Treni ya umeme inakuja July 2017

Treni ya umeme inakuja July 2017

Daraja la Surrender halina umuhimu wowote zaidi ya kupendezesha jiji, nahisi focus kubwa ingewekwa kuboresha dodoma, Mwanza, Mbeya na Arusha.
 
images
images
images
 
Uzuri wa serikali /awamu zote zinapendelea mjini.
Wa mikoani mtusubiri kidogo mjini kuendelee kuwa mjini😀😀😛
 
Tujiandae kuishi kama mashetanani kwa kulazimisha hata visivyowezekana.

Salary Slip;

Naomba nitofautiane na wewe kwa hili.

Nadhani hapa ishu si kutowezekana. Kila kitu kinawezekana kabisa

Tatizo ninaloliona mimi ni kutamka kwa hisia tu kuwa serikali itafanya hivi au vile bila kuonesha ni kwa namna gani

Chukulia mfano ishu hii ya treni ya umeme ifikapo mwezi juni, 2017.

Kutamka tu si ishu na ofcoz kila mtu angependa kuliona hilo linafanyika hata kabla ya desemba, 2016 achilia mbali hadi hiyo juni 2017

Changamoto inayojitokeza na hata watu kutia mashaka ukiwemo wewe ni kipi kianze kwanza (setting priorities) kati ya umeme au treni yenyewe au zile ndege zingine moja ya kubeba abiria 160 na nyingine zaidi ya 240 au Tanzania ya viwanda

Mimi nasema hili kwa sbb mpaka sasa umeme bado ni shida ktk nchi yetu. Tuna umeme usio wa uhakika kwa 100% na hautoshi. Mimi siishi DSM, niko zangu Shinyanga.

Hebu tuelezane ukweli. Kuna siku inapita bila kukatika kwa umeme hata mara mbili hadi sita? Huku kwetu Shy ni kila siku na ilishakuwa ni "culture" na tumezoea, sina hakika huko DSM ambako wanatarajia kuletewa treni ya umeme unaokatikakatika ovyo ndani ya chini ya mwaka mmoja ujao!!

Sasa swali la kujiuliza ni kipi kianze kwanza? Uimarishe upatikanaji wa umeme kwanza au Tanzania ya Magufuli ya viwanda au madege makubwa ya Airbus??

Kingine ni muda. Tunaambiwa ni ndani ya mwaka mmoja tu yaani juni, 2017 treni za umeme na ndege zingine mbili kubwa za kupaa kutoka DSM hadi New York - USA ama Beijing - China bila kutua popote zilete watalii. Kwa hiyo tunajiuliza hii mipango ni realistic kweli au ni hisia za mwendokasi wa kilevi tu?

Naweza kuhitimisha kwa kusema hivi;

Kuwa na mipango ya kupata hiki au kile ni jambo moja lakini kupata kitu hicho ni jambo jingine kabisa!

Ndo kusema tunayo mikakati na njia halisia za kupitia ili kukiendea tunachokitaka au ni ndoto za mchana tu hizi?

Hili halina tofauti na lile tamko la kimwendokasi la mtakatifu sana na watakatifu wadogo wadogo kudaka na kuigiliza kama ndege kasuku la "ifikapo septemba, 2016 serikali itakuwa imehamia Dodoma!!"....

Lakini mwisho wa siku waka retreat na kumeza matapishi yao wenyewe walipoingia ktk utekelezaji na kuona kumbe hii ni "mipango hewa" na badae wakaja na rekebisho kuwa sasa itakuwa ni hadi 2020!!
 
View attachment 408957

Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais John Pombe Magufuli imepanga kununua treni ya umeme inayotarajiwa kuwasilini nchini mwezi Juni, 2017.

Treni hiyo inatarajiwa kufanya safari katika jiji la Dar es Salaam. Rais Magufuli amesema serikali inauwezo wa kutekeleza ahadi hiyo kwa kuwa fedha za kununulia treni hiyo zipo.

Pia Rais Magufuli amesema serikali iko katika harakati za uboreshaji na ujenzi wa miundo mbinu ya usafiri, ikiweno ujenzi wa reli za kisasa kuanzia Dar es Salaam, Mwanza na nchi jirani ikiwemo ya Rwanda.

Vile vile serikali yake iko katika hatua za ujenzi wa daraja la kisasa litakalo anzia maeneo ya daraja la Sarenda litakalo pitia baharini.

Hadi sasa miradi mbalimbali ya ujenzi wa miundombinu inaendelea nchi nzima ikiwemo mradi wa barabara za juu (Flyover) maeneo ya Tazara.

Aidha, Dk. Magufuli amesema serikali yake iko katika hatua za kutengeneza na kuboresha miji yake ili iwe ya kisasa.

Kila la heri katika ndoto zako ze mtukufu. Hopefully zitatimia.
 
Salary Slip;

Naomba nitofautiane na wewe kwa hili.

Nadhani hapa ishu si kutowezekana. Kila kitu kinawezekana kabisa

Tatizo ninaloliona mimi ni kutamka kwa hisia tu kuwa serikali itafanya hivi au vile bila kuonesha ni kwa namna gani

Chukulia mfano ishu hii ya treni ya umeme ifikapo mwezi juni, 2017.

Kutamka tu si ishu na ofcoz kila mtu angependa kuliona hilo linafanyika hata kabla ya desemba, 2016 achilia mbali hadi hiyo juni 2017

Changamoto inayojitokeza na hata watu kutia mashaka ukiwemo wewe ni kipi kianze kwanza (setting priorities) kati ya umeme au treni yenyewe au zile ndege zingine moja ya kubeba abiria 160 na nyingine zaidi ya 240 au Tanzania ya viwanda

Mimi nasema hili kwa sbb mpaka sasa umeme bado ni shida ktk nchi yetu. Tuna umeme usio wa uhakika kwa 100% na hautoshi. Mimi siishi DSM, niko zangu Shinyanga.

Hebu tuelezane ukweli. Kuna siku inapita bila kukatika kwa umeme hata mara mbili hadi sita? Huku kwetu Shy ni kila siku na ilishakuwa ni "culture" na tumezoea, sina hakika huko DSM ambako wanatarajia kuletewa treni ya umeme unaokatikakatika ovyo ndani ya chini ya mwaka mmoja ujao!!

Sasa swali la kujiuliza ni kipi kianze kwanza? Uimarishe upatikanaji wa umeme kwanza au Tanzania ya Magufuli ya viwanda au madege makubwa ya Airbus??

Kingine ni muda. Tunaambiwa ni ndani ya mwaka mmoja tu yaani juni, 2017 treni za umeme na ndege zingine mbili kubwa za kupaa kutoka DSM hadi New York - USA ama Beijing - China bila kutua popote zilete watalii. Kwa hiyo tunajiuliza hii mipango ni realistic kweli au ni hisia za mwendokasi wa kilevi tu?

Naweza kuhitimisha kwa kusema hivi;

Kuwa na mipango ya kupata hiki au kile ni jambo moja lakini kupata kitu hicho ni jambo jingine kabisa!

Ndo kusema tunayo mikakati na njia halisia za kupitia ili kukiendea tunachokitaka au ni ndoto za mchana tu hizi?

Hili halina tofauti na lile tamko la kimwendokasi la mtakatifu sana na watakatifu wadogo wadogo kudaka na kuigiliza kama ndege kasuku la "ifikapo septemba, 2016 serikali itakuwa imehamia Dodoma!!"....

Lakini mwisho wa siku waka retreat na kumeza matapishi yao wenyewe walipoingia ktk utekelezaji na kuona kumbe hii ni "mipango hewa" na badae wakaja na rekebisho kuwa sasa itakuwa ni hadi 2020!!

Kokosekana kwa umeme wa grid hakutamaanisha train hiyo ya kuhudumia wananchi wa dar itakosa umeme wa kuiendesha, huwezi kurun project ya huduma kwa kutegemea one source(grid), lazima uwe na standby source, kwahiyo sidhani kama upungufu wa umeme wa uhakika nchini kinweza kuwa ndio kikwazo kikubwa cha kutunyima maboresho ya jiji la dar ambapo ndio image ya TZ.

Rais pia asisahau ahadi nyingine Muhimu ya viwanda kwasababu watz wengi hawana ajira za uhakika lakini pia wawasimamie waajiri wengi wa binafsi ambao ajira zao zinawakandamiza watu wengi.
 
Kila kitu kinawezekana, watanzania bado wana ile dhana waliyojengewa tangu awali kuwa Tanzania ni maskini, na hakuna linalowezekana nchini...

Kwa hiyo kwa sasa ndo serikali hii inawaambia kuwa kila kitu kinawekana, na wao hawaamini hadi waone...

Zile safari alizofanya JK. miaka 10 yake, Zaidi ya safari 400, pesa hizo zingefanya mambo makubwa sana chini
Huo umeme kuwaka hapa mjini hautoshi hizo treni zitaendeshwa na makaa ya mawe au hebu jaribu kufikiri nje ya box
Mwezi hauwezi kuisha siku moja haujakatwa bila hata ya taarifa maalum kutoka tanesco au wewe mwenzetu unaishi magogoni
 
Kuandaa miundombinu ya train ya umeme si kazi ndogo.
 
Back
Top Bottom