Tujikumbushie matukio na mambo ya miaka 2000

Tujikumbushie matukio na mambo ya miaka 2000

Usinikumbushe enzi ze ambapo ukimwi ulikuwa kwenye kilele chake. Nakumbuka nilifungua duka kubwa la kondom kwa kuamini kuwa wateje watakuwa wengi lakini niliambulia hasara.

Enzi hizo bado sijaanza kumgonga bibie Mnachihanguuu .
ukimwi wa kipindi hicho ulikuwa ni ukimwi haswa, ukiupata unakwenda na maji fasta. Watu walikondeana mpaka inatisha, tofauti na siku hizi kuna ARV watu wanabugia na kunenepa huwezijua kama mtu ana UKIMWI
 
Ndio miaka ambayo muziki wa bongo fleva unashika hatamu kwenye anga la Tanzania na kuishusha miziki ya congo, dansi na taarabu. Mdj wakali wakali kama kina sebastian maganga, abubakary sadiki wanaibuka kuupiga sana muziki wa bongo fleva katika vituo vya redio
 
Miaka hiyo luninga ya ITV aliibuka mtangazaji wa vipindi vya muziki aliyejipatia umaarufu wa kupangilia aina ya muziki kuanzia jumatatu mpaka jumapili kila siku ina aina yake ya muziki. Huyo jamaa aliitwa Misanya Bingi a.k.a Mnyamwezi. Pia kulikuwa na mzee wa Charanga, hayati Charles Hilary na kipindi chake cha Charanga time. Mipangilio ya vipindi vya muziki nyakati hizo ilieleweka tofauti na siku hizi hawa vijana wanaweka miziki yote katika faili moja, mpangilio unakuwa si mzuri kusikiliza muziki tofautitofauti kwa kipindi kimoja
 
Hii ndio miaka millenials wapo primary and secondary huku bado wadogo zao gen z wapo kwenye mifuko na mayai🤣

Miaka hio tunsulzana mbna isidingo Haiishi maana tangu late 90s watu wanaangalia😬

Miaka 2000 ndio ilikuwa golden age ya burudani na media katika nchi hii

Between 2000 hadi 2009 taifa lilikuwa limeshatengeneza watu ambao leo ni legends katika taifa hili.

Maigizo/mchezo ya kaole ndani ya ITV, pale ndipo tulipomtambua kanumba na ray, hadi wao kuanza safari ya filamu. Ile filamu ya girlfriend ya wakina TID ilishika kasi sana😁

Nakumbuka kanda za albamu za wasanii zilimiminika katika nyumba za watu, mimi binafsi nakumbuka albamu ya wachuja nafaka, ile nyambizi ya dully sykes, maisha na muziki ya mr 2, etc zilikuwa pale home.

Miaka 2000 star wa mpila alikuwa juma kaseja, huku mastaa wengine wakiwa wakina sunta, huyu dada ambae alitaka kula hela za mengi zote😁,

Miaka 2000 ilikuw na original comedians, wakina kibakuli🤣, bambo, pembe, joti na mpoki pamoja wakifanya vituko😂

Miaka ya 2000 yalitokea matangazo ya TV maarufu, kama chai jaba, lile tangazo la wasanii kuimba usione soo sema nae nafikiri kampeni ya ugonjwa wa ukimwi, alafu matangazl ya condom yalikuwa mengi sanaa maana ukimwi ulikuwa mkali 🤣

Miaka ya 2000 ujambazi hatarii, kuna tukio moja la kuvamia benk hata itv walionesha tena kwa kuiba kuiba marisadi yanapiga (taarifa ya habari)
View attachment 3536714
View attachment 3536715
View attachment 3536717
Vitu kama hivi watoto wa juzi kina Harmful hawawezi vijua,
Kijana njoo uone jinsi wakubwa zako tulivyokuwa tunaishi 😁
 
Vitu pekee nilivyokuwa najua kufanya miaka ya 2000

Journey to the west
Need for speed 2




Journey_to_the_West_(1986_TV_series).jpg
hq720.jpg
 
Miaka hiyo kulikuwa na tv chache kama DTV na ndugu zake kina,CTN channel ten na C2C, naona imebaki channel ten tu na imekuwa mali ya CCM. Media zingine ilikuwa ni ITV, Star tv na TVT ambayo kwa sasa ni TBC1. Tv bora wakati huo ilikuwa ni ITV tu ndio ilikuwa na watazamaji wengi kutokana na vipindi vyake na mawimbi ya upatikanaji wake. Huu ni upande wa tv kwa wakati huo
 
Noti ya shilingi elfu kumi ya wakati huo ilikuwa bluu, a.k.a bluu bluu, ya sasa ni nyenkundu a.k.a msimbazi, wekundu wa msimbazi. Hiyo noti ya bluu ilipelekea dogo mmoja mwanamuziki wa kizazi kipya aliyejiita Lil Sama kupata idea ya kutunga wimbo wenye maneno bluu bluu, kila kitu kwake ikawa ni bluu bluu tu. Hatimaye dogo huyo akabadili jina la kiuanamuziki na kujiita Mr. Blue, asili ya jina hilo ni noti ya elfu kumi yenye rangi ya bluu ya wakati ule
 
Miaka hiyo liliibuka bifu la wanamuziki wa bongo fleva wawili wa kike, Zay B na Sister P. Wakaanza kutungiana nyimbo kupeana makavu bila chenga, nyimbo zikaenda hewani maredioni na kupokelewa vema na mashabiki wao. Bifu likawa zito ikabidi waandishi wa habari wawakutanishe ana kwa ana waombane msamaha ugomvi uishe. Mmoja akawa hataki 'maridhiano' tifu likabaki vilevile. Haijulikani bifu lao liliishaje na hao wanamuziki haijulikani kama wapo kwenye game au waliishaachana na muziki, bila shaka umri umesonga na wako nje ya game la muziki
 
Jumapili nilikuwa natengeneza means nyingi sana ili nisiende kanisani kama kujifanya naumwa manake asubuhi kuna cartoon kina bakugan,ben ten ...hayakuwa mambo ya kukosa haya
Maisha yame tusurprise Sana, Leo hii naweza maliza miezi mitatu bila kutizama.

Sitasahau alhamisi kuu niliondoka kwenye ibada kabla ya kumalizika ili ni wahi zecomed east Africa TV!
 
Hii Bongo fm ndani TBC enzi hizo iliitwa City radio kisha ikaitwa PRT na baadaye ikaitwa TBC fm, hatimaye sasa inaitwa Bongo fm. Hii ilianzishwa kushindana na redio mpya za wakati huo zilizopendwa na vijana kwa maudhui yake tofauti na RTD ya kipindi hicho
 
Basi ulikuwa wakishua wajuba tulikuwa enzi hizo games na movies mpaka vibanda umiza , majirani Wenye Tv masharti kibao wanavimba

Wazazi walikuwa hawapendi tukae kae mtaani kwa hiyo waliweka means za kutufanya tukae ndani kama hivyo tunaletewa games tofauti tofauti kwenye computer ya nyumbani

Ushua? Sidhani 😂
 
Kila mwenye simu alionekana ana mobitel, Mobitel ilikuwa ni kampuni ya mawasiliano ya simu za mkononi. Kwa hiyo ukiwa na simu ya mkononi utasemwa una mobitel. Ilipelekea mwanamuziki mmoja wa kike mnenguaji kuitwa kimobitel
 
Kipindi Bora kabisa dunia imewahi kupitia ni 2000s hadi 2010

Filamu
Jumba la dhahabu ya Tuesday Kihangala
Shumileta na Nsyuka ya Musa Banzi na Sultan Tamba
Johari njia panda ya ray na kanumba
Misukosuko ya J bras na Seba

Muziki
1. Juma nature na hakuna kulala, ugali, mugambo wanaruka na kukanyagana
3. Temba na chege na Tmk wanaume family na Dar mpaka Moto
4. Mb Dogg na sagabrasha, latifa
5. Z anto na bint kiziwi na mpenzi jini
6. Ferooz na profess J state he
7. Mandojo na domokaya bila kusahai sog dogg

TV NA RADIO
1. Chemsha bongo ya redio one stereo
2. Mizengwe ya ITV
3. Nani zaidi ya redio one
4. Kwetu fleva ya DJ majizo ya magic FM
5. Mchezo ya Mzee jangala radio Tanzania
6. Matangazo ya chai Jaba na fataki na funda moja la ziada litakuumbua
7. Channeli ya C2C mtu kwao ilikuwa inapiga muziki balaa
8. Redio free afrika na kipindi cha sitasahau na je huu ni uungwa cha fredwaa

Kulikuwa ni kipindi cha dhahabu kwa kweli haitakaa itokee, sasa hv ni kama vile kila kitu kimepoteza mvuto
Hance Mtanashati 😆😆
 
Back
Top Bottom