Tujikumbushe kidogo

Tujikumbushe kidogo

Magonjwa Mtambuka

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2016
Posts
34,023
Reaction score
32,804
Duh, mambo ni mengi lakini muda ni mchache.

1581815690600.png


1581816482900.png
 
Ahaaa hizi picha kuna watu wanatamani zipotee kabisa lkn haiwezekani

Sent using Jamii Forums mobile app
Hakuna mpenda mabadiliko halisi anayetaka kupoteza kumbukumbu. Safari ya kutafuta mabadiliko imeanza siku nyingi nchini na wengine walifanya makubwa zaidi ya haya.

Kina KAMBONA walitafutiwa kila jina baya na kuwa wakimbizi, wakaimwa wameolewa lakini walichokipigania (Vyama vingi) kilifanikiwa kabla hawajafa. Bibi Titi, Mohamed Babu, Nassoro Moyo na wenzao waliokataa kuburuzwa waliishi kuona waliyopigania yakitokea baada ya kuishiwa nguvu za mwili.

Picha hizo ni kielelezo halisi cha wananchi waliochoshwa na Ukaburu wa CCM na wako tayari kujenga urafiki na yeyote atakayeqasaidia kuitoa CCM madarakani. Tena CCM ya sasa ya kutesa na kuua,!!?

Tutaendelea kupigana kuiondoa ccm na vibaraka wao kama nyie hata kama tutakaojiunga nao watatusaliti na kurudi nyuma. Hii ni vita, hatuwezi kuwa na ujasiri unaofanana, tukikatwa tunachipuka, tunaota tunasonga mbele.

Hata Afrika Kusini kulikuwa na Waafrika waliokuwa upande wa Makaburu tangu mwanzo kwa vile walifaidi katika utawala wao, lakini waliponyimwa faida za utawala walirudi kwa waafrika wenzao na waliminywa kidogo wakarudi kwa Makaburu. Usaliti ni sehemu ya mapambano, huwezi kuacha kupambana kwa sababu silaha imebackfire. Toa risasi weka nyingine piga. Aluta Continua!!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom