Tume ya ushindani kuchunguza udhamini wa GSM ligi kuu

FCC wakibariki basi naamini upande wa pili nao wapinzani wa Yanga wataweka mzigo,hapo sasa itakua patashika nguo kuchanika.
Hakuna anayezuiwa kuweka hela kwenye ligi Mkuu,tatizo ni haya mambo ya uSimba na uYanga ndo unaleta kelele zote hizi.

Ukichunguza kwa makini sana,hakuna mahali TFF na GSM wamekosea,ila usumbufu tu.

Hivi kweli kati ya sisi tunaopiga tumba hapa JF na bodi ya ligi,ni nani anazijua sheria na kanuni za mpira!?
 
Ila ukumbuke tofauti iliyopo kati ya GSM na NBC ni milioni 400 tu.
Tena GSM yuko juu coz ni biln 2.1 two years,ilhali NBC ni biln 2.5 miaka mitatu.

So GSM ndo katoa pesa nyingi kuliko mdhamini mkuu kwa kipengele cha muda.
Na GSM si kama alishindwa kuweka pesa zaidi ta NBC,ila akutaka kuipiku yeye ndio main sponsor
 
GSM kafanya kihuni Sana kujaza viongozi wa Yanga siku ya kusaini contract Kama wasemaji wake......Ni bora angetafuta watu wengine kumwakilisha.....maana hao ndio wanaoharibu kuonekana timu ya yanga itakuwa na mgongano wa maslai badala ya GSM Kama kampuni .huo ndio ukiukwaji number moja..

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
Hili kosa kubwa Sana walilifanya....

Yaani Hersi anasimamia usajili Yanga... Baadaye tena anakuja kusaini kudhamini ligi kuu....

Haiingii akilini..

Sent from my TECNO LA7 using JamiiForums mobile app
 
Hakuna anayezuiwa kuweka hela kwenye ligi Mkuu,tatizo ni haya mambo ya uSimba na uYanga ndo unaleta kelele zote hizi.

Ukichunguza kwa makini sana,hakuna mahali TFF na GSM wamekosea,ila usumbufu tu.

Hivi kweli kati ya sisi tunaopiga tumba hapa JF na bodi ya ligi,ni nani anazijua sheria na kanuni za mpira!?
Nakuelewa sana jamaa.
 
nenda kadhamini wewe basi kama hio 2b unaiona ni ndogo
Kwanza tuna nashaka hata hiyo 2b kama ipo kweli au ni siasa tu na ndio maana wamezuia watu wasihoji

Kitendo cha kina manara kupiga picha wakiwa wameshika cheki ambayo hata barcode haina lazima tutilie mashaka

Kipindi mo anatoa bilion 20 mlisema ni uzushi kutokana na cheki kutojitosheleza kuthibitisha pesa imewekwa kweli, sasa mmeenda kurudia kosa lile lile halafu mbaya zaidi hamtakai watu wahoji
 
Uropokaji wa Haji Manara ndiyo umeleta mtafaruku huu wasipomuonya atawaharibia sana Yanga na GSM. Anatamba kuwa kuanzia sasa Simba imeshakuwa mikononi mwa Yanga kupitia GSM.

Sent from my Nokia 5.1 Plus using JamiiForums mobile app
Ni Tanzania tu ndipo uropokaji wa mtu unaweza kushinda sheria!!hayo malalamiko wala hayana mashiko yoyote, na yatatupiliwa mbali!!kwani ni Tz tu ambapo kampuni ina dhamini ligi na ina timu kwenye ligi hiyo?siasa za usimba na uyanga tu na ndio maana soka la nchi hii haliwezi kuendelea.Haya ana kwenda kudhamini ni ligi daraja la kwenza na la pili, mpira wa sasa ni pesa watu hawawezi kuacha pesa kwa kuendekeza siasa zenu za kipuuzi!!hapo kwa GSM, kuwa mdhamini mwenza wa NBC, mgongano wa kimasilahi uko wapi wa kuifanya yanga iwe bingwa?!!
 
Sikuelewi!

Kwani GSM ni ya Hersi?

Ebu angalia utumbo uliouandika
Ha ha haaa hapo umempa za uso kwani makolo wao wamezuiwa kuleta hizo hela zao za familia yamejaa wivu tu sasa wenye hela zao wanaenda kudhamini championship nako lalamikeni tena.
 
Ni dhahiri FCC watatupilia mbali hili swala
1: Mkataba ni kati ya TFF na GSM,
Hakuna uhusiano wa mkataba huu na upangaji wa matokeo

2: GSM hamiliki timu yoyote ya ligi
Ila anadhamini baadhi ya timu na
na udhamini huu ni wa kibiashara

3: GSM wangekua wanataka kupanga matokeo ili yanga achukue ubingwa, wangeweza tu kufanya hivyo tena kwa gharama ndogo isiyofika hata bilioni moja.
Ndio wanaongoza kuhonga waamuzi
 
Hukutilia shaka Azam kuidhamini ligi upande wa haki ya matangazo kwa miaka 10,na bado akasaini tena na Yanga na Simba mkataba mwingine wa zaidi ya bil 34 kwa kila mmoja kwa miaka 10?

Hukutilia shaka Azam kuidhamini ligi kuu upande wa matangazo na bado akalidhamini kombe la shirikisho ilhali na yeye bado ana timu yake huko!?
Wadau wengi wa soka bongo,Wana Imani na kampuni za Azam media ni WaAdiLiFu na wakweli,siyo ile kampuni ya Ji_es_em hawana uhadilifu ktk soka letu la Bongo land.
 
Hukutilia shaka Azam kuidhamini ligi upande wa haki ya matangazo kwa miaka 10,na bado akasaini tena na Yanga na Simba mkataba mwingine wa zaidi ya bil 34 kwa kila mmoja kwa miaka 10?

Hukutilia shaka Azam kuidhamini ligi kuu upande wa matangazo na bado akalidhamini kombe la shirikisho ilhali na yeye bado ana timu yake huko!?

Azam media na Azam FC zina muundo na watu tofauti kabisa wa kiuongozi

Azam media CEO wake ni Tido Mhando wakati Azam FC ni Amin Popat

Pia ukiangalia hata siku TFF wanasign deal na Azam media hakukuwa na kiongozi hata mmoja wa Azam FC

Ila ukiangalia GSM viongozi wake na watendaji wengine ndio wale wale ambao wanajihusisha moja kwa moja na uongozi/maslahi ndani ya Yanga
Pia kauli ya Haji Manara kusema kuwa Vilabu vyote ikiwemo Simba vipo mikononi mwa GSM ni kauli tata sana

Kingine ni kuwa usiri uliopo ktk vipengele vya mkataba wa GSM na TFF unazidi kuleta mashaka na sintofahamu nyingi kwenye mkataba huu

Kwahyo huu udhamini wa GSM ndani ya Yanga na TFF unazua mgongano mkubwa wa kimaslahi

FCC tafadhali chunguzeni hili kwa umakini mkubwa, linahatarisha Afya ya soka letu
 
Ni Tanzania tu ndipo uropokaji wa mtu unaweza kushinda sheria!!hayo malalamiko wala hayana mashiko yoyote, na yatatupiliwa mbali!!kwani ni Tz tu ambapo kampuni ina dhamini ligi na ina timu kwenye ligi hiyo?siasa za usimba na uyanga tu na ndio maana soka la nchi hii haliwezi kuendelea.Haya ana kwenda kudhamini ni ligi daraja la kwenza na la pili, mpira wa sasa ni pesa watu hawawezi kuacha pesa kwa kuendekeza siasa zenu za kipuuzi!!hapo kwa GSM, kuwa mdhamini mwenza wa NBC, mgongano wa kimasilahi uko wapi wa kuifanya yanga iwe bingwa?!!
Mimi sipingi udhamini wa GSM hata kidogo,ila kauli ya msemaji wa Yanga Haji Manara kuikejeli Simba kuwa sasa itakuwa mikononi mwa Yanga kupitia udhamini wa GSM ni kauli yenye ukakasi. GSM na Yanga wangemkana Haji Manara kwa upotoshaji huu.

Sent from my Nokia 5.1 Plus using JamiiForums mobile app
 
Ni Tanzania tu ndipo uropokaji wa mtu unaweza kushinda sheria!!hayo malalamiko wala hayana mashiko yoyote, na yatatupiliwa mbali!!kwani ni Tz tu ambapo kampuni ina dhamini ligi na ina timu kwenye ligi hiyo?siasa za usimba na uyanga tu na ndio maana soka la nchi hii haliwezi kuendelea.Haya ana kwenda kudhamini ni ligi daraja la kwenza na la pili, mpira wa sasa ni pesa watu hawawezi kuacha pesa kwa kuendekeza siasa zenu za kipuuzi!!hapo kwa GSM, kuwa mdhamini mwenza wa NBC, mgongano wa kimasilahi uko wapi wa kuifanya yanga iwe bingwa?!!

Unakataa siasa za Simba na Yanga na wakati huo huo unacomment ukiegemea siasa hizo hizo,kwa comment hii tayari unaonekana wewe ni Yanga lia lia.

Tupe sababu zenye mashiko kwanini Hersi na GSM yake asitiliwe shaka wakati ni muendeshaji (mkuu?) wa Club ya Yanga na wakati huo huo anakimbilia kwenda kusign udhamini wa TFF? Kwanini basi hakuwaachia wengine ndani ya GSM Group kudeal na swala la TFF yeye akabaki na mambo ya Yanga? Ina maana kwa GSM Group yote mtendaji anaeaminika ni Hersi peke yake?
 
Tatizo GSM pia ni viongozi ndani ya Yanga.Hapo ndio tatizo linapoanzia.Hersi atoke kwenye uongozi wa Yanga abakie kama mdhamini.Aachane na kujihusisha na usajili na kadhalika
Hersi ni mwajiriwa na sio mmiliki wa GSM
 
Unakataa siasa za Simba na Yanga na wakati huo huo unacomment ukiegemea siasa hizo hizo,kwa comment hii tayari unaonekana wewe ni Yanga lia lia.

Tupe sababu zenye mashiko kwanini Hersi na GSM yake asitiliwe shaka wakati ni muendeshaji (mkuu?) wa Club ya Yanga na wakati huo huo anakimbilia kwenda kusign udhamini wa TFF? Kwanini basi hakuwaachia wengine ndani ya GSM Group kudeal na swala la TFF yeye akabaki na mambo ya Yanga? Ina maana kwa GSM Group yote mtendaji anaeaminika ni Hersi peke yake?
Hersi naye ni kama zamtanga fulani asiyejielewa, naskia siku ambayo wana sign hilo deal yeye na bumbuli wakamwita pembeni dauda

Dauda akaitikia wito kusikiliza jamaa wana kipi wanataka kushare, wakaanza kusema "ooh unajua yanga ni timu kubwa hapa bongo hakuna club ya kuifananisha nayo, inaweza kufanya chochote"
 
Back
Top Bottom