Treni ya umeme inakuja July 2017

Treni ya umeme inakuja July 2017

Treni ya Umeme inakuja July Mwakani, kulingana na maelezo yako
Reli ya kisasa itaanza kujengwa lini na itakamilika lini?

Utotole;
Hilo ndo swali. Inaletwa iwekwe kwanza stoore au? Kwani, japo miye ni mshamba flan, sidhani ka zinatembea juu ya reli ya Tazara au Trl. Sasa, kipi kinatakiwa kuanza, treni au reli?? Hebu tuwekeni sawa wajameni. Nitafurahi sana ka uliyeleta hoja utasema kuwa njia yake itaanza kutengenezwa mwakani.
Naona kosa la sekondary za kata linataka kutokea tena hapa. Kujenga majengo na kuandikisha wanafunzi kabla ya kuandaa waalim. Mliona mlichofanya. Sekondary yenye Form 1 hadi 4 ina waalim 2 tu bila hata mlinzi.
 
Ila jamani vijijini kuna hali ngumu? Nashauri tutekeleze kwanza ilani zinazolenga huko!!!!
 
ila kwa kumnukuu mtoa uzi kasema treni hiyo itaoperate dar es salaam... sa swali ni kuwa vipi hizo mabasi za mwendokasi mtatupa? je hizo treni zitapita town kama pale posta?? na nadhan tutakuwa wa kwanza kutumia treni mjini kati... dunia nzima hamna mtu wa namna hyo
 
Kama haya ni kweli yanatoka kinywani mwa JPM naamini kwa asilimia 80 kwa sababu tangu ameingia madarakani ameanza utekelezaji kwa zaidi ya asilimia 50 ktk yale aliyoahidi...tulizoezwa uongo kwa hiyo bado ni unyasi gusa mguu!
 
View attachment 408957

Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais John Pombe Magufuli imepanga kununua treni ya umeme inayotarajiwa kuwasilini nchini mwezi Juni, 2017.

Treni hiyo inatarajiwa kufanya safari katika jiji la Dar es Salaam. Rais Magufuli amesema serikali inauwezo wa kutekeleza ahadi hiyo kwa kuwa fedha za kununulia treni hiyo zipo.

Pia Rais Magufuli amesema serikali iko katika harakati za uboreshaji na ujenzi wa miundo mbinu ya usafiri, ikiweno ujenzi wa reli za kisasa kuanzia Dar es Salaam, Mwanza na nchi jirani ikiwemo ya Rwanda.

Vile vile serikali yake iko katika hatua za ujenzi wa daraja la kisasa litakalo anzia maeneo ya daraja la Sarenda litakalo pitia baharini.

Hadi sasa miradi mbalimbali ya ujenzi wa miundombinu inaendelea nchi nzima ikiwemo mradi wa barabara za juu (Flyover) maeneo ya Tazara.

Aidha, Dk. Magufuli amesema serikali yake iko katika hatua za kutengeneza na kuboresha miji yake ili iwe ya kisasa.

Hii nchi kwa sasa kila kitu pesa zipo![emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Back
Top Bottom