Trust katika Mahusiano

Trust katika Mahusiano

Kweli Kaunga, huo uongo anaoongelea FP hauna tija kabisa....

Ila nilishasema kwamba, uongo mtakatifu au kutosema baadhi ya mambo ni vitu vya muhimu na haviepukiki katika mahusiano.

Mfano, kwa nini umweleze mpenzi wako kwamba umekutana na ex-BF/GF mahali wakati unajua itamuumiza?

Kwa nini umweleze kuwa utapita kwa rafiki yako John/Amina wakati unajua hampendi?

Babu DC!!

Hata ukimkuta Juma/Amina njiani bora useme kama mlikutana na kuzungumza zaidi ya salam tu

Bora ajue unamwambia ukweli japo hampendi hiyo rafiki, kuliko kuonekana unaficha ficha
 
hapo kwenye RED sasa ndo adha ya uongo..... ukishaanza kuusema, ili mwenzio akuelewe, basi hiyo chain itaendelea..... there is no way utaokoka. kinachonishangaza tu ni kwa nini mtu ujiingize kwenye hiyo chain kwa uongo usio na tija? ule wenye tija labda, ingawa kwangu uongo ni uongo, wenye/usio na tija....
umenichekesha sana ulivyo-narrate hizo scenarios, lol!

FP katika mahusiano kuna masuala really serious... Ila mwisho wa siku unaweza ishia kucheka. Lol!

BTW kuna watu ni waongo hadi baas! Hata watoto wenyewe ndani; unaweza kuta mtoto wako ambaye constantly yeye majibu yake muongo kwa vitu vidogo dogo hata hastahili kuongopa - sasa huyu katika mahusiano kimbembe...

Asante kwa mada yako relevant.
 
Hahahaaaaaa!!! Leo sijui FP umeamkia wapi dada yangu?
Vipi dada unaenda kwa shangazi au kwa kaka?

Back to topic.
Uaminifu umekuwa ni kitu hadimu sana katika maisha yetu ya kila siku. Ni watu wachache sana ambao katika maneno yatokayo mdomoni mwao kila neno huwa la kweli. Watu tumekua na udanganyifu katika maisha yetu ya kila siku, hii inatokana na jinsi tulivyojichagulia kuishi.

Binafsi nimekua mdanganyifu pale ninapoona mambo yanakuwa magumu, ila naamini sio mimi tu, tupo wengi wenye tabia hii ya udanganyifu.

Mfano:Mmeahidiana na Boss wako mkutane mahali fulani kwaajili ya kitu fulani, ila muda unakwenda halafu unakuta Boss amefika kabla yako na anapokupigia simu kukuuliza uko wapi? Unamjinu upo maeneo ya karibu na pale mlipoahidiana mkutane, wakati unawezakuta hiyo simu aliyokupigia Boss wao ndo imekukumbusha kwamba mlikua na appointment.

Hapo tunaona udanganyifu unaweza kukusaidia kufanikisha dhumuni mlilokuwa mnataka mlikamilishe au inaweza kukufanya upoteze uhusiano mzuri na wenzako pale utakapomdanyanya na akakusubiri kwa kipindi kirefu nila wewe kutokea.

Tumuomba Mungu atuomdolee tabia ya udanganyifu akilini mwetu huku nasi tukihjitahidi kujifunza kusema kweli ambayo itatuweka huru.
 
Last edited by a moderator:
FP hivi unapoanza kufikiria kwa umakini namna hii utafikiri unabalance redox reaction ya complex compound huwa unakuwa umekula nini??

to me jamani hili swala linategemea sana unaish na mtu wa namna gani. Binafsi hubby ni bora umwambie ukweli tu hata kama ni mchungu manake atafume kisha mtaenda sawa. ila lying halafu baadae aje agundue hilo nimeshaonaga ni kosa ambalo halisameheki kirahisi kwake.

kwangu mimi ni bora niseme ukweli hata kama unauma sana najua maumivu yake yatapoa life itasonga but lying to him sithubutu.
na wewe kila siku nakuambiaga sisi wengine sayansi ilitutupa mkono tangu tunazaliwa sasa hapo kwenye RED umeandika nini? najua huwezi kunitusi, lol! mwenzio ukiona naandika mada kama hizi ujue kuna kitu kinanikula akili yangu.... si unajua mimi mama ushauri? sasa nikipataga kesi ambazo ninanikosesha usingizi ndo matokeo yake yanakuwa hivi.
kiukweli hakuna kitu kinachoniuma sana kama kuhisi nimedanganywa........ you know me, ni mwelewa sana, inapotokea hata mwanangu tu anidanganye huwa naumia sana, najiuliza maswali mengi, hivi kanionaje?
 
Sidhani kama kuna kutaka au la. Nadhani ndo asili yake tu. Ndiyo maana kuna msemo wa Kizungu usemao 'the phenomenon of love'. Maana yake ni kwamba hata ufanye nini kuyaelewa kikamilifu ni jambo gumu sana.

Ndiyo maana unakuta mwanaume kaoa mcheza filamu za ngono na eti wanapendana sana na wala hasumbuliwi na ajira ya mkewe au unakuta mama mzima (mwalimu) mwenye miaka 30 na kitu na ni mke wa mtu lakini anagegedana na mmoja wa wanafunzi wake ambaye ni teenager na hadi anafikia kubeba ujauzito wa huyo bwa'mdogo, hali inayopelekea kutalikiana na mumewe wa ndoa na kuanza maisha na huyo serengeti boy.

Hayo nayo ni mapenzi.
nilikuelewa rafiki, nikakukatia kiu tu, hakuna la zaidi
 
Da Mkubwa, aksante kwa salamu jamani huyu FirstLady1 anajua ninavyomwonea wivu.............. haha. Ni kweli dada kama mpenzi ni mwelewa kuna uwongo mwingine ambao hauna tija sana sana hata akigundua kuwa unamdanganya atakushangaa. Na kwa nini utengeneza uwongo ilhali wajua kuwa mwenzio ukimwleleza atakuelewa? Ni hulka au?
hapo ndo point yangu dada mdogo, na ndo kitu kinachouma zaidi. mtu anajua kabisa kuwa nikimwambia hivi atanielewa, kwa nini useme uongo? kuna ajenda gani hapo mpaka useme uongo? hapa sasa ndo inakuja ile dhana ya Baba_Enock kuwa inawezekana unadanganya sababu una mpango mwingine, tofauti kabisa na haya unayoyasema
 
Last edited by a moderator:
Kwa ujumla uongo sio kitu kizuri na hakuna anaependa kudanganywa au kudanganya . Naona AshaDii amejaribu kuzungumzia uhalisia au mazingira yanayopelekea mtu kusema uongo. Tunapoishi pamoja tunajuana mapungufu yetu na wakati mwingine nini hapendi/anapenda mwenzangu. Au una avoid hofu na kumvunja moyo mwenzio . kiukweli kudanganya/kudanganywa hakupendezi na ikumbukwe kuwa si kila wakati unapaswa kusema ukweli yapasa uzingatie mazingira na hisia za mwenzio.
 
Simpendi mtu mwongo kabisa hasa katika mahusiano.
Na kwa bahati mbaya ni rahisi kujua "huyu amenidanganya". Usipokuwa mwaminifu kwa mambo madogo makubwa je?
I can stand mpenzi wangu anitukane akiwa na hasira lakini siyo kunidanganya.
ha haaaa, nimekuelewa sana mtani. mimi pia sipendi uongo. nyumbani kwangu tunaambiana nataka kufanya hili, kama mwenzio hataki anakuambia usifanye na anakupa sababu kwa nini usifanye, mkielewana yanaishia hapo (itategemea nani atashinda katika maongezi yenu).
Mtu akinidanganya naona ananiona mimi mjinga, I can't think/ I don't understand...... yaani hawezi niambia kitu nikaelewa, ndo maana anaona dawa yake ni kunidanganya tu. I can stand mtu akinidanganya jambo lenye tija..... for God's sake husband hawezi niambia ukweli kuwa ana mpango wa kando, lazima adanganye.... nikimbamba kwa hilo nitaelewa kuwa hakupaswa kusema ukweli, alipaswa kunidanganya. hapo atasema kilichomsibu na kuomba msamaha.
cc. Kaizer, Dark City, Asprin, BAK, The Boss, KakaKiiza, Arushaone, Baba V
 
Last edited by a moderator:
Nadhan ukiwa na mtu mwenye mawivu ivi vtu vinakuwepo kupunguza maugomvi .hata mimi huwa nadanganya coz my bf anamaswali ya kero yanayopelekea tugombane.et"kila cku kwa aunt yako mnaendaga kuongea nini"mtu wa ivi lazma udanganywe cjui hamjiamini yan mnakera ndo sababu.
 
FP katika mahusiano kuna masuala really serious... Ila mwisho wa siku unaweza ishia kucheka. Lol!

BTW kuna watu ni waongo hadi baas! Hata watoto wenyewe ndani; unaweza kuta mtoto wako ambaye constantly yeye majibu yake muongo kwa vitu vidogo dogo hata hastahili kuongopa - sasa huyu katika mahusiano kimbembe...

Asante kwa mada yako relevant.
mimi mdada wangu ananayenisaidia home!uuuuuuuwih!anadanganya kila kitu!anaweza akaulizwa uko chumbani hachelewi kusema alitaka kwenda maliwato!eheehehhehhehe nishamzoea lakini hii tabia inanikera sana kwa kweli!zitu vingine yuko poa hadi raha!ila mwongo jamani! uuuuuuwih!sijui nafanyaje!
 
ha haaa, rafiki unanilazimisha twende huko, hakuna ubaya lakini.
Inawezekana mtu anaaga kwenda kwa shangazi kumbe anaenda kwa dada ili akakutane na mtu wake, sijui....
sasa mbona unakimbia wakati ndo kwanza ngoma inaanza?
natamani sana kuwasikia Mtambuzi na Himidini (mzee wa maombi kabla ya mlo, lol!)
Halafu hii ya kuaga unaenda kwa shangazi kumbe unaenda kwa dada sio nzuri kabisa kiufupi uongo si kitu chema na ukisha kosa uaminifu ni vigumu sana mtu kukuamini tena hata kama siku nyingine utasema ukweli. Hasa kwenye mahusiano ndio mbaya kabisa
 
ha haaa, babu huo uongo usio na tija ndo haswa ninaotamani kuujadili hapa.....
unajua tunaweza ona hauna tija lakini labda sababu za huo uongo zina tija..... ndo maana nauliza kwa nini uuseme huo uongo ambao unaonekana kabisa hauna tija?
kama mwenzio hapendi wewe uonane na John, unadanganya na unaenda kumwona John, akigundua ulienda kumwona itakuwaje?
Unapoamua kusema uongo, mara nyingi unajaribu kutokumuudhi mwenzako kwa suala ambalo unajua hapendezwi nalo. Unakuwa unajua kwamba ukimwambia ukweli .. kwa kitu ambacho hapendi ataudhika, hivyo unadanganya. lakini madhara ya uongo ni makubwa zaidi kuliko kama ungemweleza ukweli, ingawaje pia angechukia.
 
hapo ndo point yangu dada mdogo, na ndo kitu kinachouma zaidi. mtu anajua kabisa kuwa nikimwambia hivi atanielewa, kwa nini useme uongo? kuna ajenda gani hapo mpaka useme uongo? hapa sasa ndo inakuja ile dhana ya Baba_Enock kuwa inawezekana unadanganya sababu una mpango mwingine, tofauti kabisa na haya unayoyasema

@FP,

Hakuna mtu anayesema uongo bila ya kuwa na sababu...No, NEVER...!

Halafu pia, ni vigumu sana "kusoma ubongo" wa mtu mwingine, so, swali la "kufikiri" kuwa "x" nikimwambia hivi "atanielewa" siyo kweli hata kidogo. Na ndiyo maana unachoita "mambo ya kawaida", si sawa, hakuna "mambo ya kawaida".

Uongo mwingine unatengenezwa na mazoea katika mahusiano, na ni vizuri uwepo ili "kupitisha siku"...!

"Chakula tayari"? haiwezi kujibiwa na kauli ya "bado"....!
"Upo wapi"? haiwezi kujibiwa na kauli ya "nipo gesti hausi"...!
"Unafanya nini"? haiwezi kujibiwa na kauli ya "nina-do"...!
"Watoto wameshakula"? haiwezi kujibiwa na kauli ya "bado"...!

Kuna swali ambalo unaulizwa, na unajibu bila hata kufikiria, kwa maana unafahamu yule aliyekuuliza anataka jibu gani...!
 
mi nahama kabisa kwenye vintage!
hv unajua kuna watu wataalamu wa uongo kiasi moka unajiuliza hiv why did he/she lie here?
hv ukisema nimevaa rangi nyeupe wakati tunakuona umevaa ya kijani ujue ni tatizo!
lakini kutokuwa mkweli wakati mwingine ni kujikataa!
yumkini unafanya maovu sana kiasi cha kuaminini nikihakikisha naonekana mwema pengine itanipa faraja kiasi fulani!
lakini tunaweza pia kuwa tumeengukwa na watu tunaoamini wako waaminifu sana kiasi cha kuamini sisi ni waovu so let me jus be this cyrstal kumbe duh!
lakini wakati mwingine matarajio ya jamii zinazotuzunguka zinatulazimisha kuwa sio sisi!
au pengine ni vile sisi tumeiaminisha jamii inayotuzunguka kuwa sisi ni hawa na kuwa mtumwa wa hiyo image tunayoamini jamii inayo kutuhusu!
mi sijui nawazza tu kwa sauti!
huwa sielewi kwa kweli!
ha haaa, nimekupata saaana mdogo wangu, hapo sasa.....
hebu fikiria sasa hapo shostito kama huyo utamweka katika kundi gani? anafaa au ndo wa kumwaga tu!
hivi cacico bado ananyonyesha? kawa adimu sana siku hizi mitaa hii
 
Last edited by a moderator:
mimi mdada wangu ananayenisaidia home!uuuuuuuwih!anadanganya kila kitu!anaweza akaulizwa uko chumbani hachelewi kusema alitaka kwenda maliwato!eheehehhehhehe nishamzoea lakini hii tabia inanikera sana kwa kweli!zitu vingine yuko poa hadi raha!ila mwongo jamani! uuuuuuwih!sijui nafanyaje!
Umenikumbusha mbali nilikua na mdada wa kazi bwana alikua muongo hata umbambe na kitu mkononi atakudanganya tu. Uzuri alikua mchapa kazi sana n aliwapenda sana wanangu .
 
Hata ukimkuta Juma/Amina njiani bora useme kama mlikutana na kuzungumza zaidi ya salam tu

Bora ajue unamwambia ukweli japo hampendi hiyo rafiki, kuliko kuonekana unaficha ficha
ha haaa, hiyo kali.....
kuna mkaka alipigwa kwara na mkewe asionane na mimi. mimi nikamwambia kwa kweli naheshimu sana ndoa za watu, mimi nawe hatuna chochote kitakachoharibika kama hatutakutana, nikamwambia tusionane tangu hiyo siku. Kuna siku tulionana barabarani na tukasalimiana, sasa sijui alienda mwambia mkewe kuwa tulionana? lol!
 
  • Thanks
Reactions: BAK
FP katika mahusiano kuna masuala really serious... Ila mwisho wa siku unaweza ishia kucheka. Lol!

BTW kuna watu ni waongo hadi baas! Hata watoto wenyewe ndani; unaweza kuta mtoto wako ambaye constantly yeye majibu yake muongo kwa vitu vidogo dogo hata hastahili kuongopa - sasa huyu katika mahusiano kimbembe...

Asante kwa mada yako relevant.
ha haaa, hapo kwenye watoto ndo usiseme my dear, yaani ni majanga........
mimi huwa nasema tu mmmmmmmmhhhhhhhhhhh na jicho nimemkazia, utasikia Nimedanganya, lol!
 
ha haaa, nimekupata saaana mdogo wangu, hapo sasa.....
hebu fikiria sasa hapo shostito kama huyo utamweka katika kundi gani? anafaa au ndo wa kumwaga tu!
hivi cacico bado ananyonyesha? kawa adimu sana siku hizi mitaa hii

AH!kunyonyesha huko ananyonyesha kituo!
atupishe kule!hebu aje hapa!
ish kwani hapa mbn kama nna hasira sana!
we mke mwenza hebu kuja huku!
 
Back
Top Bottom