Tujadili: Hoja tano ngumu za mchakato wa Katiba Mpya kuanzishwa tena

dndagula

JF-Expert Member
Jul 24, 2016
1,460
1,444
Ni kweli katiba mpya na bora inahitajika kulingana na mabadiliko ya kisiasa, kiuchumi, kijamii na kitekinolojia nchini na duniani kote. Inawezekana kabisa tangu 1977 nchi imepita kwenye changamoto nyingi za kiutawala, kiuongozi, kisiasa, kijamii na kiuchumi hivyo uwepo wa mahitaji mapya ya mwongozo wa kikatiba ili kujenga nchi yenye ustawi. Watanzania tulio wengi tunakubaliana na hili. Hata hivyo kuna hoja mbalimbali muhimu na ya msingi zinaibiliwa na zinahitaji tafakari kwa kina.

1. Je, ni wakati mwafaka sasa hivi kuanza mchakato huo ambao kimsingi hauko kwenye ilani ya uchaguzi ya ccm na hakuna bajeti yake au tunamtwika Rais jambo ambalo ni non starter kwa sasa na ambalo litamshughulisha na kumtoa kwenye malengo yaliyopo mbele yake na taifa.

2. Ndani ya chama cha mapinduzi vuguvugu hili likoje na kitaifa mapokeo ya wananchi yakoje? Je hoja hii ya manufaa kwa wanasiasa au jamii yote kwa ujumla?

3. Je, ikikubalika tuanze mchakato upya, tuanzie wapi kwa mujibu wa sheria ya mabadiliko ya katiba. Wapo wanaosema tuanze na rasimu ya warioba lakini hoja nyingine mbadala ni kwamba rasimu hii ilijadiliwa na kupitiwa na Bunge la katiba 2014 kwa akidi iliyokamilika na bunge kuandaa rasimu inayojulikana ya Sita je tuachane nayo hii ya Samwel Sita wakati mchakato ulikamilishwa kwa mujibu wa sheria hata km baadhi ya wajumbe walitoka nje na kususa lakini mchakato uliendelea hadi rasimu kukamilika. Hapa napo kuna mkanganyiko wa kisheria pia. Je hali hii irekebishwe kwa kupitia Bunge kwa kurekebisha sheria? Je kwa tamko la Rais hatakiuka sheria?

4. Je, turudi mezani na kuboresha rasimu ipi ya Sita au ya Warioba na pia kwa kuzingatia kipindi cha miaka aghrabu miaka 8 imepita je tujiulize mazingira hayajabadilika kweli kuhitaji mambo mapya kuingizwa? Au mchakato uanze upya kwa kuchukua maoni ya wananchi upya na kuachana na rasimu ya Warioba na ya Sita zenye migongano ya kimaudhui.

5. Je, hivi katiba ya sasa haifai moja kwa moja,wapo wanaoamini kuwa tunachohitaji sasa ni ustawi wa uchumi na kijamii kwanza kabla ya katiba mpya.Hoja ni kwamba katiba hii ni bora wakirejea kuwa imetuvusha kwenye matukio mbalimbali mf msiba wa juzi.Katiba mpya siyo mwarobaini wa changamoto zilizopo. Kundi lingine linasema katiba ya sasa ina matobo mengi mno na ina mifumo dhaifu inayokanyangwa. Wanarejea utawala uliopita kuwa ulikuwa mgumu na udhaifu wa Muundo wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

a) Hoja nyingine ni kwamba wananchi wa kawaida hawahitaji mabadiliko ya katiba wanachohitaji ni kuwaondolea kero za maisha kiuchumi na kijamii. Hivyo hoja ya katiba mpya ni ya wanasiasa tena wanalenga uchaguzi wa 2025. Je hakuna njia nyingine ya kuboresha katiba au mifumo iliyopo kimkakati ili uchaguzi uwe wa haki badala ya kubeba hoja nzima ya katiba mf kuiangalia upya Tume ya uchaguzi na madaraka ya Rais kuhusiana na tume hiyo ili kuleta usawa na haki kwenye uchaguzi.

b) Hoja ya katiba mpya ni ya upinzani na wanaharaki pekee. Vipi ushiriki wa makundi mengine misimamo yao wakulima,wafugaji, wavuvi, viongozi wa dini, wafanyakazi nk.

c) Hoja ya hofu ni kuwa tukianza mchakato je hautaishia njiani tena na kupoteza raslimali kwa vile upande wa upinzani tayari baadhi wameanza na hoja zenye masharti kabla hata ya majadiliano kuwa wanataka rasimu ya warioba tu iheshimiwe na si vinginevyo(pre emptying discussion).

d) Je, kuanzisha mchakato huu kuna manufaa au hasara kwa sasa? Je, mazingira ya kisiasa yanaruhusu! Zipo hoja nyingi za kutafakari kwa umakini kwa pande zote ili huko mbeleni tusikwame
 
Hii Issue ya Katiba, Wanasheria karibuni, Wengine wenzangu na Mimi Sociologist and Botanica tujiweke pembeni kidogo ili tuelemishwa. Best Regards.
 
Kuna haja kubwa kuwepo na katiba mpya..yenye kukidhi maitaji ya watanzania....dunia ya Leo .spika wa bunge ,Rais wa nchi hawatakiwi kuwa na Kinga....wanafanya madudu mengi hku wkijua katiba inawalinda....Leo hii tunsikia report ya C.A.G pesa zmepotea lkn hkuna htua zaidi...Leo hii Raising wa nchi anateua zaid ya watu 500 ma RC,DC DED,nk Dunia imeshatok hko....
 
Ni kweli katiba mpya na bora inahitajika kulingana na mabadiliko ya kisiasa, kiuchumi, kijamii na kitekinolojia nchini na duniani kote. Inawezekana kabisa tangu 1977 nchi imepita kwenye changamoto nyingi za kiutawala, kiuongozi, kisiasa, kijamii na kiuchumi hivyo uwepo wa mahitaji mapya ya mwongozo wa kikatiba ili kujenga nchi yenye ustawi. Watanzania tulio wengi tunakubaliana na hili. Hata hivyo kuna hoja mbalimbali muhimu na ya msingi zinaibiliwa na zinahitaji tafakari kwa kina.

1. Je, ni wakati mwafaka sasa hivi kuanza mchakato huo ambao kimsingi hauko kwenye ilani ya uchaguzi ya ccm na hakuna bajeti yake au tunamtwika Rais jambo ambalo ni non starter kwa sasa na ambalo litamshughulisha na kumtoa kwenye malengo yaliyopo mbele yake na taifa.

2. Ndani ya chama cha mapinduzi vuguvugu hili likoje na kitaifa mapokeo ya wananchi yakoje? Je hoja hii ya manufaa kwa wanasiasa au jamii yote kwa ujumla?

3. Je, ikikubalika tuanze mchakato upya, tuanzie wapi kwa mujibu wa sheria ya mabadiliko ya katiba. Wapo wanaosema tuanze na rasimu ya warioba lakini hoja nyingine mbadala ni kwamba rasimu hii ilijadiliwa na kupitiwa na Bunge la katiba 2014 kwa akidi iliyokamilika na bunge kuandaa rasimu inayojulikana ya Sita je tuachane nayo hii ya Samwel Sita wakati mchakato ulikamilishwa kwa mujibu wa sheria hata km baadhi ya wajumbe walitoka nje na kususa lakini mchakato uliendelea hadi rasimu kukamilika. Hapa napo kuna mkanganyiko wa kisheria pia. Je hali hii irekebishwe kwa kupitia Bunge kwa kurekebisha sheria? Je kwa tamko la Rais hatakiuka sheria?

4. Je, turudi mezani na kuboresha rasimu ipi ya Sita au ya Warioba na pia kwa kuzingatia kipindi cha miaka aghrabu miaka 8 imepita je tujiulize mazingira hayajabadilika kweli kuhitaji mambo mapya kuingizwa? Au mchakato uanze upya kwa kuchukua maoni ya wananchi upya na kuachana na rasimu ya Warioba na ya Sita zenye migongano ya kimaudhui.

5. Je, hivi katiba ya sasa haifai moja kwa moja,wapo wanaoamini kuwa tunachohitaji sasa ni ustawi wa uchumi na kijamii kwanza kabla ya katiba mpya.Hoja ni kwamba katiba hii ni bora wakirejea kuwa imetuvusha kwenye matukio mbalimbali mf msiba wa juzi.Katiba mpya siyo mwarobaini wa changamoto zilizopo. Kundi lingine linasema katiba ya sasa ina matobo mengi mno na ina mifumo dhaifu inayokanyangwa. Wanarejea utawala uliopita kuwa ulikuwa mgumu na udhaifu wa Muundo wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

a) Hoja nyingine ni kwamba wananchi wa kawaida hawahitaji mabadiliko ya katiba wanachohitaji ni kuwaondolea kero za maisha kiuchumi na kijamii. Hivyo hoja ya katiba mpya ni ya wanasiasa tena wanalenga uchaguzi wa 2025. Je hakuna njia nyingine ya kuboresha katiba au mifumo iliyopo kimkakati ili uchaguzi uwe wa haki badala ya kubeba hoja nzima ya katiba mf kuiangalia upya Tume ya uchaguzi na madaraka ya Rais kuhusiana na tume hiyo ili kuleta usawa na haki kwenye uchaguzi.

b) Hoja ya katiba mpya ni ya upinzani na wanaharaki pekee. Vipi ushiriki wa makundi mengine misimamo yao wakulima,wafugaji, wavuvi, viongozi wa dini, wafanyakazi nk.

c) Hoja ya hofu ni kuwa tukianza mchakato je hautaishia njiani tena na kupoteza raslimali kwa vile upande wa upinzani tayari baadhi wameanza na hoja zenye masharti kabla hata ya majadiliano kuwa wanataka rasimu ya warioba tu iheshimiwe na si vinginevyo(pre emptying discussion).

d) Je, kuanzisha mchakato huu kuna manufaa au hasara kwa sasa? Je, mazingira ya kisiasa yanaruhusu! Zipo hoja nyingi za kutafakari kwa umakini kwa pande zote ili huko mbeleni tusikwame
Wapinzani na wanaharakati siyo wananchi wa wakawaida??

Mnatumia muda mwingi.kuandika propaganda za kijinga
 
Wapinzani na wanaharakati siyo wananchi wa wakawaida??

Mnatumia muda mwingi.kuandika propaganda za kijinga
Hapa tunataka uchambuzi na maoni ya nini kifanyike. Mods uzi huu ni muhimu sana usiutoe watu wachangie.
 
Katiba ndiyo dira ya maendeleo ya kiuchumi, kisiasa na kijamii, hivyo katiba mpya haikwepeki. Tuna mikwamo mingi sana katika kuleta mabadiliko ya kweli katika Taifa letu ambayo haina afya kwa mustakabali wa nchi lakini hupuuzwa kisiasa na wakati mwingine kwa nguvu ya dola.

Wakati wa kupata katiba mpya ni sasa kwa sababu hata maendeleo ya kiuchumi yatasuasua sana kwa kutumia katiba ya sasa ambayo inategemea hisani ya Rais. Ukiwa na Rais fisadi kama Magufuli tusitegemee kupata maendeleo ya watu bali tutaishia kuonyeshwa miundombinu, kupewa vitisho vya maisha yetu, kupata vifo visivyojulikana, kuleta ubaguzi wa kikabila na kikanda, kuzalisha miungu watu kama Sabaya na Makonda na madhila mengi ya kutisha.

Tunahitaji katiba mpya itakayoleta usawa, haki na itakayo heshimisha kila raia bila ubaguzi.
 
Ni kweli katiba mpya na bora inahitajika kulingana na mabadiliko ya kisiasa, kiuchumi, kijamii na kitekinolojia nchini na duniani kote. Inawezekana kabisa tangu 1977 nchi imepita kwenye changamoto nyingi za kiutawala, kiuongozi, kisiasa, kijamii na kiuchumi hivyo uwepo wa mahitaji mapya ya mwongozo wa kikatiba ili kujenga nchi yenye ustawi. Watanzania tulio wengi tunakubaliana na hili. Hata hivyo kuna hoja mbalimbali muhimu na ya msingi zinaibiliwa na zinahitaji tafakari kwa kina.

1. Je, ni wakati mwafaka sasa hivi kuanza mchakato huo ambao kimsingi hauko kwenye ilani ya uchaguzi ya ccm na hakuna bajeti yake au tunamtwika Rais jambo ambalo ni non starter kwa sasa na ambalo litamshughulisha na kumtoa kwenye malengo yaliyopo mbele yake na taifa.

2. Ndani ya chama cha mapinduzi vuguvugu hili likoje na kitaifa mapokeo ya wananchi yakoje? Je hoja hii ya manufaa kwa wanasiasa au jamii yote kwa ujumla?

3. Je, ikikubalika tuanze mchakato upya, tuanzie wapi kwa mujibu wa sheria ya mabadiliko ya katiba. Wapo wanaosema tuanze na rasimu ya warioba lakini hoja nyingine mbadala ni kwamba rasimu hii ilijadiliwa na kupitiwa na Bunge la katiba 2014 kwa akidi iliyokamilika na bunge kuandaa rasimu inayojulikana ya Sita je tuachane nayo hii ya Samwel Sita wakati mchakato ulikamilishwa kwa mujibu wa sheria hata km baadhi ya wajumbe walitoka nje na kususa lakini mchakato uliendelea hadi rasimu kukamilika. Hapa napo kuna mkanganyiko wa kisheria pia. Je hali hii irekebishwe kwa kupitia Bunge kwa kurekebisha sheria? Je kwa tamko la Rais hatakiuka sheria?

4. Je, turudi mezani na kuboresha rasimu ipi ya Sita au ya Warioba na pia kwa kuzingatia kipindi cha miaka aghrabu miaka 8 imepita je tujiulize mazingira hayajabadilika kweli kuhitaji mambo mapya kuingizwa? Au mchakato uanze upya kwa kuchukua maoni ya wananchi upya na kuachana na rasimu ya Warioba na ya Sita zenye migongano ya kimaudhui.

5. Je, hivi katiba ya sasa haifai moja kwa moja,wapo wanaoamini kuwa tunachohitaji sasa ni ustawi wa uchumi na kijamii kwanza kabla ya katiba mpya.Hoja ni kwamba katiba hii ni bora wakirejea kuwa imetuvusha kwenye matukio mbalimbali mf msiba wa juzi.Katiba mpya siyo mwarobaini wa changamoto zilizopo. Kundi lingine linasema katiba ya sasa ina matobo mengi mno na ina mifumo dhaifu inayokanyangwa. Wanarejea utawala uliopita kuwa ulikuwa mgumu na udhaifu wa Muundo wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

a) Hoja nyingine ni kwamba wananchi wa kawaida hawahitaji mabadiliko ya katiba wanachohitaji ni kuwaondolea kero za maisha kiuchumi na kijamii. Hivyo hoja ya katiba mpya ni ya wanasiasa tena wanalenga uchaguzi wa 2025. Je hakuna njia nyingine ya kuboresha katiba au mifumo iliyopo kimkakati ili uchaguzi uwe wa haki badala ya kubeba hoja nzima ya katiba mf kuiangalia upya Tume ya uchaguzi na madaraka ya Rais kuhusiana na tume hiyo ili kuleta usawa na haki kwenye uchaguzi.

b) Hoja ya katiba mpya ni ya upinzani na wanaharaki pekee. Vipi ushiriki wa makundi mengine misimamo yao wakulima,wafugaji, wavuvi, viongozi wa dini, wafanyakazi nk.

c) Hoja ya hofu ni kuwa tukianza mchakato je hautaishia njiani tena na kupoteza raslimali kwa vile upande wa upinzani tayari baadhi wameanza na hoja zenye masharti kabla hata ya majadiliano kuwa wanataka rasimu ya warioba tu iheshimiwe na si vinginevyo(pre emptying discussion).

d) Je, kuanzisha mchakato huu kuna manufaa au hasara kwa sasa? Je, mazingira ya kisiasa yanaruhusu! Zipo hoja nyingi za kutafakari kwa umakini kwa pande zote ili huko mbeleni tusikwame
Kwanza kuna swali moja la kuuliza. Unapokuwa madarakani unaweza ukawa unakuja kwa nia njema kabisa ya kupigania haki za wananchi na sio maslahi binafsi na kulinda serikali hata kama inakosea.

Kwa maneno hayo sasa. Tujiulize, ni wangapi ambao wanaweza kuweka kipaumbele shida za wananchi na kuweza ku sacrifice hata uhai wake. Tunajua kupigania haki ni jambo linalohitaji ujasiri sana. Ili uwe kiongozi bora katika hili ni lazima pia usiwe mlafi wa pesa na uroho wa madaraka, pia unahitaji kua na mindset ya mwanafalsafa.

Kwa mfano tunawalaumu sana viongozi/wanasiasa juu ya uwajibikaji. Lakini ukweli mchungu kwa dunia ya sasa viongozi ni wafanyabiashara. Na siku zote mfanya biashara atafanya chochote hata kudiriki kudanganya wananchi ilimradi lengo lake litimie. Hawa huwa hawana uchungu na jamii wanazotoka, huwa ni waoga wa kupoteza mali na pesa kwa ajili ya kupambana dhidi ya matatizo ya nchi.

Kiongozi wa aina hii, huwa anahakikisha anacheza karata yake kwa umakini sana akiwa madarakani au nyazfa yoyote ya uongozi.
Sisi wananchi tunabaki kulia mara ooh mbona mbunge fulani anajua tuna matatizo fulani wilayani lakini haongei. Anaweza asiongee kwa sababu kwake ni rahisi kuishi vizuri aki defend serikali kuliko ku defend wananchi. So wanachofanya wanaaangalia sehemu yenye influence ya power. Kama kusifia raisi kutamfanya maisha yake yawe mazuri na salama atasifia sana hata kama ni ujinga.

Ndo maana tunasema kwa dunia ya sasa 2021 tuna wafanya biashara wengi sana kwenye nyazifa za uongozi kuliko wazalendo na viongozi wa kweli. Sifa kuu ya mfanyabiashara ni kufanya chochote kinachomwezesha kupata hela na usalama wa maisha yake sio ya wananchi.

Sasa solution ya hii mambo ni nn wakuu? South afrika imetuonesha ni kiasi gani kuna wafanya biashara wengi kuliko viongozi. Kuna swala la kujifunza hapa kama nchi.
 
Katiba ndiyo dira ya maendeleo ya kiuchumi, kisiasa na kijamii, hivyo katiba mpya haikwepeki. Tuna mikwamo mingi sana katika kuleta mabadiliko ya kweli katika Taifa letu ambayo haina afya kwa mustakabali wa nchi lakini hupuuzwa kisiasa na wakati mwingine kwa nguvu ya dola.

Wakati wa kupata katiba mpya ni sasa kwa sababu hata maendeleo ya kiuchumi yatasuasua sana kwa kutumia katiba ya sasa ambayo inategemea hisani ya Rais. Ukiwa na Rais fisadi kama Magufuli tusitegemee kupata maendeleo ya watu bali tutaishia kuonyeshwa miundombinu, kupewa vitisho vya maisha yetu, kupata vifo visivyojulikana, kuleta ubaguzi wa kikabila na kikanda, kuzalisha miungu watu kama Sabaya na Makonda na madhila mengi ya kutisha.

Tunahitaji katiba mpya itakayoleta usawa, haki na itakayo heshimisha kila raia bila ubaguzi.
Kwanza kuna swali moja la kuuliza. Unapokuwa madarakani unaweza ukawa unakuja kwa nia njema kabisa ya kupigania haki za wananchi na sio maslahi binafsi na kulinda serikali hata kama inakosea.

Kwa maneno hayo sasa. Tujiulize, ni wangapi ambao wanaweza kuweka kipaumbele shida za wananchi na kuweza ku sacrifice hata uhai wake. Tunajua kupigania haki ni jambo linalohitaji ujasiri sana. Ili uwe kiongozi bora katika hili ni lazima pia usiwe mlafi wa pesa na uroho wa madaraka, pia unahitaji kua na mindset ya mwanafalsafa.

Kwa mfano tunawalaumu sana viongozi/wanasiasa juu ya uwajibikaji. Lakini ukweli mchungu kwa dunia ya sasa viongozi ni wafanyabiashara. Na siku zote mfanya biashara atafanya chochote hata kudiriki kudanganya wananchi ilimradi lengo lake litimie. Hawa huwa hawana uchungu na jamii wanazotoka, huwa ni waoga wa kupoteza mali na pesa kwa ajili ya kupambana dhidi ya matatizo ya nchi.

Kiongozi wa aina hii, huwa anahakikisha anacheza karata yake kwa umakini sana akiwa madarakani au nyazfa yoyote ya uongozi.
Sisi wananchi tunabaki kulia mara ooh mbona mbunge fulani anajua tuna matatizo fulani wilayani lakini haongei. Anaweza asiongee kwa sababu kwake ni rahisi kuishi vizuri aki defend serikali kuliko ku defend wananchi. So wanachofanya wanaaangalia sehemu yenye influence ya power. Kama kusifia raisi kutamfanya maisha yake yawe mazuri na salama atasifia sana hata kama ni ujinga.

Ndo maana tunasema kwa dunia ya sasa 2021 tuna wafanya biashara wengi sana kwenye nyazifa za uongozi kuliko wazalendo na viongozi wa kweli. Sifa kuu ya mfanyabiashara ni kufanya chochote kinachomwezesha kupata hela na usalama wa maisha yake sio ya wananchi.

Sasa solution ya hii mambo ni nn wakuu? South afrika imetuonesha ni kiasi gani kuna wafanya biashara wengi kuliko viongozi. Kuna swala la kujifunza hapa kama nchi.
 
Kuna haja kubwa kuwepo na katiba mpya..yenye kukidhi maitaji ya watanzania....dunia ya Leo .spika wa bunge ,Rais wa nchi hawatakiwi kuwa na Kinga....wanafanya madudu mengi hku wkijua katiba inawalinda....Leo hii tunsikia report ya C.A.G pesa zmepotea lkn hkuna htua zaidi...Leo hii Raising wa nchi anateua zaid ya watu 500 ma RC,DC DED,nk Dunia imeshatok hko....
Kwanza kuna swali moja la kuuliza. Unapokuwa madarakani unaweza ukawa unakuja kwa nia njema kabisa ya kupigania haki za wananchi na sio maslahi binafsi na kulinda serikali hata kama inakosea.

Kwa maneno hayo sasa. Tujiulize, ni wangapi ambao wanaweza kuweka kipaumbele shida za wananchi na kuweza ku sacrifice hata uhai wake. Tunajua kupigania haki ni jambo linalohitaji ujasiri sana. Ili uwe kiongozi bora katika hili ni lazima pia usiwe mlafi wa pesa na uroho wa madaraka, pia unahitaji kua na mindset ya mwanafalsafa.

Kwa mfano tunawalaumu sana viongozi/wanasiasa juu ya uwajibikaji. Lakini ukweli mchungu kwa dunia ya sasa viongozi ni wafanyabiashara. Na siku zote mfanya biashara atafanya chochote hata kudiriki kudanganya wananchi ilimradi lengo lake litimie. Hawa huwa hawana uchungu na jamii wanazotoka, huwa ni waoga wa kupoteza mali na pesa kwa ajili ya kupambana dhidi ya matatizo ya nchi.

Kiongozi wa aina hii, huwa anahakikisha anacheza karata yake kwa umakini sana akiwa madarakani au nyazfa yoyote ya uongozi.
Sisi wananchi tunabaki kulia mara ooh mbona mbunge fulani anajua tuna matatizo fulani wilayani lakini haongei. Anaweza asiongee kwa sababu kwake ni rahisi kuishi vizuri aki defend serikali kuliko ku defend wananchi. So wanachofanya wanaaangalia sehemu yenye influence ya power. Kama kusifia raisi kutamfanya maisha yake yawe mazuri na salama atasifia sana hata kama ni ujinga.

Ndo maana tunasema kwa dunia ya sasa 2021 tuna wafanya biashara wengi sana kwenye nyazifa za uongozi kuliko wazalendo na viongozi wa kweli. Sifa kuu ya mfanyabiashara ni kufanya chochote kinachomwezesha kupata hela na usalama wa maisha yake sio ya wananchi.

Sasa solution ya hii mambo ni nn wakuu? South afrika imetuonesha ni kiasi gani kuna wafanya biashara wengi kuliko viongozi. Kuna swala la kujifunza hapa kama nchi.
 
Back
Top Bottom