Ukweli tunataka kupandikiza ukabila udini na ukanda awamu hii kuliko kipindi chochote .
Serikali inapandikiza Ukanda, wananchi wanapandikiza ukabila
Dini zinapandikiza udini kwa kuleta mpaka CV za waslamu jamii forum sijui ndio zitusaidie nini.
Tumeamua kuondoa utaifa na kuwa wabaguzi lakini makosa makubwa yapo kwa rais wetu ambaye anaonekana wazi wazi kupendelea chato halafu kuna watu wanamsapoti.
Tatizo lipo tena kwa watanzania kuamini kutoendelea kwao ni kwa sababu kumesababishwa na watu wa kasikazini maana wao wameendelea yaani watu wa kasikazini kwa ujumla.
Leo hii tunashangilia uwanja wa ndege wa kiwango cha kimataifa kujengwa kwenye population ya ya watu 17,000 hii haijawai fanyika duniani kote.
Ukabila ukabila ukabila Nyerere hatukumuelewa alipokuwa akipigania utaifa kwanza.
Hivi wahaya,wachaga na wasukuma tukijifanya nchi hii ni yetu makabila mengine yakiungana nini kitatokea?
Waislamu hii nchi wakijifanya ni yao Christians wakiungana nini kitatokea
Christian hii nchi wakijifanya ni yao waislamu wakiungana nini kitatokea?
Huku mtaani tunaishi na watu wa kila aina mwingine mmakonde,Mjaluo,Waha wanyamwezi tunacheka tunakunywa tunafurahia lakini unaamka asubuhi unaanza kueneza ukabila kwa vile unatumia I'd fake jamii forum wakati ukute wewe ni kiongozi wa kitaifa au chama.
Wengine kama mimi ni wakatoriki lakini tulisoma shule za waislamu. Vijini waislamu na dini zingine wanashirikiana sana tena kwa upendo mkubwa .
Lakini mijitu misomi ndio inashinda jamii forum kupandikiza chuku na uhasama wa kidini ukanda na ukabila.
Lazima tukubali ukweli kuwa Rais anapopendelea kwao tuungane kama taifa tumshauri ajirejebishe.
Serikali inapotutangazia kuwa mkoa wa Kagera ni mkoa masikini wakati una umeme kila kijiji tena kila nyumba karibu ina luku lazima tutafakari kuwa kwanini watangaze kagera ni mkoa masikini?
Kumbukeni makabila yote ya Tanzania Tanzania sio kwenu ni waamihaji walio wengi ukiondoa wagogo ndio wazawa .
NYERERE WAKO ALIKUWA NDIYE MDINI NAMBARI MOJA
Desemba 1993
MJADALA unaendelea nchini kote juu ya kuundwa kwa serikali ya Tanganyika na muundo wa Muungano wa Zanzibar na Tanganyika. Inavyoelekea yapo matatizo, dosari na sababu za msingi zilizopelekea wananchi kuhoji muundo wa sasa wa Muungano na kuleta hoja ya kuundwa kwa serikali ya Tanganyika ni yenye kuundwa kama si leo kesho.
Lakini wapo pia wanaopinga kabisa kuundwa kwa serikali ya Tanganyika.
Aliyejitokeza kwa nguvu na kwa ukali hadharani kupinga hoja hiyo ni Mwalimu Julius Nyerere, katika kupinga hoja hiyo Mwalimu anatoa hoja zifuatazo:
Hoja ya kuundwa kwa serikali ya Tanganyika imeletwa kwa kuwachoka Wazanzibari na Waislamu. Ufupi wa maneno Mwalimu Nyerere anadai hoja ya kuundwa Serikali ya Tanganyika imetokana na chuki za kidini - Wakristo kuwachukia Waislamu.
Hoja haipo katika sera za CCM na taratibu zimekosewa.
Kuundwa kwa serikali ya Tanganyika kutavunja Muungano na kutavunja Tanganyika pia.
Ukizingatia sifa nyingi ambazo Nyerere alijilimbikizia wakati wa utawala wake na sasa si vigumu kuelewa kwa nini anapinga kuundwa kwa serikali ya Tanganyika. Mambo yake yote aliyoyaanzisha kwa vishindo huku akisifiwa kuwa zidumu fikra zake, yamekuwa yakiporomoka moja baada ya jingine huku mwenyewe akiona. Lililosalia ni Muungano; nao ukiporomoka haitaleta picha nzuri katika historia yake katika siasa.
Lakini lililo gumu kueleweka ni hatua ya Mwalimu Nyerere kutumia Turufu ya udini kuwagawa Wabunge; wana-CCM na Wa-Tanzania kwa ujumla katika suala hili. Kauli hiyo ingesemwa na Muislamu ingepewa mtizamo tofauti na labda isingeeleweka hasa miongoni mwa Waislamu. Lakini kusemwa na Mwalimu Nyerere kunaleta mkanganyiko zaidi. Kwanini; (udini ulikuwa umejengeka). Hali hiyo ilipelekea Masheikh kumlalamikia lakini akawanyamazisha kwa kuwashutumu kuwa wanachanganya dini na siasa. Miongoni mwa Masheikh hao wapo waliofukuzwa nchini; waliowekwa kizuizini, waliofukuzwa katika chama na kadhalika.
Sheikh Hassan bin Amir katika waraka wake kwa Waislamu mwaka 1963 aliutaja udini uliokuwa unajengwa Tanzania kwa kutoa mifano ifuatayo:
Kuingizwa nchini Tanganyika mara tu baada ya uhuru vimedali vidogo vidogo vyenye picha ya bendera ya Tanganyika usoni na katikati ya bendera hiyo amesimama Mama Maria na mtoto mchanga na nyuma yake maandiko '
MARIA MTAKATIFU ULINDE UHURU WA TANGANYIKA'.
Gazeti la
KIONGOZI la tarehe 1/8/1963 lilimuonyesha Bwana George Kahama akipewa cheo cha dini na Pope kwa
kuwakilisha serikali ya Tanganyika katika mkutano wa Makanisa ya Roma.
Mwaka huo huo wa 1963, mnamo tarehe 24 mwezi wa nane, Baraza Kuu la Makanisa ya Kilutheri Tanganyika lilitoa matangazo kuwa Uhuru wa Tanganyika ulikuwa '
Chini ya Msalaba'.
Tarehe 17/5/1963 Makanisa yalifanyia mkutano wao ndani ya Bunge.
Alipokufa Pope Yohana wa 23 bendera ya taifa ilipepea nusu mlingoti nchi nzima!
Kabla ya kifo chake Pope Yohana wa 23 alimletea Mheshimiwa Nyerere barua ya pongezi kwa kuupanua Ukristo- barua ambayo ilitiwa saini na Pope mwenyewe. Barua hiyo imetangazwa kwenye gazeti la
Tanganyika Standard.
Gazeti la
Reporter la Kenya la tarehe 20/6/1963 lilitangaza katika ukurasa wake wa mbele: "
KUIBADILI AFRIKA YA MASHARIKI KUWA KATIKA DINI YA ROMANI CATHOLIC". Ndani ya gazeti hilo ukurasa wa 18 liliwataja waliopewa dhamana ya kufanikisha jambo hilo kuwa ni: Uganda - Kiwanuka, Kenya - Mboya na Tanganyika Mheshimiwa Nyerere.