Tumefikaje hapa tulipo?

Tumefikaje hapa tulipo?

Lakini hiyo ya "kugeuza kibao" haikuwa sababu ya kuwaua watu wa CHADEMA.

Sasa iwepo hofu au isiwepo, ni jukumu la waTanzania wasiokubaliana na upuuzi huu kuwakataa na kuwaondoa kwa njia zozote zitakazowezekana..
Na kwa vile wanayo hofu tayari, maana yake ni kwamba kuua ndiyo njia pekee waliyobaki nayo kuendelea kuwa madarakani.
Hawana njia nyingine hawana ushawishi kwa wananchi wanaenda enda tu wamechoka sana aibu kwao ni kubwa na kinachowaweka hadi saivi ni kulinda mali zao za wizi
 
Mkuu wangu mimi nasikiliza sana Hotuba za Viongozi wote. Labda nikeambie tunkwamba wote hutumia neno hao MAADUI ZETU kama ni Upinzani. Huamini nitazieeka hapa.
Umeulizwa swali rahisi tu. Toa mifano ya "matendo ya kikatili", ya kuharibu UTU wa wanaCCM uliofanywa na hao CHADEMA kwa "adui zao" CCM.
"Neno "adui" katika maswala ya kisiasa unalitafsiri vipi kuwa kusigina UTU wa mtu mwingine?
 
Mkuu wangu, ukiwa Kiongozi ikiwa mabadiliko mnayoyataka hayaendani na fursa nilizonazo unategrmea nani atakubali?

Kumbuka Bunge la Katiba lilivunjika kwa sababu pande mbili hazikuafikiana na ukitazama sababu zenyewe tunarudi pale pale hoja zote hazikuzingatia UTU wetu bali tofauti zetu - Tuliishia Patupu.
Acha upotoshaji usio na tija, bunge maalum la katiba halikuvunjika bali lilienda hadi mwisho, ikapatikana katiba pendekezwa iliyokuwa inasubiri kura ya maoni. Ila alipoingia Magufuli akasema hakuahidi katiba mpya kwenye kampeni zake. Sema kundi la Ukawa liligomea kuendelea na bunge lile, baada ya kuona wabunge wa ccm wakichezea maoni ya wananchi yaliyokuwa kwenye rasimu ya Warioba.
 
Mada hii ni swali:
"Tumefikaje Hapa tulipo".

Kama wewe siyo mtu unayependa majibu ya mizunguko mingi na unafiki chungu nzima ndani yake, swali hili ni rahisi tu.

Kwamba wakati uliwadia, na fursa ikajitengeneza kwa kundi ambalo siku zote limekuwepo likiwa na madai yake maalum, limetumia fursa hiyo (seized the moment) kujinyanyua.

Sasa kuna ugumu gani hapo kuelewa!
 
Hivi ilikuwaje Zanzibar wakaandika katiba yao 1984 yenye kuifanya Zanzibar huru bila Tanganyika kupewa Uhuru,na wasomi pamoja na Mwalimu Nyerere wakaangalia na kuacha hiyo katiba ifanye kazi wakati Tanzania bado ipo?
 
Acha upotoshaji usio na tija, bunge maalum la katiba halikuvunjika bali lilienda hadi mwisho, ikapatikana katiba pendekezwa iliyokuwa inasubiri kura ya maoni. Ila alipoingia Magufuli akasema hakuahidi katiba mpya kwenye kampeni zake. Sema kundi la Ukawa liligomea kuendelea na bunge lile, baada ya kuona wabunge wa ccm wakichezea maoni ya wananchi yaliyokuwa kwenye rasimu ya Warioba.
Magufuli aliandaa ukumbi bila kujuwa sherehe itakuwa vipi, Samia kaleta sherehe iliyosheheni burudani ambazo waTanzania walijisahaulisha kuwa zilikuwepo chinichini miongoni mwao tokea uhuru.
 
Hivi ilikuwaje Zanzibar wakaandika katiba yao 1984 yenye kuifanya Zanzibar huru bila Tanganyika kupewa Uhuru,na wasomi pamoja na Mwalimu Nyerere wakaangalia na kuacha hiyo katiba ifanye kazi wakati Tanzania bado ipo?
Hapana. Utakuwa umechanganya mwaka wa hiyo Katiba ya Zanzibar, na mabadiliko mengine yaliyofuata wakati huo

Haya ya Katiba yalikuja baadae sana wakati wa Kikwete.
 
Nimekuelewa mkuu. Unayo hoja ya msingi.

Sasa tunaomba muongozo wa namna gani tutatekeleza suala la sisi wenyewe kukubali mapungufu yetu kimaadil. Nani anaanza kukubali? Nani anafuata? Nani anasimamia zoezi la kukubali mapungufu? na maswali.mengine ya namna hiyo.

Kisha ni nani atasimamia.kuhakikisha upungufu wa kiamaadili haujitokezi tena? Na anapewa instruments zipi kuhakikisha hili linatekelezeka?

Natanguliza shukrani kwa majibu.
Shukran saana, kwa hoja hii ya msingi kabisa ambayo hata mimi yanipa shida kusema kwa uhakika tunawezaje kutoka hapa.

Hatuwezi kurudisha UTU wetu kwa maandishi kwa sababu hata Katiba hii mnayosema mbovu haifuatwi katika maswala ya msingi kabisa.

Ninewahi tolea mfano HAKI ambayo ipo ndani ya Katika Sura ya kwanza sehemu ya 3 lakini imekiukwa wazi wazi kabisa mpaka tumefikia mauaji ya Watu wasokuwa na hatia na hata walikuwa na hatia utawala ulishindwa kufuata taratibu za Kisheria. Hii yote ni kutokana na kupoteza Heshima na thamani ya UTU wetu badala yake tumeishi kwa Mazoea...

Ukiniuliza mimi nitasema hivi. Hatuwezi kuwa na siku ya maombolezi, siku ya Maridhiano wala Katika Mpya/Mpito pasipo kuwa na - SERIKALI YA MPITO. Tunaipataje?

Sina maana rais apinduliwe au aondolewe kwa nguvu madarakani kwa sababu hatutaki kumwaga zaidi damu za Watanzania na kusababisha uadui mkubwa zaidi isipokuwa dhahiri hatuwezi kifikia muafaka wa aina yeyote Rais akiendelea kuwepo madarakani.

Ataondokaje Madarakani?
- Rais akubali kuwa Bangusilo kwa kulinusuri Taifa hili na manufaa ya wote - AJIUZURU yeye mwenyewe kwa hiari yake akithamini UTU wa Watanzania na Katiba itamlinda. Hakuna njia nyingine salama na yenye baraka kwetu nayoiona mimi.

Tukubali sote hatashtakiwa, atalindwa na mafao yake ataendelea kupata kama marais wengine wastaafu walomtangulia. (It's Win win situation on both sides) Tukumbuke rais ana mamlaka makubwa sana na akikataa hakuna kitakacho fanyika iwe maombolezi, maridhiano wala Katiba Mpya/ya Mpito. Huu ndio Ukweli mchungu.

Kustaafu kwake, Kikatiba kutatupa mwanzo mpya, tutaunda Serikali ya Mpito, tutaweza kuomboleza sote kwa pamoja, tutaweza kufanya maridhiano ya pamoja na sii lazima Uchaguzi Mkuu ufanyike 2030. Ni mpaka pale tumeweza kukamilisha maswala yote ya kutuunganisha Wananchi Upya kama jamii moja ya Watanzania.

Nimeandika haya kama mtazamo na maoni yangu naomba sana isitafsiriwe vinginevyo.

Maasalaam
 
Umeulizwa swali rahisi tu. Toa mifano ya "matendo ya kikatili", ya kuharibu UTU wa wanaCCM uliofanywa na hao CHADEMA kwa "adui zao" CCM.
"Neno "adui" katika maswala ya kisiasa unalitafsiri vipi kuwa kusigina UTU wa mtu mwingine?
Marekani katika siasa zake husema wazi Russia ni Adui zao, wamewahi kuuana? Au kwako wewe Uadui ni vita tu! Hata mauaji ya Wana Chadema mimi sina Ushahidi kuwa ni CCM ila nayasoma. Acha mauaji najua Mbowe leo hii ni Adui wa Chadema hii haifichiki.

Ukiniuliza mimi nitoe Ushahidi utakuwa unanionea ila najua fika UADUI upo kubali usikubali haiondoi mtazamo wangu na hatuwezi fikia muafaka wa aina yeyote ikiwa tutakuwa in denial of the facts..
 
Leo hii nimechukua zaidi ya masaa manne kuwasikiliza viongozi wastaafu, maprofesa na wadau mbali mbali katika mdahalo uloandaliwa na TLS.

Hakika nimejifunza mengi na yanilazimu kuwashukuru sana Mzee wetu Jaji Warioba, Profesa Shivji, Mwanasheria kutoka Kenya, Profesa Tibaijika, viongozi wa vyama vya Siasa na taasisi nyinginezo hususani TLS wenyewe. Wote kwa ujumla wao wamezungumzia mambo muhimu kwa mustakabali wa Taifa letu.

Pamoja na yote yale wameniachia maswali magumu zaidi nimekaa na kujiuliza hivi tatizo hasa lipo wapi? Na tumefika hapa kwa sababu gani?

Kubwa zaidi lilojitokeza kwangu linatokana na hotuba ya Profesa Shivji alipozungumzia Misingi mikuu ya Demokrasia akifafanua juu ya pande mbili yaani upande Wananchi na upande wa Utawala. Na kilichojitokeza wazi kwangu ni Kupotea thamani na heshima ya UTU wetu. UTU ndio kiashiria cha ujenzi na usimamizi wa Uhuru na Usalama.

Taifa letu limepoteza UTU kiasi kwamba Utawala hauthamini wala kuheshimu Wananchi na Wananchi hawawathamini wala kuheshimu Viongozi wake. Haiishi hapo, tumefikia kiasi kwamba Utawala hauheshimu viongozi wenzao na Wananchi hawathamini wala kuheshimu Wananchi wenzao.

Na katika hali hii, Uhuru na Usalama wa wananchi upo hatarini kama ilivyo kwa viongozi wenyewe hawaaminiani wala hawaheshimiani isipokuwa kwa yule mwenye nguvu ya utawala na fedha, hii ndio Tanzania ya leo (status quo)

Swali linakuja tumefikaje hapa? Naamini kila mtu ana mtazamo wake lakini binafsi yangu akili yangu inanambia yote haya yametokana utovu wa nidhamu katika miiko na maadili ya UTU wetu kwa kuiga mifumo ya kigeni ambayo ilidhalilisha mila na tamaduni zetu kama ni misingi ya kale (primitive) ilopitwa na wakati.

Mifumo ya Demokrasia tuloichukua ndio chanzo cha kuharibika kwa misingi ya Demokrasia kupitia mabadiliko ya Katiba ya mwaka 1984 na 1992 upande wa Jamhuri pia Uandishi wa Katiba ya Zanzibar mwaka 1984 na mabadiliko yalofuatia mwaka 2002. Isipokuwa nitaacha pembeni Katiba ya Zanzibar, hii inahitaji mada nyingine tofauti kabisa.

Najua hoja yangu inahitaji mjadala mpana zaidi lakini niseme kwamba mabadiliko haya ndio mwanzo wa matatizo yote yanayofuatia katika miongo tofauti ya Kiutawala kufikia leo hii.

Katika makosa makubwa yalofanyika ni kuondolewa kwa Miiko na Maadili ya Viongozi hivyo kupoteza Sifa zinazotakiwa za viongozi wetu Kitaifa. Kwa nafasi walizokuwa nazo viongozi serikalini, Wabunge na hata majaji wakaanza kumiliki utajiri pasi kuulizwa wamepataje mali na utajiri huo, hii njia panda ndio ikawa mwanzo wa mmomonyoko wa maadili na chachu ya rushwa kuzaliwa.

Jambo la pili lilikuwa ujio mfumo wa Vyama Vingi ambavyo havikuzingatia misingi ya Demokrasia ( Uhuru, Utu na Usalama) bali ilikuwa ni tiketi ya jicho la Uheshimiwa na kuingia Ikulu kutawala (mfumo wa Vyama vingi). Vyama vingi ndivyo viloweka nadharia ya kina nani watakuwa Waheshimiwa kati ya Wananchi wote na hii ikazaa tamaa ya utukufu wa nyadhifa hizo. Hakuna Chama hata kimoja kinachosimamia itikadi na Sera zake wakati wote ila kulingana na fursa zinazojitokeza.

Katika mukhtadha huo tulipoteza Siasa safi za vyama Kiitakadi, hasada ikachukua nafasi baina ya vyama vya Siasa, viongozi kwa viongozi, Wananchi na vyama pinzani na kibaya zaidi rushwa na upendeleo vikatumiwa kama zana katika teuzi toka chaguzi za ndani ya Vyama vya Kisiasa hadi Viongozi wa Kitaifa – Yakaibuka makundi ya timu za Wana, hasada ikazaa Chuki na Uadui matokeo yake UZALENDO kwa Taifa letu UKAPUKUTIKA.

Kwa hiyo tukiacha hoja ya Katiba Mpya pembeni, sisi Watanzania tuna wivu na chuki za kuhasimiana wenyewe kwa sababu ya fursa za madaraka na utajiri zimeletwa kupitia vyama vingi.

Viongozi waliopo madarakani hujiona wapo katika nafasi adimu sana ya Utajiri wa hadhi na mali na wanajua kuna macho ya wivu dhidi yao hata kama wanayofanya nia njema ama kinyume cha misingi ya demokrasia, bado utachikiwa tu. Siasa zetu zimekuwa ni za Ukinzani ambazo kiitikadi hazifanani kabisa na Upinzani kwa nia, dhamira na malengo ya Demokrasia.

Tujiulize wenyewe mpaka hapa tumefika ni viongozi wangapi wameuawa kwa ajali, risasi au sumu na hakuna watu walotiwa hatiani wala kuchukuliwa hatua. Nini hasa sababu za viongozi hao kuuawa? Bila shaka ni kunatokana na UADUI wa kisiasa walojenga dhidi ya kiongozi ama viongozi wengine iwe kwa nia safi au mbaya.

Wivu na Chuki sii lazima vitumike kwa wale washindani tu bali inaweza toka chini kwa wale wanaotaka kufika pale kiongozi alipofika ama kiongozi kulinda maslahi yake dhidi ya wale wanaotaka nafasi yake.

Kwa hiyo tunapozungumzia leo Maombolezi, Maridhiano na sijui Katiba Mpya ni muhimu kwanza sisi wenyewe tukubali mapungufu yetu kimaadili ili TUBADILIKE - Heshima ya Utu wetu na Uzalendo kwa Taifa ni utamaduni ulopitwa na wakati.

Hatuwezi fanya maombolezi ambayo baadhi yetu hawaoni umuhimu wala sababu. Hatuwezi fanya Maridhiano kwa kuwekeana masharti yasiyojali Utu wetu na Uzalendo kwa Taifa hili bali maslahi ya mtu au chama.

M inwisho hatuwezi kuwa na Katiba mpya inayotokana na maoni ya Wananchi wenye wivu, chuki na uadui isipokuwa Katiba lazima iwe ni mwongozo wa Wananchi hao bila kujali tofauti zao - Katiba ni ya Wananchi iheshimiwe na wote.

Maasalaam
Kama mtu umejipachika hakuna atakaye kuheshimu hata ufanyeje!
 
KWANZA KABISA, wafuasi wa CCM watambue na kukubali kuwa chama chao ambacho ni chama dola kimeunda na kulea mfumo wa kiimla (authoritarian) ambao una kasoro za msingi zilizoleta madhara makubwa sana kwa taifa na wananchi kwa ujumla. Ni mfumo ambao umetumika kuongoza nchi hii tangu awamu ya kwanza. Muda wote huo umekuwa ukitegemea utashi wa mtu mmoja, Rais, na kundi lake (inner circle). Mtu mmoja katika kiti cha uRais wa JMT (na uenyekiti wa CCM) amekuwa na mamlaka yote juu la nchi na vyote vilivyomo absolute power.

Ni kukosa uelewa au hila kutaka kulinganisha CCM na vyama huru vya siasa.

Rais (wa CCM) akiwa mwema na mzalendo kwa nchi yake kama alivyokuwa JKN (Nyerere) - benevolent dictator - wananchi wanakuwa na amani na kushiriki shughuli za maendeleo kwa juhudi kubwa. Rais akiruhusu utawala wa sheria na uwazi kama awamu za pili, tatu na nne, angalau watu wanaongea, taasisi zinafanya kazi na taarifa muhimu zinasambaa kiasi chake. Rais akiamua kupuuza katiba, kupuuza utawala wa sheria, kuzuia uwazi na kutawala kwa hofu, vitisho, mateso, udhalilishaji, hata mauaji kwa kutumia vikundi vya mauaji (hit squads), nchi inaingia gizani, unafiki, uchawa, na ujinga (idiocy) vinatamalaki. Hizo ni awamu za 5 & 6.

Endapo, wafuasi wa CCM hawataona hayo kuhusu chama hicho na kukimbilia kujificha kwenye udini, muungano, jinsia, watu fulani fulani (individuals), CHADEMA, n.k., hakika safari itakuwa ndefu sana kuelekea kwenye ufumbuzi.
 
Hakuna sehemu CCM itakwepa hili
Tumefika hapa kwasababu ya CCM
Kila wanayofanya na wanayofikiria kufanya ni kusalia madarakani
Kwasababu tuu inajulikana siku wakikubali mabadiliko ndoutakua mwanzo wa kulipia Yale waliyosababisha ndani ya miaka zaidi ya sitini kwenye nchi ya Tanganyika
 
Hakuna sehemu CCM itakwepa hili
Tumefika hapa kwasababu ya CCM
Kila wanayofanya na wanayofikiria kufanya ni kusalia madarakani
Kwasababu tuu inajulikana siku wakikubali mabadiliko ndoutakua mwanzo wa kulipia Yale waliyosababisha ndani ya miaka zaidi ya sitini kwenye nchi ya Tanganyika

KWANZA KABISA, wafuasi wa CCM watambue na kukubali kuwa chama chao ambacho ni chama dola kimeunda na kulea mfumo wa kiimla (authoritarian) ambao una kasoro za msingi zilizoleta madhara makubwa sana kwa taifa na wananchi kwa ujumla. Ni mfumo ambao umetumika kuongoza nchi hii tangu awamu ya kwanza. Muda wote huo umekuwa ukitegemea utashi wa mtu mmoja, Rais, na kundi lake (inner circle). Mtu mmoja katika kiti cha uRais wa JMT (na uenyekiti wa CCM) amekuwa na mamlaka yote juu la nchi na vyote vilivyomo absolute power.

Ni kukosa uelewa au hila kutaka kulinganisha CCM na vyama huru vya siasa.

Rais (wa CCM) akiwa mwema na mzalendo kwa nchi yake kama alivyokuwa JKN (Nyerere) - benevolent dictator - wananchi wanakuwa na amani na kushiriki shughuli za maendeleo kwa juhudi kubwa. Rais akiruhusu utawala wa sheria na uwazi kama awamu za pili, tatu na nne, angalau watu wanaongea, taasisi zinafanya kazi na taarifa muhimu zinasambaa kiasi chake. Rais akiamua kupuuza katiba, kupuuza utawala wa sheria, kuzuia uwazi na kutawala kwa hofu, vitisho, mateso, udhalilishaji, hata mauaji kwa kutumia vikundi vya mauaji (hit squads), nchi inaingia gizani, unafiki, uchawa, na ujinga (idiocy) vinatamalaki. Hizo ni awamu za 5 & 6.

Endapo, wafuasi wa CCM hawataona hayo kuhusu chama hicho na kukimbilia kujificha kwenye udini, muungano, jinsia, watu fulani fulani (individuals), CHADEMA, n.k., hakika safari itakuwa ndefu sana kuelekea kwenye ufumbuzi.
Nadhani unatazama upande mmoja tu wa sarafu kwa sababu kumbuka Nyerere alipata upinzani mkubwa sana, tena naweza sema ni rais alokoswa koswa sana kupinduliwa kuliko marais wrngine wote. Toka anaapishwa hadi anastaafu ilikuwa sii.shwari.hata kidogo.

Kwa njia za kipekee kabisa Nyerere (dictatorship) aliweza kukomesha Udini na Ukabila ambao ulikuwa ndio Siasa za wakati wake. Aliweza kupambana na walopinga UJAMAA kwa maneno na vitendo toka (1967 - 1984). Haikuwankazi ndogo hata kidogo ilihitaji ujasiri usokuwa na huruma. Baada yake ndio tukashindwa kuendeleza alotuachia. ( Marekebisho ya Katiba 1984) Tukaingizwa shimo la chewa.

2015 Akaja Magufuli ambaye pia alikuwa Dikteta mwema (mtazamo wangu) lakini nae alikutana na Upinzani mkubwa sana mapema tu nje ya chama chake na ndani ya Chama Chake. Sababu kubwa haikuwa Itikadi wala sera zake bali Kiti alichokalia! Mwisho wake sote tunaujua.

Mimi naamini tatizo linaanza na sisi Wenyewe tumepoteza thamani UTU wetu na UZALENDO kwa Taifa. Kumbuka hawa viongozi wote wanatoka miongoni mwetu.

Nina hakika hata wewe unawajua baadhi ya viongozi ambao kablanya madaraka walikuwa karibu na wewe, lakini baada tu ya kupata madaraka hayo walikutenga.

Pengine hata simu yako hapokei tena, umegeuzwa mzigo hata kama kutaki msaada wowote toka kwake. Mimi naamini katika uhalisia huu ( Money and Power) hata akiingia Tundu Lissu madarakani hatatofautiana na viongozi wengine kwa sababu sote NDIVYO TULIVYO.

Nakumbuka Bashite amewahi kusema kitu kama hiki ya kwamba "Hawa wooote wanaopiga kelele ni kwa sababu hawajashika madaraka lakini siku wakiyashika watageuka na wao kama sisi"
Hotuba hiyo ilinipa picha ya Waziri wa ndani alokuwa Chadema leo yupo CCM utadhani sio yule alokuwa Chadema. Tumepoteza UTU kwa kupigania vyeo na maslahi Binafsi.
 
Acha upotoshaji usio na tija, bunge maalum la katiba halikuvunjika bali lilienda hadi mwisho, ikapatikana katiba pendekezwa iliyokuwa inasubiri kura ya maoni. Ila alipoingia Magufuli akasema hakuahidi katiba mpya kwenye kampeni zake. Sema kundi la Ukawa liligomea kuendelea na bunge lile, baada ya kuona wabunge wa ccm wakichezea maoni ya wananchi yaliyokuwa kwenye rasimu ya Warioba.
Kwa hiyo wewe kujitoa kwa wadau wa UKAWA na taasisi nyingine unaamini Katiba ile Pendekezwa ndio ilipata maamuzi halali kabisa ya Bunge lile?

Umewahi wasikia Mzee Warioba na hata Polepole wakizungumzia Katiba Pendekezwa! Umewahi wasikia Wananchi wakizungumzia Katiba Pendekezwa dhidi ya Rasimu ya Katiba? Mimi naamini Bunge lile halikufikia muafaka na hata jana Prof. Tibaijuka kazungumzia.

Yawezekana mimi nina mitazamo tofauti sana na watu wengi hapa na hainishangazi kwa sababu hata zamani nilipokuwa hapa nilipitia Upinzani mkubwa kwa sababu watu wanazumgumza hoja zao kwa hisia za UCHAMA ilihali mimi natazama Uhalisia.
 
Marekani katika siasa zake husema wazi Russia ni Adui zao, wamewahi kuuana? Au kwako wewe Uadui ni vita tu! Hata
Najuwa wewe ni mtu mbishi.
Basi tutajie nchi yoyote yenye vyama pinzani wanaoitana kuwa ni vyama rafiki.

Mkuu 'Mkandara' wewe unajulikana siku zote msimamo wako upo wapi katika haya maswala ya Tanzania. Huna tofauti kubwa sana na 'zealots' wengi humu kama akina Ritz, BIG SHOWW na wengine.
Tofauti yako ni kuwa huwi bayana kama wao. Unajaribu kila uwezavyo kufunika maana ya maandishi yako uonekane upo balanced.; kama utumiaji wa maneno kama "UTU" niliyoyanyanyua hapo mwanzo kabisa.

Kwa ufupi, watu wa aina yako ndio hatari zaidi ya hao wanaojitokeza waziwazi kama hao niliowataja hapo juu.

Sasa wewe nieleze uhasama huu utatatua vipi hali yetu hii inayotukabili, huku watu kama wewe mnafunikafunika uwazi wenu usijulikane.

Halafu unauliza na swali kabisa: Eti "Tumefikafikaje hapa tulipo"?

Kwani hujui?
 
..wamewauwa kwanza.

..halafu ndio wameanza kuogopa kugeuziwa kibao.

..sasa jiulize kwanini waliwauwa wenzao?

..Katiba Mpya na bora haitaruhusu kulipiziana visasi, na kuchukua sheria mkononi.
Mimi nafikiri tuachane kabisa sasa na hili swala la Katiba, ambalo ni wazi Samia na Genge lake wameamua hawawezi kuruhusu bila ya shurti ambayo inaweza kuwa ni ya kuuana.
Jitihada sasa ziwe kuinyanyua Tanganyika.

Muungano na Zanzibar kwa hali tuliyopitia sasa sioni huo muungano ukiwa tulivu.

Muungano umetufikisha pabaya sana, sioni uhitaji wa huu muungan

Sikumbuki kuwahi kuusema muungano huu kwa haya maneno niliyotumia leo.
Kwa hiyo nitajiwekea kumbukumbu.
 
Back
Top Bottom