Tuko serious Lowassa awe Rais?

Tuko serious Lowassa awe Rais?

Lowasa ni janga la taifa pia ni janga sugu la wazawa mungu atuepushe na dhahama hii isitukute tutakuwa tumepata hasara kubwa sana kama taifa.

Lowassa hawezi kuwa janga la Taifa kwa sababu yeye anabeba bendera ya UKAWA ambao ajenda yao kuu iliyowaunganisha ni kutuletea katiba sisi wananchi tuliyoipendekeza; katiba tulitoipendekeza ndio itakuwa mkombozi wa sisi walala hoi tofauti na katiba ya ccm inayotaka kutukandamiza milele, yaani Kikwete na genge lake watawale nchi hii bila ukomo na waendelee kutuibia na kuficha fedha huko ughaibuni!!!

Lowassa akiingia madarakani kitu cha kwanza ni kutupa katiba yetu period.
 
Magufuli ni Rais wa awamu ya tano tumwamini ataweza kukutumikia vema watanzania kunyoosha mafisadi.

Yeye mwenyeweni fisadi.......halafu ni manager na siyo leader kabisa.....but anahitaji washauri hasa kipindi hiki cha kampeni manake anachoongea anawakilisha wapinzani....
 
Wakuu, Natumaini wote ni wazima wa afya.

Sasa twende kwenye mada. Ndugu yetu Lowassa ni mbunge kwa miaka 25 katika jimbo la Monduli. Na amekuwa akinadiwa kama mchapa kazi na mwenye maamuzi magumu.

Lakini ustawi wa maendeleo katika jimbo la Monduli ni tofauti na kile tunachoambiwa.

Lakini tafiti za UNDP, zinabainisha illiteracy rate au wanaojua kusoma ni wachache mno, ajira ni tatizo kubwa sana monduli... Vijana wengi wamekimbilia Arusha, Namanga, Nairobi, DSM na Zanzibar kama walinzi, wasusi, na wauza shanga.

Hii ni aibu kubwa iliyofunikwa na fedha isionekane, michango kwenye taflija mbali mbali nayo imekuwa kama kisafishio cha aibu hii. Jaribu kufananisha kazi anayo fanya Deo Firikunjombe Ludewa ndani ya muda mchache na kazi ya Lowassa monduli ndani ya miaka 25.

Kinachoonekana kwa jicho la pili ni maandalizi ya muda mrefu ya kutaka urais kwa gharama zozote ikiwa ni pamoja na kuupumbaza umma kwa techniques mbali mbali.

Namaliza kwa kusema, zile milioni Mia 200 anazotoa Lowassa kwenye taflija mbali mbali, zingeweza kutengeneza ajira za wamasai wanao suka dada zetu pale mwenge, Ubungo etc.

Tajiri siku zote hushughulika na matajiri wenzake.

Tupo serious kuiondoa CCM madarakani...
 
Kwa mamlaka aliyonayo rais (kikatiba) bora rais safi kwenye chama kichafu maana ana uwezo wa kufurukuta na kuwanyoosha....nchi hii inataka rais aliye na political will baas...waliopita sidhani kama walishindwa...hawakuwa nayo...nina imani kubwa sana na Magufuli...hata ukimtizama usoni....unaona kabisa jamaa ni mkweli...

Hawezi kulibadili hili JINAMIZI (CCM) hana jeuri hiyo, na wala hujasikia akiligusia
 
Tupo serious kuiondoa CCM madarakani...

Umeniwahi, huyu kumbe hajajua kwamba tatizo ni CCM. Yale mambo ya ndiyoooooooooo hata kwenye hoja ambazo ziko wazi kabisa kwamba zinawaumiza waTanzania, zimewaudhi watu. Kama yuko serious ajitahidi kuyaangalia hayo, atajua kwanini watu wanamtaka Lowassa. Dr. Magufuli ameshayatambua hayo, ndiyo maana kila anapopita anawaomba waTanzania wasiiue CCM.
 
Ndio Lowasa Ntampigia Kura yangu ya ndio.
 
Lowasa mimi huwa sitaki hata kumuona mwizi na fisadi asiyekuwa na aibu kwa kuibia watanzania halafu anajidai yeye ni mchapa kazi.
Mpeleke mahakamani usiishie kulialia tu au huna uthubutu???
 
Yes.very serious.LOWASA is our next president.whether you like it or not.vote for hon.LOWASA.
 
Tokea Lowassa awavutie maji wananchi wa jimbo la Monduli, na kuwajengea madarasa ya sekondary kila kata maccm yalimchukia to the maximum.
CCM ilimchukia mno Lowassa pia baada ya kuwasaidia vijana wa kimasai kupata ajira kwenye hifadhi za taifa kama Tanapa, Ngorongoro conservation, pia kwenye makampuni ya uchimbaji wa madini, TRA nk.


CCM hawakupenda kabisa jamii ya watu wa Monduli waone mlango wa darasa.

Wamasai ni wafugaji, huyu mleta mada ni kenge maana hakuna hata ukosefu wa ajira.
Inaonekana CCM imefanya mambo makubwa sana heko CCM. Mchague Magufuli ndugu. #HapaKaziTu
 
Bora mchafu mmoja aingie kwa wasafi, kuliko msafi mmoja aingie kwenye kundi la wachafu
 
kwanza kabisa una kiswahli kibovu kama cha mwanafunzi wa darasa la 3, SIO TAFLIJA NI TAFRIJA. ...na ikiwezekana kumwajiabisha nacho...
Na wewe: sio kumwajiabisha bali kumwajibisha.
 
Lowasa mimi huwa sitaki hata kumuona mwizi na fisadi asiyekuwa na aibu kwa kuibia watanzania halafu anajidai yeye ni mchapa kazi.

Lowasa akiwa rais maana yake nchi itakuwa chini ya kina Lowasa, Rostam, Karamaji, Chenge na wale wengine bila kujali nani yuko chama gani cha siasa. Nikijaribu kufikiria hawa watu eti wamekutana wanajadili namna ya kuiletea maendeleo Tanzania kweli sipati picha. Yaani watu wenye tuhuma lukuki za kuikosesha Tanzania mapato na kuingiza mifukoni mwao leo ndio wanajadili maendeleo ya watanzania!!! Jamani tuache utani.
 
Well said mkuu

Correct 100%. Mbowe not chadema is taking Lowasa for a ride and will dump by 1st Nov 2015. Serous chadema know that lowasa is a non starter. He is not whatvl he seems to be. Wafugaji wanajua utajiri wake wa mifugo lkn ni mchoyo. Marehemu Sokoine alichimba mabwawa makubwa ya kunyweshea mifugo lkn leo hayapo. Tulitegemea Monduli au mkoa wa Arusha kungekuwa na viwanda vya maziwa, ngozi na hata viatu ili kuwapa wamasai wapiga kura wake ajira na utajiri lkn Monduli kuna umaskini wa kutupwa. He is a performing artist kama Diamond tu anayewakusanya watu na kuwaacha walivyokuja. Ukawa sasa ni ccm B tu.
 
Tusubiri kesho upepo utakavyobadilika kwa mgombea wa UKAWA kushindwa kueleza sera zake na kuishia kuhutubia kwa dakika 7:08
 
Back
Top Bottom