Tuirudishe Tanganyika Kwanza - Kiini cha Suluhisho

Tuirudishe Tanganyika Kwanza - Kiini cha Suluhisho

December 9 1961, Tanganyika ilipata Uhuru wake kutoka kwa Muingereza.

December 1963, Zanzibar ilipata Uhuru wake kutoka kwa Muingereza.

January 12 1964, Mapinduzi ya kuingoa Serikali ya Zanzibar iliyopata Uhuru kutoka kwa Muingereza December 1963 yalitokea.

April 26 1964, Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ulitokea na kuundwa kwa Taifa au Nchi mpya, Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

February 5 1977, vyama tawala vya Zanzibar ASP na Tanganyika (au kama inavyojulikana sasa Tanzania Bara) TANU viliungana na kuzaa CCM, Chama cha Mapinduzi ambacho kimfumo kina Makamu wawili, Makamu Bara na Makamu Zanzibar chini ya Mwenyekiti. Mgawanyo wa Uongozi na Uwakilishi ni nusu kwa nusu.

Rais wa kwanza wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoka Zanzibar, alikuwa na Makamu wa Rais ambaye alikuwa ni Waziri Mkuu wa Tanzania Bara.

Mfumo wa Utawala na Urais unasema Raisi akitoka Bara, ni lazima makamu atokee Zanzibar, na Waziri Mkuu wa Muungano anatokea Bara. Mfumo huo huo unasema Rais wa Muungano akitokea Zanzibar, Makamu wa Rais lazima atokee Tanzania Bara na Waziri Mkuu atatokea ... hapa ni utata, baada ya mabadiliko ya kuondoa nafasi ya Makamu wa Rais kutoka Bara kuwa Waziri Mkuu, nafasi hii sijui kama itakuwa ni ya Zanzibar au itashinikizwa kuwa ya Bara.

Bunge la Muungano, linaongozwa na Serikali ambayo hujenga hoja na bajeti kwa manufaa ya Tanzania bara na hata pamoja na kuwa kuna uwakilishi kutoka Zanzibar, nafasi ya Spika na Naibu siku zote wamepewa Watanzania Bara na si Wazanzibari kwa kisingizio cha kuwepo kwa baraza la Wawakilishi na Serikali yao.

Uhuru tunaosherehekea December 9, ni Uhuru wa Tanganyika na si Uhuru wa Tanzania kwa kuwa Tanzania haijawahi kuwa Koloni na kudai Uhuru. Mbaya zaidi, haijawahi kutamkwa rasmi kuwa Tanganyika, ilibadilisha jina na kuitwa Tanzania Bara. Hivyo si sahihi kabisa kusema kuwa December 9 ni Uhuru wa Tanzania. Tanzania ilizaliwa April 26 1964, itakuwaje tushangilie miaka 47 ya Uhuru wa Tanzania huku ukweli ni Uhuru wa Tanganyika na si Tanzania

Hivyo basi, kuna ubatili mkubwa sana wa mfumo mzima wa Muungano, uendeshaji wa Serikali zetu na hata mazingira mazima yaliyoleta kuundwa kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo yaliinyang'anya haki ya Utaifa na Nchi Tanganyika na kuinyang'anya mamlaka ya Utawala Zanzibar.

Swali langu ni kwa nini wakati lile kundi la G55 ambalo lilipewa nguvu na ushawishi wa kidemokrasia na aliyekuwa Makamu wa Rais na Waziri Mkuu Mzee wetu John Samuel Malecela, maarufu kama Tinga Tinga, lilikosa ushabiki kutoka kwa Watanganyika?

Kwa nini Mwalimu Julius Nyerere alikuwa akipinga kuundwa na kurudishwa kwa Serikali ya Tanganyika ndani ya mfumo mzima wa Muungano ambao una Serikali kuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania?
 
Mwanakijiji,

Mkuu mimi bado kabisa naomba kuelemishwa na matumizi ya haya maneno mawili:- NCHI na TAIFA...
Yaonyesha wewe unasema tofauti na Mheshimiwa Mwanasheria mkuu wa Zanzibar na umetoa tafsiri yako ktk matumizi ya maneno haya.. hata umefikia kutolea mfano hao National guards na kadhalika lakini hapo hapo inakuwaje tunapozungumzia - Wimbo wa Taifa na sio nchi tunakuwa na maana ya serikali ya muungano na sio States.. mathlan National Athem haisemi ni ya Michigan isipokuwa USA, Tanzania vile vile ni National athem... kwa nini usiitwe WIMBO wa NCHI ya Tanzania...

Kwanza nadhani ni muhimu tupate kiswahili ama kiingereza fasaha ktk matumizi ya maneno haya kisha hapo ndipo tunaweza kuendelea kujenga hoja zetu.
 
CCM knows the secret behind this dubious unity. We should not expect any changes as long as ccm remains in power. But their days are numberd
 
The casual use of 'country', 'state' and 'nation' as synonyms leads to confusion. Compounding this is the often confused official use: for example, the United Nations is actually a body made of 'states'; while the countries constituting the United Kingdom are sometimes called the home nations.

The United Kingdom is an internationally recognised sovereign state, which is also referred to as a country and whose inhabitants have British nationality, but the United Kingdom is a 300-year-old political union and each constituent part of the United Kingdom continues to be referred to as a 'country'. The terminology can be further complicated by the use of the word state to mean a non-sovereign sub-entity of a sovereign state, as is done in the United States of America and Australia. However, nations may also be defined by culture instead of ethnicity.

The physical creation and recognition of a new state is ruled by international law, which lists three requirements for 'statehood': a permanent and settled population, effective control by a government, and a fixed territory.

Under these requirements, a 'fixed territory' is defined as a 'natural segment of the Earth's surface' -- an apartment, artificial island or other constructed body does not suffice. 'Effective control by a government' means that a governing body must be able to maintain control over its claimed territory, while a 'permanent and settled population' must be a 'cohesive community with a common destiny' -- such a population can't merely be a group of people with a loose or superficial connection, such as a hobby or a commercial interest.

Finally, while the above is required for even the consideration of statehood, existing countries retain discretion over the formal political recognition of a newly-founded state.


Naomba ufafanuzi wa haya maneno matatu kwa kiswahili country, state na nation na hasa kwa mazingira ya Tanzania. Kazi kwenu wataalamu.
 
Naomba ufafanuzi wa haya maneno matatu kwa kiswahili country, state na nation na hasa kwa mazingira ya Tanzania. Kazi kwenu wataalamu.

Country=Nchi
State=Dola
Nation=Taifa
Government=Serikali au serekali(kutegemea ni pwani au mrima)

Asha
 
Uhuru tunaosherehekea December 9, ni Uhuru wa Tanganyika na si Uhuru wa Tanzania kwa kuwa Tanzania haijawahi kuwa Koloni na kudai Uhuru.

...Hivyo si sahihi kabisa kusema kuwa December 9 ni Uhuru wa Tanzania. Tanzania ilizaliwa April 26 1964, itakuwaje tushangilie miaka 47 ya Uhuru wa Tanzania huku ukweli ni Uhuru wa Tanganyika na si Tanzania

Kwani nani kasema tunasherehekea Uhuru wa Tanzania?

Naomba fungua Sheria ya Sherehe hapa:

http://www.parliament.go.tz/Polis/PAMS/Docs/No.%2057-1964.pdf
 
Kwani nani kasema tunasherehekea Uhuru wa Tanzania?

Naomba fungua Sheria ya Sherehe hapa:

http://www.parliament.go.tz/Polis/PAMS/Docs/No. 57-1964.pdf


Kuhani,

Shukrani kwa hiyo nakala ya mwaka 1964. Kwa kufuata Sheria ya 1964, bado December 9 1961 ni Uhuru wa Tanganyika.

Lakini maandiko ya baadaye na hata matumizi ya Siku hii, kiserikali na hata kupitia CCM, ni kuwa December 9 ni siku ya Uhuru wa Tanzania.

Viongozi na Serikali vikitoa tamko, vinajivunia miaka 47 ya Uhuru wa Tanzania, lakini wanaachilia Utata kuwa ni Tanzania ipi inayozungumziwa.

Kifupi Tanzania haijawahi kupata Uhuru. Zilizopata Uhuru ni Tanganyika na Zanzibar.

Hivyo, pendekezo langu ni kuwa December 9 tusiite tena siku ya Uhuru, bali tuiite Tanganyika day!
 
Ndio maana mwenzenu nimesema kwanza kabisa turudisha jina la "Tanganyika" halafu mengine yatakuja pole pole.
 
Nchi haina uwezo wa kuchagua raisi wake? Raisi wa Zanzibar anachaguliwa wapi kama si Dodoma? Unakumbuka yaliyompata Jumbe kujifanya anajua kuongea? aliishia wapi? Wa Zanzibar mu wafinyu wa kufikiri mno.
 
December 9 1961, Tanganyika ilipata Uhuru wake kutoka kwa Muingereza.

December 1963, Zanzibar ilipata Uhuru wake kutoka kwa Muingereza.

January 12 1964, Mapinduzi ya kuingoa Serikali ya Zanzibar iliyopata Uhuru kutoka kwa Muingereza December 1963 yalitokea.

April 26 1964, Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ulitokea na kuundwa kwa Taifa au Nchi mpya, Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

February 5 1977, vyama tawala vya Zanzibar ASP na Tanganyika (au kama inavyojulikana sasa Tanzania Bara) TANU viliungana na kuzaa CCM, Chama cha Mapinduzi ambacho kimfumo kina Makamu wawili, Makamu Bara na Makamu Zanzibar chini ya Mwenyekiti. Mgawanyo wa Uongozi na Uwakilishi ni nusu kwa nusu.

Rais wa kwanza wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoka Zanzibar, alikuwa na Makamu wa Rais ambaye alikuwa ni Waziri Mkuu wa Tanzania Bara.

Mfumo wa Utawala na Urais unasema Raisi akitoka Bara, ni lazima makamu atokee Zanzibar, na Waziri Mkuu wa Muungano anatokea Bara. Mfumo huo huo unasema Rais wa Muungano akitokea Zanzibar, Makamu wa Rais lazima atokee Tanzania Bara na Waziri Mkuu atatokea ... hapa ni utata, baada ya mabadiliko ya kuondoa nafasi ya Makamu wa Rais kutoka Bara kuwa Waziri Mkuu, nafasi hii sijui kama itakuwa ni ya Zanzibar au itashinikizwa kuwa ya Bara.

Bunge la Muungano, linaongozwa na Serikali ambayo hujenga hoja na bajeti kwa manufaa ya Tanzania bara na hata pamoja na kuwa kuna uwakilishi kutoka Zanzibar, nafasi ya Spika na Naibu siku zote wamepewa Watanzania Bara na si Wazanzibari kwa kisingizio cha kuwepo kwa baraza la Wawakilishi na Serikali yao.

Uhuru tunaosherehekea December 9, ni Uhuru wa Tanganyika na si Uhuru wa Tanzania kwa kuwa Tanzania haijawahi kuwa Koloni na kudai Uhuru. Mbaya zaidi, haijawahi kutamkwa rasmi kuwa Tanganyika, ilibadilisha jina na kuitwa Tanzania Bara. Hivyo si sahihi kabisa kusema kuwa December 9 ni Uhuru wa Tanzania. Tanzania ilizaliwa April 26 1964, itakuwaje tushangilie miaka 47 ya Uhuru wa Tanzania huku ukweli ni Uhuru wa Tanganyika na si Tanzania

Hivyo basi, kuna ubatili mkubwa sana wa mfumo mzima wa Muungano, uendeshaji wa Serikali zetu na hata mazingira mazima yaliyoleta kuundwa kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo yaliinyang'anya haki ya Utaifa na Nchi Tanganyika na kuinyang'anya mamlaka ya Utawala Zanzibar.

Swali langu ni kwa nini wakati lile kundi la G55 ambalo lilipewa nguvu na ushawishi wa kidemokrasia na aliyekuwa Makamu wa Rais na Waziri Mkuu Mzee wetu John Samuel Malecela, maarufu kama Tinga Tinga, lilikosa ushabiki kutoka kwa Watanganyika?

Kwa nini Mwalimu Julius Nyerere alikuwa akipinga kuundwa na kurudishwa kwa Serikali ya Tanganyika ndani ya mfumo mzima wa Muungano ambao una Serikali kuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania?

G55 walikuwa wanafiki kama tulivyo watanzania wengi na ndio maana hawakupata kuungwa mkono na Nyerere wengi wetu hatukumfahamu na hata wao wenyewe G55 hivyo hivyo - kwa mtazamo wake Nyerere aliona kuwa ile ndio nafasi ya nchi kuwa na upinzani wa kweli kaa alivyokwisha sema - alitaka G55 waendeleze madai yao nje ya CCM kwanisera ya CCM katika Muungano ni serikali mbili.

G55 waliweka madaraka mbele badala ya kusimamia hoja yao na wakaamua kubaki CCM na kufata sera ya chama.
 
CCM knows the secret behind this dubious unity. We should not expect any changes as long as ccm remains in power. But their days are numberd


Mkuu napingana na wewe hapo hasa katika suala la muda kwani kwa mazngira haya tuliyonayo tunajidanganya CCM wataendelea kuwa madarakani kwa muda mrefu - si nia yangu kuvunja moyo jitihada za ukombozi lakini ukweli ni lazima usemwe.
 
G55 walikuwa wanafiki kama tulivyo watanzania wengi na ndio maana hawakupata kuungwa mkono na Nyerere wengi wetu hatukumfahamu na hata wao wenyewe G55 hivyo hivyo - kwa mtazamo wake Nyerere aliona kuwa ile ndio nafasi ya nchi kuwa na upinzani wa kweli kaa alivyokwisha sema - alitaka G55 waendeleze madai yao nje ya CCM kwanisera ya CCM katika Muungano ni serikali mbili.

G55 waliweka madaraka mbele badala ya kusimamia hoja yao na wakaamua kubaki CCM na kufata sera ya chama.

Nyerere alilizuga Taifa.

Moja ya mabadiliko makubwa, makubwa kuliko yote katika historia ya sera za CCM ni Azimio la Zanzibar. Ambalo lili eviscerate Azimio la Arusha.

Azimio la Zanzibar lilifanywa na watu ndani au nje ya CCM?

Kingine cha ujanja ujanja wa Nyerere ni pale alipoteka nyara hoja ya kutaka Tanganyika akaliambia Taifa kwamba wanataka kuvunja Muungano.

Nyerere ali hijack matakwa ya Serikali tatu, akayafanyia ukarabati, halafu akasema Wabunge hawataki Muungano.

Historia imerekodi hivyo lakini sivyo ilivyokuwa.

Nyerere alijua sawia kwamba kusema kuna kero za Muungano haina maana tunataka kuuua. Alichota yeye ni kwamba usibadilike, ubakie kama ulivyonenwa hapo mwanzo kwenye imla aliyomsomea Mwanasheria wake, Roland Brown.
 
Kuna tafauti gani kati ya madai yako ya kutaka kuibua Tanganyika iliyomezwa kwenye muungano na "madai ya Kihaini' ya wazee wa Pemba walioomba wasaidiwe Pemba yao iwe na uhuru kama walivyosema kwenye barua, ombi lao la "creating an environment for the formation of a federal state in Zanzibar" ?

Umefanya uhaini?

hakuna tofauti.
Lakini hakufanya uhaini bali katumia haki yake ya kutoa maoni. Na kama kutoa maoni ni uhaini, watanzania tutakuwa tumekwisha.😱
 
Kama ambavyo Mwalimu alibashiri kuwa zanzibar ni mzigo kwa tanganyika you can see what is coming up, hawawezi kukubali kuwa wao sio nchi na taifa kwani taifa linaweza kuwa na kila kitu isipokuwa amiri jeshi mkuu na kutambulika na mataifa mengine, nafikiri hiki zanzibar lazima wakiweke kwenye akiri zao kwani ili taifa liitwe nchi ni lazima kuwe na majeshi na kutambulika na kushirikiana na nchi nyingine kitu ambacho zanzibar hawatakipata hata wafanye nini.

kuwa na wimbo na bendera zao sio tatizo kwani hata simba na yanga wana bendera na shule za sekondari zote tanzania zina nyimbo za shule ambazo zinasifia shule zao kama wimbo wa zanzibar unavyosifia taifa lao. hawawezi kwenda vitani bila amri ya raisi wa tanzania na hawana balozi kwenye nchi yeyote ulimwenguni.
 
hawawezi kwenda vitani bila amri ya raisi wa tanzania na hawana balozi kwenye nchi yeyote ulimwenguni.

..maneno haya ya maana sana, na nadhani haikuwa wazi mawazoni mwao walipokuwa wanadai nchi.

..au wana-send message kwamba wanataka nchi yao?
 
Ndio maana mwenzenu nimesema kwanza kabisa turudisha jina la "Tanganyika" halafu mengine yatakuja pole pole.

..ikirudi na muungano kwishilia mbali.

..ngoja tukubaliane namna ya kugawana mapato mafuta kwanza, halafu ndio tuje kwenye hayo.
 
Country=Nchi
State=Dola
Nation=Taifa
Government=Serikali au serekali(kutegemea ni pwani au mrima)

Asha

Tabaan. Kwa mujibu wa "definitons" hizi hivyo Zanzibar inastahili kuwa Nchi kwa kuwa ina mipaka maalum inayotambulika tokea enzi na enzi na kutawaliwa na Watawala mbali mbali kabla ya kupewa uhuru wake na kufanyika kwa Maoinduizi ya Januari 1964 na kufuatiwa na Tanzania ya l964. Zanzibar ni Dola kwa kuwa ina mamlaka kamili ya kuendesha Dola (Baraza la Wawakilishi. Rais, na Mahkama). Zanzibar si Taifa (kwa mintarafu ya kuwa madaraka yake katika mtizamo wa Kimataifa yameambatanishwa na ya mwenza katika Taifa jipya la Tanzania)
Tanzania ni Taifa lenye -Washirika-nchi mbili za Tanganyika na Zanzibar zilizoamua kushirikiana kuunda Taifa moja la Tanzania.
 
..ikirudi na muungano kwishilia mbali.

..ngoja tukubaliane namna ya kugawana mapato mafuta kwanza, halafu ndio tuje kwenye hayo.
Nakubaliana nawe.Lakini kuhusu mafuata kila Nchi na ifaidi ya kwake . Kumbuka tu kuna mpaka pale unaotenganisha Zanzibar na Tanganyika-katika Zanzibar Channel. Haujafutika huo, ,na wala hauwezi kufutwa. Asilan.
 
Sululisho bora la kero za MUUNGANO ni kuvunjika kwa MUUNGANO huu,unaboa munoo.
Wadugu zanzibar kama zenj wanatusaidia nini sisi watanganyika?pia watanganyika kama watanganyika tunawasaidia nini wazenj?Niliwaambieni zamani muno,wazenj wana ajenda zao na wakoloni wao(waarabu),kuvunjika kwa Muungano ni jawabu zuri kabisaaaaaaaa.
Siupendi Muungano hata punje,ni hasara tuu.
 
Back
Top Bottom