakuna kiongozi au mtu anayekufa kwa kifo cha kawaida! Vifo vingi kama siyo vyote hutafutiwa maelezo ya kishirikina au njama!

Wakati Sokoine anakufa kuna watu waliodai kuwa amechukuliwa msukule, na kuna watu hata walidai ati "alionekana" mahali fulani! Hili si kwa viongozi tu hata watu wengi wanapopoteza ndugu zao kitu cha kwanza wanajaribu kutafuta "nini kilimuua". Hapa imani za kishirikina hutana, watu watatafuta nani kalogwa na nani? Nani aliapizwa na nani kabla hajafa na nani alinyoshewa kidole na nani!!

Vifo katika Tanzania ni vitu ambavyo vinatokea kwa sababu ya watu wengine hata kama mtu atakufa kwa Ukimwi watu watasema labda kalogwa! Ukweli wa mambo ni kuwa ajali hutokea na watu hufa hata wawe wamependwa vipi.

Suala la njama za vifo vya viongozi siyo geni kwani tunatarajia kuwa viongozi wana utaratibu mzuri wa kuhakikisha usalama wao. Kwa wale mnaokumbuka maelezo ya jinsi ajali ilivyotokea utaona kwamba ilionekana kuwa kana kwamba Dumisane Dube "alilenga" gari la Waziri Mkuu baada ya kuyapita magari ya usalama yaliyotangulia hadi kulifikia la Waziri Mkuu!
 
Mzee Mwanakijiji,

Nipo mjini hapa nayaona yote LIVE. Na kwa mara ya kwanza nimegundua kuwa pamoja na kwamba Watanzania walio wengi hawafahamu maana halisi ya neno UHURU na matumizi yake, sasa nimekuja gundua kuwa - pia wengi hawafahamu maana halisi ya neno la kibiashara SOKO HURU. Na hii inawafanya wengi kuamini ama kukubali mfumo mzima wa uongozi huu wa -CHUKUA CHAKO MAPEMA - unaoendelea. Brother, sasa hivi ni kweli chukua chako mapema sii CCM, Chadema wala mjomba wake. Lawana hazina nafasi tena maanake Tatanic ndio imeisha jaa maji!...uzalendo ni kuokoa abiria ama kujiokoa mwenyewe lakini sii meli tena. Tanzania hakuna tena Politician ila ni viongozi wafanya biashara.

Kwa mtazamo wa haraka haraka nadiriki kusema kwamba leo hii Tanzania wakulima ni aslimia chini ya 20, wababaishaji 40, Wajasiriamali 10 kati yao asilimia 90 ni ndugu ama jamaa za viongozi ktk taasisi mbali mbali. Kila kampuni kubwa ina mkono wa kiongozi na kila jengo kubwa mijini ama kiwanja kikubwa kina mkono wa kiongozi. Yaani kuna kiongozi ana redio kila mkoa na TV, bob pima mwenyewe!

Sasa Bi. Asha hiii habari sijui anaipokea vipi....

Lakini pamoja na yote hayo jamani TZ ni nchi ya kuchuma....purchasing power ni ndogo sana kwa mtazamo wa kiuhumi lakini bob watu wanafanya matusi ktk matumizi ya anasa....damn nimechokaa!

Watu wana hela kama vile hakuna kesho yaani huwezi kuzungunzia 2/m USd kama ni deal mbele ya wanaume (wenye nazo).

Wanabodi, tutazungumza zaidi nikirudi huko kwenye nyenzo za uhakika ili nikamilishe lile hoja nililoacha kiporo na kifupi nitasema kwamba SIDHANI kama TZ itakuja kujikwamua kiuchumi kama nchi hivi karibuni... Gonjwa hili limeisha kuwa sugu halina dawa tena. Siii kisayansi, Kisiasa wala kwa kupitia kamati za ufundi.

Join the Club!
 
Family friend wangu mmoja ambaye alikuwa waziri ktk awamu ya kwanza na ya pili amenisimulia visa vifuatavyo kuhusu Marehemu Sokoine;

Anasema Marehemu Mwalimu Nyerere alikuwa na tabia kuna siku akifanya kazi sana asubuhi mchana akienda lunch huwa analala kidogo kabla hajarudi Ikulu kuendelea na kazi. Kuna siku ilitokea dharura ya kikazi na Marehemu Sokoine akiwa ni PM alitaka maelekezo ya Mwalimu. Akapiga siku akaambiwa Mwalimu kapumzika kidogo, akasema muamsheni, Mwalimu akaamshwa tatizo likatatuliwa.

Anaendelea kusema huyu Bwana alikuwa mfuatiliaji SANA ktk utendaji wa kazi, alinipa mfano Sokoine alipokuwa PM alimwita waziri wa ulinzi ampe update ya silaha zilizopo katika makambi mbalimbali ya jeshi. Siku ya pili bila waziri kujua, Sokoine akawa anapiga simu kwa wakuu wa vikosi mwenyewe wampe data kazi ambayo imemchukua siku moja tu. Baada ya wiki 2 waziri anakuja na "update" yake na anakuta tayari mwenzie anayo na la kushangaza iliyo sahihi zaidi!

He was true leader, big loss to the nation.
 
Ukweli wa mambo kuhusu kifo cha Sokoine,haujulikani,lakini kuna Tetesi ambazo sikudhani kama ilikuwa muhimu kupuuzwa kwamba Sokoine ameuwawa.Katika msafara wake kulikuwa na magari matatu yaliyotangulia,yalivukwa magari mawili na lile la tatu lilijaribu kulikinga gari la marehemu bila mafanikio,sasa kwa hesabu za haraka haraka ni rahisi kupata wazo kwamba kulikuwa na mkono wa Mtu! na ukizingatia kipindi hichi ndio kile cha kuwabana Wahujumu Uchumi.

Tetesi za kwamba Sokoine ameuwawa zilienea na kulikuwa na uvumi pia kwamba wakati wa jioni alikuwa anaonekana ktk viwanja vya Bunge la zamani Karimjee Hall (Dar).Mwalimu alihutubia Taifa mahsusi kuhusu tetesi hizo,na alitoa maelezo kwamba "Mpendwa Sokoine amekufa kwa amri ya Mwenyezi Mungu" na hataki kusikia uvumi wowote kuhusu kifo chake! na atakayebainika kuvumisha mambo hayo atamfunga!Huo ndio ulikuwa mwisho wa Tetesi hizo!.

Kwa wale wenye wazo la kuandika kitabu ni vyema,kwani ndio itakuwa njia sahihi ya kumuenzi Mzee Sokoine vinginevyo Historia itamsahau mapema!.Katika uandishi wako jaribu kumtafuta Mzee Philemon Mgaya na Hans Kitine wana hadithi nzuri itakayorutubisha kitabu hicho.

Dada Asha naomba uondoe maneno yako ya kumfananisha Moringe na Ngoyayi ni watu tofauti.Kumbuka maneno ya Mwalimu kwamba "wamasai wote sio kama Sokoine"!Kiona mbali cha Mwalimu kilikuwa kinafanya kazi vizuri,kwani Lowasa aliyekuwa anamzungumzia wakati huo alikuwa msafi! Sio huyu wa leo aliyejaa tope mwili mzima!!Namkumbuka Mwalimu kwani aliwahi kusema kuwa "angalieni sana vijana wenye sura za Mama zao,wanapendeka/za lakini ni wajanja wajanja na wahuni tu!,hawana cha maana cha kutueleza",alisema hayo alipowafukuza viongozi walioanzisha mgomo kule Sokoine University - Morogoro.Leo hii naona tena kigezo cha Sura kinatumiwa kuwapa watu Uongozi wa Nchi!!
 
Mwawado,
Tulipuuza tahadhari ya Mwalimu angalia aina ya uongozi tulio nao leo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…