Tumtengeneze Mwigulu kuwa Rais bora ajae

Tumtengeneze Mwigulu kuwa Rais bora ajae

Kubwa jinga na chawa la Madelu tulizomee kabisa hiloo hilooo.
downloadfile-270.png
 
Kuna mfumo wa kupata wagombea urais hapa nchini. Wakishajulikana ndio kila mtu ampambe mgombea wake. Wa kwangu awe mtu mwenye uwezo wa kututoa katika hii hali ya umaskini, kwa kubadilisha mfumo wa elimu yetu uwe kama wa India au China. Ili ndani ya miaka kadhaa tuwe tunafanya mambo yetu kivyetuvyetu. Mfano tuwe na uwezo wa kutengeneza baiskeli, sahani, vikombe, sindano, nguo nk kwa kutumia rasilimali za hapa nchini!
 
Dalili gani.. Nijuze pia mkuu

Ameshika nafasi nyingi kubwa Tu, kina kitu ameshawahi kufanya cha kuonesha vision, charisma na utendaji kazi wake.

Simaanishi huu wa camera nyingi, namaanisha ule ambao ukisema leo hii wizara ya fedha ipo namna A kwa sababu yake etc
Binafsi simkubali kutokana na tabia za hovyo za sifa na bullying ya watumishi ila kwamba amefanya nini hapo ana Cha kuonesha.

Ni katika nafasi yake kama Waziri wa fedha ambapo uchumi umefanya vizuri sana na ndio kipindi ambacho Serikali imemwaga mabilioni mengi kuliko wakati mwingine wowote.
 
Ccm sio chama cha kizazi hiki. Wajinga wameshaisha, angekuwa rais mzuri kama bado wajinga wangekuwepo. Waziri mkuu anasikiliza kero eti mtu analalamika mke wake anamdharau baada ya kupata ajira, na anasema anaona aibu kwenda kwenye dawati la jinsia, lakini mtu huyo huyo ameweza kusema hadharani kwenye umati aibu anayoiona kwenye dawati la jinsia! Na waziri mkuu wa mchongo anaona kweli anatatua kero.

Kama Mwigulu anapambana na wezi kweli, ripoti ya CAG ipo, na ina ushahidi wa wizi kwa vielelezo. Aache siasa za kitoto.
asikwambie mtu, kazi ya mwanasiasa ni kutatua kero za wananchi hata kama kinafiki tu. Kero iliyotatutuliwa haijali kama imetatuliwa kinafiki au kidhati. Mwanasiasa anaangalia sasa, leo na kesho kwa wakati mmoja. Hata Trump anafanya hivyo, Macron anafanya hivyo, Museven anafanya hivyo nk.
 
Huyu Mwigulu huwa namuona kama hana akili timamu. Aidha ana IQ ndogo au aliwahi kupata ajali ya kichwa
Ubongo wake una struggle hata kutengeneza simple sentences zenye kuleta maana. Ukisikiliza speech zake utajua tu huyu jamaa IQ ni ndogo sana
View attachment 3558565
Wewe mwenye akili timamu umefika wapi? Huyu jamaa ana PhD wewe umesoma hadi wapi? Alishakuwa mfanyakazi wa Benki Kuu, mbunge, waziri wa mambo ya ndani, Katiba, fedha na sasa waziri mkuu katika awamu za Kikwete, Magufuli na sasa Samia. Kama angekuwa mbovu kama Lugola, January, Jaffo, au Nape Mnauye. siangeshapigwa chini?
 
Binafsi simkubali kutokana na tabia za hovyo za sifa na bullying ya watumishi ila kwamba amefanya nini hapo ana Cha kuonesha.

Ni katika nafasi yake kama Waziri wa fedha ambapo uchumi umefanya vizuri sana na ndio kipindi ambacho Serikali imemwaga mabilioni mengi kuliko wakati mwingine wowote.
Yeye ni msomi wa PhD, hana maneno mengi kama yale ya akina kasheku Musukuma ambao wanasema sena ili kufidia elimu ndogo yao.
 
Wewe mwenye akili timamu umefika wapi? Huyu jamaa ana PhD wewe umesoma hadi wapi? Alishakuwa mfanyakazi wa Benki Kuu, mbunge, waziri wa mambo ya ndani, Katiba, fedha na sasa waziri mkuu katika awamu za Kikwete, Magufuli na sasa Samia. Kama angekuwa mbovu kama Lugola, January, Jaffo, au Nape Mnauye. siangeshapigwa chini?
Mimi bado nasoma
Pia unaweza kupata PhD na bado usiwe na akili timamu. Mwigulu ni mfano mzuri tu. Hata wanafunzi wa form 4 wapo wengi wanamzidi kwenye uwezo wa kufikiri
 
Yeye ni msomi wa PhD, hana maneno mengi kama yale ya akina kasheku Musukuma ambao wanasema sena ili kufidia elimu ndogo yao.
Ndio majibu ya Kupenda sifa za camera ,dharau na bullying au?

Ndio sifa za nyie wasomi?
 
Makonda aka Bashite kashasema wazi piga uwa garagaza Urais 2030 una muhusu na hakuna wa kumzuia, hayupo.

Ndugu zangu ni hivi bila Katiba mpya tutakuja kutawaliwa na ma taahira.. pole Tanganyika yangu.
 
Kama angekuwa hana kitu JPM angeshamtimua kama alivyofanya kwa Kange Lugola. Haya makusanyo serikali ya JPM na Samia inayotamba nayo yameletwa na Mwigulu.
Unatamba na makussnyo Kisha unajadili MATUNDU ya vyoo shileni. Seriously unajua unachojadili hapa
 
Ukishakuwa waziri mkuu possibility ya kuwa rais ni ndogo, aliweza mwalimu Nyerere. Kama Salim Ahmed Salim alikosa, itachukua miaka mingi huko mbele kuja kupata rais aliyekuwa PM.
 
Kwani JPM ni nani, au unadhani kila mtu alishoboka na propaganda zake? Makusanyo gani, hayo makusanyo ya kupika figure? Naona mnadhani wote tulitekwa na propaganda za Magufuli, naona Mwigulu anazunguka kufanya kiki za kitoto eti anaiga swaga za Magufuli, akidhani atawachota watu akili.
Makusanyo ni makubwa, wasingetuingiza kwenye nchi zenye uchumi wa kati. Tusingeweza kujenga barabara, reli, meli, mashule, mahospitali, mabwawa ya umeme, na kuhamia Dodoma kama hatuna pesa kabisa. Mbona nchi nyingine hakuna vitu hivi?
 
Back
Top Bottom