Steven Joel Ntamusano
JF-Expert Member
- Jun 17, 2023
- 8,787
- 5,536
Kigwangallah alikuwa na miaka 40 mwaka ule, sidhani kama kipengele hicho kina umuhimu sana.Kama ni kweli ilikuwaje akajitosa kugombea urais 2015 wakati hakuwa amefikisha miaka 42?
Kigwangallah alikuwa na miaka 40 mwaka ule, sidhani kama kipengele hicho kina umuhimu sana.Kama ni kweli ilikuwaje akajitosa kugombea urais 2015 wakati hakuwa amefikisha miaka 42?
Hakina umuhimu kwakuwa kinavunjwa na ccm. Je umri sahihi wa kugombea urais ni miaka mingapi au unaweza kugombea hata ukiwa na miaka 30?Kigwangallah alikuwa na miaka 40 mwaka ule, sidhani kama kipengele hicho kina umuhimu sana.
Kaka nikwambie kitu. Yale mauaji hayakuwa na namna ya kuyazuia. Na hakuna Rais duniani hata angekuwemo na TAL ambaye angeweza kuyazuia. Hakuna dola ambayo itaachia kakundi kadogo ka watu kaharibu mali na maisha ya wengi. Serikali ya aina hiyo ni dhaifu kupindukia; haiaminiki na haiheshimiki na haikubaliki. Tanzania tuna sleeper cells (sleeper agents) za wakoloni wetu wa zamani waliondoka hapa kishingo upande. Hakuna nchi ambayo haina sleeper cells za mabeberu, wanasubiri muda muafaka tu waziactivate.Kama ingekuwa watu wanaokotwa kirahisi hivyo, usingeona mauji kama yale ya juzi. Zama zikishapita zimepita boss.
Hujajibu kitu, huyu kijana ni mzalendo kwelikweli, na bahati mbaya sana Rais lazima awe mmoja tu kwa kipindi cha miaka 5 hadi 10. Tumtengeneze ili afae kuwa Rais wetu 2030-40. Kama anayo mapungufu wakati ni huu wa kumrekebisha.Zina tofauti gani na mropokaji mwegulue? Kumbe ni garbage mnajua na mnampigia debe! Yani unajibiwa unavyokuja kijana
Miaka 40 umri sahihi wa kugombea, Mwigulu mwaka 2015 alikuwa na miaka 41.Hakina umuhimu kwakuwa kinavunjwa na ccm. Je umri sahihi wa kugombea urais ni miaka mingapi au unaweza kugombea hata ukiwa na miaka 30?
2030 atakuwa na miaka 55 umri sahihi wa kuanza kuongoza nchi.Hujajibu kitu, huyu kijana ni mzalendo kwelikweli, na bahati mbaya sana Rais lazima awe mmoja tu kwa kipindi cha miaka 5 hadi 10. Tumtengeneze ili afae kuwa Rais wetu 2030-40. Kama anayo mapungufu wakati ni huu wa kumrekebisha.
Huyu anazo sifa zifuatazo:
1. Anatoka katikati kabisa ya nchi. Hii inaondoa uwezekano wa kupata Rais ambae ana changachenga za utaifa mwingine kama Malawi, Zambia, Burundi, Uganda, Mkenya, Mnyarwanda au Msumbiji kutoka na geografia ya nchi yetu.
2. Ana uzoefu wa kuitumikia serikali katika nafasi mbalimbali. Sifa hii ni muhimu sana kwakuwa akifika Ikulu anaanza kazi moja kwa moja.
3. Ni msomi mchumi. Dunia ya sasa inaongelea uchumi kuliko majigambo mengine
4. Hana kashfa mpaka sasa hapa alipo pamoja na kuwa waziri wa fedha kwa miaka mingi. Angekuwa ametoka makabila yale tunayoyajua angeshakuwa na kashifa nyingi za ufisadi.
5. Anatoka kabila ambalo hawapendani wala kusaidiana wenyewewe kwa wenyewe: Wanyiramba hawaitani ofisini bwana, kila mtu na lwake. Hii itasaidia kuepusha ukabila katika teuzi.
6. Sio mwisilamu wala mkatoliki: Tanzania itapata flava nyingine kabisa ya uongozi ambayo haijawahi kutokea pale Ikulu. Tumezoea waislamu na wakatoliki pale Ikulu kama vile wao ndio wenye hakimiliki wa mjengo ule. Hebu tujaribu wasabato, waluteri, waanglikana, wahindu, wapagani, nk pia, kwakuwa nao ni watanzania kamili.
7. Umri wake ni wa kati kwa kati, sio kijana sana na sio mzee sana. Ataendana na kasi ya vijana na wazee pia kwa wakati mmoja.
Dunia nzima inashindana kuvutia wawekezaji waje kwenye mataifa yao. Yaani wewe bado unawaza watu waendelee kulima kwa vijembe vya mkono, kuvua kwa madau na ndoana na kuchimba madini kwa sululu. Duniani kodo faida ya wawekezaji iko kwenye kutoa ajira kwa wazawa na kulipa kodi, finito. Tunahitaji wawekezaji wenye mitaji na teknolojia kwenye kilimo cha mashamba makubwa ili watu wetu wenye elimu ya chini na kati wapate ajira huko. Ni mjinga tu na mchunga ng,ombe ana question bandari kukodishwa kwa wenye mitaji, utaalam, uzoefu na teknolojia kubwa.Ni katika kipindi chake kodi na madeni ya nchi yaliongezeka huku mfumuko wa bei ukipanda kiasi cha fedha kudhoofika dhidi ya US dollar..
Hapo hujaongelea privatization ya vitu kama bandari na kuingia mikataba mipya ya madini mfano helium lakini na movement ya wamasai loliondo
Kukusanya na kutoa pesa pekee sio efficiency ya kiuchumi. Tunaangalia factors zote, ni sawa na kusema pati la mtu mmoja mmoja limekua na wakati GDP inakua kwa investment ya mchina na wawekezaji wa nje ambao wengi wanaweka mitaji na faida inaenda kwenye nchi zao.
Hivyo wakati figures zinakua, hazitokuwa na reflection ya maisha ya wananchi kwa ujumla...
Ndio maana nilitamani kujua specific metrics.. Sio tu kusema pesa zimetoka, vipi kuhusu human development index, au tax efficiency, inflation etc
Wanataka bandari tuimiliki ili waendeleze michezo ya upigaji kwenye uendeshaji wa shughuli za kila siku.Dunia nzima inashindana kuvutia wawekezaji waje kwenye mataifa yao. Yaani wewe bado unawaza watu waendelee kulima kwa vijembe vya mkono, kuvua kwa madau na ndoana na kuchimba madini kwa sululu. Duniani kodo faida ya wawekezaji iko kwenye kutoa ajira kwa wazawa na kulipa kodi, finito. Tunahitaji wawekezaji wenye mitaji na teknolojia kwenye kilimo cha mashamba makubwa ili watu wetu wenye elimu ya chini na kati wapate ajira huko. Ni mjinga tu na mchunga ng,ombe ana question bandari kukodishwa kwa wenye mitaji, utaalam, uzoefu na teknolojia kubwa.
Anafaa, lakini sio kama Mwigulu. Nchimbi kila anapopata nafasi ya kusema anataka watu wajue kuwa yeye pia ni Mkatoliki. Sijui hii anaisema kwa kurudiarudia kila wakati kwasababu gani. Tanzania tumeshavuka kwenye makabila na dini zetu, tuko kwenye level ya kuchagua mtu safi atakaeweza kutuvusha kwenye dunia hii ya kiushindani wa uchumi.Nchimbi je
Ninaziona kwake dalili njema za yeye kuwa Rais ajae. Sijui wewe kama huzioni.
View: https://www.youtube.com/live/J_snXwqMPgU?si=9KenaV6X_GGepwnA
Huko ndiko kujiamini kwenyewe. Zamani sisi mwanafunzi wa chuo kikuu tayari alikuwa ni mtu na nusu. Anaweza kumoji hata Rais wa nchi na kupewa majibu ya kina kabisa. Sasa hivi vijana wetu wa vyuo vikuu wanaogopa hata kungulu, hawawezi kujenga hoja wala kujieleza. Eti kijana unadangwangwa na mange kimambi ukachome mwendokasi wako unaokusaidia kwenda kwenye pilika zako, na kweli unaenda kuchoma eti kumkomoa Samia ambae hapandi madaladala.Kama ni kweli ilikuwaje akajitosa kugombea urais 2015 wakati hakuwa amefikisha miaka 42?
Asikwambie mtu, kuna watu wa makabila na madhehebu fulanifulani walijichimbia kwenye bandari zetu wakituhujumu utadhani mali yao. hata ufanye panguapangua ya namna gani pale bandari hawaondoki. Kilio hiki cha bandari sio cha burebure kabisa. Ni ulaji, upigaji na upendeleo uliovurugwavurugwa pale na ujio wa DP world.Wanataka bandari tuimiliki ili waendeleze michezo ya upigaji kwenye uendeshaji wa shughuli za kila siku.
Wanatumia kisingizio cha bandari kumilikiwa na wazalendo kumbe kilicho nyuma yake sio uzalendo bali mipango yao miovu ya kupiga pesa kwa kutegemea madili yanayokuwepo wakati bandari ikiwa chini yetu.
Huyu mama kama ingewezekana tungemuondolea ukomo kwenye Katiba. Sio rahisi kumpata Rais kama huyu tena. Pale Ujerumani wanamkumbuka kwa mengi Counsellor Mama Angela Makel.Hongereni naona wananchi wana raha ambayo hawajawahi ipata tangu uhuru
vyakula bwelele, shilingi ipo imara, kodi kiduchu, biashara zinafanyika kirahisi, viongozi wapo imara kusimamia rasilimali na ustawi wa wananchi wao
Usafiri safiii, afya safiii, kilimo na ufugaji safiii, utalii safiii, elimu safii
Mama mitano tena 🔥🔥
Ww itakuwa ni mzee, au kijana zombie. Watu hao tu ndio wanaweza kuandika huu ujinga ualiondika hapa. Yale mauji yalifanyika ili kulinda kikundi kidogo kukaa madarakani kwa shuruti, na wala sio kulinda amani. Kulinda amani yangetumika maji ya washawasha na mabomu ya machozi.Kaka nikwambie kitu. Yale mauaji hayakuwa na namna ya kuyazuia. Na hakuna Rais duniani hata angekuwemo na TAL ambaye angeweza kuyazuia. Hakuna dola ambayo itaachia kakundi kadogo ka watu kaharibu mali na maisha ya wengi. Serikali ya aina hiyo ni dhaifu kupindukia; haiaminiki na haiheshimiki na haikubaliki. Tanzania tuna sleeper cells (sleeper agents) za wakoloni wetu wa zamani waliondoka hapa kishingo upande. Hakuna nchi ambayo haina sleeper cells za mabeberu, wanasubiri muda muafaka tu waziactivate.
Kumbukeni wananchi, wale wakoloni walikuja kututawala kwa malengo matatu tu ambayo ni kupata rasilimali zetu (malighafi) kwaajili ya viwanda vyao huko kwao, pili, kupata wafanyakazi wa dezo kwaajili ya mashamba, mifugo na viwanda vyao huko walikotoka na kwenye makoloni yao mengine, na tatu, walikuwa wanataka masoko ya kuuzia bidhaa zao walizotengeza kwenye viwanda vyao kwakumia malighafi walizopora kutoka kwetu. Shida zote hizi bado wangali wanazo hadi leo pamoja na kuondoka kwao. Sleeper cells zinatumika kuendelea kuvipata vitu hivi hata baada ya wao kuondoka.
Mbona Jpm alimtimua, amekuja kumrejesha sa100 ?Kama angekuwa hana kitu JPM angeshamtimua
Katiba mpya haizuii taahira kwenda Ikulu. Mbona hata Marekani wametawaliwa na vizee vinavyosinzia na kuanguka hovyo kwenye kadamnasi, na sasa hivi wana kichaa kabisa pale Ikulu. Mfano, wewe unaona TAL anazo akili sawasawa?Makonda aka Bashite kashasema wazi piga uwa garagaza Urais 2030 una muhusu na hakuna wa kumzuia, hayupo.
Ndugu zangu ni hivi bila Katiba mpya tutakuja kutawaliwa na ma taahira.. pole Tanganyika yangu.
Ninaziona kwake dalili njema za yeye kuwa Rais ajae. Sijui wewe kama huzioni.
View: https://www.youtube.com/live/J_snXwqMPgU?si=9KenaV6X_GGepwnA
Duu!! eti wangetumia mabomu ya machozi na maji ya washawasha, una akili timamu wewe? Watu waliotaka kuingia Ikulu kwa nguvu walizuiwa kwa nguvu na watu waliotaka kubakia Ikulu pia. Survival for the fittest. Ni mwehu tu atakaeamini kuwa yale yalikuwa maandamano tu ya amani, tena mwehu kabisa. Yalikuwa ni maandamano ya kutoka wapi kuelekea wapi kudai nini?, nani alikuwa anapelekewa ujumbe wa maandamano yale?. Waandamaji walikusudia kuharibu nini na nini ili ujumbe wao uonekane umefika kule walikotaka ufike?Ww itakuwa ni mzee, au kijana zombie. Watu hao tu ndio wanaweza kuandika huu ujinga ualiondika hapa. Yale mauji yalifanyika ili kulinda kikundi kidogo kukaa madarakani kwa shuruti, na wala sio kulinda amani. Kulinda amani yangetumika maji ya washawasha na mabomu ya machozi.
Halafu mahali nimekuona ww ni mjinga, ni hapo unaposema wazungu bado wanataka vitu toka kwetu. Ni hivi, hakuna chochote wazungu watataka kwenye nchi wakakiosa tena bila kutumia nguvu. Kama huamini nenda kaangalie mikataba yote ya raslimali ni nani wameingia. Kuhusu bidhaa zao hawana muda hata wakuzileta huku maana wanajua sisi ni masikini, hivyo wameacha tuuziwe bidhaa fake toka China, kwani zakwao hatufiki bei. Hivyo unavyosema wanavitaka wanaweza kuvipata hata sasa tena kwa bei cheap. Na bidhaa zetu wananua kwa bei poa kwani hazina ubora. Kuhusu cheap labour sisi ndio tunazamia kwao kusaka maisha.