Tracing mobile phone

Tracing mobile phone

Inkoskaz

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2010
Posts
6,359
Reaction score
2,379
Wakuu..
kwa bahati mbaya nimemtumia mtu pesa kwa makosa dakika chache baadae nilipogundua tatizo nilijaribu kupiga ile namba ikawa imezimwa,nikapiga vodacom m-pesa wakasema pesa imechukuliwa mudamfupi baada ya kutumwa.
Kesho yake ile namba ikawa hewani,juhudi za kuipigia hazikuzaa matunda kwani hakupokea,tukamtumia msg kuwa tumeshajua jina lake na location yake yupo Moshi hivyo arejeshe hizo pesa kwani ushahidi kamilitunao..hapo ikaanza danadana mara simu ilizima mara oh mnanitisha marakosa ni la nani lakini lastly akaconclude kuwa do whatever yo want
Vodacom wameassist kublock account na kutupa location lakini police bado hawajampata na simu yake anawasha kwa machale
Je kuna mbinu nyingine ya kuweza kumtrace mtu at least nearby na mahali alipo?
Kwa kuzingatia makosa ya kiubinadamu hivi mtu akikosea akautumia pesa hutakiwi kumrejeshea?
Take position ya mtumaji au ya mtumiwaji kuwa ni wew na ulikuwa na dharura like ugonjwa,msiba etc
Kama kuna mdau ana knowledge zaidi ya kubana watu wa aina hii atumwagie kwa faida ya wengi..najua ni mambo yanatokea kila siku japo mimi nahesabu hasara lakini at least huyu aliyejisevia apate haki yake..
bila kusubiri kuulizwa huyo mtu aliyetumiwa namba yake ni0754 525862 jinsia ni ke anaitwa Elinaike Makundi
 
Duu mchaga kwa pesa!maana pesa zote duniani wanafikiri ni zao kama vile mmasai na ng'ombe.ALLAH atakupa zaidi samehe!
 
Dah . Hiyo sijui kama utakaa uipate. Ndio weakness za mobile pesa .
 
Duu mchaga kwa pesa!maana pesa zote duniani wanafikiri ni zao kama vile mmasai na ng'ombe.ALLAH atakupa zaidi samehe!
Bongolala..nimesamehe ila nikifikiri ingekuwa ni mtu katumiwa salary yake yote halafu imepotea njia angesurvive vipi
 
Dah . Hiyo sijui kama utakaa uipate. Ndio weakness za mobile pesa .

kwa kweli ni majaliwa,ila su jambo jema
niliwwhi kutumiwa 30,000 kumbe ni ada ya mtoto nilipoirejesha jamaa hawakuamini wakanitumia 3,000
Jamaa mwingine aliwahi kukosea kumtumia rafiki yangu..tulipompigia jamaa akasema ni kweli nimeingiziwa 40,000 lakini dakika mbili zijazo nitazichukua hapo kwa wakala maana nipo vibaya ila tuwasiliane kesho saa kumi...aisee tukawa wapole lakini kesho yooake kumi kasoro dk mbili tukasikia kimeseji kimeingia jamaa akazirejesha na
kisha akapiga simu kuconfirm
alijipa soft loan keshi yake akarudisha bila riba
 
Hao Vodacom hawajawasaidia vya kutosha, inategemea na userious wenu labda kutokana na kiwango chenyewe cha pesa. Voda wanaweza kupata jina la huyo jamaa na utambulisho wake kamili (?), then wanaweza kutrace anawasiliana sana na nani, mnaweza kutumia watu anaowasiliana nao kufika karibu naye kwa urahisi, then kwa kushirikiana na police...BUM...HUYU HAPA!:scared:
 
Hao Vodacom hawajawasaidia vya kutosha, inategemea na userious wenu labda kutokana na kiwango chenyewe cha pesa. Voda wanaweza kupata jina la huyo jamaa na utambulisho wake kamili (?), then wanaweza kutrace
anawasiliana sana na nani, mnaweza kutumia watu anaowasiliana nao kufika karibu naye kwa urahisi, then kwa kushirikiana na police...BUM...HUYU HAPA!:scared:
ni kweli mku..amount ni 72K Na hilo la watu anaowasiliana nao tumeliona lakini tukaona tutajichosha na kuwasumbua tu..ipo siku atajichanganya mwenyewe
 
Is there any method to trace the location of the mobile phone?
 
bora umtafute ana kwa ana ila usitegemee itafika wakati ataweka pesa ktk account yake maana anajua atakatwa tu juu kwa juu, pole! Kuhusu kutrace huyo jamaa nadhani ni ngumu ingawa mtandao husika unaweza kukusaidia vizuri zaidi ikiwa utakidhi vigezo vyao vya kutoa hizo details
 
bora umtafute ana kwa ana ila usitegemee itafika wakati ataweka pesa ktk account yake maana anajua atakatwa tu juu kwa juu, pole! Kuhusu kutrace huyo jamaa nadhani ni ngumu ingawa mtandao husika unaweza kukusaidia vizuri zaidi ikiwa utakidhi vigezo vyao vya kutoa hizo details
ni kweli mkuu..ila watu tunatofautiana maadili..how comes you swindle money which is not yours
 
kwa faida ya wanajamvi wote iwapo utapatwa na tatizo kama hili piga namba 15366 pindi tu upokeapo meseji ya mpesa na kubaini kuwa umekosea utumaji wa pesa. Muda huo huo watazui fedha uliyotuma na kuirudisha kwenye account yako ya Mpesa ndani ya masaa 24.
 
Yesuu na maria babangu pesa na mchaga ni kama wangoni na mademu
 
kwa faida ya wanajamvi wote iwapo utapatwa na tatizo kama hili piga namba 15366 pindi tu upokeapo meseji ya mpesa na kubaini kuwa umekosea utumaji wa pesa. Muda huo huo watazui fedha uliyotuma na kuirudisha kwenye account yako ya Mpesa ndani ya masaa 24.

unaposema ndani ya masaa ishirini na nne ni kuwa hiyo account ya aliyepokea inakuwa imezuiliwa? Au wkt huo anaweza kwenda kwa mtoa huduma akatoa na pesa?
 
Is there any method to trace the location of the mobile phone?
Sidhani mkuu kama kuna namna unaweza kutrace location ya simu ilipo zaidi ya kujua simu inatumia mnara wa sehemu gani.

Kinacho nishangaza katika hili ni namna Vodacom wanavyoshindwa kuwasaidia wateja wanapopatwa na shida kama hii
Nilitaraji labda Voda watawasiliana na mwenye kutumiwa pesa kimakosa na kumtaka azirejeshe haraka, na akikaidi basi wao kama Voda ndio wenye access zote na mamlaka kisheria kutafuta namna ya kumpata huyo mtu kwa kuwabana hata watu anao wasiliana nao mara kwa mara ambao wanaweza kumshawishi arudishe hizo pesa.
Au kublock no zao na wakija ofisini wataelezwa wasaidie kumpata

Lakini hii ya kutafuta individual ni ngumu kidogo mkuu

 
lakini anapatikana manake nimejaribu kumpigia simu yake inaita!, sasa nashangaa kama Vodacom na polisi wameshindwa kukusaidia kwasababu kama inaita simu yake akipokea tu voda wanaweza kufuatilia hadi location specifically mnara anaotumia ikawa njia rahisi ya kumonitor, lakini pia wanaweza kukusaidia kwa kukamata namba za watu anaowasiliana nao halafu wakabanwa wale then wakakupeleka hadi eneo aliko!!!! mbona polisi wamekuwa wakifanya hivyo mara nyingi?
 
Mkuu unaweza kuniambia baada ya kugundua umetuma pesa kwa mtu ambaye ukukusudia kumtumia ilichukua mda gani kuwasiliana na vodacom?
 
M2 AKIIBA BLACKBERRY AU I-PHONE ANAKAMATWA SIMPLY KWA NJIA ILIYONIFURAHISHA=> Halow naitwa Janeth napiga simu toka VODACOM, wewe ni fulani fulani na namba yako ya simu ni ___ ___ , NDIO basi umefanikiwa kushinda mill1 kweny bht nasibu, thn wakamwambia afike OFISINI apo ujanja wake wote ukaisha, Mbna ht kwa hli linawezekana fatilia VODA labda km una hela nyingi ndo umuache.
 
Back
Top Bottom