Duu!! eti wangetumia mabomu ya machozi na maji ya washawasha, una akili timamu wewe? Watu waliotaka kuingia Ikulu kwa nguvu walizuiwa kwa nguvu na watu waliotaka kubakia Ikulu pia. Survival for the fittest. Ni mwehu tu atakaeamini kuwa yale yalikuwa maandamano tu ya amani, tena mwehu kabisa. Yalikuwa ni maandamano ya kutoka wapi kuelekea wapi kudai nini?, nani alikuwa anapelekewa ujumbe wa maandamano yale?. Waandamaji walikusudia kuharibu nini na nini ili ujumbe wao uonekane umefika kule walikotaka ufike?
Akili yako inaongozwa na mange Kimambi wewe. Akili ambayo inashindwa kutofautisha maandamano na mapinduzi, mali ya umma na mali ya Samia, mali ya serikali na mali ya watu binafsi, mali ya umma na mali ya CCM. Eti watu kama hao tuwakabidhi nchi, over my dead body!!!!