China na nchi za Afrika kushirikiana kwenye kujenga Jumuiya yenye mustakbali wa pamoja kwenye mambo ya mtandao wa Internet

China na nchi za Afrika kushirikiana kwenye kujenga Jumuiya yenye mustakbali wa pamoja kwenye mambo ya mtandao wa Internet

ldleo

JF-Expert Member
Joined
Jan 9, 2010
Posts
1,285
Reaction score
1,249
VCG111603348423.jpg


Mwezi Agosti mwaka 2021, China ilizindua Mpango wa China na Afrika wa Kujenga Jumuiya yenye mustakbali wa pamoja kwenye mambo ya mtandao wa internet, na kuwa jukwaa la kwanza la Maendeleo na Ushirikiano kwenye mambo ya mtandao wa Internet kati ya China na Afrika. Ushirikiano huo ni mwendelezo wa juhudi ambazo tayari zimefanywa kati ya pande mbili, kuwawezesha watu wa Afrika kuwa na huduma ya Internet.



Tehama ni moja kati ya sekta zenye maendeleo ya kasi kwenye nchi za Afrika. Licha ya maendeleo yaliyopatikana ikiwa ni pamoja na kufikisha mkonga wa mawasiliano (optic fibre) katika sehemu nyingi na kuongezeka kwa watu wanaotumia internet kwa njia ya simu na internet, usalama wa internet bado ni eneo ambalo nchi nyingi za Afrika ziko nyuma.



China ambayo jamii yake kwa kiwango kikubwa imeunganishwa na mtandao wa internet, imepitia changamoto mbalimbali za kiusalama kwenye eneo hilo na sasa kimsingi mtandao wa internet wa China ni safi. Kwenye nchi za Afrika changamoto kama ukatili wa kimtandao, wizi wa kimtandao, habari za kupotosha na za uzushi zinazoleta taharuki, na hata wizi wa pesa zimekuwa zinajitokeza mara kwa mara.



Wakati huo huo nchi nyingi za Afrika zinatambua umuhimu wa mtandao wa internet kwenye maswala ya uchumi, kwa hiyo zimekuwa zikihimiza maendeleo ya uchumi wa kidigitali. Kutokana na mahitaji ya maendeleo katika eneo hilo, kwenye mkutano wa Mawaziri wa Kuratibu Utekelezaji wa Hatua za ufuatiliaji na Ushirikiano wa baraza la ushirikiano kati ya China na Afrika (2025-2027) uliofanyika mwaka jana, China ilitangaza kuwa iko tayari kutoa msaada na kushirikiana na nchi za Afrika kuendeleza mtandao wa internet ulio wa haki, wenye usawa, wazi, jumuishi, salama na thabiti zaidi, na kuharakisha juhudi za kujenga Jumuiya yenye mustakbali wa pamoja kati ya China na Afrika kwenye masuala ya mtandao wa Internet.



China ilitangaza kuwa tayari kushirikiana na nchi za Afrika katika miundombinu ya mawasiliano, ikiwa ni pamoja na uzalishaji wa vifaa vya mawasiliano na kufanya mawasiliano na ushirikiano mkubwa zaidi na wenzao wa Afrika, na kuwezesha makampuni yenye uwezo ya China kuwekeza kwenye maendeleo ya miradi ya mikonga ya mawasiliano kwenye baharini za kimataifa barani Afrika. Makampuni hayo pia yatahimizwa kufanya kazi na watoa huduma za mawasiliano wa Afrika katika usambazaji wa huduma ya 5G.



Katika hatua nyingine China pia ilitangaza kuwa itaunda “mtandao wa Ushirikiano wa Makampuni ya Internet ya China barani Afrika” ili kuruhusu makampuni zaidi ya internet ya China kupanua biashara zao za ushirikiano barani Afrika, ili kuweka jukwaa la mawasiliano kati ya makampuni ya internet kutoka pande zote mbili kwa ajili ya kubadilishana na ushirikiano wa kina wa internet kati ya China na Afrika.



Mbali na hayo, China pia iko tayari kufanya kazi na nchi za Afrika kupanua ushirikiano wa “Njia ya Hariri ya Biashara ya Mtandao wa Internet” ili kuanzisha mfumo wa ushirikiano wa biashara ya mtandao wa internet. Ikiwa ni sehemu ya juhudi hizo, China imefanya aina mbalimbali za sherehe za ununuzi wa bidhaa bora za Afrika na shughuli za kuhimiza biashara ya utalii.
 
Yan viongozi wa Africa kila Ngoma inayo pigwa nje wao wanaicheza,
Sio kwa juhudi viongozi wa Africa wakijenga uchumi wao wa ndani ili waje kuuza nje
 
Nadhani baadhi tutakuwa tunajua kule kuna the great firewall na kila kitu kiko controlled sana.

Je, huku kwetu Afrika wanakuja kutusaidia kuzuia wezi wa mtandao, au wanatuletea mfumo wa kudhibiti raia wasikosoe serikali zao?
 
Nadhani baadhi tutakuwa tunajua kule kuna the great firewall na kila kitu kiko controlled sana.

Je, huku kwetu Afrika wanakuja kutusaidia kuzuia wezi wa mtandao, au wanatuletea mfumo wa kudhibiti raia wasikosoe serikali zao?
Hakuna kitu kama hicho, china inawadanganya viongozi wa Africa TU 😂.

Tena Bora western technology ina uwanda mpana Nchi kama Nchi inaweza kutumia wataalamu wake wa ndani ku implement vizuri. Kuliko hizo china state controlled technology.

Shida ya viongozi wengi wa Africa ni selfishness, ni group kadogo chenye elimu na maarifa machache , wakitaka support ya ku control Nchi zao kwa mkono wa chuma,

Ndio unakuta wanaangukia mkononi mwa china,mara Russia, ili wapate support ya kifedha na technology na silaha.

Sasa unaacha kupata support nyumbani kwa mamia ya wasomi walisomeshwa , unaenda kutafuta support kwa MTU usiye kujua.
 
Hakuna kitu kama hicho, china inawadanganya viongozi wa Africa TU 😂.

Tena Bora western technology ina uwanda mpana Nchi kama Nchi inaweza kutumia wataalamu wake wa ndani ku implement vizuri. Kuliko hizo china state controlled technology.

Shida ya viongozi wengi wa Africa ni selfishness, ni group kadogo chenye elimu na maarifa machache , wakitaka support ya ku control Nchi zao kwa mkono wa chuma,

Ndio unakuta wanaangukia mkononi mwa china,mara Russia, ili wapate support ya kifedha na technology na silaha.

Sasa unaacha kupata support nyumbani kwa mamia ya wasomi walisomeshwa , unaenda kutafuta support kwa MTU usiye kujua.
Umenikumbusha ule msemo wa kwamba when the deal is too good, think twice.

Mkuu ni kweli unaweza kutumia wataalamu wa ndani ku-implement mifumo yao, lakini usisahau yale mambo ya surveillance kapitalism, makampuni makubwa ya Marekani kama Google na Meta tayari yanajua kila kitu kuhusu sisi kuliko hata serikali zetu zinavyotujua tofauti tu ni kwamba hawa wa Magharibi wanatafuta hela zetu, China wao wanatafuta udhibiti.
 
Umenikumbusha ule msemo wa kwamba when the deal is too good, think twice.

Mkuu ni kweli unaweza kutumia wataalamu wa ndani ku-implement mifumo yao, lakini usisahau yale mambo ya surveillance kapitalism, makampuni makubwa ya Marekani kama Google na Meta tayari yanajua kila kitu kuhusu sisi kuliko hata serikali zetu zinavyotujua tofauti tu ni kwamba hawa wa Magharibi wanatafuta hela zetu, China wao wanatafuta udhibiti.
AU walijengewa jengo na china kilicho tokea ni huzuni, ni western technology Ndio iliyogundua kuwa China inasikiliza kila kitu kinacho endelea ndani ya jengo.

ECOWAS nao majuzi wamejengewa jengo lao na china.

Kipindi cha jiwr na yeye kule ngerengere akawaachia wachina wakarabati Kambi.

Viongozi wajifuze kutokana na makosa
 
AU walijengewa jengo na china kilicho tokea ni huzuni, ni western technology Ndio iliyogundua kuwa China inasikiliza kila kitu kinacho endelea ndani ya jengo.

ECOWAS nao majuzi wamejengewa jengo lao na china.

Kipindi cha jiwr na yeye kule ngerengere akawaachia wachina wakarabati Kambi.

Viongozi wajifuze kutokana na makosa
Haha umenikumbusha kuhusu hiyo skendo, lile jengo lilikuwa zawadi kutoka kwa Wachina, lakini baadaye ikagundulika kuwa kila usiku, data zote za siri za kompyuta zilikuwa zinajituma zenyewe kwenda kwenye ma-server ya kule Shanghai! Yaani unajengewa nyumba, halafu fundi anaacha matundu ya siri ya kukuchungulia ukiwa chumbani. What a shame! 😂
 
Haha umenikumbusha kuhusu hiyo skendo, lile jengo lilikuwa zawadi kutoka kwa Wachina, lakini baadaye ikagundulika kuwa kila usiku, data zote za siri za kompyuta zilikuwa zinajituma zenyewe kwenda kwenye ma-server ya kule Shanghai! Yaani unajengewa nyumba, halafu fundi anaacha matundu ya siri ya kukuchungulia ukiwa chumbani. What a shame! 😂
Yah lakini Bado viongozi wa Africa hawajifunzi
 
Back
Top Bottom