Traffic police ni janga la kitaifa, wanazidisha ugumu wa maisha kwa wananchi

kavulata

JF-Expert Member
Aug 2, 2012
12,319
12,622
Bei ya mafuta imepanda sana, mishahara ni midogo sana na bidhaa zote sokoni zimepanda kwa kila mtu duniani wakiwemo hata polisi traffic.

Polisi wanazidisha ugumu wa hali hii kwa njia ya kutafuta makosa kwa wenye magari na wasafirishaji wa abiria na mizigo, hali inayosababisha gharama kubwa za usafiri na usafirishaji mijini na barabarani. Ukiendesha gari lazima uwe na hela ya askari barabarani, kwanini iwe hivi?

Wanatekeleza ukatili huu kwa njia zifuatazo.
1. Wanaanza msako wa magari yenye kasoro ndogondogo na madeni ya kubambikia ambayo hayalipwa kuanzia asubuhi kabisa wakati ule watu wanawahi kwenda kazini. Jambo hili linachelewesha watumishi, wafanyabiashara, wanafunzi, wasafiri wa mikoani na wagonjwa kufika kwa wakati waendako.
2. Kuwapiga fine madereva au kudai kitu kidogo ili kuwasamehe. Makosa yenyewe ni hata ukikosa triangle moja kati ya mbili, mkwaruzo kwenye gari.

3. Kujificha vichakani na kupiga picha kwa kificho magari yaendayo spidi na kurusha picha hizo kwa wenzao mbele ambao watakudai kitu wakuachie uendelee na safari yako, wanakuchelewesha njiani bila sababu za msingi. Yaani nililipishwa kitu kidogo kwa spidi ya mwendo wa km 54/hr. Njia zote za kwenda mikoani zimejaa viota vya kujifichia askari hawa wasioonekana njiani.

3. Pikipiki za maguta, bodaboda, kirikuu na gari za mizigo wanatembea roho juu kwenye nchi Yao wenyewe, askari wanaondoka na faida yote unayotarajia kuipata kwenye mzigo huo. Huu ni wizi sawa na wizi mwingine TU.

4. Watoto wanachanganyikiwa, shuleni wanafundishwa kuwa taa nyekundu simama, lakini wanapofika barabarani sio hivyo, traffic wanaruhusu magari kwenye taa nyekundu na kusimamisha kwenye taa ya njano na kijani, hadi inakuwa kero.

Ugumu wa maisha unazidishwa na hawa watu bila sababu za msingi. Wanaichonganisha serikali na raia wake, ili maisha ya mpiga kura wa kawaida yawe magumu sana.

Mama yetu tusaidie hili pia.
 
Nilikuwa natafuta gari ya kupakia mzigo wangu kila dereva anakuambia ongeza elfu 10,hapa mpaka kwako kuna vituo vitano, kila kituo buku 2.
 
Traffic wamegeuka kuwa kero sana! Kwa kifupi wamegeuka kuwa wanyang’anyi waliopangwa/kuwekwa kisheria!
Safari zimekuwa Ndefu sana pia sababu ya kusimamishwa kwa kaguzi zisizo na maana kwa kila baada ya km 20 au 50.
 
Unakuta kibao ni 50KPH wewe ukitembea 51KPH unaambiwa umezidisha mwendo na aidha uwape kitu kdg au wakuandikie fini 30,000 badala ya kuonya kwa vikosa vidogo. Hwa jamaa hapana!
Dhamira Yao sio kusaidia usalama wako bali kipato kwao. Hekaheka zote hizi za kujificha vichakani na kusimamisha magari sio kusaidia kupunguza ajali bali kipato kwao.
 
Wana vikoba vya laki kwa siku hela watatoa wapi zaidi ya kwenu wanyonge?
Yani kumiliki gari tu mjini ushageuka mtaji kwa askari😂😂😂
Vitendo hivi hakuna asiyevijua, watu Wana wasiwasi ya kuendesha magari Yao ndani ya taifa lao wenyewe. Eti utembee na hela ya kuwalipa polisi kipumbavu kabisa.
 
Dhamira Yao sio kusaidia usalama wako bali kipato kwao. Hekaheka zote hizi za kujificha vichakani na kusimamisha magari sio kusaidia kupunguza ajali bali kuna kipato kwao.
Kuna mmoja nilimkuta Mbugani mikumi yupo Juu ya mti, anapiga picha ya speed, hapo hata akukute uko na speed ya 52km unae mbele. Nikajisemea huyu kuna siku ataliwa na simba tu
 
Dhamira Yao sio kusaidia usalama wako bali kipato kwao. Hekaheka zote hizi za kujificha vichakani na kusimamisha magari sio kusaidia kupunguza ajali bali kipato kwao.
Yaani mkuu hawa jamaa nikiwaona barabarani huwa nachefuka kwa viswali vyao uchwara wakati wa kutaka hela!
 
Bei ya mafuta imepanda sana, mishahara ni midogo sana na bidhaa zote sokoni zimepanda kwa kila mtu duniani wakiwemo hata polisi traffic.

Polisi wanazidisha ugumu wa hali hii kwa njia ya kutafuta makosa kwa wenye magari na wasafirishaji wa abiria na mizigo, hali inayosababisha gharama kubwa za usafiri na usafirishaji mijini na barabarani. Ukiendesha gari lazima uwe na hela ya askari barabarani, kwanini iwe hivi?

Wanatekeleza ukatili huu kwa njia zifuatazo.
1. Wanaanza msako wa magari yenye kasoro ndogondogo na madeni ya kubambikia ambayo hayalipwa kuanzia asubuhi kabisa wakati ule watu wanawahi kwenda kazini. Jambo hili linachelewesha watumishi, wafanyabiashara, wanafunzi, wasafiri wa mikoani na wagonjwa kufika kwa wakati waendako.
2. Kuwapiga fine madereva au kudai kitu kidogo ili kuwasamehe. Makosa yenyewe ni hata ukikosa triangle moja kati ya mbili, mkwaruzo kwenye gari.

3. Kujificha vichakani na kupiga picha kwa kificho magari yaendayo spidi na kurusha picha hizo kwa wenzao mbele ambao watakudai kitu wakuachie uendelee na safari yako, wanakuchelewesha njiani bila sababu za msingi. Yaani nililipishwa kitu kidogo kwa spidi ya mwendo wa km 54/hr. Njia zote za kwenda mikoani zimejaa viota vya kujifichia askari hawa wasioonekana njiani.

3. Pikipiki za maguta, bodaboda, kirikuu na gari za mizigo wanatembea roho juu kwenye nchi Yao wenyewe, askari wanaondoka na faida yote unayotarajia kuipata kwenye mzigo huo. Huu ni wizi sawa na wizi mwingine TU.

4. Watoto wanachanganyikiwa, shuleni wanafundishwa kuwa taa nyekundu simama, lakini wanapofika barabarani sio hivyo, traffic wanaruhusu magari kwenye taa nyekundu na kusimamisha kwenye taa ya njano na kijani, hadi inakuwa kero.

Ugumu wa maisha unazidishwa na hawa watu bila sababu za msingi. Wanaichonganisha serikali na raia wake, ili maisha ya mpiga kura wa kawaida yawe magumu sana.

Mama yetu tusaidie hili pia.
DAWA NI WENYE VYOMBO VYA MOTO
KUPAKI MAGARI TU

OVA
 
Utafanya nini mkuu, hata Rais analifahamu hili? Hata jaji mkuu analifahamu hili? Hata IGP analijua. Utapeleka kwa nani?
Wellcome to police state, katiba mpya ingetuletea kitu inaitwa IPID, hawa ni police wenye uwezo wa to arrest their own, wewe unapoona hujatendewa haki let's say mikumi check point, unalenga kituo cha police pale mikumi na kumfungulia mashitaka, IPID watachunguza even do arrest kwa suspect, kwa sasa bado sana....ILA nimeota kuwa Botswana 🇧🇼 police wote watakuja kufanya kazi Tanzania, na hawa wa kwetu wataenda Botswana!!no just kidding mkuu ila tuna safari ndefu na tusitegemee watu watupiganie mkuu
 
Kuna mmoja nilimkuta Mbugani mikumi yupo Juu ya mti, anapiga picha ya speed, hapo hata akukute uko na speed ya 52km unae mbele. Nikajisemea huyu kuna siku ataliwa na simba tu
Loooooo mkuu kumbuka MM za JKT, tambaa usiku tu, magari ya IT ndio taa yako, always funga nao convoy
 
Tuseme kirikuu kapakia mzigo elf 30, hapo hapo anunue mafuta abaki na angalau faida kidogo, hapo hapo trafiki anataka apige bao, hawa watu nafikiri ifike mahali serikali iwalipe mshahara unaowatosheleza maana inaonekana hawatosheki na mishahara yao au wasilipwe mishahara kabisa wabaki kuokota pesa ya kiwi ili tujue moja.
 
Watu wamejawa na hofu ndani ya taifa lao, yaani dereva akiona mtu yeyote mbele kuleee kavaa nguo nyeupe/kanzu mapigo yake ya moyo yanabadilika akidhani ni traffic polisi, aandae pesa.
Yashanikuta nikiwa way to Mbeya, hasa ikukute siku ya ijumaa saa 7.20mchana uwe road kuna kuwa na kanzu nyingi na vikofia vyeupe kwa mbali, moyo unafanya paa, ukishani ndio wenyewe. Tabu tupu, watoke tu kwakweli barabara I.
 
Back
Top Bottom