TUKUMBUSHANE: Tukio gani la hatari uliwahi kufanya utotoni?

Mohammed wa 5

JF-Expert Member
Jun 20, 2022
1,215
2,992
Hope ni wazima wana JF,

Je, uliwahi kufanya tukio gani la hatari kipindi unakua?

Sitosahau siku moja ilikuwa ni likizo ya Pasaka siku ya Ijumaa tukiwa group la watoto kama 6 hivi, mmoja alikuwa wa kike Jesca, tulienda porini sio mbali sana na maeneo tunayoishi.

Baada ya kutembea tembea kidogo kuna sehemu tulikuta mzinga wa nyuki mkubwa, kwa akili za kitoto, tukaanza kurusha mawe kwenye mzinga, wale nyuki muda mfupi tu walisambaa eneo lote, ile siku tuliumwa na nyuki balaa.

Tukaanza kulia huku tukipiga kelele za maumivu, tusaidieni tunakufa, baada ya muda tulikuja kuokolewa na wakata miti waliopo eneo lile. Nakumbuka Jesca na Isam walikuwa na hali mbaya walishambuliwa sana na nyuki. Jesca na Isam walilazwa ICU maana hali yao ilikuwa taabani.

Ikabidi tukimbizwe hospital kwa matibabu, tunamshukuru Mungu wote tulipona, nakumbuka ilikuwa story kubwa mtaani.

Naomba kuwasilishaa 🙏

images (15).jpeg
 
Mimi niliponyea unga uliokuwa umehifadhiwa vizuri.Kisa hasira zimenipanda kwa nini hawajapika wali na nilikua nimezoea daily lazima wali na mandondo kwa ajili yangu yawepo. Kile kisago namshukuru Mungu bado navuta pumzi.
Kukuletea habari,
Cee.
 
Mimi niliponyea unga uliokuwa umehifadhiwa vizuri.Kisa hasira zimenipanda kwa nini hawajapika wali na nilikua nimezoea daily lazima wali na mandondo kwa ajili yangu yawepo.Kile kisago namshukuru Mungu bado navuta pumzi.
Kukuletea habari,
Cee.
Nafikiri tangu siku hiyo na ugali ukaanza kuupenda na kuula kwa bidii Wazee zamani waletee masikhara kote lakini si swala la chochote kinachohusu kuhusu msosi, Heshima ya kwanza wao, Heshima ya pili inabidi uheshimu msosi iwe unaupenda au huupendi,,kinachotakiwa ni heshima tuu!!!
 
Nafikiri tangu siku hiyo na ugali ukaanza kuupenda na kuula kwa bidii Wazee zamani waletee masikhara kote lakini si swala la chochote kinachohusu kuhusu msosi,,,Heshima ya kwanza wao ,Heshima ya pili inabidi uheshimu msosi iwe unaupenda au huupendi,,kinachotakiwa ni heshima tuu!!!
Kwa kifupi nilikoma.Nililia nikanyama,nikalia upya .
 
Mimi niliponyea unga uliokuwa umehifadhiwa vizuri.Kisa hasira zimenipanda kwa nini hawajapika wali na nilikua nimezoea daily lazima wali na mandondo kwa ajili yangu yawepo.Kile kisago namshukuru Mungu bado navuta pumzi.
Kukuletea habari,
Cee.
😂😂😂😂
 
bana we tulienda kuiba mapera shamba moja liko juu huko milimani.shamba la bibi yake majuto.
mara wakatukuta majuto nasoma nae kimekomaa kama mzee ole tukachapana sana kule juu wao walikua wengi wakanishinda ikabidi waaanze mchakato wakanishtaki.
wao wenyewe walishangaa nilipowatoka nikarudi maskani nikatulia .
majuto alikua kujuta kweli baadae nilimpa kibano mahali ye mwenyewe aliomba poo

no2
Hosea kilikua kiyanki flani kijinga sana,kidogo nafkiri miaka 8 tunakiambia kuwa mwangalifu wewe una papara kinabisha .siku hiyo kuna gari bus leyland la bank linamleta mshua mmoja kahamia pale mtaani.
tukaenda tukalidandia,washamba wa magari 🤣 🤣 🤣 🤣 .
gari limetembea; halijafika lami mi nimeruka,jua karuka mwingine simkumbuki karuka .
Hosea sasa aruke kakosea step kadondoka katikati ya matairi ile double diff kanasa kichwa katikati dereva hana habari wala hajui kinachoendelea anaendesha tu.
Dogo kapasuka kichwa na kaburuzwa sana tu.ubongo nyama nje
nimeona ile kitu ikabidi mbio nyumbani kumweleza maza noma,dingi ndo kabisa ataua.bahati nzuri namkuta bibi nje ananisubiri alikua ananipenda sana RIP:mad:
hapo sina shati sijui limedondoka wapi maana kwenye mbio nilichanja shamba la mahindi nikatokelezea home bana🤣🤣🤣🤣🤣
akanipa shati chap ili niingie home nisishtukiwe.
Bibi ;ulikuwa wapi mme wangu?
Namwambia we ngoja kidogo tu. nipumzike kuna mtu kafa hapo mbele.
hajakaa sawa tayari mayowe yakaanza mi nimetulia huku nimeona kila kitu.
Aisee Hosea pole sana
no 3 na zingine zinakuja
 
Sitosahau siku niliyokufa aisee yule jama anaroho mbaya sio kwa mapanga yale........
Sauti ya mwisho namsikia padri mungu alitoa na Mung u alitwaaaha..... Juu bonge la msalaba mpaka nikahisi fund msalaba nilikia na ugomvi nayeee..........
 
Sitosahau siku niliyokufa aisee yule jama anaroho mbaya sio kwa mapanga yale........
Sauti ya mwisho namsikia padri mungu alitoa na Mung u alitwaaaha..... Juu bonge la msalaba mpaka nikahisi fund msalaba nilikia na ugomvi nayeee..........
😁😁😁😁
 
Skumbuki ilikuwajekuwaje, nilikalia supu inayochemka

Ngozi ilibanduka ikabidi niwe naenda hospitali mama kuchomwa sindano ili kuondoa makovu, na mama akawa ananipakapaka asali

Nilikosa shule mwezi mzima, Niko la 2 kipindi hicho
 
Daaah utoto raha nimetoka tu kutailiwa braza mkubwa akaninunulia baisikeli ile Mountain bike y kukunja katikati mm na mshono wangu bado w moto si nipige misele nikadondoka nayo vibaya Uzi ukafumuka n kupelekwa tena Hospital kushonwa upya hv U.B.O wng kwa ss nikama umechongwa flani na wadada wanaupenda hatare. Wakiniuliza natunga majibu y uongo.
 
Kipindi hiko natumikia altareni parokia ya Mafinga.
Siku hiyo ya jumapili nimepangwa kushika chetezo na jamaa anaitwa Frank.

nakumbuka siku hiyo ilikuwa ni misa ya kwanza na kulikuwa na misa ya shukrani ya upadre baada ya upadrisho.

ngoma inaanza tumechelewa kufika so moto tumechelewa kuukoleza.
Paroko namkumbuka ni padri Henry Tucholski mPoland mmoja alikuaa mkali balaa.

tunatoka Sakrastia tumesujudu msalaba anageuka aweke ubani kwenye chetezo ili tuingie maandamano then church kakuta moto kidogo tu Ila limkaa lipo tu.
aloo alikaripa akasema tokeni hapa.
basi wao wakaenda ndani kanisani bila chetezo.

mi na Frank tukasepa hii so na huyu paroko ni Kali balaa najua watu wa Mafinga wanamkumbuka.Nikapata wazo

siku hiyo umeme ulikuwa haupo .Tanesco walikuwa wamefanya yao basi kulikuwa na jenereta nje ya sakrastia linanguruma.

Nikachukua kigai .Tega mdomo wakigai kwenye exhaust ya genereta basi moto ukawa unakolea chap balaa.
.tukachukua moto jaza kwenye chetezo hao tukachoma ndani wakati wa kusoma Injili .
huku tunawaza jamaa hawehawezi kutuchenjia mule ndani maana yule mpoland alikuwa hanogi.

ila alivunga na misa ikaendelea.

Huwa najiuliza ya kuwa hivi si tungechoma kanisa na kuua waumini maana petrol ya miaka ile ilikuwa Ina nyege sana na moto.

nb nilikuwa nataka niwe padre lkn sahv me muhuni .sio mimi tu ila hadi wenzangu ila huwa najiuliza kwa nini watumishi wa altare baadae huwa wanakuja kuwa vijana wa hovyo sana??

nisaidieni kumtag Analyse maana yenye alisoma Don bosco au Mafinga seminary.
Hili kanisa analijua sana.
Kwako Apostle.
 
Hope ni wazima wana JF,

Je, uliwahi kufanya tukio gani la hatari kipindi unakua?

Sitosahau siku moja ilikuwa ni likizo ya Pasaka siku ya Ijumaa tukiwa group la watoto kama 6 hivi, mmoja alikuwa wa kike Jesca, tulienda porini sio mbali sana na maeneo tunayoishi.

Baada ya kutembea tembea kidogo kuna sehemu tulikuta mzinga wa nyuki mkubwa, kwa akili za kitoto, tukaanza kurusha mawe kwenye mzinga, wale nyuki muda mfupi tu walisambaa eneo lote, ile siku tuliumwa na nyuki balaa.

Tukaanza kulia huku tukipiga kelele za maumivu, tusaidieni tunakufa, baada ya muda tulikuja kuokolewa na wakata miti waliopo eneo lile. Nakumbuka Jesca na Isam walikuwa na hali mbaya walishambuliwa sana na nyuki. Jesca na Isam walilazwa ICU maana hali yao ilikuwa taabani.

Ikabidi tukimbizwe hospital kwa matibabu, tunamshukuru Mungu wote tulipona, nakumbuka ilikuwa story kubwa mtaani.

Naomba kuwasilishaa 🙏

View attachment 2578256
Huyu sasa kafikaje huku?
 
Kipindi hiko natumikia altareni parokia ya Mafinga.
Siku hiyo ya jumapili nimepangwa kushika chetezo na jamaa anaitwa Frank.

nakumbuka siku hiyo ilikuwa ni misa ya kwanza na kulikuwa na misa ya shukrani ya upadre baada ya upadrisho.

ngoma inaanza tumechelewa kufika so moto tumechelewa kuukoleza.
Paroko namkumbuka ni padri Henry Tucholski mPoland mmoja alikuaa mkali balaa.

tunatoka Sakrastia tumesujudu msalaba anageuka aweke ubani kwenye chetezo ili tuingie maandamano then church kakuta moto kidogo tu Ila limkaa lipo tu.
aloo alikaripa akasema tokeni hapa.
basi wao wakaenda ndani kanisani bila chetezo.

mi na Frank tukasepa hii so na huyu paroko ni Kali balaa najua watu wa Mafinga wanamkumbuka.Nikapata wazo

siku hiyo umeme ulikuwa haupo .Tanesco walikuwa wamefanya yao basi kulikuwa na jenereta nje ya sakrastia linanguruma.

Nikachukua kigai .Tega mdomo wakigai kwenye exhaust ya genereta basi moto ukawa unakolea chap balaa.
.tukachukua moto jaza kwenye chetezo hao tukachoma ndani wakati wa kusoma Injili .
huku tunawaza jamaa hawehawezi kutuchenjia mule ndani maana yule mpoland alikuwa hanogi.

ila alivunga na misa ikaendelea.

Huwa najiuliza ya kuwa hivi si tungechoma kanisa na kuua waumini maana petrol ya miaka ile ilikuwa Ina nyege sana na moto.

nb nilikuwa nataka niwe padre lkn sahv me muhuni .sio mimi tu ila hadi wenzangu ila huwa najiuliza kwa nini watumishi wa altare baadae huwa wanakuja kuwa vijana wa hovyo sana??

nisaidieni kumtag Analyse maana yenye alisoma Don bosco au Mafinga seminary.
Hili kanisa analijua sana.
Kwako Apostle.
Pole Sana ww siyo muhuni bahana ila japo Kuna ka ukweli ndani yake kuwa watot baadhi was wachungaji Ni wahunj sna Kuna bint hapa jirani yet ni msagji mzuri tu
 
Wakt fln nikiwa dogo tu aged 7 HV nilkuwa namuona Bab angu mdgo akimdhibiti ngombe kwa kufunga kamba kiunoni mwake na Kisha ngombe anatangulia mbele kuelekea mnadani ,bas na mm could moja nikamfunga ngombe wetu kiunoni ili nidhibiti aloo nilirushwa rushwaa kilibaki kidogo nife
 
Back
Top Bottom