Tukubali tukatae, mtu kuwa na Tattoo ni kielelezo cha malezi mabovu

The Assassin

JF-Expert Member
Oct 30, 2018
4,355
17,321
Tukubali tukatae, ukiona mtu ana tattoo yoyote ujue ni matokeo ya malezi mabaya.

Tattoo ni ishara ya mtu kutokujijali, kutojali afya wala thamani ya mwili wake na pia kutokutumia akili sawasawa.

Ndio maana China kwa ajili ya kulinda kizazi cha sasa na kizazi cha baadae imepiga marufuku ukengeufu na kuzuia watu kutokuchora tattoo. Sio China tu, nchi nyingi sasa zimeshaanza kuona kwamba tattoo ni mwenendo mbaya kwa jamii hivyo kuanza kuzipiga marufuku.

Ukiangalia, huwezi kukuta familia zinazojielewa na zenye heshima katika jamii kama wanasiasa, wafanya biashara wakubwa, wanasayansi, wasomi nk watoto wao ama wao wenyewe wamechora tattoo. Na hata kama ikitokea alichora kwa bahati mbaya akiwa mdogo, lazima utakuta anaificha sana isionekane katika jamii. Sababu ya kufanya hivyo ni moja tu kwamba tattoo ni ishara ya malezi mabaya ama tabia mbaya.

Huku Afrika hasa Tanzania ambako usimamizi wa maadili na mwenendo mwema katika jamii imeachwa kwa mtu binafsi, vijana wengi huona kuchora tattoo ni ufahahari kua kama Messi ama 50 Cents.

Tulinde kizazi chetu cha sasa na cha baade kutoka kwenye uharibifu huu wa Tattoo, tueleze vijana tattoo sio jambo jema na sio ufahari, ni ujinga.
 
Kwa kweli ni upumbavu wa kiwango cha lami. Juzi nimeona li kijana limejichora kwenye paji la uso eti sura ya Saa-Mia (angalia kwenye kiambatanisho hapo) si ujuha huo? Mavi-jana mengi ya TZ ni majuha, yanaiga mambo ya kizungu!

uiiiii-660x400 (1).jpg
 
Tattoo zimeharamishwa kwenye Biblia, nilishangaa sana yule mchungaji wa Kenya, mwanamke alipojichora tattoo.
Nenda na vifungu vya biblia mkuu, kifungu gani kilichoharamisha tatoo na jee aina hiyo ya urembo ilikuwepo enzi na enzi na ilijulikana kwa jina hilo?

Siungi mkono hayo makitu, isipokuwa tuunge mkono hoja kwa vifungu.

Nimefuatilia kuanzia mtoa mada anavyolaani, lakini sijaona mtu akasema kiufasaha madhara yatokanayo na hiyo michoro ya ngozi.
 
Nenda na vifungu vya biblia mkuu, kifungu gani kilichoharamisha tatoo na jee aina hiyo ya urembo ilikuwepo enzi na enzi na ilijulikana kwa jina hilo...
Mambo ya Walawi 19:28
[28]Msichanje chale yo yote katika nyama ya miili yenu kwa ajili ya wafu, wala msiandike alama miilini mwenu; mimi ndimi BWANA.
Ye shall not make any cuttings in your flesh for the dead, nor print any marks upon you: I am the LORD.
 
Tukubali tukatae, ukiona mtu ana tattoo yoyote ujue ni matokeo ya malezi mabaya.

Tattoo ni ishara ya mtu kutokujijali, kutojali afya wala thamani ya mwili wake na pia kutokutumia akili sawasawa...
China imekataa kwasababu ya mambo ya kisiasa inajua mwanamichezo anaweza akashangilia ushindi akavua jezi hafu akaonesha tattoo yenye ujumbe ambao hautawapendeza watawala, na siyo kama unavyochukulia wewe.
 
Usiwe mkurupukaji, jaribu nawe kufanya utafiti. Unaonekana ni mtu wa ovyo kupinga wakati hujui au huna uhakika Kwani unampa credits huyo unayempinga
Nadhani haukunielewa mkuu.

Sipo kupinga na wala sijapinga, isipokuwa nilichomuomba huyo mtoa comment ni kuweka vifungu kukazia hoja ili kuweka mada kisomi.

Sababu unaposema tu kuwa: "vibaya", "kosa" ama "dhambi" bila kuweka vifungu vya kisheria ama toka maandishi matakatifu kukazia hoja yako, huko ni kufoka!

Amefanya hivyo na nikaridhika naye kwa "like" kubwa.

Ama unieleze sasa mantiki yako, ku like hoja ya mtu katika maongezi ya kubadilishana mawazo ni kosa mpaka mtu kuonekana mbumbumbu na ni mjinga?
 
Back
Top Bottom