Tujadili kuhusu matuta barabarani

Tujadili kuhusu matuta barabarani

Kaizer

Platinum Member
Joined
Sep 16, 2008
Posts
25,330
Reaction score
17,857
Wakuu habari ya Ijumaa?

Kwa wale watumiaji wa vyombo vya moto hususani kwenye bara bara kuu yaani highway, iwe kwa usafiri wa public au wa binafsi, kuna hii ninayoona binafsi kama kero ya matuta:

Kwanza, yapo mengi katika umbali mdogo
Pili, yapo matuta 'yasiyokidhi viwango' kwa maana ya kwamba matuta yote kwenye bara bara zetu hayana kiwango kinachofanana, mwengine makubwa, mwengine madogo, membamba lakini yamechongoka, ya lami na yasiyokuwa ya lami, ili mradi hakuna raha/comfort tena ya kusafiri

Najiuliza kwa nini serikali iingie garama kuweka lami kwa mfano, bara bara nzuri tu, kisha ije "iharibu" kwa kuweka matuta tena makubwa mno? Kwa mfanio bara bara kuu kutoka minjingu kwenda hadi dareda kuna matuta yamewekwa siku hizi, nahofia kiwango chake cha ubora na hivyo usalama wa watu na magari yao.

Ningeomba na wengine wenye uzoefu wa hii makitu watupie hapa tujadili huenda Magufuli akasikia maana kuna wakati nishamsikia akisema kuwa matuta kwenye highway yaondolewe

Niseme kwamba hii sio disrespect kwa waenda kwa miguu au wananchi wanaoishi kando kando mwa sehemu hizo....hapana...ni suala la aina na sehemu matuta yenyewe yanapowekwa...yanakidhi viwango? Kuna standards? kwa nini yanatofautiana hivi?

cc Bigirita watu8 KakaKiiza Mtambuzi Nyamayao Chocs neggirl Asprin Madame B @@amu Kipaji Halisi Remote Rejao Preta PakaJimmy Mzee wa Rula Filipo marejesho LiverpoolFC Lily Flower Eeka Mangi Kimey Teamo
 
Last edited by a moderator:
Mkuu ni ukweli usiopingika kuwa madereva wengi wa nchi hii hawazingatii sheria za usalama wa barabarani...

Kwa mantiki hiyo nadhani ndiyo maana wasimamizi wa usalama walikuja na idea ya kuweka matuta kama moja ya njia ya kudhibiti mwendokasi wa vyombo vya usafiri...

Hilo ni wazo zuri sana tu, lakini kasoro iliyopo ni kwenye utekelezaji wa lengo hilo...fine wameamua kuweka matuta lakini kuna matuta mengine aisee nadhani ni adhabu kwa madereva na magari...

Hapa Dar kuna baadhi ya njia zina matuta makali mno mathalani barabara ya Akachube na nyinginezo kadhaa...
 
Mkuu ni ukweli usiopingika kuwa madereva wengi wa nchi hii hawazingatii sheria za usalama wa barabarani...

Kwa mantiki hiyo nadhani ndiyo maana wasimamizi wa usalama walikuja na idea ya kuweka matuta kama moja ya njia ya kudhibiti mwendokasi wa vyombo vya usafiri
...

Hilo ni wazo zuri sana tu, lakini kasoro iliyopo ni kwenye utekelezaji wa lengo hilo...fine wameamua kuweka matuta lakini kuna matuta mengine aisee nadhani ni adhabu kwa madereva na magari...

Hapa Dar kuna baadhi ya njia zina matuta makali mno mathalani barabara ya Akachube na nyinginezo kadhaa...


Mkuu watu8 hapo nakubaliana na wewe kabisa. tatizo hizo instruments...kama matuta (hoja ya ving'amuzi tuliijadili majuzi hapa na mambo ya speed ya 50)

Hii habari ya matuta kwa nini hayana standards? yaani mkandarasi anajiamulia tu kwamba awekeje au ni namna gani? ni kero kweli na hatari kwa usalama hasa pale ambapo hakuna alama za usalama bara barani

Isitoshe, in a way inawapunguzia 'ulaji' matrafic sehem zile za speed 50, maana sio rahisi wakudake

Lakini tuende mbele zaidi kwamba matraffic wawezeshwe zaidi wasimamie sheria hizi kuliko matuta maana pia yanaharibu pia bara bara nzuri zinazojengwa kwa mamilioni ya fedha..
 
Last edited by a moderator:
Matuta yanatuharibia sana magari hasa sisi tulio na Vitz tunapata tabu sana.........

umeona eeh Mtambuzi..fikiria vitz inakutana na mtuta wa kufa mtu...lol lazima ukache hapo
 
Last edited by a moderator:
Magufuli akataza matuta barabarani

Posted by B.M.T on Tuesday, January 04, 2011 // 0 comments

I WAZIRI wa Ujenzi, John Magufuli, amepiga marufuku ujenzi wa matuta kwenye barabara zote kuu nchini kwa kuwa kitendo hicho ni kinyume cha sheria.

Pia ameagiza Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), kukagua na kusimamia miradi yote ya barabara za lami inayojengwa kwenye maeneo yao, tofauti na utaratibu uliokuwapo wa
miradi hiyo kukaguliwa na wataalamu wa makao makuu.

Magufuli alitoa maagizo hayo juzi alipozungumza na wafanyakazi wa Wizara hiyo mjini hapa, baada ya kukagua barabara ya Singida-Katesh wakati wa ziara yake ya ghafla ya siku moja.

Katika ziara hiyo pia alimwagiza mkandarasi anayejenga barabara ya Singida- Katesh - Sinohydro Corporation Limited ya China, kukamilisha kazi hiyo kwa wakati, vinginevyo Serikali haitaipa zabuni nyingine siku zijazo.

Kabla ya kutoa maagizo hayo, Kaimu Meneja wa Tanroads wa Mkoa, Joseph Masige, alisema ujenzi wa barabara hiyo uko nyuma kwani kazi iliyofanyika hadi sasa ni asilimia 51 tu badala ya asilimia 70 iliyopangwa.

"Ni kweli ujenzi unakwenda vibaya. Lazima mbadilike, mmalize kazi hiyo kwa wakati bila visingizio vyovyote, vinginevyo nitahakikisha hampati zabuni yoyote nchini.

"Kwanza mmelipwa fedha nyingi sana. Badala ya kununulia mitambo na zana mpya, nyie mnafanya mchezo wa kuhamisha vifaa hivyo kutoka mradi mmoja hadi mwingine kitendo kinachodhoofisha ufanisi wenu.

Hapa si mahali pa kuja kucheza," Waziri alimwonya mkandarasi huyo ambaye aliwakilishwa na Meneja Mradi huo, Xhinhua Chen.

Awali Chen alisema moja ya sababu za kuzorota kwa ujenzi huo ni kucheleweshwa malipo yao na Serikali suala ambalo Waziri aliahidi kulifanyia kazi.

Barabara ya Singida - Katesh yenye urefu wa kilometa 65.2 inafadhiliwa na Benki ya Maendeleo ya Afrika (ADB) kwa asilimia 60 na Serikali ya Tanzania asilimia 40 na inatarajiwa kukamilika Septemba mwaka huu.

The THOMCOM Inc.: Magufuli akataza matuta barabarani

Sasa wataalam kumbe hii makitu ni kinyume na sheria na mwenye bara bara zake alishawahi kukataza

Cha ajabu, bara bara hiyo hiyo ndo ina matuta ya kufa mtu hasa kutoka Singida kuelekea Katesh.....!

Naombeni mwongozo, hili agizo la Magufuli lilipuuzwa? Au sio kweli kwamba ni kinyume na sheria? kama ni sheria, ni sheria ipi inaruhusu kuweka au kutowekwa kwa matuta bara barani?
 
Hivi mkuu hekimatele kwa hekima kabisa huoni kuna haja yankuwa na viwango vya haya matuta? Maana apo ndo kuna balaa

Nakubaliana na wewe lakini kwa uzoefu wangu katika pita pita zangu humu Tanzaniano ni ngumu kufanya kama unavyosema. Unakuta sehemu nyingine ni high way ila kwa sababu kuna vijiji na makazi ya watu lazima tuta liwekwe la sivyo tutapoteza watanzania wengi sana huku nchini. Madereva tulionao wengi ni careless sana. Wao ndo wana haraka kuliko mtu yeyote huku duniani. Binafsi napenda sana kuheshimu wapita njia (pedestrians) kwa sababu hata mi kuna siku natumia njia hizo kama wao.
 
Nakubaliana na wewe lakini kwa uzoefu wangu katika pita pita zangu humu Tanzaniano ni ngumu kufanya kama unavyosema. Unakuta sehemu nyingine ni high way ila kwa sababu kuna vijiji na makazi ya watu lazima tuta liwekwe la sivyo tutapoteza watanzania wengi sana huku nchini. Madereva tulionao wengi ni careless sana. Wao ndo wana haraka kuliko mtu yeyote huku duniani. Binafsi napenda sana kuheshimu wapita njia (pedestrians) kwa sababu hata mi kuna siku natumia njia hizo kama wao.

sawa mkuu tupo pamoja...kuna madereva vichwa mbuzi hawapo careful...lakini pia tukubali kuna pedestrians hawapo pia careful pia....it goes both ways, ila sasa kimsingi ili kulinda maisha ya watu, matuta yawekwe ila ya aina/kiwango gani?

Maana uzoefu ni kwamba ukichunguza yaliyowekwa mengine hayajazingatia aina za magari waliyonayo watanzania wengi pia ...kwa nini kusiwe na standard ya hayo matuta?
 
Bila matuta wenye Vitz mnatumalizia ndugu na watoto wetu

hahahahh Zanta bana......matuta sawa. hata ukiwa kwenye basi, kuna matuta unaona kabisa hili hapana

Mara kibao nimeona magari yakiwa yameviringika kutokana na kukutana na matuta makubwa pengine yasiyokuwa na alama na hivyo kusababisha uharibifu mkubwa
 
Last edited by a moderator:
wengi wetu tunaoendesha vitz tukipata ka upenyo ka kutanua tu ili tukwepe tuta ahh tunatanua haswaa..wanatutesa bwana.:bored:

Na hapo uombe traffic asikuone! manake 30K inahusu chaaaap!
 
hahahahh Zanta bana......matuta sawa. hata ukiwa kwenye basi, kuna matuta unaona kabisa hili hapana

Mara kibao nimeona magari yakiwa yameviringika kutokana na kukutana na matuta makubwa pengine yasiyokuwa na alama na hivyo kusababisha uharibifu mkubwa
Nakubaliana na wewe kabisa kwenye point ya standard za matuta hapo ndo tunakosea ila kuondoa matuta ni kukaribisha janga kwa watoto wetu. Kiuhalisia madera wa bongo hatufuati sheria kabisa kwa hiyo dawa ni matuta, kwasababu tuta huwezi kulihonga upite itabidi upunguze tu mwendo
 
mie katika pita pita zangu huko nje sijaona matuta. Kaizer
Katika pita pita zako huko nje umeona hao madereva wa nje wanavyotii sheria? huwezi kulinganisha na wakwetu
hapa yaani kwenye Zebra crossing mtu ndo anapisha gari.. wakati huko nje unakosema yaani ukikanyaga tu zebra dereva anaanzia kilometa kufungu break !
 
Wakuu naomba na mimi nichangie kidogo kuhusu hoja hii, kwanza ieleweke hiki kinachoitwa highway kimepoteza maana yake hapa Tz maana watu wamehamishia makazi kuwa kando kando za barabara na hata ukiangalia shule nyingi zimejengwa kando kidogo tuu ya barabara na makazi yanaendelea kujengwa kandoni mwa barabara hivyo baada ya muda mfupi ujao tutakuwa na matuta mengi sawa na nyumba zilizopo barabarani. Ikumbukwe pia kwamba hawa jamaa wa tanroads wamefanya kama mradi maana wakisikia mtu yeyote kagongwa hata kama alikuwa kalewa kesho yake linawekwa na kukunja mkwanja mrefu. Hivyo kuna changamoto nyingi za kujadili na pia kuondoa mazoea ya kurithi mambo yaliyopitwa na wakati. Elimu ya matumizi ya barabara kuanzia mashuleni na kwenye vipindi vya redio na tv ziwepo ili mtu anayevuka barabara ajue la kufanya kabla ya luvuka barabara na dereva ajue jukumu lake. Matuta sio suluhisho watu watadumaa akili. Tujifunze kwa wenzetu hata kwa nchi ndogo kama Swaziland wanajua highway ni nini.
 
Back
Top Bottom