Tumefikaje hapa tulipo?

Tumefikaje hapa tulipo?

Hakuwa strong! Mbona mwaka 2015 Kikwete alimfuta Lowasa, ni vivyo hivyo Mkapa angeweza kumfuta Kikwete na timu yake yote!
Kikwete alikuwa ana mgombea wake amemuandaa mwenye ushawishi pia, hilo lilichangia kumfuta Lowassa.

Kulikuwa na kundi kubwa lenye nguvu ikiwemo wakongwe wa Ccm waliokuwa hawamtaki Lowassa hilo pia lilichangia..

Mkapa pia alionekana kuwa na nguvu ya ushawishi kuamua nani awe mgombea Urais wa Ccm mwaka 2015, hilo lilichangia Lowassa kufutwa.

Mwaka 2005 mazingira kama ya 2015 hayakuwepo na kama yalikuwepo yalikuwa dhaifu mno kumfanya Mkapa kumfuta JK.

Mtandao wa Mwaka 2005 ulikuwa hatari mno na athari zake mpaka leo tunaziishi.
 
Nimalizie kwa kusema hivi. Katika ule mchoro alouweka Profesa Shivji ni muhimu sana Wananchi tuelewe jambo moja muhimu sana. Ya kwamba sisi tuna WAJIBU kama Wananchi na ndio maana zipo sehemu mbili. Sehemu ya Wananchi akaeleza mambo matatu ambayo ni UHURU, UTU na USALAMA.

Haya mambo matatu, ni YETU sisi wananchi kuyalinda, tusiyatazame hayo kama ni WAJIBU wa UTAWALA bali wetu sisi Wananchi na nimeona kuna baadhi yetu tunadhani ni wajibu wa Utawala kutuhakikishia sisi Uhuru, Utu na Usalama.

Sasa ikiwa wewe mwananchi unashindwa kuulindwa Uhuru wa watu wengine, huthamini UTU wa wenzako wala Usalama wa jamii haukuhusu hii bila shaka hata Utawala utaongozwa na watu wenye akili hizo, wasiothamini misingi hiyo kwa sababu wametokana baina yetu (Wananchi). Matokeo yake hata misingi yao ya Utawala waiwezi kuwaongoza watu wasiojali misingi ya UTU wao.

Hivyo basi Watawala wanatumia mamlaka yao tulowakabidhi kuendelea na mazoea walokuzwa nayo Uraiani kutothamini wala kuheshimu misingi ya UTU wetu sote. Mamlaka alokabidhiwa ni rungu kupambana na watu wa aina yake mwenyewe.

Natamani sana somo hili lingefundishwa shuleni, vyuoni na hata vyama vyote vya Siasa ili kujenga foundation ya vijana wa kesho ili misingi hii iwe ndio mila na utamaduni wetu.

- Mtoto Umleavyo Ndivyo Akuavyo.
 
Uchaguzi wa Mwaka 2005 ndio uliopanda siasa mpya za nchi hii. Matokeo mengine yote mbegu ilianzia pale na mnakumbuka pia 2010 JK alivyosaka kura kwa kusaidiwa na familia! Kila uchaguzi umekuwa chanzo cha mipasuko na kuzaa makundi yanayohujumiana. Uchaguzi wa 2025 ilikuwa kilele cha matatizo ya muda mrefu. Kuelekea 2030 kama tusiporudi kwenye misingi tutaingia nchi kwenye matatizo yaliyopo Congo.

Kama wataendelea kuwasikiliza akina Wassira, Butiku na Kabudi. Hii nchi tutaizika rasmi 2030. Hawa wazee wanajari matumbo yao kuliko nchi.
 
Nimemsikiliza mzee wangu Butiku, yeye nu tafsiri halisi ya kile nilichoandika.ana Chuki na Chadema ni Maadui zake, hivyo hivyi kibaya zaidi hata Chadema mtu yeyite bdani ya CCM ni adui yao. Sababubsio Itikadi wala sera bali Chama.

Samahani Chukulia Magufuli ambae aliiba itikadi na Sera za Chadema mwaka 2015 lakini yeye ndite akawa Adui wa Chadema toka anaapishwa! Halafu Chadem walokuwa wakipinha Ufisadi wakamchukua Lowassa na kumoa sifa zote!

Yote haya ni kutazamwa fursa za kuingia Ikulu hapakuwa na Siasa safi wala Uzalendo kwa nchi yetu. ACT wanaojiita Wajamaa na Wazalendo leo wanapigania Uzanzibar! Tena kibaya zaidi wanarudisha siasa za Hizbu ambazo zilipigwa marufuku baada ya Mapinduzi.
Swali kwako, ufisadi wa Lowasa ulithibitika au ilibakia kuwa maneno tu??

Pia kwanini unazunguuka sana mbuyu na kushindwa kusema viongozi wa ccm ndio wametufikisha hapa tulipo??

Nakubaliana kabisa na wewe khs mmomonyoko wa maadili kwa viongozi hasa kwy kujilimbikizia mali na ccm kuachana na suala la maadili ya uongozi.
Hicho ndio chanzo cha minyukano na dharau ndani ya ccm, kisha wakatoka nje na kufanya watakavyo bila kujali wananchi ndio wenye nchi.
 
Swali kwako, ufisadi wa Lowasa ulithibitika au ilibakia kuwa maneno tu??

Pia kwanini unazunguuka sana mbuyu na kushindwa kusema viongozi wa ccm ndio wametufikisha hapa tulipo??

Nakubaliana kabisa na wewe khs mmomonyoko wa maadili kwa viongozi hasa kwy kujilimbikizia mali na ccm kuachana na suala la maadili ya uongozi.
Hicho ndio chanzo cha minyukano na dharau ndani ya ccm, kisha wakatoka nje na kufanya watakavyo bila kujali wananchi ndio wenye nchi.
Ushahidi wa Lowassa waulize Chadema maana Dr.Slaa alimtaja 2007! Halafu ndugu yangu kuna kesi gani ya Ufisadi wa viongozi ambayo wewe unaijua ilithibitishwa?

Maswali mengine bana khaaa!
 
Uchaguzi wa Mwaka 2005 ndio uliopanda siasa mpya za nchi hii. Matokeo mengine yote mbegu ilianzia pale na mnakumbuka pia 2010 JK alivyosaka kura kwa kusaidiwa na familia! Kila uchaguzi umekuwa chanzo cha mipasuko na kuzaa makundi yanayohujumiana. Uchaguzi wa 2025 ilikuwa kilele cha matatizo ya muda mrefu. Kuelekea 2030 kama tusiporudi kwenye misingi tutaingia nchi kwenye matatizo yaliyopo Congo.

And what we see is the beginning of the end of 2005 legacy . Mtoto wa mjini style na ujanja ujanja wake, umefeli. Imebakia kutumia nguvu na kutapatapa. Kuzima watu wasikiri.

The power behind 2005 culmination, combined very ambitious people,, with the appetite and desire to get rich quickly. In the process, they have not been able to produce the rightful successors of the throne.

Hapa tulipo tuna changamoto sio za kitoto. Udini umeshamiri kweli kweli. Maadili ya utumishi wa umma yamepungua. Kutokujari na kutiowajibika ndio imekuwa fashion.

Mwenye macho haambiwi ona....tumeanza kukwama kidogo kidogo. Hatutaweza kuendelea mbele tukiwa isolated au kama tumekuwa kisiwa
 
Swali kwako, ufisadi wa Lowasa ulithibitika au ilibakia kuwa maneno tu??

Pia kwanini unazunguuka sana mbuyu na kushindwa kusema viongozi wa ccm ndio wametufikisha hapa tulipo??

Nakubaliana kabisa na wewe khs mmomonyoko wa maadili kwa viongozi hasa kwy kujilimbikizia mali na ccm kuachana na suala la maadili ya uongozi.
Hicho ndio chanzo cha minyukano na dharau ndani ya ccm, kisha wakatoka nje na kufanya watakavyo bila kujali wananchi ndio wenye nchi.

Sio siku nyingi wataparurana mpaka waite maji mmma 😂 😂 😂 😂 . Wanabadilisha spe taili tu..zile kuuukuu
 
Back
Top Bottom