Tujadili kuhusu mtandao wa Halotel

Tujadili kuhusu mtandao wa Halotel

Hao wana rollout 3G tu kwa taarifa yenu na vi torch vyenu ambavyo havina 3G Capability mtaishia kunawa tu
 
kabla ya kampuni kusajiliwa kuna vigezo lazima vipitiwe mfan

-je, wanasajili kama profitable au non-profit?

^hapa jibu ni wanajisajili kufanya biashara na si kutoa msaa

-je, wizara kupitia TCRA hawana sheria zinazosimamia makampuni ya simu?

^^wizara ya mawasiliano kupitia kitengo (TCRA) wameweka sheria (EPOCA tariff regulation) inayowaelekeza wamiliki wa makampuni ya simu namna ya kutoza na kutoa huduma kwa wateja wao.

je, bodi ya ushindani wa kibiashara ipo au haipo?
^^^kama ipo unategemea hao VIETTEL wataweza kukiuka sheria zilizowekwa?

~~mwisho wanachokifanya Halotel kwa sasa ni kujitangaza tu na hakuna jipya lolote wanaloweza kulifanya. TTCL ndiye kampuni itakayokuja kutukomboa na si haya makampuni binafsi ya kigeni.
-TTCL ikifufuliwa itakuwa bora kuliko haya mafafa mengine.
 
Msibipishane kuhusu halotel mm nshachkua lain nmepata free 5312mb,dk300 halt-halt,sms bila kikomo kwa mda wa mwez bt vocha hazjaanza kuuzwa ad wazndue
 
Kuungia kwny competition ya biashara ya huduma za simu kwa sasa unabidi uje na unique product, unless ushindani ni mkubwq sana, yako wapi makampuni km Sasatel, Smart na hatq Zantel....hawa Vietel labda waje na huduma nzuri za internet zenye bei ndogo sana na zinazopatikana kila pembe ya nchi!

Unless hizi kampuni zilizopo huduma zao ni ghari sana...!

Kama wakiwa na internet ya uhakika hasa vijijini nadhani watachukua nafasi kubwa sana vijijini kuliko mijini.

Wawekeze zaidi kwenye internet ya uhakika na iliyo fast.
 
Ila nilisikia nyepesi nyepesi kwamba hii kampuni inaendeshwa na jeshi la Vietnam, sijui ni kweli? Naomba mwenye kujua anijuze, manake kama kweli inaendeshwa na jeshi la Vietnam napata wasiwasi kidogo

ni kweli isiyo na shaka viettel inaendeshwa na wizara ya ulinzi na usalama ya Vitnam!
 
Kama wakiwa na internet ya uhakika hasa vijijini nadhani watachukua nafasi kubwa sana vijijini kuliko mijini.

Wawekeze zaidi kwenye internet ya uhakika na iliyo fast.

Intanet iko fasta sana minara haishuk
 
Kama wakiwa na internet ya uhakika hasa vijijini nadhani watachukua nafasi kubwa sana vijijini kuliko mijini.

Wawekeze zaidi kwenye internet ya uhakika na iliyo fast.

Kwa mjini watateka soko km watakuwa na bei nzuri kulinganisha na makampuni mengine
 
yan kwel wapo fresh hata kama mtandao unasoma E yan bado unaweza kudownload kwa spd kubwa sana ila mm tayar nnayo lne yao
 
Hivi tukiamua kuhamasisha watu wetu wa karibu wajiunge na huu mtandao voda watabaki vipi? Let us do it wakuu
 
mbona hawafanyi marketing. tujue vufurushi vyao na huduma zimekaaje
 
hapa arusha huwa naona chata zao ila maeneo ya karibu na sheli ya puma iliyopo soko kuu nadhani kuna ofisi yao pale
 
Itakuwa ana 10pacent huyu tayari, mitandao hata kama ni mizuri ni kwa mda tuu, wa kipindi kile cha misamaha ya kodi, yote baadae inafuata kama wenzake.
 
ni kweli isiyo na shaka viettel inaendeshwa na wizara ya ulinzi na usalama ya Vitnam!

Nchi itabaki salama kweli? Jeshi la nchi nyingine kuendesha kampuni ya mawasiliano ndani ya nchi nyingine
 
Hivi tukiamua kuhamasisha watu wetu wa karibu wajiunge na huu mtandao voda watabaki vipi? Let us do it wakuu

ukiona watu wanaipondea holetel , jua hao ndio beneficiary wa UNYONYAJI WA VODACOM , akina EDO , fred, tanil , wanahofia mkate wao ,
inashangaza wakati huu makampuni ya mawasiliano yanaingia kwenye soko la ushindani , bado kampuni kama voda inapandisha vifurushi pamoja na GHARAMA za kutoa pesa MPESA
 
Natamani wangeweza kurusha mawimbi yao kwa setelite...ili wasipate adha nyingine kama za umeme na uharibifu wa minara.nk
Hiyo ingewafanya wawe na bei stable...
Pia ingeweza kufika kila mahali kwa urahisi..mijini vijijini na kwenye maziwa/baharini
 
Kama wakiwa na internet ya uhakika hasa vijijini nadhani watachukua nafasi kubwa sana vijijini kuliko mijini.

Wawekeze zaidi kwenye internet ya uhakika na iliyo fast.

hawa jamaa tatizo lao kubwa ni kuweka internet ya 2g vijijini hivyo czan kama watateka soko kwani kwa kuweka 2g netwek vjijin kutafanya watu wengi wasivutiwe mtandao huu
 
Back
Top Bottom