Umewahi kufanya kazi gani yenye hatari kubwa ambayo kidogo ikutoe uhai?

monta

JF-Expert Member
May 6, 2014
1,125
1,459
Sitosahau siku nilipotaka kufa pale kiwandani​

Ilikua mapema tar. 1/June 2022 nilipitia kipindi kigumu sana baada ya kuyumba kiuchumi na degree yangu mkononi ikanilazimu kujizima data na kutafuta kazi yoyote iwe rasmi au isiwe rasmi. Nikazama zangu JF ndipo nikapata muongozo wa kwenda kiwanda cha unga kwa kurubuniwa kwamba kwa siku malipo inafika hadi buku 8 nikajipa moyo.

Basi nikafata tafatibu zote siku ya pili nikaenda na barua ya mtendaji then nikaambiwa siku ya pili usiku nikaanze kazi. Basi bwana nikazama zangu pale mida ya saa 1 jioni nikawakuta wenzangu wapo tayari wanasubiri kuanza kazi.

Wakagawa msosi pale ndani kila mtu sahani ya wali(upo kama makande) na maharage na ndizi mbivu. Kwa kua ni siku ya kwanza nikawa na uoga uoga wa kula ule msosi na niliogopa kuja kukatwa kwenye malipo.

Jamaa wakawa wananishangaa huyu msela vipi huu msosi ni lazima kuchukua haijalishi unataka au hutaki. Basi kuna jamaa akasema chukua nipe mimi nitakula, wakawa wanagombania nipe mimi nipe mimi. Basi nikachukua ule msosi nikampa jamaa mmoja akala na wa kwake.

Kimbembe kilianza baada ya masaa mawili viroba vilipoanza kushuka toka kwenye vinu vinashuka kama mvua na vinu vipo vya kutosha mule ndani. Ili kusubiria viwe vingi ndio kazi ianze wale jamaa wakasema tuchezeni boli humu ndani (mpira wa makaratasi).

Basi tukagawana huku na huku tukaanza kucheza mpira.Katika harakati za kuucheza ule mpira nikajibamiza vibaya sana kwenye kinu kipo kama upinde afu kule mbele kama wembe kwa makali yake.

Ghafla bin vuu nikajikuta nipo chini nimezungukwa na watu kibao damu zinavuja kama kuku katoka kuchinjwa. Aisee nilijua leo ndio siku yangu siwezi kutoboa maana nilipasuka katikati ya kichwa. Wakaniinua pale sina hata nguvu wakasema nikapumzike pale kazi inataka kuanza. Nilishindwa coz damu zilikua zinavuja sana kuna jamaa akanielekezaa bafu akasema nikaoge ili niwe sawa.

Nilijivuta nikaenda kuoga kule bafuni maji yote yalijaa damu tu yani ili siku ilikua ndio bye bye sema Mungu hakupanga tu. Nikarudi kule ndani jamaa ndio wanagawana watu kwa makundi waanze kazi. Cha ajabu na mimi nikaitwa nikapangiwa kundi nibebe viroba.

Nikawaeleza siko sawa damu zinavuja sana lakini hakuna aliyeelewa. Wakasema humu ndani ni lazima kila mtu afanye kazi. Kazi ikaanza nikaambiwa na mm nibebe kichwani zile kilo 25 kwa 50 yena viwili trip moja.

Ilikua ngumu sana kubeba lakini sikua na jinsi nikajaribu tripu moja nakashindwa kichwa kilikua kinauma sana. Wakanibadilisha section wakasema niwe nawapakia watu kichwani wenyewe wanaita kijiko, yani unabeba viroba viwili pale chini na kumpa mtu kichwani.

Nimefanya mara moja tu kuna jamaa akanigusa pale kichwani na kiroba basi damu zikaanza upya kutoka nikaamua kuacha nikasema liwalo na liwe cha kufia nini. Basi nikatoka pale nikaenda nje kukaa toka ile saa 4 mpaka saa 12 asubuhi jamaa wanabeba tu vile viroba.

Walikua kama 30 hivi lakini viroba walivyobeba ni zaidi ya 6,000 yani kila mmoja kama mia 2 hivi. Asubuhi ya saa 1 tukaitwa wote kwenye mgao wa pesa. Kaja kiongozi wao akasema leo kazi hamna hivyo kila mtu atapata elfu 2,aisee nilichoka mwili na akili yani kazi yote ile mtu alipwe elfu 2.

Kuna watu walikua wanapinga mimi kupewa ile elfu 2 kisa sijafanya kazi. Sema jamaa akanipa ile buku 2 akasema ukatibiwe. Nimetoka pale naona kama ndoto nikarudi zangu geto ile pesa nikafanya nauli sikubakiwa hata na senti.

Nimefika home kichwa chote kimeloa damu na nimepasuka vibaya sana. Sikua na pesa hivyo nikachukua chumvi na beseni nikaanza kujisafisha huku nikipata maumivu makali sana. Sikwenda kabisa hospitali hadi leo hii na nilipona kwa uwezo wa Mungu baada ya mwezi kupita. Leo nilipita ile njia ya kiwandani nikakumbuka kuleta kisa hiki.
Nimeamua nilete uzi kamili maana nili reply tu kwenye uzi wa kazi za viwandani huko nyuma.

Je, ni kazi gani ushawahi kufanya ilikuwa na risk ya kupoteza kitu au uhai kwenye maisha yako?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom