Tume ya mabadiliko ya katiba

Tume ya mabadiliko ya katiba

Pumbavu kabisa, sasa wewe nani katuma! Tunachotaka ni katiba, sasa udini unatoka wapi! Tunataka andaka biblia au karuani?
 
Kule kwenye thread ya Mzee nimejibu na hapa najibu tena!

Kazi ya tume ni kukusanya maoni, hoja ya msingi sio dini za wajumbe wa hiyo tume bali competences zao!. Upatikanaji wa katiba nzuri, utategemea maoni tunayoyatoa na uwezo wa mkusanyaji kuya compile na sio dini yake!.

Natishwa na "the motive behind" wa hii karata ya udini kwenye tume ya katiba na sasa kuinganisha na suala la IOC na Mahakama ya Kadhi!. Mimi ni Mkisto tena Mkatoliki die hard!, kwenye suala la matumizi ya "protection", nimetofautiana na msimamo wa kanisa langu, vivyo hivyo sina tatizo na Tanzania kujiunga OIC au kuwepo kwa Mahakama ya Kadhi, kwani mahakama hiyo ilikuwepo enzi za mkoloni, mahakama hiyo ipo Zanzibar, Kenya na Uganda!.

Hivyo kitakachoingizwa kwenye katiba mpya hakitokani na wajumbe wengi ni wa imani gani, bali Watanzania waliowengi wanataka nini. Hata kama wajumbe wote 28 wa tume hiyo wangekuwa Wakristu, halamu maoni ya asilimia 30% ya Watanzania wakaitaka mahakama ya kadhi, mahakama hiyo itakuwepo!. Sambamba na suala la uwepo wa muungano, hata kama Wanzanzibari asilimia 99% hawaitaki na asilimia 0.1% tuu ndio wanautaka, muungano utaendelea!.

Kinachohitajika sasa more than anything else ni elimu kwa umma kuhusu zoezi hili!.

Please stop this "udini" nonsense!

Pasco

Mimi ni Muislam lakini sijaridhika na hii tume kwani etatuletea chukidhidi ya ndugu zetu wa kristu kwani waislam tumependelewa sana kuhusu mahaka ya kadhi nivyema tungeachiwa waislamu wenyewe bila kuihusisha serikali isiyofungamana na dini yoyote ile
 
Hoja yasngu hapa siyo kuongelea ubaguzi wa kidini wala nini ila ni kutazama malengo ya kiudini yaliyojificha humu ndani.nafikirei hapa mahakama ya kadhi nchini tanzania inanukia.

tazama team hii hapa chini

angalizo-mimi nimetazama majina yao kuwapanga kidini.

Hata mtei kaandika hivi "Mfano wa pili ni kwamba, licha ya kwamba Tanzania siyo nchi inayozingatia dini katika maamuzi yake ya kisiasa, ni lazima tukubali kuwa madhehebu ya dini yana influence katika mchakato na hatimaye maamuzi. Nikihesabu Waislamu katika hii Tume kwa kuzingatia majina naona zaidi ya theluthi mbili ni Wao. Wengine ni Wakristo au watu wasiokuwa na dini yoyote.
"



wakiristo wapo 11
Waislam wapo 23

WALIOTEUA
1.Rais Kikwete -Mwislam
2.Rais Shein---Mwislam


1. Mhe. Jaji Joseph Sinde WARIOBA - Mwenyekiti-Mkiristo

2. Mhe. Jaji Mkuu Mstaafu, Augustino RAMADHANI - Makamu Mwenyekiti -Mwislam

WAJUMBE KUTOKA TANZANIA - BARA
1. Prof. Mwesiga L. BAREGU--Mkiristo
2. Nd. Riziki Shahari MNGWALI--Mwislam
3. Dr. Edmund Adrian Sengodo MVUNGI--Mkiristo
4. Nd. Richard Shadrack LYIMO--Mkiristo
5. Nd. John J. NKOLO--Mkiristo
6. Alhaj Said EL- MAAMRY--Mwislam
7. Nd. Jesca Sydney MKUCHU--Mkiristo
8. Prof. Palamagamba J. KABUDI--Mkiristo
9. Nd. Humphrey POLEPOLE--Mkiristo
10. Nd. Yahya MSULWA--Mwislam

11. Nd. Esther P. MKWIZU--Mkiristo
12. Nd. Maria Malingumu KASHONDA--Mkiristo
13. Mhe. Al-Shaymaa J. KWEGYIR (Mb)--Mwislam
14. Nd. Mwantumu Jasmine MALALE--Mwislam
15. Nd. Joseph BUTIKU-Mkiristo

WAJUMBE KUTOKA TANZANIA - ZANZIBAR
1. Dkt. Salim Ahmed SALIM--Mwislam
2. Nd. Fatma Said ALI=-Mwislam
3. Nd. Omar Sheha MUSSA--Mwislam
4. Mhe. Raya Suleiman HAMAD--Mwislam
5. Nd. Awadh Ali SAID--Mwislam
6. Nd. Ussi Khamis HAJI--Mwislam
7. Nd. Salma MAOULIDI--Mwislam
8. Nd. Nassor Khamis MOHAMMED--Mwislam
9. Nd. Simai Mohamed SAID--Mwislam
10. Nd. Muhammed Yussuf MSHAMBA--Mwislam
11. Nd. Kibibi Mwinyi HASSAN--Mwislam
12. Nd. Suleiman Omar ALI--Mwislam
13. Nd. Salama Kombo AHMED--Mwislam
14. Nd. Abubakar Mohammed ALI--Mwislam
15. Nd. Ally Abdullah Ally SALEH--Mwislam

UONGOZI WA SEKRETARIETI
1. Nd. Assaa Ahmad RASHID - Katibu --Mwislam
2. Nd. Casmir Sumba KYUKI - Naibu Katibu --Mwislam


wewe ukienda pakstan,ama misri ama iraq utalia kabisa

maana majina yote kule ni akbal,almjahidini,al...........lakini bado utamkuta kanisani

sisi watanzania tunakasumba sana
kwa mfano zitto kabwe,kingunge ngombare ,ukiwaona ditopile.matekenya mtolera.hao utawaweka ktk dini gani?

tuache kubaguana kwa dini jamani,tunachokitafuta kitakuja tuumiza baadae,na hao wanaotutumia hawatakuwepo
 
Hivi hii tume imeteuliwa kutengeneza kitabu cha dini au katiba? Waacheni wafanye kazi tuliyowatuma msiwatishie nyau!!

Amini nawaambieni tutaanza kulalamikiana siku zijazo. Kwanza jiulize kwa nin waznz wengi kiasi hicho? Wao si wana katiba yao.? Huu muungano lazima tuuvunje! Hawa jamaa wanatunyonya sana.
 
Hivi kumbe kigezo cha kujua mtu ni Muislamu au Mkristo ni jina?

Miongoni mwa watu hawa, kuna walio waadilifu sana. Hawajui haya mambo yetu ya kipuuzi puuzi ya udini. Kama watakiuka yale wanayoyaamini, sauti ya kisasi cha kutengeneza katiba mbovu italia juu yao na vizazi vyao. Sidhani kama ni watu wasiojua athari za kutengeneza katiba mbovu zitakuwaje. Lets give them the space they need...they will have the daunting task of proving themselves right or wrong! Kwangu mimi dini sio hoja....hoja nini wateleta mbele ya meza.
 
Jaji augustino ramadhani ni mkristo pure kama ulikuwa hujui!
kwa hiyo inshort mwenyekiti na msaidizi wake ni wagala hatari sana kwa taifa!

Na mpiga kinanda mzuri pale kanisa la Anglikana Mkunazini Zanzibar anaweza kwenda kumuona akiwa yupo zanzibar.
 
Umendika mengi lakini mie takujibu yale ya muhimu..

Vyovyote utakavyosema lakini Zanzibar itabaki ni nchi huru, umetoa mifano dhaifu ya asilimia ili kujengo hoja yako lakini hamna kitu.

Udogo wa Zanzibar haifanyi kutokuwa nchi, Vatican City ina wakazi 800 na ina ukubwa wa eneo acres 110 ni nchi sembuse Zanzibar.

Ritz,

Mimi sina tatizo na Zanzibar "kuwa nchi huru" .. mimi nipo radhi zaidi wakipewa uhuru wote wa kujiondowa kwenye Muungano ili waweze kuwa (1) Nchi kamili na (2) Nchi huru zaidi

Udogo na ukubwa wa nchi siyo hoja yangu. Mimi ninachoogopa ni ule woga wa kuwaudhi wa-Zanzibar wakati wao hawaogopi kutuudhi sis. Haki hapo iko wapi? Wewe unaridhika kuburuzwa na wenzetu kama vile sisi ni watoto yatima? Kwahiyo hata Tanganyika na ukubwa wake nayo inataka kuwa nchi huru kama ilivyo huru nchi ndogo ya Zanzibar
 
udini ni dhambi mbaya sana ...
Mbona tz kuna watu wengi tu ambao hawafungamani na dini yoyote na wapo kimya tu,mimi ni mmoja wapo siamini mafundisho ya kibaguzi yanayotolewa na dini zote ukristo /uislamu.
 
tena tunasali naye pale Anglicana St. Albano (posta).
hakika jaji Ramadhan ni Mkristo kweli.

Tanzania tumeanza kubaguana kwa majina,kazi ipo kwelikweli
hivi mnataka kutambika? ama mnataka kuandika vitabu vya dini?

nawapenda sana wa china,mliosoma china nadhani mnaliona hilo

wachina bwana hakuna cha idd ndogo wala kubwa,hakuna pasaka ,ijumaa kuu wala x-mass,hakuna cha juma wala musa
haukna msikiti wala kanisa,hakuna cha ijumaa,Jmosi wala Jpili,lakini maisha kwao yanakwenda bila shaka

nyie endeleeni kubaguana na kuuwana,wenzenu wanasonga mbele
 
Mkuu kwa ujumla hapa hamna jipya ni udini tu tunaendeleza..Tujaribu kujifunza kwa wenzetu Nigeria. Mkuu wa kaya ni mmoja ya watu waliosababisha hii attension ya kidini..kuna haja gani ya kulinganisha udini katika utendaji. Tuache huu ijinga maana hata mkuu siku hizi ameacha baada ya kuona hailipi kwenye siasa ya leo!
 
udini ni dhambi mbaya sana ...
Mbona tz kuna watu wengi tu ambao hawafungamani na dini yoyote na wapo kimya tu,mimi ni mmoja wapo siamini mafundisho ya kibaguzi yanayotolewa na dini zote ukristo /uislamu.Think big acha uvivu wa kufikiri ukizani wakiweka waislamu idadi sana na wakristo ndio kutakuwa na ufanisi.
 
Katuletee tahmin zaid tujue wakatoliki wangapi?,waanglikana wangapi?,Ansaar wangapi na Bakwata wangapi ili tuchambue zaidi maana naona huna muda wa kujadili elimu ya wajumbe,uzalendo wao,uzoefu wao ukimaliza pitia kujua wachaga,wahaya,wahehe,waha wapo? Ukimaliza ulizia chadema,CUF na CCM wapo? Sie tutaendelea kujadili hadidu za rejea,integrity yao,sifa zao n.k!
 
Tuweke udini pembeni tupate Katiba Bora. Dini ni imani ya mtu. Unaweza ukawa Mwislamu lakini ukawayakubali ya Wakristo zaidi kuliko Waislam hala kadhalika Mkiristo. Mimi nadhani Wailslam kuwa wengi siyo tiketi ya wao kukubaliwa chochote watakacho. Rais kama mteuzi hawezi mfurahisha kila moja. Je akichagua Wakristo wengi wasio na msimamo thabiti inaweza kuwa bora kuliko Wakristo wachache wenye mtizamo thabiti? Think Twice!!
 
Licha ya kwamba J.K. kajitahidi kuwa na vigogo kweli kweli, na Katiba ya sasa imezingatiwa ktk kuandaa m'badala wake, muundo wa hii Tume umedhihirisha kwamba demokrasia ya kweli ni ndoto kwa Watanzania wa leo. Kama tunanuia kwa dhati kuwa na Demokrasis ya kweli, itabidi Watanzania wanaoamini kwamba hilo ni muhimu, waendelee na juhudi za kuandaa hata Mabadiliko kwa Katiba Mpya ijayo.

Kwa mfano ni jambo la kichekesho kwamba Tanzania Bara ambayo ina Watu takriban 42 milioni iwakilishe na wajumbe sawa na Tanzania Zanzibar ambayo ina watu wasiozidi 1.5 milioni. Mfano wa pili ni kwamba, licha ya kwamba Tanzania siyo nchi inayozingatia dini katika maamuzi yake ya kisiasa, ni lazima tukubali kuwa madhehebu ya dini yana influence katika mchakato na hatimaye maamuzi. Nikihesabu Waislamu katika hii Tume kwa kuzingatia majina naona zaidi ya theluthi mbili ni Wao. Wengine ni Wakristo au watu wasiokuwa na dini yoyote.

Hata kama ni lazima tujali Muungano wa Jamhuri yetu, hatuwezi kupuuza ukweli kuwa sasa kuna matatizo ya umilikaji wa raslimali maliasili (e.g. gas), na kuna wananchi wamediriki hata kwenda Umoja wa Mataifa kudai Zanzibar ijiondoe.

Haya ni mambo mazito na nimeona ni vema niyataje sasa, siyo tu yajadiliwe na Tume, bali ikiwa ni lazima, basi mjadala uendelee hata baada ya Tume kutoa taarifa na Bunge Maalum kupitisha Katiba Mpya.

This account must be hacked!! Unbelievable
 
Hoja yasngu hapa siyo kuongelea ubaguzi wa kidini wala nini ila ni kutazama malengo ya kiudini yaliyojificha humu ndani.nafikirei hapa mahakama ya kadhi nchini tanzania inanukia.

tazama team hii hapa chini

angalizo-mimi nimetazama majina yao kuwapanga kidini.

Hata mtei kaandika hivi "Mfano wa pili ni kwamba, licha ya kwamba Tanzania siyo nchi inayozingatia dini katika maamuzi yake ya kisiasa, ni lazima tukubali kuwa madhehebu ya dini yana influence katika mchakato na hatimaye maamuzi. Nikihesabu Waislamu katika hii Tume kwa kuzingatia majina naona zaidi ya theluthi mbili ni Wao. Wengine ni Wakristo au watu wasiokuwa na dini yoyote.
"



wakiristo wapo 11
Waislam wapo 23

WALIOTEUA
1.Rais Kikwete -Mwislam
2.Rais Shein---Mwislam


1. Mhe. Jaji Joseph Sinde WARIOBA - Mwenyekiti-Mkiristo

2. Mhe. Jaji Mkuu Mstaafu, Augustino RAMADHANI - Makamu Mwenyekiti -Mwislam

WAJUMBE KUTOKA TANZANIA - BARA
1. Prof. Mwesiga L. BAREGU--Mkiristo
2. Nd. Riziki Shahari MNGWALI--Mwislam
3. Dr. Edmund Adrian Sengodo MVUNGI--Mkiristo
4. Nd. Richard Shadrack LYIMO--Mkiristo
5. Nd. John J. NKOLO--Mkiristo
6. Alhaj Said EL- MAAMRY--Mwislam
7. Nd. Jesca Sydney MKUCHU--Mkiristo
8. Prof. Palamagamba J. KABUDI--Mkiristo
9. Nd. Humphrey POLEPOLE--Mkiristo
10. Nd. Yahya MSULWA--Mwislam

11. Nd. Esther P. MKWIZU--Mkiristo
12. Nd. Maria Malingumu KASHONDA--Mkiristo
13. Mhe. Al-Shaymaa J. KWEGYIR (Mb)--Mwislam
14. Nd. Mwantumu Jasmine MALALE--Mwislam
15. Nd. Joseph BUTIKU-Mkiristo

WAJUMBE KUTOKA TANZANIA - ZANZIBAR
1. Dkt. Salim Ahmed SALIM--Mwislam
2. Nd. Fatma Said ALI=-Mwislam
3. Nd. Omar Sheha MUSSA--Mwislam
4. Mhe. Raya Suleiman HAMAD--Mwislam
5. Nd. Awadh Ali SAID--Mwislam
6. Nd. Ussi Khamis HAJI--Mwislam
7. Nd. Salma MAOULIDI--Mwislam
8. Nd. Nassor Khamis MOHAMMED--Mwislam
9. Nd. Simai Mohamed SAID--Mwislam
10. Nd. Muhammed Yussuf MSHAMBA--Mwislam
11. Nd. Kibibi Mwinyi HASSAN--Mwislam
12. Nd. Suleiman Omar ALI--Mwislam
13. Nd. Salama Kombo AHMED--Mwislam
14. Nd. Abubakar Mohammed ALI--Mwislam
15. Nd. Ally Abdullah Ally SALEH--Mwislam

UONGOZI WA SEKRETARIETI
1. Nd. Assaa Ahmad RASHID - Katibu --Mwislam
2. Nd. Casmir Sumba KYUKI - Naibu Katibu --Mwislam
Sasa wewe ulitaka nani afanye uteuzi?
Mwai Kibaki au Mseveni?
Kikwete ndiyo prezidar wa tz na shen ni prezidar wa znz na ndio wenye majukumu ya kuteua tume.Na pia tume hii ni kwa ajiri ya kukusanya maoni tuu.
Sasa wewe mbona imekuuma sana?
Basi kama vipi mwambie babako akuteue wewe na shangazi zako,dada zako,wajomba zako,shangazi yake bibi yako,mtoto wa wifi yako,mjukuu wa shangazi yako,kaka ake mama ako kisha katuleteeni maoni ya watanzania juu ya katiba mpya....why kila siku humu ndani ya jamvi ni udini tuuuuuuuu!!
Au wenzetu mnashiba sana so mnatafuta pa kupunguzia shibe?kuna wa tz wanakufa kwa kukosa maji safi na huduma za afya,ebu tutumie nafasi hii kuunganisha mawazo ili tuwanusuru bila kujari itikadi zao kidini na kichama.
 
Kwanini tunapenda kuanzisha mada za udini sehemu isizostahili? Mbona kati ya wajumbe wa tume, wapo watu wengi tu ambao wanajua Tanzania inataka nini? Why dont we support the team and deal with the shortcomings if any? Prejudicing the good intention want provide the solution...
Kwa mfano ingekuwa wewe Mzee Mtei, unafikiri tume ingeundwaje?
 
Udini lazima uonekane sasa..kwa sababu umeletwa. Mtu kichwa nazi hana hoja kaishia kuleta udini. Sasa waukemee, mbona wapo kimia? Udini sasa upo na watu wanahoji, msiwabane sana kwa sababu wanaongea kitu kilichopo na kilicholetwa nchini kwetu.

Udini ni hatari, lakini sasa hivi ni mbinu ya wakubwa kupata kuchaguliwa. Hivyo hautokuja ondoka udini hadi hapo utakapotekeleza madhara yake..

Sisi tunaolalamika kwenye keyboards hatuwezi kuondowa udini. Tukitaka udini utoweke sharti huyo aliyeuleta afanye yafuatayo..
(1) aukemee kwa nguvu zote
(2) matendo yake yafanane na maneno yake..
(3) Sisi tukimwangalia usoni tuone ile seriousness ya maneno yake

bila kufanya hivyo, udini upo na hautoki. Waacheni watu waangalie majina ya dini, wahesabu composition za kamati, walalamike hadi jambo litokee..
 
Mimi ni Muislam lakini sijaridhika na hii tume kwani etatuletea chukidhidi ya ndugu zetu wa kristu kwani waislam tumependelewa sana kuhusu mahaka ya kadhi nivyema tungeachiwa waislamu wenyewe bila kuihusisha serikali isiyofungamana na dini yoyote ile

Muislam wa wapi?
Tanganyika au zanzibar?
 
udini ni dhambi mbaya sana ...
Mbona tz kuna watu wengi tu ambao hawafungamani na dini yoyote na wapo kimya tu,mimi ni mmoja wapo siamini mafundisho ya kibaguzi yanayotolewa na dini zote ukristo /uislamu.

Mwakalinga kwa tafsiri ninayoijua mimi! ni kuwa DINI NI MFUMO AU UTARATIBU WA MAISHA ANAYOISHI MWANADAMU: kwa hiyo na wewe pia una dini yako hiyo hiyo ya kutoamini uislam/ukristo
 
Back
Top Bottom