Tunaitaka Tanganyika yetu! Wakati ni huu...

Wadau,

Baada ya CCM kushindwa na nguvu ya mageuzi ya kudai uwepo wa KATIBA MPYA ya wananchi(tofauti na ile ya 1977 ambayo ilitengenezwa na wachache kwa niaba ya Watanzania) hatimaye mchakato wa kupata KATIBA mpya ukaanza.

Baada ya patashika nguo kuchanika hatimaye rasimu zikaanza kutengenezwa na mabaraza kupatikana. Mwisho wa yote wajumbe wakapatikana(kundi la 201 na wale wabunge wa bunge la JMT na BWZ).

Bunge Maalumu la Katiba likazinduliwa na Mh rais wa JMT na tukayasikia tuliyoyasikia na mijadala mizito yenye mashiko ikaanza Ndani ya Bunge na NJE ya Bunge.

suala la Muundo wa serikali likabeba kwa kiasi kikubwa hisia za watanzania wengi.Ikatokea hata wajuzi wa mambo kuhoji uhalali wa muungano ulioisshi miaka Hamsini.

Baada ya mvutano mkubwa yakatokea makundi mawili UKAWA na "INTARAHAMWE". Kundi la UKAWA likaona lina buruzwa na kuja kwa wananchi kutoa kilio chao na hao wengine wakabaki na kuendelea na vikao.

Katika vikao vya UKAWA hoja ya ujio wa TANGANYIKA ukaonekana kushika kasi.

Mie mleta hoja nawauliza wanabodi:
1: Tanganyika ikirudi je na chama chetu cha TANU ambacho kiliipigania Tanganyika huru na chenyewe KITARUDI?
2: Kama hakitarudi je, misingi yake itabebwa na chama gani kati ya hivi vilivyopo;CCM,CHADEMA, CUF,UMD,NCCR,ACT
TLP nk?
3: Kama kitarudi kipo tayari kuongoza nchi nje ya malengo na itikadi yake ya Ujamaa na Kujitegemea?

Naomba kufungua mjadala.

cc Mchambuzi Nguruvi3, Tumaini Makene, Ritz, Mwigulu Nchemba MSALANI, @Dr Kitila Mkumbo, kababu
 
Kaka sasa hivi ni TZ kwanza habari ya vyama baadaye. Shime tushirikiane kwa lengo la kujenga na tuache siasa za Uvyama ili tuijenge Nchi. Hivyo vyama siyo pepo bali ni moto kama vitatumika kunyonya maslahi ya wengi. Nadhani swali lako sintaweza kulijibu kwa kuwa mimi msimamo wangu ni Tz kwanza vyama baadaye.
 
Hivi Chama cha TANU kinarudishwaje jamani? Yaani watu badala ya kufikiria kusonga mbele tunafikiri kurudi nyuma!
 
Hilo jina Tanzania asili yake ni Tanganyika si Zanzibar jina alipendekeza Nyerere hivyo Sidhani Kama kuna shida kuitwa majina yote mawili yaani Tanzania aka Tanganyika . Cha Msingi ni Hawa Watu Milion 44 kupelekeshwa na Watu Milion 1.5 tu kama Nyumbu , Zanzibar imewageuza Tanganyika Ndondocha .
Mkuu, maneno yako nimakali kuyasikia. Ila lazima Tanganyika yetu ipatikane.
 
Ni ile tunayoisherehekea tarehe 09/12 kila mwaka................
Ni kiini macho, hebu tazama maudhuiyote ya sherehe hizo na upime uzani wa kumbukumbu za Muungano, katu huwa haitajwi Tanganyika au ule uwanja wa Taifa/Uhuru upande mmoja uwe ni wananchi toka Zanzibar na mwingine uwe ni wananchi toka Tanganyika (iwe hadharani).
 
Tanganyika ni buzi la Zanzibar wanachunwa mpaka ngozi hawajitambui ! Watanganyika wamegeuzwa ndondocha na wazenji !
Haya maneno makali, ila Watanganyika tupo na ndio maana tunaililia.
 
Tambua pesa inayopelekwa Zanzibar ni Matirioni na matirioni hizo Fedha zikisalia Tanganyika Uchumi utakuwa kwa kasi huduma za jamii zitaimarishwa japo kuna ufisadi lakini si kigezo cha kuwazuia Watanganyika wasidai Nchi Yao
Nakuunga kwa ulilonena hapa.
 
Wanabodi!!!

  1. Unawachukua wabunge 80 toka Visiwani (kwa miaka50!) wanakaa Dodoma wanajadili Barabara za Geita na Katavi. Unawalipa msharahakila mwezi na posho kwa kodi toka Tanganyika!
  2. Unammchukua Makamu wa Raisi, Mawaziri, Mabalozi na 20% ya wafanyakzi wa Wizara za Muungano toka visiwani.. kisha unawalipa mishahara na posho (kwa miaka 50!) kwa kodi za Watanganyika!
  3. Tunajuinga na Afrika Mashariki. Bara wanalipia pesa ya kodi gharama za Afrika Mashariki.. Wabunge ni 9 kama walivyo wabunge toka Rwanda (9), Kenya (9). Then!!!!! Tanyanyika inatoa Wabunge (6) Na Visiwan iwabunge (3). Then Bara kwa kodi zao unawalipia wabunge wa Visiwani katika Bungela Afrika Mashariki!!!
  4. Unawateua wabunge toka Visiwani kamati za Bunge Muungano kukagua barabara kule Ngara na Tandahimba unawalipa pesa ya kodi ya Tanganyika kwa miaka 50!
  5. Halafu unakaa unajivuna Muungano huu ni waKuigwa Bara la Afrika na Dunia yote na unajipiga2 kifua kuwa na fikra sahii za waasisi wa Taifa hili!
  6. Miaka 50! Wewe unakuwa rafiki au mshirika wangu!Siku zote tukionana mimi nakununulia tu soda au bia wewe.. wewe hata siku mojahaununui… na unaona ni poa tu! Kwa mika 50!
  7. Halafu watoto wetu wa shule kule Handeni naKondoa wanakaa Chini hawana madawati na tunalalamika na kuona ni sawa!
SAA INGINE NAONA KAMA TANGANYIKA AU TANZANIA BARA TUMEROGWA AND WE ACTUALLY DO NOT KNOW OUR PRIORITIES!
WATOTO NA WAJUKUU ZETU WATAULIZA SIKU MOJA NA HATUTAKUWA NAMAJIBU!

WATANGAYIKA TUAMKE TUACHE UNAFIKI HUU!
Brilliant input, umenena vema sana mkuu.
 
Muungano upo ICU umebakia kofia tu ,Maana Zanzibar ana Katiba yake,wimbo,bendera zake sasa wanaandaa Sarafu zao ,Ardhi ni Mali yoa peke yao si ya Muungano ,Hawalipii Gharama za kuhudumia muungano,anayeng'ang'ania muungano kwa njia ya Kujipendekeza ni Tanganyika tu ! Kwani Zanzibar wamefanya Visa vingi wazi wazi ili Ndoa ivunjike lakini Tanganyika wameziba masikio na kufumba macho wanaubembeleza Muungano kwa Mamilioni ya fedha huku Huduma za jamii zakidumaa.. Tambua huu muungano kwa sasa hauna Faida kwa Tanganyika anayefaidika na matunda ya muungano ni Zanzibar .
Inadaiwa Muungano unang'ang'aniwa kwa sababu za kiusalama tu.
 
Hakuna maneno yanayonitia kinyaa km "uhuru wa Tanzania bara"...najiuliza hii ndo nchi gani?na ilipata huo uhuru toka kwa nani?...ya kwangu mm ni TANGANYIKA tu full stop!...
...ooh Tanganyika,Tanganyika nakupenda kwa moyo wote
Tanganyika,Tanganyika jina lako ni tamu sana!
Well said comrade.
 
Unachotakiwa kujua kuwa Tanganyika ipo..ndo maana kuna mambo yasiyokuwa na muungani kama umewahi kushughulika na mambo ya viwanja utaona mhuri unaopigwa ni watanganyika, Tanganyika ipo kwny kivuli cha serikali ya muungano
 
Wakuu, Kama mtu akiuliza Tanzania Ni zao la Muungano wa nchi mbili yani Zanzibar na Tanganyika, je Tanganyika iko wapi? Mbona haipo Kama Zanzibar? Mbona Muungano umekaa Kama vile Ni Muungano wa Tanzania na Zanzibar, huku Zanzibar ipo Kama state?

Zanzibar ina serikali yake,, ina Bunge lake, ina mahakamani yake, Mbona Tanganyika Haina mihimili hiyo muhimu na haijulikani iko wapi kikatiba?

Wakuu,, Tanyanyika ya watanganyika iko wap kikatiba?

Watanganyika wote tutoane tongotongo, huu ni Muungano kati ya Tanganyika na Zanzibar au Tanzania na Zanzibar??
 
Ccm wanajitahidi sana kupotosha. Muungano ni kati ya Tanganyika na Zanzibar! Na siyo Tanzania Bara na Zanzibar.
 
Back
Top Bottom