TRA wanavyofunga biashara za wazalendo

TRA wanavyofunga biashara za wazalendo

Mkuu yamewakuta wafanyabiashara wengi.Na serikali sikivu iko kimya.
Hata waziri wa sasa Nd Mwambe alivyokuwa TIC alilieleza tatizo wazi kabisa lakini serkali hailifanyii kazi.
Tax base inazidi kupungua na ni dhahiri matokeo yake ni kodi kupungua.
Seikali sikuvu-kimya!
Mkuu nilikuwa nina fanya biashara ninaona dalili za watu wakubwa wenye kulipa kodi zaidi ya 300m kwa mwezi wakikaribia kufunga biashara zao
 
  • Thanks
Reactions: PNC
Siku moja niliona Messi na Ronaldo wanashitakiwa kwa kukwepa kodi nikajua huu ni utani..nikafikiria na pesa zote walizonazo wanaweza kweli kufanya hivyo.Kumbe TRA ndo wanasababisha haya .

Sasa nimeamini dunia haiko fair yaani mtu anakula rushwa ya kutosha kutoka kwa wafanyabiashara anaowabambikizia kodi kwa kisingizio cha kuwapunguzia Jodi endapo watampa rushwa inayozidi hata mshahara wake baadae tena anapokea mshahara wake kuilaini.

Aisee..ndo raha ya usomi rahisi kutapeli wajinga
 
Wala usifunge biashara unahama nchi kidogo patulie unapotezea muda wako hata kwa nchi jirani maisha yanasogea
 
Hongera sana. Kuamua kufunga biashara kwa kufuata taratibu na kujipa muda wa kutafakari upya nalo ni jambo la busara. Mabadiliko siku zote yana maumivu, lakini maumivu yanakua makali zaidi kama wahusika hawaandaliwi sawasawa kukabiliana na hayo mabadiliko
Sio mabadiliko aisee wana hujumu!
 
Sio mabadiliko aisee wana hujumu!

Kuna ujinga mwingi sana pale. Nimekua nafanya kazi na wafanyabiashara na nimekutana na vitu ambavyo mtu unajiuliza hawa TRA nia yao haswa ni nini. Kwani hawaoni kwamba wasiposaidia wawekezaji kukua ni sawa tuu na kuhujumu uchumi??

TIC nao walikua hivyohivyo wamebadilisha wakurugenzi weweee lakini wapi. Kuna hujuma kubwa sana kwenye hivi vyombo vya serikali

Na hizi hujuma zinaumiza wananchi na wawekezaji wote wa nje na wazawa.. pamoja na watanzania wengine wanaotegemea huu uwekezaji kuendesha maisha yao

TRA wafike mahala wawe chombo cha kuhamasisha uwekezaji kwa wawekezaji wenye nia njema
Na iwashughulikie wahujumu uchumi bila kuumiza wengine
 
Lipeni kodi au mfunge biashara hizo nyingine ni kelele tu, hazijengi nchi !
Kodi zipi? Maana kodi za kawaida zinalipwa vizuri au unataka walipe kodi VAT za kubambikiwa kwa uonevu? Wewe utakuwa ni mmojawapo wa maofisa wanawafungia A/C wafanyabiashara, wewe ni mnufaika wa huo uonevu wote
 
Bank zitaanza kukosa imani za wafanyabiashara
Mkuu huu ni mkakati maalum wa kuhakikisha wafanyabiashara wanamalizwa kiuchumi kisha kuzikimbia biashara zao. Ule usemi wa Jiwe kuwa "wataishi kama mashwtani"usifikiri ulikuwa ni bahati mbaya. Kumbuka aliwahi kuwapa Wamiliki wa Vituo vya Mafuta siku 14 wawe wamefunga mashine za EFD vinginevyo vitageuzwa kuwa vya kupigia matofali. Sasa TRA wafanye nn??

Kumbuka pia kumuweka ndani aliyewahi kuwa Kamishina wa TRA kwa muda mrefu ulikuwa na lengo la kuwatisha na kuwajaza hofu Watendaji wengine wa TRA kuwa anything might happening to them. Ndiyo matokeo yake tunayoyaona sasa.

Wafanyabiashara hawana pa kukimbilia zaidi ya kuzifunga biashara zao kwani Mahakamani hawataambulia kitu. Unakumbuka wakati wakazi wa Jija la Dar wakivunjiwa nyumba zao alisema kuwa ukifuata sheria utachelewesha maendeleo? Mf ukitaka kpanua barabara laziba baadhi ya nyumba zivunjwe. Hivyo wamiliki watakimbila Mahakamani kuweka zuio. Kwenye utawala wangu hicho kitu hakipo.

Mkuu Jiwe hataki kabisa sekta binafsi zikue. Tizama makampuni ya Ulinzi walivyonyang'anywa malindo yao na kupewa SUMA-JKT. Angalia hata Shule binafsi nyingi zinapumulia mashine.
 
Siku moja niliona Messi na Ronaldo wanashitakiwa kwa kukwepa kodi nikajua huu ni utani..nikafikiria na pesa zote walizonazo wanaweza kweli kufanya hivyo.Kumbe TRA ndo wanasababisha haya .
Sasa nimeamini dunia haiko fair yaani mtu anakula rushwa ya kutosha kutoka kwa wafanyabiashara anaowabambikizia kodi kwa kisingizio cha kuwapunguzia Jodi endapo watampa rushwa inayozidi hata mshahara wake baadae tena anapokea mshahara wake kuilaini.
Aisee..ndo raha ya usomi rahisi kutapeli wajinga
Sasa wengi hutumia VAT kuwabambikia kodi huku wakiwatishia kesi za utakatishaji fedha na uhujumu uchumi
 
Back
Top Bottom