Wakuu, Natumaini wote ni wazima wa afya.
Sasa twende kwenye mada. Ndugu yetu Lowassa ni mbunge kwa miaka 25 katika jimbo la Monduli. Na amekuwa akinadiwa kama mchapa kazi na mwenye maamuzi magumu.
Lakini ustawi wa maendeleo katika jimbo la Monduli ni tofauti na kile tunachoambiwa.
Lakini tafiti za UNDP, zinabainisha illiteracy rate au wanaojua kusoma ni wachache mno, ajira ni tatizo kubwa sana monduli... Vijana wengi wamekimbilia Arusha, Namanga, Nairobi, DSM na Zanzibar kama walinzi, wasusi, na wauza shanga.
Hii ni aibu kubwa iliyofunikwa na fedha isionekane, michango kwenye taflija mbali mbali nayo imekuwa kama kisafishio cha aibu hii. Jaribu kufananisha kazi anayo fanya Deo Firikunjombe Ludewa ndani ya muda mchache na kazi ya Lowassa monduli ndani ya miaka 25.
Kinachoonekana kwa jicho la pili ni maandalizi ya muda mrefu ya kutaka urais kwa gharama zozote ikiwa ni pamoja na kuupumbaza umma kwa techniques mbali mbali.
Namaliza kwa kusema, zile milioni Mia 200 anazotoa Lowassa kwenye taflija mbali mbali, zingeweza kutengeneza ajira za wamasai wanao suka dada zetu pale mwenge, Ubungo etc.
Tajiri siku zote hushughulika na matajiri wenzake.