Judgement
JF-Expert Member
- Nov 13, 2011
- 10,326
- 4,789
Mpendwa my fellow Jf membar, awali ya yote nakuomba unipe macho na maskio na uvumilivu wako uisome hii story.
Kwa kuyahifadhi majina halisi ya wahusika, nitatumia majina ya kubandika.
Mzee Karama alikua muhamiaji hapa Tanzania katika miaka ya 70"s. Hakua raia wa nchi hii.
Alikuja Tz kwa dhumuni la kutafuta maisha.
Akiwa hapa nchini, Mz. Karama alikutana na Shangazi yangu wakapendana na hatimae ndoa.
Maisha yao yaliwapatia watoto wa 5 kati ya hao wa kike watatu na wa kiume wawili.
Mfuatano wao mtoto wa kwanza hadi wa tatu wa kike ndiyo walifuatana na wa4 na wa5 walimalizia uzao.
Katika miaka ya 80"s Mz. Karama aliihamisha familia yake yote kwao, nchi aliyotoka.
Kuanzia Shangazi na watoto wote, mistake aliyofanya Mz Karama ni kutofanya utaratibu kisheria kwa kanuni za uhamiaji za uraia wa familia yake, kwakua watu wa familia yake hawakutambulika katika nchi hiyo.
Hivyo familia ya Mz Karama ikawa inaishi kinyume na sheria.
Mwaka mmoja kupita tangu wahamie Shangazi yangu akafariki na akazikwa hukohuko.
Miezi 6 kupita tokea shangazi afe, binti wa kwanza Riza akaolewa, na mume aliemuoa Riza nae hakua raia wa nchi hiyo waliohamia, alikua ni raia toka nchi jirani na hiyo.
Hivyo baada ya kuolewa Riza alihamia huko kwa mumewe, ambako alikumbana na maisha magumu kwani shughuli ya mumewe ilikua ni kilimo, ufugaji na kwa kua palikua ni kijijini sana miundo mbinu ilikua ya shida, vitu kama utafutaji kuni maji ndiyo ilikua changamoto kwa Riza.
Kwenye mji wa Mz Karama wakabaki Bebiy na Mariyamu na wale wa kiume wadogo.
Katika story hii niliyemlenga ni Bebiy bint wa 3 kuzaliwa.
Babiy alipata kibarua Super market, alifanya kazi kiujaujanja siku akisikia fununu ya msako wa wahamiaji haramu hatoki.
Kwa kua Bebiy alikua ni makini na capacity yake ya uelewa pale kazini, muda si muda akapewa usupervisor.
Hilo liliwauma baadhi ya staff wenzake, na kati ya staff wale mmojawao waliishi jirani, na alikua akiijua familia ya Karama haina uhalali wa uraia.
Huyo jirani yake staff alimchoma Bebiy kwa maofisa uhamiaji, na Bebiy akakamatwa na polisi, badae kotini kisha Prison.
Bebiy alihukumiwa jela miaka miwili, kule gerezani akakuta mpango ni kila room wafungwa wawili,
chumba alichopangiwa Bebiy alimkuta mdada ambae alikua ana mtoto mdogo wa kiume wa mikononi. Kama ilivyo kawaida wakaanza kuulizana haya na yale, kwanza wakajikuta wote wanaongea kiswahili.
Kumbe na yule mdada nae kosa alilofungiwa, ni kosa kama la Bebiy la uraia, ni bahati ilioje ufungwe nchi ya mbali na ukutane na mfungwa mwenzio mnaongea lugha moja ?.
Yule mdada alimwambia Bebiy yeye na mme wake walihamia hapo wakitokea Zanzibar, na walihamia bila kanuni za sheria.
Na tangu akamatwe mumewe imebidi atorokee kwenye miji mingine tofauti na huo.
Wiki mbili baada ya hapo mdada akaanza kuumwa, kuumwa kukazidi ikalazimu kitengo cha magonjwa hapo prison kimpeleke hospitali kubwa nje ya gereza.
Mdada yule kabla hajapelekwa hosp alimkabidhi Bebiy mtoto, akavua Herini, Bangili, Mkufu, vyote vya dhahabu na kijikaratasi chenye No ya simu ya mumewe Baba wa huyo mtoto aliekua akiitwa J.
Akiwa analengwa machozi mama J alimwambia Bebiy kwamba hategemei kurudi gerezani akiwa hai. (namnukuu)
"Ndg yangu Bebiy nakuachia mtoto nakuachia na rasilimali kidogo Mungu alizoniwezesha kua nazo, mlee huyo mtoto awe mwanao, sina namna nyingine ya kufanya ukijaaliwa kumaliza kifungo jaribu kumtafuta Babaake J , anaitwa Mr. Tiba, na kwa tatizo lolote la mtoto ama ataugua au vinginevyo unaweza ukauza chochote katika hivyo vipuli vitakusaidia mbele ya safari." (mwisho kunukuu)
wote machozi yakawamwagika mama J, akachukuliwa na gari ya jela na kupelekwa hosp na kupita siku 3 mama J akafariki, habari zikafika gerezani za msiba Bebiy akalia sana na akashukuru Mungu.
Mwaka mmoja, baadae askari mmoja wa gereza akaanza kumtongoza Bebiy huku akimuhadaa kua akiwa atamkubalia basi anao uwezo wa kumfanyia mpango Bebiy akatoka jela kwa kupitia misamaha ya kiongozi wa nchi.
Bebiy hakuyumbishwa na hilo, alimkatalia huyo askari mzee mpango wake.
Bebiy alikomaa akamaliza kifungo chake.
Na wakati Bebiy anaingia gerezani palikua na form ya kujaza ambapo ktk hiyo form kuna kipengele cha kujaza uraia wako unatoka nchi gani.
Bebiy alijaza anatoka ile nchi jirani alipoolewa dadaake Riza, hivyo siku amemaliza kifungo alipakiwa kwenye gari la serikali hadi nchi ile ya jirani, akiwa na mwanae J aliyempata jela, ikumbukwe miezi mi3 nyuma kabla Bebiy hajamaliza kifungo Mz Karama alifariki.
Bebiy baada kubatwa hapo kilichoanza kumsaidia No ya simu ya dadaake Maryamu alikua nayo kichwani, hivyo alitafuta duka la sonara akauza bangili moja, kisha akatafuta callbox na kumpigia kumpa habarize.
Then akamuomba Mariyamu ampe No za simu za Riza, akapewa na akampigia Riza.
Haikua rahisi Bebiy kufika huko kwani palikua ni umbali (kama Mtwara na Bukoba).
Ilimlazimu Bebiy kubadili magari ma3 kumfikisha huko. NITAENDELEA N
Kwa kuyahifadhi majina halisi ya wahusika, nitatumia majina ya kubandika.
Mzee Karama alikua muhamiaji hapa Tanzania katika miaka ya 70"s. Hakua raia wa nchi hii.
Alikuja Tz kwa dhumuni la kutafuta maisha.
Akiwa hapa nchini, Mz. Karama alikutana na Shangazi yangu wakapendana na hatimae ndoa.
Maisha yao yaliwapatia watoto wa 5 kati ya hao wa kike watatu na wa kiume wawili.
Mfuatano wao mtoto wa kwanza hadi wa tatu wa kike ndiyo walifuatana na wa4 na wa5 walimalizia uzao.
Katika miaka ya 80"s Mz. Karama aliihamisha familia yake yote kwao, nchi aliyotoka.
Kuanzia Shangazi na watoto wote, mistake aliyofanya Mz Karama ni kutofanya utaratibu kisheria kwa kanuni za uhamiaji za uraia wa familia yake, kwakua watu wa familia yake hawakutambulika katika nchi hiyo.
Hivyo familia ya Mz Karama ikawa inaishi kinyume na sheria.
Mwaka mmoja kupita tangu wahamie Shangazi yangu akafariki na akazikwa hukohuko.
Miezi 6 kupita tokea shangazi afe, binti wa kwanza Riza akaolewa, na mume aliemuoa Riza nae hakua raia wa nchi hiyo waliohamia, alikua ni raia toka nchi jirani na hiyo.
Hivyo baada ya kuolewa Riza alihamia huko kwa mumewe, ambako alikumbana na maisha magumu kwani shughuli ya mumewe ilikua ni kilimo, ufugaji na kwa kua palikua ni kijijini sana miundo mbinu ilikua ya shida, vitu kama utafutaji kuni maji ndiyo ilikua changamoto kwa Riza.
Kwenye mji wa Mz Karama wakabaki Bebiy na Mariyamu na wale wa kiume wadogo.
Katika story hii niliyemlenga ni Bebiy bint wa 3 kuzaliwa.
Babiy alipata kibarua Super market, alifanya kazi kiujaujanja siku akisikia fununu ya msako wa wahamiaji haramu hatoki.
Kwa kua Bebiy alikua ni makini na capacity yake ya uelewa pale kazini, muda si muda akapewa usupervisor.
Hilo liliwauma baadhi ya staff wenzake, na kati ya staff wale mmojawao waliishi jirani, na alikua akiijua familia ya Karama haina uhalali wa uraia.
Huyo jirani yake staff alimchoma Bebiy kwa maofisa uhamiaji, na Bebiy akakamatwa na polisi, badae kotini kisha Prison.
Bebiy alihukumiwa jela miaka miwili, kule gerezani akakuta mpango ni kila room wafungwa wawili,
chumba alichopangiwa Bebiy alimkuta mdada ambae alikua ana mtoto mdogo wa kiume wa mikononi. Kama ilivyo kawaida wakaanza kuulizana haya na yale, kwanza wakajikuta wote wanaongea kiswahili.
Kumbe na yule mdada nae kosa alilofungiwa, ni kosa kama la Bebiy la uraia, ni bahati ilioje ufungwe nchi ya mbali na ukutane na mfungwa mwenzio mnaongea lugha moja ?.
Yule mdada alimwambia Bebiy yeye na mme wake walihamia hapo wakitokea Zanzibar, na walihamia bila kanuni za sheria.
Na tangu akamatwe mumewe imebidi atorokee kwenye miji mingine tofauti na huo.
Wiki mbili baada ya hapo mdada akaanza kuumwa, kuumwa kukazidi ikalazimu kitengo cha magonjwa hapo prison kimpeleke hospitali kubwa nje ya gereza.
Mdada yule kabla hajapelekwa hosp alimkabidhi Bebiy mtoto, akavua Herini, Bangili, Mkufu, vyote vya dhahabu na kijikaratasi chenye No ya simu ya mumewe Baba wa huyo mtoto aliekua akiitwa J.
Akiwa analengwa machozi mama J alimwambia Bebiy kwamba hategemei kurudi gerezani akiwa hai. (namnukuu)
"Ndg yangu Bebiy nakuachia mtoto nakuachia na rasilimali kidogo Mungu alizoniwezesha kua nazo, mlee huyo mtoto awe mwanao, sina namna nyingine ya kufanya ukijaaliwa kumaliza kifungo jaribu kumtafuta Babaake J , anaitwa Mr. Tiba, na kwa tatizo lolote la mtoto ama ataugua au vinginevyo unaweza ukauza chochote katika hivyo vipuli vitakusaidia mbele ya safari." (mwisho kunukuu)
wote machozi yakawamwagika mama J, akachukuliwa na gari ya jela na kupelekwa hosp na kupita siku 3 mama J akafariki, habari zikafika gerezani za msiba Bebiy akalia sana na akashukuru Mungu.
Mwaka mmoja, baadae askari mmoja wa gereza akaanza kumtongoza Bebiy huku akimuhadaa kua akiwa atamkubalia basi anao uwezo wa kumfanyia mpango Bebiy akatoka jela kwa kupitia misamaha ya kiongozi wa nchi.
Bebiy hakuyumbishwa na hilo, alimkatalia huyo askari mzee mpango wake.
Bebiy alikomaa akamaliza kifungo chake.
Na wakati Bebiy anaingia gerezani palikua na form ya kujaza ambapo ktk hiyo form kuna kipengele cha kujaza uraia wako unatoka nchi gani.
Bebiy alijaza anatoka ile nchi jirani alipoolewa dadaake Riza, hivyo siku amemaliza kifungo alipakiwa kwenye gari la serikali hadi nchi ile ya jirani, akiwa na mwanae J aliyempata jela, ikumbukwe miezi mi3 nyuma kabla Bebiy hajamaliza kifungo Mz Karama alifariki.
Bebiy baada kubatwa hapo kilichoanza kumsaidia No ya simu ya dadaake Maryamu alikua nayo kichwani, hivyo alitafuta duka la sonara akauza bangili moja, kisha akatafuta callbox na kumpigia kumpa habarize.
Then akamuomba Mariyamu ampe No za simu za Riza, akapewa na akampigia Riza.
Haikua rahisi Bebiy kufika huko kwani palikua ni umbali (kama Mtwara na Bukoba).
Ilimlazimu Bebiy kubadili magari ma3 kumfikisha huko. NITAENDELEA N