Tukubali tu: Sisi wajinga... (I know, it hurts)


MMEPATA UKUMYA KAMA WA MKAPA UKWELI UNAUUMA EHE KWA KWA KWI KWI POLENI NA KARIBUNI TENA LAKINI MSIWE NA HASIRA MKIAMBIWA UKWELI KWANI HATUWEZI WOTE KUWA NA AKILI SAWA VINGINEVYO DUNIA ISINGEENDELEA. MKITAKA KUJA TUFAHAMISHENI TUWAPOKEE BONGO YETU HII TUACHIENI LA SIVYO RUDINI TUUNGANE. mSINUNE MKASUSA NIMEWAPATA LEO UKWELI UMEJULIKANA UR JUST A BUNCH OF LOOSERS. sORRY KAMA ENGLIZ YANGU MBOVU LAKINI NIMESOMEA BONGO NA NITAFIA BONGO NAAPA KUTOIKIMBIA NCHI YANGU CHAO.
 

Wakubwa, ni vyema kama tukiweza ku-maintain focus ya mada..hizi disorders chache zipo katika jamii..kwa hiyo Mkubwa Mushi achana na huyo..shusha mambo ya kueleweka hapa...ujumbe unawafikia..si unaona wanavyokuwa wakali..kumbe na wao wanafika huku sio...safi sana
 

Maskini!
Kumbe ni kweli ulikuwa UK
Pole sana!
 

Wamo humu hata Kikwete naye yumo humu!
 

Disorders zipi kakaaaaaa. Nadhani hiyo ya kwenu ni disorder kubwa zaidi mnaogopa kurudi bongo maana wengine mlizamia mtabaki kuandika kwenye jumboforums tu maana hamuwezi kuja bongo, kupata tena visa ya kurudi ulaya au marekani noma ndio maana hasira zenu mnamalizia kwenye kuandika. Andikeni sawa fichueni mafisadi sawa lakini msituite wajinga hiyo ndio ilikuwa hoja yangu na wala si vinginevyo. Mkimbia kwao mgonjwa wa akili. Ngoja nikalale mie niachane na nyie maana hamna dira ila blaaaaa blaaaaaaa tu sisi huku tutatapambana na mafisadi mpaka kieleweke ila tukifanikiwa mkae huko huko maana wengine hata matumizi kidogo hamleti nyumbani ndugu zenu wana shida lukuku halafu badala ya kuwasaidia au kutafuta namna ya kuwasaidia mnachonga tu, nyie endeleeni tu kuandika maneno ya kwenye karatasi hayana faida bali vitendo. Adios
 

Hivi kweli utapambanaje dhidi yako mwenyewe?
Una uhakika hauitaji msaada hapo kweli?
Halafu msomi mzima ukitaka kujua ni fisadi..Angalia umetumia neno "Tutapambana"

Kwetu hapa JF ni "TUNAPAMBANA"

OUT OF TOUCH..HUWEZI KUJIFICHA HAPA JF..KWI KWI KWI..YANI WE UNAFIKIRI KWASABABU HATUONANI USO KWA USO BASI HATUTAMBUANI?

KWA TAARIFA YAKO THIS IS THE BEST WAY TO GET INSIDE YOUR FISADI MIND! KWI KWI KWI..USTAKE NCHEKE!
 
Maskini!
Kumbe ni kweli ulikuwa UK
Pole sana!

Labda kwa fikra zako. Lakini haifuti ukweli wa mambo. Rudi nyumbani tufanye kazi ulaya kwa wazungu mnakuwa watumwa wa wazungu bora sisi watumwa wa waafrika wenzetu pamoja na umaskini wetu. Mcheza kwao hutunzwa nyie huko vipi
 
Hivi kweli utapambanaje dhidi yako mwenyewe?
Una uhakika hauitaji msaada hapo kweli?


Wewe naona ni mgonjwa wa akili maana unadhani kila aingiaye hapa ni fisadi. Labda na wewe una matatizo kamwone daktari lakini hata hapa tunao madaktari wa ugonjwa wako njoo tukupeleke muhimbili.
 
Jamani eeeh vipi nyie mbona mnataka kuharibu mada hii?..
Kwetu,
Tafadhali mkuu kukaa kwako Bongo hakukupi mamlaka yoyote zaidi ya watu wengine kiasi kwamba unaanza kutudharau wote tunaoishi nje..
Tafadhali kama ni Ujinga tumesema Watanzania sasa kama unafikiri Utanzania ni kuisho Bongo mkuu unapoteza muda wetu, kwani hapo ulipo huwezi kunambia wewe binafsi umepambana vipi na Mafisadi..
JMushi1, Please turdi kwenye mada haya maswala yenu hanazidi kutuchefua tu..
 
Sasa kama wasomi wetu "wamechimba" sana kuliko wa Ulaya na Marekani (ingawa ma theory na mavitabu wanayotumia mengi yametungwa na kuandikwa na wazungu) sasa kwa nini sisi hatuendelei?

Ngabu:

Nilitoa ahadi ya kujibu lakini naona ukumbi kama umejaa posti nyingi ambazo zinatoka nje ya mada.


Kuna posti niliyosema utaalamu uupatao shuleni ni taaluma tu. Lakini kazi zinazoendelea nchi ni miradi inayotumia pesa, muda, na human capital (watu wenye taaluma zao).

Na watu wanapohamua kutumia taaluma zao kupata faida au maendeleo hapo wanafanya BIZNIS NA sio kufanya project za shule. Katika project ya shule mwanafunzi anatakiwa ku-prove au kijifunza kitu fulani.

Lakini mwanafunzi huyohuyo akipata shahada na kuhamua kufanya BIZNIS kwa kutumia taaluma yake mambo yanakuwa complex kuliko zile project za shule. Kwanza anatakiwa awe na model ya business yake. Vilevile anatakiwa awe na wateja au aweze kupata market share na kikubwa zaidi awe na mtaji.

Hivyo sehemu kubwa ya kushindwa kwetu hakutokani na sisi kukosa ujuzi bali kutokuwa na BIZNIS model zinazo-support kile ulichosomea.

Konoike ni kampuni. Na kama ni kampuni basi itakuwa na BIZNIS model yake, hivyo mhitimu kutoka Japan au Tanzania anaweza kujiunga na kutokana na support ya BIZNIS model iliyopo anaweza kushika kile anachotakiwa na kufanya kazi vizuri tena kwa ufanisi mkubwa sana.

Tatizo la Tanzania ni kuwa Wahitimu wengi wa sayansi na Engineering wanapomaliza shule wanakuta hakuna makampuni yenye BIZNIS models zitakazofanya wahitimu hao kujifunza chochote cha maana na wao kujiendeleza.

Naweza kuendelea lakini nywele zinauma.
 

Pundit:

Nilipata bahati ya kusoma Tanzania na nje ya nchi. Kuna ukweli ya unayoyasema lakini mimi bado nipo KWENYE BIZNIS.

Kwa mfano wakati wa enzi ya utawala wa kirumi au wakati wa Renaissance kuna miji mikubwa ilizuka yenye mireferi ya maji, viwanja vya michezo mahekalu ya dini na mambo mengi ya maendeleo ya kijamii. Historia inasema, mtawala fulani ali-COMMISSION ujenzi wa uwanja au mirefeji ya maji safi (Aqueductis). Ku-COMMISSION kuna maana kutengana budget kwa ujenzi wa mradi ambao utambatana na kuwalipa mafundi na wafanyakazi wengine mishahara (BIZNIS).

Kama knowledge ya ufundi pekee yake ilikuwa so fabolous kwanini basi wenye knowledge hizo waliweza kufanya kazi pale pesa ilipotengwa ?
 

BM,

Unapokuwa na adaptive knowledge halafu uchumi unaruhusu ku-commission hayo ma-project hapo ndipo textbook knowledge na school project zinapopata opportunity ya kumchallenge kijana anayeingia katika workforce kufanya vizuri.

Sasa sisi uchumi wetu mdogo, hata hao graduates wanakaa mtaani miaka sita, by the time wakipata ajira hata hiyo knowledge ya ku cram nayo inakuwa ishaanza kutoweka.

Somehow it becomes a vicious cycle, uchumi mdogo partly kwa sababu hatuna wataalamu imaginative, na hatuna wataalamu imaginative kwa sababu uchumi mdogo.

To top it off wale wataalamu imaginative wachache (the Sarungi's Mwandosya etc) wanapelekwa kwenye administration badala ya kutia chachu vijana wengine.
 

Ni vicious kubwa. Nirudi Tanzania na kwa kile nilichosomea na uzoefu wangu wa kazi ninaweza kuunda timu au kampuni ya kupata faida na kuzibakia pesa palepale nyumbani. Lakini hiyo mizunguko yake na 10 percent ya kupata tenda siiwezi.

Ukweli nina wazazi wawili waliostaafu wanaonitegemea na sina mpango wa kucheza bahati nasibu. Kama ni uzalendo namwachia Mwanakijiji na Aunt Mwafrika wa kike.
 

Mkubwa..sio wote waliopo nnje ni kwamba wamekimbia makwao..WA(T)upo wenye uwezo wa kufanya mambo mbali mbali ya maana..lakini hatukubaliani na jinsi mfumo unavyoenda na hivyo tunaona ni rahisi kufanya kazi na hawa wanaotukubali na ku appreciate uwezo wa vichwa vyetu, na hivyo kutupa dhamana ya kufanya na kusimamia shughuli mbali mbali katika taasisi zao.. kuwepo hapa JF na kuchangia maada pindi pale tunapoona mfumo unaenda ndivyo isivyo ni wajibu wetu kama watanzania ambao tumeelimika na kuhekimika..Pumzika salama tu ndugu yangu..usiku mwema..
 
Shukrani sana mkubwa..kama ulivyosema ndani ya JF hatuonani, ila michango yetu ni identity tosha..wapo humu humu..once again shukrani..
 

Nadhani neno la msingi hapa ni imaginative! Kitu ambacho wasomi wetu wengi hawana. Uchumi mdogo si kisingizio. creativity yetu ndiyo utaoukuza.

Nitatoa mfano rahisi. Kuna wakina dada waligundua kuwa kuna wafanyakazi maofisini wanakufa na tai shingoni kwa sababu wanaona aibu kwenda kwa mama nitilie wakati uwezo wa kwenda kwenye restaurant za maana hawana. Wakina dada hawa wakaanza kuzungukia maofisini na kuchukua oda za chakula ambacho walikuwa wanawapelekea wateja wao kila mchana! Wote tunajua vijana wengi hata wakina Bin Maryam ambao uzalendo umewashinda wangependa kujijengea kibanda nyumbani ambacho kingewasitiri wazee wake wastaafu na yeye mwenyewe kumpatia heshima katika jamii. Ni makandarasi wangapi, wahandisi, ma'architects' waliolichangamkia soko hili la wakina Bin Maryam kwa zati? Hasa ukitambua kuwa kijana anabeba maboksi, majukumu kibao lakini anaweza kujipigapiga angalau! Waheshimiwa huku hawaoni wanashinda kugombea vitenda maana hivyo vina ulaji na status! Mimi naamini kama wakikata overheads, na kujikita katika kuangalia namna gani wanavyoweza kumpunguzia gharama Bin maryam bila kuathiri ubora na kuonyesha uaminifu wa hali ya juu, wasingekosa kazi. Tatizo letu hatutaki kuanza na baiskeli hata kama ni uwezo wetu, wote tunataka Hummer! Tutafika kweli kwa mwendo huo? Tunalaumu serikali kwa kutokuwapatia mikopo bila kujiuliza hiyo mikopo yote ya awali kama tumelipa!
 
Bado nitaendela kusema kwamba SYSTEM nzima ni bmovu na inahitaji changes...Tanzania bado tunamtumia Punda aliyechoka....Bila mabadiliko ya Uongozi namfumo mzima wa serikali ikiwa ni pamoja na katiba Tanzania haiwezi kubadilika hata kama kina Bin Maryam 10,000 watapelekwa TZ leo hii kwa sababu watakachokuta ni utaratibu unawalazimu kumwendesha Punda yule yule aliyechoka..sasa hata kama utakuwa na elimu ama maarifa ya aina yeyote huwezi kufanya kitu isipokuwa ku deal na Punda kwanza...
Ndio maana nasema hivi Tanzania NJAA sote tupo ktk mafungu mawili moja lipo la wale wanaokula kwa Uma, kisu na kijiko kutokana na elimu waliyopewa na mzungu lakini hawafahamu kwa nini mzungu alitumia vitu hivyo to begin with - MALIMBUKENI, wameshindwa kuitumia elimu yao ktk mazingara yetu.
Na kundi la Pili ndio kina sisi tulokaa janvini, chakula kipo ktk sinia moja, mpango ni mashindano ya shibe tu...
Mkusanyiko wa makundi haya hjauwezi kuwa na mwelekeo mzurti hata kidogo na ndio maana wenyewe waliokwisha fahamu haya husema TUTABANANA HUMU HUMU...hawafikirii changes zozote.
hadi leo miundombinu iliyojengwa toka wakati wa Nyerere kama sio mkoloni ndio inaendesha nchi (Punda aliyechoka) pamoja na ukweli kwamba kuna ongezeko kubwa sana la watu Tanzania.
 
Kuna kitu kimebadilika?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…