Tujadili kuhusu mtandao wa Halotel

Tujadili kuhusu mtandao wa Halotel

Mtandao wa simu mpya toka Vietnam Halotel (vietel),utazinduliwa rasmi jumatano 14/10/2015.
Ni mtandao utakaotoa Huduma kwa bei ndogo kabisa kuliko mitandao yote nchi nzima na Huduma zao zitapatikana vijijini,njiani,mijini,maporini na baharini,kila sehemu utayokua utakua hewani,
Watazindua na smart phones zao zenye ubora na garama nafuu kabisa,kwa kuzingatia kipato cha mtanzania Wa kawaida,
Mimi nitakuwa Wa kwanza kununua line ya halotel na smart phone ya halotel(vietel) sababu nimechoka unyonyaji Wa Vodacom na Airtel.
Kwani unakimbizwa,au umeambiwa uwahi kutoa habari utapewa zawadi,unasema utakuwa rahisi kupita mitandao yote tueleze kivipi,kwa mfano ungesema kwa sekunde au dakika bei yake itakuwa hivi,kupiga kwenda mitandao fulani itakuwa kiasi hiki kwa muda wa sekundu au dakika,kifurushi cha data kituwa GB fulani kwa TZS halafu hapo ndio tuone huo utofauti,lasivyo subiri kuanza ,ukipata maelezo ya kina ndio uje utuhabarishe hapa kwa sasa hayo maelezo ni kama propanganda za uchaguzi wa raisi,wabunge na madiwani utakaofanyika mwezi huu
 
Mkuu huo mtandao si mchezo juzikat nilienda boda Rusumo kupitia Dodoma Singida Tabora Kahama Geita adi Kagera Ngara Rusomo halotel wapo. sehemu nyingine mapori ya hatari nakuta halotel wamefika wamesimamisha nguzo na minara yao hawa jamaa ni balaa. naskia wakipita sehem wakikuta network yao iko 3G tu wanawela kambi adi ifike 4G hawa jama hawataki mchezo.

Hizi habari za kusikia si nzuri kabisa . . ukweli ni kwamba Viettel (halotel) Wamepewa Leseni ya kutoa huduma za mawasiliano kwa mfumo wa 2G & 3G pekee.
 
Tunataka na Tanesco iingie ktk soko shindani kama hawa!
 
Nimewasikia Hao jamaa, wako mda wanaandaa infrastructure throughout the country. Wageni kibao wako mtaani wanchimba mitaro
 
copy & paste.

Katika taarifa iliyotolewa na TCRA imejikita kuelezea jambo lilotokea na hii ikiwa ni pamoja na kuelezea ni jinsi gani gharama za mawasiliano nchini bado zipo chini kulinganisha na wastani wa gharama duniani kote.


Je kuna lolote kubwa lilotolewa uamuzi?

6¦1 Imeagiza watoa huduma kuzingatia sheria kila wanapobadilisha bei za bidhaa zao;
(a) Kuziwasilisha kwa Mamlaka kabla hazijaanza kutumika,
(b) Kutoa taarifa za tozo za msingi na vifurushi kwa njia ambayo itaweza kuwafikia watumiaji wa simu za mkonini,
(c) Kupitia upya bei na tozo mpya kwa kuzingatia mapendekezo haya na kuwasilisha kwa Mamlaka kama inavyotakiwa kwa mujibu wa Kanuni za EPOCA za 2011 kuhusu tozo ( EPOCA (Tariff Regulation of 2011).

6¦1 Imewaagiza watoa huduma kuhakikisha kwamba mabadiliko yoyote yanatekelezwa kidogo kidogo na sio ya ghafla ili kuepuka sintofahamu katika soko;
(a) TCRA inawaagiza watoa huduma kuwapa wateja wao nafasi ya kuchagua mpangilio wa vifurushi tofauti kwa huduma wanazohitaji:

-Kifurushi cha mazungumzo, Meseji na Intaneti cha siku, siku saba au mwezi ambacho kinampa mtumiaji uhuru wa kuchagua kiasi ambacho wako tayari kulipia kwa mazungumzo, meseji na intaneti.
(b) Vifurushi vya mazungumzo tu: Hivi navyo kwa siku saba au siku 30 kwa ajili ya watumiaji ambao hawahitaji intaneti na meseji kwa sababu moja au nyingine na wako tayari kulipia vifurushi vya sauti pekee;

(c) Vifurushi cha Meseji (SMS) tu: Kwa watumiaji ambao hawahitaji intaneti au muda wa mazungumzo kwa sababu moja au nyingine, au ambao wanatumia SMS kwa wingi. Hivi navyo viwe kwa siku, siku saba au siku 30 kwa bei ambazo mtumiaji atachagua.

(d) Vifurushi vya Intaneti tu: Kwa watumiaji ambao wanatumia intaneti kwa wingi. Hawa wapewe uhuru wa kuchagua vifurushi vya siku, siku saba au siku 30.
 

Attachments

  • wastani-gharama-kupiga-simu-tanzania.jpg
    wastani-gharama-kupiga-simu-tanzania.jpg
    12.3 KB · Views: 384
Ni kampuni ya jeshi la vietnam ..wana mtaji wa kutosha wataleta ushindani sana kama walivyofanya msumbiji.
 
nawasubiri sana nimechoka na haya matapeli mengine. mabadilikoooooooooo.......! Halotel

Lowassa ana hisa nyingi sana Vodacom ndio maana gharama za Vodacom ziko juu. Kama kweli lowassa angekuwa anauchungu na maskini wa Tanzania asingekubali kampuni ambayo na yeye ana hisa iendelee kuwanyonya Watanzania. Halafu bila aibu anasimama kwenye majukwaa na kusema "nauchukia sana umaskini". Ni kweli anauchukia umaskini ndio maana anawanyonya na kuwakamua maskini kila siku. #HapaKaziTu CHAGUA MAGUFULI.
 
Mabadilikooooooooooooooo

Fisadi papa lowassa ana hisa nyingi sana Vodacom ndio maana Vodacom inawanyonya Watanzania bila aibu wala uwoga. Halafu vilaza mnaonyonywa eti mnataka mabadiliko ya kumpeleka mnyonyaji ikulu, huko si ndio atawakamua kisawa sawa! Lowassa angekuwa na uchungu na hii inchi, asingeruhusu Vodacom kuwanyonya Watanzania wakati yeye pia namiliki sehemu ya Vodacom. Tafakari Chukua Hatua. CHAGUA MAGUFULI #HapaKaziTu
 
Lowassa ana hisa nyingi sana Vodacom ndio maana gharama za Vodacom ziko juu. Kama kweli lowassa angekuwa anauchungu na maskini wa Tanzania asingekubali kampuni ambayo na yeye ana hisa iendelee kuwanyonya Watanzania. Halafu bila aibu anasimama kwenye majukwaa na kusema "nauchukia sana umaskini". Ni kweli anauchukia umaskini ndio maana anawanyonya na kuwakamua maskini kila siku. #HapaKaziTu CHAGUA MAGUFULI.


Ana hisa ngapi? Taja numbers.
 
Lowassa ana hisa nyingi sana Vodacom ndio maana gharama za Vodacom ziko juu. Kama kweli lowassa angekuwa anauchungu na maskini wa Tanzania asingekubali kampuni ambayo na yeye ana hisa iendelee kuwanyonya Watanzania. Halafu bila aibu anasimama kwenye majukwaa na kusema "nauchukia sana umaskini". Ni kweli anauchukia umaskini ndio maana anawanyonya na kuwakamua maskini kila siku. #HapaKaziTu CHAGUA MAGUFULI.

Kumbe voda inamuhusu Edo?Basi ngoja tumchangie kwanza ili aitoe mbio ccm kisha tutayamaliza baadae haya mambo yetu na raisi wetu.
 
Mtandao wa simu mpya toka Vietnam Halotel (vietel),utazinduliwa rasmi jumatano 14/10/2015.
Ni mtandao utakaotoa Huduma kwa bei ndogo kabisa kuliko mitandao yote nchi nzima na Huduma zao zitapatikana vijijini,njiani,mijini,maporini na baharini,kila sehemu utayokua utakua hewani,
Watazindua na smart phones zao zenye ubora na garama nafuu kabisa,kwa kuzingatia kipato cha mtanzania Wa kawaida,
Mimi nitakuwa Wa kwanza kununua line ya halotel na smart phone ya halotel(vietel) sababu nimechoka unyonyaji Wa Vodacom na Airtel.


Poa sana kama ni hivyo. Tujuze zaidi ukisha ununua nami nikufuate, maana kweli nimechoka na mitandao ya Tigo na Voda.
 
Nawafanye haraka!! Nishachoka mitandao mumiani ya voda na airtel kama nilivyoichoka CCM.
 
nawasubiri sana nimechoka na haya matapeli mengine. mabadilikoooooooooo.......! Halotel

Ungejua hiyo Vietel na jinsi ambavyo iko kinyume kisheria na TTCL ungechoka!!!??? Hii ndiyo TZ! Anyway kama ni gharama ndogo siyo neno!
 
Lowassa ana hisa nyingi sana Vodacom ndio maana gharama za Vodacom ziko juu. Kama kweli lowassa angekuwa anauchungu na maskini wa Tanzania asingekubali kampuni ambayo na yeye ana hisa iendelee kuwanyonya Watanzania. Halafu bila aibu anasimama kwenye majukwaa na kusema "nauchukia sana umaskini". Ni kweli anauchukia umaskini ndio maana anawanyonya na kuwakamua maskini kila siku. #HapaKaziTu CHAGUA MAGUFULI.

Na hiyo Vietel ya akina nani? illingiaje hapa TZ?? Iko kwenye mkongo wa taifa??
 
Back
Top Bottom